Ukitumia internet vizuri kufanya utafiti wako binafsi utagundua Uchawi haupo. Hakuna mganga wala nabii atakayekutapeli. Wajinga ndio waliwao

Ukitumia internet vizuri kufanya utafiti wako binafsi utagundua Uchawi haupo. Hakuna mganga wala nabii atakayekutapeli. Wajinga ndio waliwao

Anayesema kitu kipo ndiye mwenye mzigo wa kuthibitisha kitu kipo.

Kwa sababu kilichopo ndicho kinathibitika kipo.

Kisichopo, nje ya nadharia tupu, hakithibitiki hakipo, kwa sababu hakipo na kama hakipo, hakithibitishiki kwamba hakipo.

Ukitaka mtu anayesema uchawi haupo athibitishe uchawi haupo, ni sawa na kumwambia mtu ambaye hajavamiwa na wezi na kuibiwa athibitishe kwamba hajavamiwa na wezi na kuibiwa.

Atathibitishaje?

Anayeweza kuthibitisha ni yule anayesema jambo limetokea.

Anayesema kavamiwa na wezi na kaibiwa anaweza kuthibitisha kwa alama za vidole za hao wezi, anaweza kutoa video ya kuonesha wezi wakiingia kwake.

Sasa mtu anayesema hakuna wezi walioingia kwake unamtaka athibitishaje kuwa hakuna wezi walioingia kwake?

Unataka atoe alama za vidole za wezi ambao hawapo? Unataka atoe video ya kuonesha wezi ambao hawapo?

Polisi wakisema una madawa ya kulevya nyumbani kwako, wao ndio wana wajibu wa kuyasaka na kuyapata.

Hawakuambii wewe mtuhumiwa ambaye unasema huna madawa ya julevya uthibitishe huna madawa ya kulevya.

Utathibitishaje huna madawa ya kulevya?

You can't prove a negative.

Wewe unayesema uchawi upo ndiye mwenye wajibu wa kuthibitisha uchawi upo.

Anayesema uchawi haupo yeye kazi yake ni kutaka uthibitisho tu kuwa uchawi upo.
Upeo wako ndugu ni mkubwa kiasi kuutumia kwa mtu anayeamini katika ushirikina ni ku misuse resources!
Ukiangalia watu kwa Mwamposa na makanisani wanavyosaka miujiza ndo utajua safari ni ndefu sana!
 
Mkuu soma biblia toka mwanzo hadi ufunuo kwa makin
then ukimaliza urudie kama mara mbili then uje usome huu uzi uloandika

Uchawi umetajwa sana huko na mambo ambayo walifanya.
Mapepo ya utambuzi n.K
hebu anza leo kufikiri nje ya hayo ma vitabu!
utajikomboa katika mengi.
fikiri hivi: biblia haipo na hujawai kuiskia, unajiridhishaje katika hoja husika!
 
Upeo wako ndugu ni mkubwa kiasi kuutumia kwa mtu anayeamini katika ushirikina ni ku misuse resources!
Ukiangalia watu kwa Mwamposa na makanisani wanavyosaka miujiza ndo utajua safari ni ndefu sana!
Safari ni ndefu sana.

Mara nyingine hata kufanya mazungumzo na mtu anayeamini ushirikina irreedemably kusipomsaidia huyo ninsyeongea naye moja kwa moja, kunaweza kusaidia wengine wanaosoma.
 
Nikikwambia Mimi ni Mungu niliyeumba vyote ila wewe huwezi kujua hilo kwa sababu hiyo ni habari mpya na huwezi kuipima kwa uwezo wako wa kizamani, utakubali?
Nitafuatilia kujua ukweli, lakini siwezi kukataa tu kabla ya kufuatilia.
 
Nitafuatilia kujua ukweli, lakini siwezi kukataa tu kabla ya kufuatilia.
Utafuatilia nini sasa wakati hiyo ni habari mpya na imezidi uwezo wa akili yako kuielewa? Utafuatilia nini?
 
Utafuatilia nini sasa wakati hiyo ni habari mpya na imezidi uwezo wa akili yako kuielewa? Utafuatilia nini?
Nitachunguza mpaka nijiridhishe kuhusu suala hilo na sio kukataa tu huenda wewe ni Mungu kweli manake yawezekana wewe ndiye. Tatizo la watu wengi ni kutofanya utafiti juu ya mambo tuliyoyakuta na kujiridhisha wenyewe. Hupaswi kuingia katika imani yoyote ile unapokuwa mtu mzima bila kujiridhisha. Ndio maana kuna watu wanaacha imani zao na wengine wanajiunga na imani zingine. Nawe fanya utafiti wa haya mambo ya kiroho ujue ukweli wake upo wapi. Kama upo curious sana na hodari nenda hata kwa waganga wa kienyeji kajiridhishe kuhusu uwepo wa masuala ya kiroho na dimensions zisizoonekana.
 
