KERO Ukitaka kukata tiketi SGR unaambiwa treni imejaa, muda wa kuondoka treni inakuwa wazi

KERO Ukitaka kukata tiketi SGR unaambiwa treni imejaa, muda wa kuondoka treni inakuwa wazi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Hii SI kweli hata kidogo
Ila nilichogundua hasta ni upande wa treni ya dodoma
Kuna watu unakuta amekata ticket ila safari inaanzia morogoro au vituo vya kati Sasa ukienda kwenye mfumo kuchagua ticket ya dar-dom inakataa lakin ukiachagua dar-moro ukakuta siti ziko wazi
 
Ukitaka kukata ticketi unaambiwa treni imejaa, muda wa kuondoka treni inakuwa wazi mabehewa hayana watu kumbe kuna hujuma ya watu wa mabasi, wanafanya booking na hawasafiri. Serikari iangalie hili swala kwa upana.

Pia, Soma=> Online booking SGR haifanyi kazi, nifanyaje?
Pale Magufuli kuna baadhi ya mabasi huondoka huku viti kadhaa vikiwa wazi, na wakati huo wahusika huwa wanasema mabasi yamejaa.

Hii ni kwa kuwa abiria waliokatia tiketi viti hivyo huwa wanapandia Kibaha au Chalinze na baada ya hapo viti vyote huwa vimejaa.

Ova
 
Mfumo wao ndio unahujumiwa, na wanalojua hilo.
Mimi juzi nilikuwa nakata tiketi ya kuondoka kesho. Mfumo ulionyesha mabehewa yapo na nikapata mpaka namba ya kiti. Lakini hatua ya mwisho ilikuwa haifanyi kazi kabisa. Wanafanya makusudi hao.
Kuna kipindi walifanya hivyo hivyo tulipofika stesheni walituingiza kwenye tren bila tiketi, na tulipoingia ndani tulikatiwa humo ndani kwa vi device vya mkononi.
huu mfumo wa ticket una changamoto kwanza sio user frendly unakuwa kama unaomba visa ya marekani, bora watumie mfumo wa mabus wa latra
 
Hiyo ni hujuma.Wanausalama wa nchi wawekwe huko kuangalia wazandiki.
Wanausalama wenyewe wanaunga mkono juhudi,hawana lolote,kama ni watu mbona Longido na maeneo ya gesiviliuzwa na Loliondo.l walinyamaza hawana kitu ni shida tupu,na hapo bado hata hazijaanza kuchakaa,watachafua uxhafu kila Kona hatimae shirika liwe kituko kwa wageni.Nchi hii ina shida.
 
Sio sifa nzuri kuingia online kila mara unataka kukata tiketi unaambiwa imejaaa, mm nadhan hiyo siyo sifa bali ilitakiwa kutumika kama fursa, kwa nn kila linapojaa behewa wasiongeze lingine ine pale pale online, lile si kama joka tu linavutana, weka hata behewa 30 kuliko kukimbia kutuandikia No SEAT,
 
Pale TRC Kuna kitengo CSO Cha kutoka TISS kipindi Cha mwendazake walikua wanafanya kazi Kwa weledi na wanaripoti direct kwake. Lkn siku hizi wamekua kazi Yao kusaka michongo ya kusafiri kwenda kulipa fidia na kuachana na usalama wa treni ni changamoto sana yaan. Bado watu wanaingia kiwepesi sana na waeza Kuta hii kitu ni IT ndo anainjinia. Ukiingia kwenye mfumo wao wa tiketi angalia zimebaki ngapi Kisha wewe kata then refresh uone idadi yake Kuna siku zilikua zinaongezeka badala ya kupungua
 
Duh mara kadhaa nimeingia online kukata ticket ina inaonekana train imejaa nikawa nasema sijui ugeni watu watalizoea maana hata asiyekuwa na safari lazima anasafiri imradi apande train ya umeme
 
Ile dhana ya kusema mtu anaweza kufanya kazi Dar es salaam na akawa anaishi Moro or Dodoma kwa sasa umakufa rasmi.
Ukitaka kujua kua hii adha itaendelea Kwa muda mrefu, waulize wamiliki wa mabasi kwa siku walikuwa wanasafirisha abiria wangapi kabla ya ujio wa treni.
 
Kweni Abiria wote wataondokea Central Station?! Si wengine wamebuku wanapandia kwenye Vituo hata Pugu.

Labda ungesema waongeze Mabehewa au hata safari ziongezwe.

Lakini watu wanaotuhumu kuwa ni Makampuni ya Mabasi ndio yanahujumu mimi naona ni UFINYU wa FIKRA.
Pugu hakuna watu wengo wa kuleta effect ya kuonekana kwa macho
 
Ukitaka kukata ticketi unaambiwa treni imejaa, muda wa kuondoka treni inakuwa wazi mabehewa hayana watu kumbe kuna hujuma ya watu wa mabasi, wanafanya booking na hawasafiri. Serikari iangalie hili swala kwa upana.

Pia, Soma=> Online booking SGR haifanyi kazi, nifanyaje?
Hawana uwezo wa kununua ticket zote hizo kwa siku 3 au 4, weww kata ticket yako kwa siku siku 3 au4 kabla, shida nini?
 
Back
Top Bottom