Ukipata milioni unaila siku tatu, ikibaki elfu kumi unaishi nayo week. Hii kitaalam mnaiitaje?

Ukizifuga kuna mpuuzi atakuja kuzifuja km aliwahi kuzitafuta
hamna kitu nafurahia katika utafutaji wangu kama kuona watu wangu wa karibu kama watoto,ndugu,wazazi na jamaa wanafaidi vilivyo nilivyovisotea mimi, habari za kufuja mali zangu wakati nimekufa haitanidhuru kwa lolote lile, kikubwa tu maisha yangu yamekuwa mfano wa kuigwa na mtu yeyeto mwenye akili timamu....
 
Nimekwambia ukizifuga kuna mpuuzi atakuja kuzifuja sijasema uzitumie vipi na kwa nani
 
na mimi nimekwambia hamna kitu nafurahia kama kuona mpuuzi mmoja ambaye ni mtu wangu wa karibu anafuja mali zangu vilivyo...
Hakuna tajiri wa hivyo wewe utakua kapuku mmoja hivi, tajiri hata watoto wanawekewa mkazo hakuna kuchezea Pesa ovyo bila kuifanyia kitu cha maana chenye kuleta faida
 
Hakuna tajiri wa hivyo wewe utakua kapuku mmoja hivi, tajiri hata watoto wanawekewa mkazo hakuna kuchezea Pesa ovyo bila kuifanyia kitu cha maana chenye kuleta faida
Wapi nimekwambia mi tajiri?...
 
Hata sielewi mi mwenyewe Nimejikuta nimekua na matumizi mabaya ya pesa kupindukia ndani ya wiki hizi 5 tangu mwaka uanze sijui nimekumbwa na nini
 
Rafiki yangu anafanya kazi mgodi mkubwa huko geita..analipwa mil4 analipiwa ada za watoto kila mtoto mil2.5 anapewa hela ya kodi laki9 kila mwezi, anapewa hela ya matumizi ya nyumbani laki3 kila mwezi anapewa bonas za skukuu na holiday, anapewa bima ya afya first class yeye pamoja na familia nzima lakini ananikopa sana na huwa anakuwa na madeni mpaka mil3 kwenye bars mbalimbali na hajajenga..hivyo hapo ni nidhamu ya pesa tu haujarogwa.
 
Natumaini ulikuwa unapasua sana essay🤣
 
Akili mbofu a.k.a akili matope🤭.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…