Ukishajua hila zao, utafanya nini?

Ukishajua hila zao, utafanya nini?

Watafutie dawa Kali kuizidi yao afu wewe ndo uwafanye makondoo sasa
Atajuaje kama hiyo dawa ni kali kuzidi wao mkuu?! I mean je kama watafanikiwa wao?! Wakamuwahi jamaa maana pia hilo suala linaendana na imani yake jamaa kama haikubali manake itakuwa ishu
 
Mimi naombeni anaye Jua Mtaalamu wa akuniondolea Wachawi wa wili wa familia wana uwa watu kwenye familia yangu na kuwafanya watu vichaa kila.uchwao

Naitaji mganga mwenye uwezo aniondolee kabisa hawa watu
Duh...mkuu pole
 
Waambie kuwa umewashtukia njama yao, watakuwa wapole kama mbwa koko.
Akiwaambia amewashtukia kama wao ni sikio la kufa si wataendelea na hatimaye watamuumiza. Maana kwa uchunguzi aloufanya jamaa anasema set up alowekewa inatakiwa ategue sio kujaribu jaribu. Seem wapo very serious.
 
Wambie ukwel kuwa umeisha washtukia. Alaf wachape na mkwala wakijaribu tu kufanya huo upuuzi wao wajue watampoteza binti yao
Kwa maelezo ya jamaa anasema anahitaji kufanya jambo...kusema haitoshi, anahisi wana plan B...ukizingatia binti hana ajuacho na amependana nae kidhati.
 
Wewe umejuaje mkuu, nani kakwambia hiyo siri yao, au na wewe umeenda kwa mtalaamu ??

Ebu tuanzie hapa kwanza. Nitarudi nikipata jibu lako!
Kwa mujibu wa maelezo yake, anasema alitonywa na ndugu mmojawapo akaanza uchunguzi rasmi, akafanikiwa kupata mawasiliano ya anaowatuhumu...pili akaoneshwa mmama anaewasukia plan ni jirani yao...akajiridhisha anavyojua yeye. Etc.
 
Kwa maelezo ya jamaa anasema anahitaji kufanya jambo...kusema haitoshi, anahisi wana plan B...ukizingatia binti hana ajuacho na amependana nae kidhati.
Amwambie binti ili ajue sasa mchezo wa ndugu zake na ikiwezekana wahame hapo kabsaa bila ata kuwatarifu
 
Kwa mujibu wa maelezo yake, anasema alitonywa na ndugu mmojawapo akaanza uchunguzi rasmi, akafanikiwa kupata mawasiliano ya anaowatuhumu...pili akaoneshwa mmama anaewasukia plan ni jirani yao...akajiridhisha anavyojua yeye. Etc.
Oky, aisee! Piga chini.
 
Ni heri na bahati kubwa kwake hilo kalijua mapema, asipoteze muda hata Kama anampenda kiasi gani huyo manzi wake, apige chini huku akiwa amejipanga vyema. Ni mhanga wa mambo hayo, na yamenitesa zaidi ya miaka mitatu...
 
Baada ya kujua hayo umemshirikisha mkeo,kwani na yeye anasemaje?
Mkuu hii ishu jamaa jana jioni kamwita bidada kamweleza kila kitu na kumuonesha baadhi ya uthibitisho. Binti amelia sana usiku kwa mujibu wa maelezo ya jamaa...akarudi kwao.
Leo asubuhi binti ametuma sms kwa jamaa na kumwambia ameamua kuhama mkoa na simu amezima na hakusema anaenda wapi. Hapa ndio jamaa amebaki ameduwaa tu.
 
Back
Top Bottom