Ukipata milioni unaila siku tatu, ikibaki elfu kumi unaishi nayo week. Hii kitaalam mnaiitaje?

Ukipata milioni unaila siku tatu, ikibaki elfu kumi unaishi nayo week. Hii kitaalam mnaiitaje?

😂 kuna waliowahi kusema hivyo sahivi wanajutia.

Mzee wangu aliwahi niambia miaka hiyo anaitiwa maeneo ya kununua kimara alipuuzia na kusema nani anunue pori, hela akaweka heshima bar kuna rafiki yake alinunua akatulia kaja kuuza kwa sasa anaponda raha za uzeeni. Kupanga ni kuchagua.
Mzee wako ni legend kama mzee wangu tofauti yao mzee wangu alishatangulia mbele za haki akatuachia msala.
 
Asilimia mia moja ni kujiendekeza tu...hamna lolote...

sijawahi kucheza kamari yeyote ile kwa zaidi ya miaka kumi na tano mpaka sasa,...
Situmii kilevi chochote kile kwa zaidi ya miaka mitano sasa...

Nikiwa najitafuta migodini, rafiki zangu walikuwa wanashangaa nawezaje kwenda kugonga nyundo maporini huko, ilihari nina zaidi ya million kwenye account yangu..wakati huo na mimi nawashanga WANASHINDWA NN...
kifupi wengi hawana ndoto kubwa,na walionazo hawawezi kujitoa muhanga vya kutosha ili kutimiza ndoto zao,wapenda sifa za kijinga zinazodumu kwa siku moja na kisha kuyeyuka kama barafu tu,na ndio sababu kama umechunguza vizuri watu wengi wakishajenga kanyumba tu ka kulaza mbavu, hata jitihada za utafutaji au uwekezaji zinapungua, akinunua kipikipiki au kigari basi kamaliza kila kitu..kinachobaki ni kujitamba huko bar, vijiweni na kwenye mitandao ya kijaamii.....

mtu ambaye akipata pesa kidogo hakamatiki, wala hashauriki na zikiisha ndo anatia huruma na kuwa msikilizaji mzuri na kuapa kuto kurudia kwingi, kamwe usimsaidie kwa kumpa pesa, anapolia njaa mkumbushe juu ya kutapanya kwake pesa kipindi alipopata kilaki moja...
Ni kweli kabisa mkuu nakubaliana na yote uliyoyasema, kamari ni addiction ambayo ilinitesa sana namshukuru Mungu nilifanikiwa kuacha baada ya kujitathimini na kuona nateketeza hela ambazo nazitafuta na kuzipata kwa shida.

Sifa za kuonekana zinawamaliza wengi, kama huyo jamaa ni kawaida kujitapa alitumia kiasi kikubwa cha pesa kulewa na starehe nyingine, alafu baada ya kuyasema hayo bado atalia shida.
 
Mchoro umetiki umepata kazi ukalipwa million hela haichukui siku mbili ya tatu chali umebaki na hewa hamna kitu ila ka elfu ulichobakiza kanadumu hata siku nne bila shida, unakabembeleza leo 2000, kesho umetumia 3000 keshokutwa 3000 na nyumbani hutoki siku nzima.

Kwanini hatuna ile roho ya kwamba hela imeingia Tayari ni yangu kwa sasa niachane nayo hiyo millioni nianze kusuka michongo mingine ya kupata nyingine.Hata kama kazi na bata ila million nyingi ukiwekeza kula nyama Choma na vya kunoga noga walahu ufaidi hata week tatu basi ila Duuh sio poa yaani siku tatu unabakia lofa.

ndo maana wanakwambia umasikini unaanzia kwene akili
 
Mchoro umetiki umepata kazi ukalipwa million hela haichukui siku mbili ya tatu chali umebaki na hewa hamna kitu ila ka elfu ulichobakiza kanadumu hata siku nne bila shida, unakabembeleza leo 2000, kesho umetumia 3000 keshokutwa 3000 na nyumbani hutoki siku nzima.

Kwanini hatuna ile roho ya kwamba hela imeingia Tayari ni yangu kwa sasa niachane nayo hiyo millioni nianze kusuka michongo mingine ya kupata nyingine.Hata kama kazi na bata ila million nyingi ukiwekeza kula nyama Choma na vya kunoga noga walahu ufaidi hata week tatu basi ila Duuh sio poa yaani siku tatu unabakia lofa.
Ni nguvu ya soko mkuu, ukiwa na milioni hata Zuchu atakupenda lakini ukiwa na elfu kumi hata mbwa anakukimbia
 
Ingawa milioni huwezi kuila siku 3 labda kama umelipa madeni sawa. Ila kama hujalipa madeni ukala milioni moja ndani ya siku 3 unataka maombi, ni matumizi mabaya ya pesa.

N.b mbinguni hakuna hotel tule tushibe hapa duniani, kitu pekee unaenda nacho kaburini ni tumbo lako. Magari na majumba vitabaki duniani vikigombaniwa so kula as much as you can.
Watu wanaitawanya milioni ndani ya masaa we unasema siku 3, hukuwahi kufika bar ukakuta watu wanamwaga Hennessy chini.
 
Ni kweli kabisa mkuu nakubaliana na yote uliyoyasema, kamari ni addiction ambayo ilinitesa sana namshukuru Mungu nilifanikiwa kuacha baada ya kujitathimini na kuona nateketeza hela ambazo nazitafuta na kuzipata kwa shida.

Sifa za kuonekana zinawamaliza wengi, kama huyo jamaa ni kawaida kujitapa alitumia kiasi kikubwa cha pesa kulewa na starehe nyingine, alafu baada ya kuyasema hayo bado atalia shida.
Watu wengi sana wanateseka kwa kujitakia tu...ndo maana sio ajabu kuona watu wakitumbua tu pesa za kazi au za mikopo ya biashara..yote ili awe tu gumzo mjini🤧😏😏🚮
 
Watu wengi sana wanateseka kwa kujitakia tu...ndo maana sio ajabu kuona watu wakitumbua tu pesa za kazi au za mikopo ya biashara..yote ili awe tu gumzo mjini🤧😏😏🚮
Ukizifuga kuna mpuuzi atakuja kuzifuja km aliwahi kuzitafuta
 
Mchoro umetiki umepata kazi ukalipwa million hela haichukui siku mbili ya tatu chali umebaki na hewa hamna kitu ila ka elfu ulichobakiza kanadumu hata siku nne bila shida, unakabembeleza leo 2000, kesho umetumia 3000 keshokutwa 3000 na nyumbani hutoki siku nzima.

Kwanini hatuna ile roho ya kwamba hela imeingia Tayari ni yangu kwa sasa niachane nayo hiyo millioni nianze kusuka michongo mingine ya kupata nyingine.Hata kama kazi na bata ila million nyingi ukiwekeza kula nyama Choma na vya kunoga noga walahu ufaidi hata week tatu basi ila Duuh sio poa yaani siku tatu unabakia lofa.
hii pia ni hatua
uko njiani kufanikiwa kwakuwa ushalijua tatizo.
 
Watu wengi sana wanateseka kwa kujitakia tu...ndo maana sio ajabu kuona watu wakitumbua tu pesa za kazi au za mikopo ya biashara..yote ili awe tu gumzo mjini🤧😏😏🚮
Na mwisho wa hayo yote huwa ni maumivu makali ya kupigika.
 
Back
Top Bottom