Ukitaka Ndoa yako iwe na Furaha; lazima uzingatie hili

Ukitaka Ndoa yako iwe na Furaha; lazima uzingatie hili

Maisha ni kama movie na MUNGU ndie director. Sisi wanadamu huwa tunaamini tunajiamulia maisha yetu kwenda vile tunataka ila si kweli.

Maisha MUNGU anayaunda mwanzo hadi mwisho, kazi yetu ni kuplay role anazotupa. Ukijipangia roles zako lazima maisha yako yawe full of complications na pain.

Ni kama movie , director anapompa actor movie huwa anataka afuate script aliyo muandikia. Actor akileta ujuaji na kuigiza anavyotaka na kuwa na script yake kinyume na ile ya story ya director then hiyo movie itaharibika.

Maisha especially ya mahusiano yanataka matumizi ya hekima ya asili ingawa watu hutumia busara eneo la hekima. Ushawahi kutana na binti mzuri kwa muonekano anakazana kwenda kanisani kufuata maombi ya ulinzi wa kupata mume mwema kwaajiri yake?!

Dhamira yake ni nzuri ila mbinu zake ndizo zina walakini. Swala hapo hajatumia hekima bali katumia busara kufanya maamuzi. Hekima inakulinda katika nyakati, busara inakusaidia usipokuwa na hekima. Hekima inataka utulivu wa akili na hakuna mwanadamu atakupa hekima ila MUNGU pekee ndio atakupa hekima. Mwanadamu mwenye hekima atakupa busara ukifuata hekima yake, ila busara haidumu vizazi na vizazi sababu ni zao la hekima ya wakati au nyakati fulani.

So kwa kumalizia, mleta mada, jifunze jambo moja, hayo uliyosema ni maneno ya busara sana tena sana. Ila yamekosa uhalali wa hekima ndani yake. MUNGU hafundishwi wala kupangiwa utendaji wake. Akishakuletea mtu wewe ukaleta ufundi matokeo yake ndio yale ya kusema wanaume ni wanyama, au siku hizi hakuna wanawake wa kuoa.

By the way.... First love wako unatakiwa umjue kuanzia miaka 16 hadi 20. Hapo baada ya 20, experience za vurugu za kimahusiano zinakuondoa katika nafasi ya kuielewa asili ya mwanadamu katika mapenzi na mahusiano. Imagine leo kuna mwanamke ukimpenda na kumjali anakuona mjinga na kilaza atatafuta mwanaume wa kumpa stress kisha aje kuomba ushauri.
Pia unaweza mpenda mwanaume kuliko chochote ila akakuona mzigo na kero muda mwingine sababu ya attention unayompa. Haya yote ni matokeo ya kujihusisha na watu wengi kimahusiano katika safari ya maisha.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Aisee haya uliyoaandika ni sahihi kabisa.....
 
Ahsante kwa muongozo, tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Ndio haina formula..wenye pesa wanaachana, maskini wanaachana...wengine maisha gayaendi wanaamua kuishi hivohivo.Ndoa haina equation..hapo umechemka aisee...Ndoa inahitaji uvumilivu na hekima tu...na kikubwa kuomba Mungu akusaidie na akujalie karama..Vingi ulivyoongea hapo havina uhalisia...

Hakuna constant variables for better marriage..
Billgates na mkewe wanahela wale lkn wamebwaga manyanga....Ndoa inahitaji hekima na busara zaidi ya hayo mambo ya nje..ambayo yamesababisha ndoa za vijana wengi wa sasa kufa..
Nidhamu, busara, uvumilivu, kuchukuliana madhaifu, kutunziana siri, kumsaidia na kumuombea mwenzako
Wewe ndio umeingia chaka tena la miba. Neno mfanano lina maana kubwa sana think big.jitathmini kwenye makuzi yako..marafiki..vitu mbalimbali..hata wanandugu pia hujitenga kwa mifanano
 
