Ukitaka kununua gari usije kuomba ushauri JF, kuna watu wana kauli za kukera, wanakatisha tamaa na hawajawahi kumiliki hata terminal ya betri ya gari.

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
MTU anakuja kutafuta ushauri ili asiumizwe huko Uswahilini anakoenda kutafuta Gari ya kuendana na kipato chake, watu watamjibu kwa kejeli, dharau, matusi na kila aina ya uchafu.

Jamani kabla huja comment hiyo negative comment yako, jitafakarini, je ni lazima niandike kukebehi? Je kama sina ushauri wa maana kwanini nisikae kimya?

 
Mercedes vitara
 
Wapondaji hao nao wana raha yao. Mimi huwa nawaona kama wachangamshaji tu, wachawi uchwara hivi na waliokata tamaa wanaostahili kupuuzwa.

Ambao huwa wananikera ni wale ambao mtu anaweka uzi hapa akisema kuwa maisha yamemchosha na anatamani sana kujiua halafu wanaanza kukomenti "Loser, jiue tu maana huna faida yo yote". Mara "Niachie chaja yako nimekuwahi". "Unajiua kwa sumu au kamba nikuletee?". "Life is not for losers". Hawa ndiyo huwa nawaona kama vile hawana ubinadamu kabisa. Wengine hawa hawana madhara!
 
Tuna watu wa hovyo sana aisee
 
Unabeba yanayokuhusu ya kwao unawaachia wenyewe...
Wengine wana mioyo midogo, wanaumizwa na kila baya. Umejipinda Mideko wa watu ukapata mkoko wako IST unakula kiyoyozi kabisa na mvua ikinyesha upo safi, hunukishwi jasho la daladala, anakuja mtu anakudhihaki..anasema IST sio gari, sasa kama sio gari ni kitu gani?
 
Kawaida ya watu.
Kuna wachambuzi wa Magari siku hizi aisee ni tabu tupu.
Nikaja kugundua ukiwa na mawe gari yeyote unamiliki..

Kama ile hoja ya gari flani kinakula mafuta ...πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
Ni shida tu za Dunia..tusake hela kuna watu aisee wanamiliki madude nawaza hii si bajeti yangu ya kustaafuπŸ˜€πŸ˜€
 
Hii collaboration ya japan na German nimeipenda πŸ˜„ 🀣
 
Mkuu ukitaka kufanya kitu usishauriane na mtu, we fanya tu
Kuna jicho la hasidi
Hiyo ni mbaya kuliko Uchawi believe me
Mtu anakuangalia tu kwa jicho unakata roho

Kuna watu ni zaidi ya sumu yaani wewe ficha yako kama ni uahauri zunguka kwenye yard kadhaa jisomee zaidi
 
Kwa wabongo kote tu kwenye mazingira walipo utapata same reaction kasoro kwa madalali tu ili wakuuzie
 
Mimi nimeanza kununua side mirror na indicator za passo. Mdogo mdogo nakusanya vifaa vyake mpaka mwaka 2027 panapo majaliwa na mimi nitamiliki gari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…