Nitachunguza mpaka nijiridhishe kuhusu suala hilo na sio kukataa tu huenda wewe ni Mungu kweli manake yawezekana wewe ndiye. Tatizo la watu wengi ni kutofanya utafiti juu ya mambo tuliyoyakuta na kujiridhisha wenyewe. Hupaswi kuingia katika imani yoyote ile unapokuwa mtu mzima bila kujiridhisha. Ndio maana kuna watu wanaacha imani zao na wengine wanajiunga na imani zingine. Nawe fanya utafiti wa haya mambo ya kiroho ujue ukweli wake upo wapi. Kama upo curious sana na hodari nenda hata kwa waganga wa kienyeji kajiridhishe kuhusu uwepo wa masuala ya kiroho na dimensions zisizoonekana.
Utafanya utafiti kwa kutumia nini kwenye habari ambayo iko nje kabisa ya uwezo wako kuielewa?
 
Nitachunguza mpaka nijiridhishe kuhusu suala hilo na sio kukataa tu huenda wewe ni Mungu kweli manake yawezekana wewe ndiye. Tatizo la watu wengi ni kutofanya utafiti juu ya mambo tuliyoyakuta na kujiridhisha wenyewe. Hupaswi kuingia katika imani yoyote ile unapokuwa mtu mzima bila kujiridhisha. Ndio maana kuna watu wanaacha imani zao na wengine wanajiunga na imani zingine. Nawe fanya utafiti wa haya mambo ya kiroho ujue ukweli wake upo wapi. Kama upo curious sana na hodari nenda hata kwa waganga wa kienyeji kajiridhishe kuhusu uwepo wa masuala ya kiroho na dimensions zisizoonekana.
nijuavyo mimi ukishaingiza neno* kuamini* umeachana na kuthibitisha!
Mambo ya kiroho tunatembelea kuamini baas!
Tunapoachana ni kwenye mambo ya kuamini.
Ndo hapo tunakutana na wanaoamini kijinga na wanaomini kwa hekima!
Ndo kusema washirikina wanaamini kijinga.
Mbaya zaidi kuna ushirikina asilia na ushirikina ndan ya imani za kimapokeo.
mf ushirikina wa kikristo
 
nijuavyo mimi ukishaingiza neno* kuamini* umeachana na kuthibitisha!
Mambo ya kiroho tunatembelea kuamini baas!
Tunapoachana ni kwenye mambo ya kuamini.
Ndo hapo tunakutana na wanaoamini kijinga na wanaomini kwa hekima!
Ndo kusema washirikina wanaamini kijinga.
Mbaya zaidi kuna ushirikina asilia na ushirikina ndan ya imani za kimapokeo.
mf ushirikina wa kikristo
Kuamini unaamini tu, ukianza habari za kutenganisha kuamini kijinga na kwa hekima itabidi uingie kwenye kuthibitisha imani gani ni ya kijinga na imani gani ni ya hekima.

Na ukishaanza kuingia kwenye kuthibitisha ndiyo ushaanza kuondoka kwenye kuamini. Maana hata hiyo imani yako mwenyewe itabidi uiweke kwenye chujio ujitafakari kama ni ya kijinga au ya hekima, hicho kitendo cha kuichuja tayari ni kupunguza imani, huwezi kuichuja na kuihakiki imani yako kama una imani 100%.

Ndiyo maana mimi sitaki habari za kuamini, nataka habari zinazoweza kuthibitishwa.
 
hebu anza leo kufikiri nje ya hayo ma vitabu!
utajikomboa katika mengi.
fikiri hivi: biblia haipo na hujawai kuiskia, unajiridhishaje katika hoja husika!
NIshafikiria kuwa biblia takatifu haipo
 
Habari wadau

Binafsi nashangaa sana watu hasa wasomi wenye smartphone wanaoamini story za ushirikina zama hizi

Ukweli ni kwamba ukijipa muda wako kujifunza zaidi kuhusu cognitive science and psychology, Human psychology na Science of Emotion ilivyo. watajua ukweli mwingi sana wa ubongo wa binadamu unavyofanya kazi na unavyodanganyika

Watu wakijipa muda zaidi na kusoma kuhusu history za uchawi hasa msako wa wachawi (Witch Hunts in the Western World) kwenye karne zilizopita ulikuaje na kwa nini kilisababisha msako huo usitishwe. pia wakasoma kuhusu msako wa wachawi uliotokea marekani pia maarufu kama The Salem Witch Hunt na ilikuaje marekani wakaachana na misako hiyo pia, watajua ukweli kuhusu uchawi.

Kisha wakarudi kwenye youtube na kuangalia video za magic tricks zinavyofanya kazi. watajua waganga na wanaojifanya wachawi wanatumia mbinu gani kuhadaa watu.