Nilishawahi kuwa na mweza mwenye tabia za kiswazi mno.kuazima vitu...kwenda vigodoro na tabia zingine za uswahiloni..niliteseka mno sku moja nilijilazmisha kuwa kama yeye na ugomvi uliisha na amani ilitawala.baada ya kimaliza research yangu nakugundua kuwa yy hanikosei makusudi bali ndio hulka yake basi nikamove on.imagn mimi nikipata pesa hata 5000 niliyopewa na ndugu ama hongera ya kuhitisha jambo siwaz kiepe yai nawaza niingize kwenye biashara na ikizaa ndio tutumie sehem ya hiyo faida ila yy mawazo hayo hana..kuna siku nilipewa maziwa lita 30 na mjomba ya kutumia nyumbani ila niliona fursa nikaweka lita tano za nyumbani na lita 25 ndio zilikuwa mwanzo wa biashara inayoniweka mjini ya kuuza maziwa ila yy alitaka tusiyauze tugaie mashoga zake
 
Maisha ni kama movie na MUNGU ndie director. Sisi wanadamu huwa tunaamini tunajiamulia maisha yetu kwenda vile tunataka ila si kweli.

Maisha MUNGU anayaunda mwanzo hadi mwisho, kazi yetu ni kuplay role anazotupa. Ukijipangia roles zako lazima maisha yako yawe full of complications na pain.

Ni kama movie , director anapompa actor movie huwa anataka afuate script aliyo muandikia. Actor akileta ujuaji na kuigiza anavyotaka na kuwa na script yake kinyume na ile ya story ya director then hiyo movie itaharibika.

Maisha especially ya mahusiano yanataka matumizi ya hekima ya asili ingawa watu hutumia busara eneo la hekima. Ushawahi kutana na binti mzuri kwa muonekano anakazana kwenda kanisani kufuata maombi ya ulinzi wa kupata mume mwema kwaajiri yake?!

Dhamira yake ni nzuri ila mbinu zake ndizo zina walakini. Swala hapo hajatumia hekima bali katumia busara kufanya maamuzi. Hekima inakulinda katika nyakati, busara inakusaidia usipokuwa na hekima. Hekima inataka utulivu wa akili na hakuna mwanadamu atakupa hekima ila MUNGU pekee ndio atakupa hekima. Mwanadamu mwenye hekima atakupa busara ukifuata hekima yake, ila busara haidumu vizazi na vizazi sababu ni zao la hekima ya wakati au nyakati fulani.

So kwa kumalizia, mleta mada, jifunze jambo moja, hayo uliyosema ni maneno ya busara sana tena sana. Ila yamekosa uhalali wa hekima ndani yake. MUNGU hafundishwi wala kupangiwa utendaji wake. Akishakuletea mtu wewe ukaleta ufundi matokeo yake ndio yale ya kusema wanaume ni wanyama, au siku hizi hakuna wanawake wa kuoa.

By the way.... First love wako unatakiwa umjue kuanzia miaka 16 hadi 20. Hapo baada ya 20, experience za vurugu za kimahusiano zinakuondoa katika nafasi ya kuielewa asili ya mwanadamu katika mapenzi na mahusiano. Imagine leo kuna mwanamke ukimpenda na kumjali anakuona mjinga na kilaza atatafuta mwanaume wa kumpa stress kisha aje kuomba ushauri.
Pia unaweza mpenda mwanaume kuliko chochote ila akakuona mzigo na kero muda mwingine sababu ya attention unayompa. Haya yote ni matokeo ya kujihusisha na watu wengi kimahusiano katika safari ya maisha.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Nimeipenda hii comment yako mkuu
 
UKITAKA NDOA YAKO IWE YA FURAHA, ZINGATIA KANUNI YA MFANANO

Kwa Mkono wa Robert Heriel

Andiko hili nimeliandika kuisaidia jamii hasa kuponya fikra za wale ambao bado hawajaoa/kuolewa. Bila shaka andiko hili litakusaidia kwa sehemu kubwa ikiwa utalizingatia.

