Ukipata milioni unaila siku tatu, ikibaki elfu kumi unaishi nayo week. Hii kitaalam mnaiitaje?

Ukipata milioni unaila siku tatu, ikibaki elfu kumi unaishi nayo week. Hii kitaalam mnaiitaje?

Mchoro umetiki umepata kazi ukalipwa million hela haichukui siku mbili ya tatu chali umebaki na hewa hamna kitu ila ka elfu ulichobakiza kanadumu hata siku nne bila shida, unakabembeleza leo 2000, kesho umetumia 3000 keshokutwa 3000 na nyumbani hutoki siku nzima.

Kwanini hatuna ile roho ya kwamba hela imeingia Tayari ni yangu kwa sasa niachane nayo hiyo millioni nianze kusuka michongo mingine ya kupata nyingine.Hata kama kazi na bata ila million nyingi ukiwekeza kula nyama Choma na vya kunoga noga walahu ufaidi hata week tatu basi ila Duuh sio poa yaani siku tatu unabakia lofa.
Hii tunaita....kupata hela sio tatizo....
Ila kumiliki hela(kufanya isikupotee)....hii ni kwa waterless wachache.....hasa walioikimbia ZINAA
 
Kwana hata Yesu si alituthibitishia hili,nashauri watu wasome maandiko [emoji23]
Mathayo 6 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁹ Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba;
²⁰ bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi;
²¹ kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.


²⁴ Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
²⁵ Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
²⁶ Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?
²⁷ Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?
²⁸ Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti
²⁹ nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.
³⁰ Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?
³¹ Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?
³² Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.
³³ Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
³⁴ Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
 
Mchoro umetiki umepata kazi ukalipwa million hela haichukui siku mbili ya tatu chali umebaki na hewa hamna kitu ila ka elfu ulichobakiza kanadumu hata siku nne bila shida, unakabembeleza leo 2000, kesho umetumia 3000 keshokutwa 3000 na nyumbani hutoki siku nzima.

Kwanini hatuna ile roho ya kwamba hela imeingia Tayari ni yangu kwa sasa niachane nayo hiyo millioni nianze kusuka michongo mingine ya kupata nyingine.Hata kama kazi na bata ila million nyingi ukiwekeza kula nyama Choma na vya kunoga noga walahu ufaidi hata week tatu basi ila Duuh sio poa yaani siku tatu unabakia lofa.
Inaitwa

Ukichengwa Tulia [emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji23][emoji2957][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom