Kama usemavyo ndivyo, basi tuna safari ndefu sana, kwa sababu tuliowategemea wauvunje Muungano, sasa ndio wasiotaka kabisa kusikia hiyo habari.
Kwa maana yako ni kwamba tutakuwa nao CCM kwa muda mrefu sana.
Matumaini tuliyokwishayaweka kwa CHADEMA na yenyewe yanazidi kuwa hafifu sana. Hatujui Mbowe alirogwa na Samia kwa uchawi toka wapi, maanake hatujapata kuuona ukitumika ndani ya nchi hii tokea tuwe nchi huru.
Mbowe anajiapiza ataendelea na majadiliano ya Maridhiano, sijui wanaridhiana juu ya jambo gani tena!
Kwa hiyo CCM ipo palepale, haiendi popote.