Moja ya makosa makubwa yanayofanywa katika zama hizi iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya, ima kwa kujua ama kwa kutojua ni kuipa nguvu dhana isemayo; "Wanadamu wote ni sawa"

Dhana ya wanadamu wote ni sawa kwa sasa imetawala ndani ya jamii, na athari zake ni dhahiri katika nyanja zote za maisha. Hata hivyo leo nitazungumzia athari hizi katika nyanja za mahusiano haswa katika NDOA na FAMILIA.

Kwanza ifahamike kuwa wanadamu hatupo sawa. Tunatofautiana kwa kiasi kikubwa, hata hivyo utofauti huo unaunda makundi ya watu miongoni mwa wanadamu.

Hata hivyo sipuuzi baadhi ya mambo ambayo wanadamu wapo sawa, mathalani mahitaji ya muhimu yamfanyayo mwanadamu kuishi.

Utofauti wa mwanadamu upo katika maeneo nyeti yafuatayo;

1. Utofauti wa Kifikra, kimtazamo, kihisia, kitabia
2. Utofauti wa Kimaumbile kama Rangi, kimo nk
3. Utofauti wa kinasaba nk

Tofauti hizo ndizo huunda makundi ya watu.

Kizazi cha sasa kinalazimisha kuwa watu wote ni sawa. Sio ajabu mtu masikini kujiona sawa na mtu tajiri. Hata hivyo tajiri hawezi jiona sawa na masikini.

Mtu mjinga kujiona sawa na mtu mwerevu, hata hivyo mwerevu hawezi jiona sawa na mjinga.

Muafrika kujiona sawa na Mzungu, angali Mzungu hawezijiona sawa na Muafrika.

Mwanamke kujiona sawa na mwanaume, hata hivyo mwanaume hajawahi kujiona sawa na mwanamke.

Siku zote unapolazimisha ufanano unatengeneza mazingira ya UNYANYASAJI NA UBAGUZI. Huwezi jilinganisha au kujifananisha na kitu ambacho hufanani wala kulingana nacho alafu ukabaki salama, lazima utanyanyaswa na kubaguliwa.

Unyanyasaji na ubaguzi utaisha pale watu watakapoacha kujiona wapo sawa kumbe hawafanani wala hawalingani.

Nataka kusema nini hapa?

Mtu unapotaka kuoa/kuolewa lazima uzingatie zaidi kundi lako. Lazima ujitathmini na kujitambua kuwa wewe ni nani. Ili uweze kumpata mwenza anayeendana na kufanana na wewe.

Huwezi mpata mwenza bora ikiwa hujajitathmini na kujitambua.

Unakuta msichana kwao ni masikini na fukara lakini anahangaika kutafuta mume tajiri. Huku ni kutafuta kunyanyaswa au kubaguliwa iwe direct au indirect.

Unakuta kijana ni masikini na fukara lakini anatafuta mke mwenye pesa. Hahaha! Ndugu unatafuta machafuko wala sio ndoa.

Unatafuta kijana hana mvuto lakini anahangaika kutafuta wanawake wazuri. Huko ni kutafuta machafuko ndani ya maisha yako. Hata uwe na Pesa aje huwezi oa mwanamke ambaye hamfanani ukabaki salama.

Oa/olewa na kundi lako acha kujipendekeza kwa makundi ya watu wengine, utateseka nakuambia labda uwe mbishi.

Unakuta mwanamke ni hana mvuto lakini anatafuta vijana wazuri/ handsome boy. Huku ni kutafuta lawama tuu. Hata uwe mwanamke mwenye pesa, huwezi olewa na mwanaume ambaye sio kundi lako alafu ukasalimika.

Huna pesa tafuta asiye na pesa mwenzako kama unataka kweli maisha ya furaha. Kisha tafuteni pesa wenyewe.

Lakini unatafuta wenye pesa wakati wewe ni apeche alolo hakika nakuhakikishia lazima utalipia, utahenyeka.

Mtu hata akifilisika atakutupia wewe lawama kuwa wewe ndio umeleta mikosi ndani ya maisha yake.

Huna elimu tafuta asiye na elimu mwezako sio huna elimu alafu unakimbilia kutafuta mwenza mwenye elimu, uliona wapi mambo haya kama sio kutafuta lawama kwa MUNGU wako.

Mtu hamfanani kimtazamo, kihisia, kifikra, kiupeo, unataka awe mwenza wako alafu baadaye unalalamika unanyanyaswa au unabaguliwa bado ujione upo sawa kichwani.

Ukiwa mlevi tafuta Mlevi mwenzako. Sasa wewe unajijua hunywi pombe alafu unatafuta mnywa pombe unatafuta lawama ndugu yangu. Hamfanani, hakuna upendo hapo.

Upendo ni mfanano na mlingano wa kihisia, kimwili, kiroho, na kiakili baina ya watu wawili ambapo wakiungana huwa kitu kimoja.

Hakuna upendo wa vitu vinavyotofautiana.

Wengi hujidanganya kuwa UPENDO unaweza kuunganisha watu wasiofanana jambo ambalo ni uongo na ulaghai wa mchana kweupe.

Mara nyingi wanaosema mimi nampenda hata kama ni Mlevi, masikini, anapesa kunishinda, nk wengi huishia kuteseka maisha yao yote na kuyajutia.

Mwanzoni wanaanzaga vizuri kabisa lakini Nature huamua mwishoni na kuwafanya wawe paka na panya.

Hata hivyo mambo haya huenda mpaka kwa watoto, sio ajabu mtoto akajisikia vibaya kuwa na mzazi kama wewe. Hujawahi kusikia Watoto wakimuuliza Mama yao kuwa hivi ni jambo gani lililokufanya umpende Baba? Hujawahi kusikia hayo.
Tafsiri yake ni kuwa wanaona Kuwa mama hakustahili kuolewa na Baba yao.

AU unashangaa mtoto anamuuliza Baba, hivi ni kipi kilikufanya umuoe Mama? Japo hii ni mara chache kutokea.

Lakini mkiwa mmeoana mnaofanana na kulingana kwa mambo mengi huwezi kuta maswali kama hayo kwani hata watoto wenyewe watakuwa wanafanana na ninyi kwa kiasi kikubwa.

Kuolewa/kuoa mwenza msiyefanana au kulingana ni kuyafanya maisha yako kuwa MATEKA.

Ndio maana vitabu vya dini vinasema katika mwanzo
Mwanzo 2:18
"Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye."

20. Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu ALIYEFANANA naye.

Ndoa ili iwe na Furaha lazima wenzi wafanane kwa kiasi kikubwa. Sio kwa vile tuu ni binadamu basi unadhani kila mwanadamu anaweza kuwa mke/mume wako hiyo sio sahihi kabisa.

Hata ukienda sokoni kununua viatu, sio kila kiatu unaweza kukivaa bali kiatu ambacho ni saizi yako, kinachokutosha.

Unakuta kijana anamaumbile madogo ya uzazi alafu anataka mwanamke mwenye maumbile makubwa ajabu hii. Tafuta mtu unayefanana naye.

Masikini kwa masikini
Tajiri kwa tajiri
Mjinga kwa Mjinga
Mcha Mungu kwa Mcha Mungu
Mlevi kwa mlevi
Asiye na elimu kwa asiye na elimu,
Huu sio ubaguzi bali ndio hali halisi.

Ubaguzi ni vile unaoa/kuolewa na mtu msiyefanana hapo lazima ubaguliwe hata ufanyeje.

Ndoa nyingi zinapumulia mashinde kwa sababu watu wameoana hawafanani wala kulingana.

Niishie hapa, nafikiri nilichotaka kueleza nimekieleza na kimeeleweka.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Skupingi ofisa ,,Na wapi ntampata wa kufanana Na Mimi maana mpaka sasa naona nakimbiwa tu
 
Skupingi ofisa ,,Na wapi ntampata wa kufanana Na Mimi maana mpaka sasa naona nakimbiwa tu

😀😀😀😀

Endelea kumtafuta Mkuu.
Jiangalie zaidi wewe upoje, kadiri unavyojijua ndivyo unavyokaribia kumpata wakufanana naye
 
Back
Top Bottom