Mfano kuna video nyingi za youtube za Sheikh Othman michael akishirikiana na Shehe Jafar kitwana ( mganga mstaafu) wakieleza kila kitu kuhusu uchawi na huku wakionesha na mifano ya jinsi waganga wa kienyeji na wachawi wanavyotapeli watu kwa kutumia Placebo effects na magic tricks. yaani ukizijua hizo hakuna mganga ataeweza kukudanganya hasa ukielewa mbinu zao na mazingaombwe yao.

Nashangaa sana kijana wa zama hizi kuamini ushirikina na kwenda kwa waganga wa kienyeji wakati elimu zinapatikana kwa urahisi sana.

Jamani kwenye internet tusiangalie tu kina mwijaku na diamond. tumieni internet kupata elimu na kuelewa jinsi ya kusolve changamoto zetu.

Uzuri wa internet utapata chochote ulichokusudia kukipata, ukitaka kupata maelezo yenye kuhusu hakuna uchawi utapata na ukitaka maelezo yenye kuhusu uchawi pia utapata.
 
Yaani hakuna watu wanakera kama wanaoamini ushirikina, ni wagumu sana kushaurika
Tatizo ni moja, mara nyingi wasioamini uchawi wanapojadili kuhusu uchawi huwa huwezi kuona uhusiano wao wa kuishi jamii zenye kujishughulisha na uchawi ndio maana wakielezea huwa wanaelezea kinadharia zaidi na kutumia mifano ileile siku zote katika kupinga uchawi, na anayeamini uchawi yeye anaishi mara nyingi unakuta anaishi kwenye jamii zenye kujishughulisha na uchawi.
 
Hakunaga uchawi isipokuwa kuna UJINGA yaani mtu kushindwa kujua changes mbalimbali za kifizikia na kikemia.


Ovaaa

Ukifa ghafla haujalogwa tunakupima pressure na heart attack n. K tunakupatieni jibu ya kilichokuua
Kwani mkuu ulikuwa unataka mtu apimwe chanzo cha kifo na ikutwe uchawi?
 
Hili jambo lina maswali mengi sana yanayohitaji majibu ili kuweza kulithibitisha.

Kwa sababu ukijaribu kuangalia unaona kuna watu wanapata matatizo wanaenda kwa waganga na matatizo yao kweli yanaisha. Ukiangalia kuna watu wanatumia ndagu kupata pesa na kweli wanapata pesa na mali zinaonekana, jambo zinakua na mambo mengi ila still watu tunamuona kua flani kapata pesa na kunakua 'na za chini' za kuaminikakua pesa alizopata ni za kishirikina(manake ushirikina umefanya kazi).

Ila still pia kuna kesi mtu kapata tatizo anakimbilia kwa waganga ila ukiangalia tatizo ni la kawaida wala sio hata la kishirikina, lakini waganga wanamwambia ni la kishirikina na mtu anawaamini, wanaishia kumpiga tu hela na kufanya kweli ionekane kua waganga na ushirikina kwa namna flani kama havina ukweli.

Kwaio ni maswali juu ya maswali
Maswali ni mengi kweli, kuna hili la mchawi kukiri kuwa ni mchawi na madhara aliyoya sababisha kwa uchawi.
 
Siamini uchawi, najua it's all psychological games. Ila mleta mada tungeomba utupe resources zaid, au links za kupata hizo evidence ulizoelezea hapo. Like how does it work step to step!
Ni wazi unaishi mbali na jamii zenye kujishughulisha na matendo ya kichawi na ndio maana uchawi kwako inakuwa kama story tu unazozisikia kwa mbali.
 
Kuna uhusiano gani kati ya jamii maskini na yenye elimu duni na uchawi?

Maana jamii zilizoendelea na zenye elimu haziamini huo uchawi.

Kimantiki unaweza ukasema, ili uamini uchawi upo itakupasa aidha uwe mjinga na upeo mdogo wa kufikiri au uwe maskini. Au vyote viwili kwa Pamoja
Mbona kuna madarasa na vitabu kibao tu vya wazungu vyenye kufundisha uchawi na hao wenzetu wameendelea na ni wasomi.
 
ukisoma human psychology na ukaelewa vizuri. utapata majibu kwa nini baadhi ya watu wakienda kwa waganga wanapona magonjwa yao. waganga wanacheza na biological, psychodynamic, behavioral, cognitive, and humanistic psychology katika kumfanya mtu ajione amepona ugonjwa wake.

kuhusu kupata pesa ama utajiri waganga wanacheza pia na human psychology ya kukupa masharti ambayo yatakufanya uwe mbahili na unatunza sana pesa na kuwekeza.
ndio maana matajiri wanaoenda kwa waganga ama wachawi huwa wanavaa rafu rafu, wanakula vibaya. ile ni financial education waliyopewa kwa masharti ya waganga bila wao kujijua kama ni human psychology wamechezewa.

ukienda kutazama video za mganga mstaafu youtube utaona ameelezea sana kuhusu hizo mbinu za waganga katika kuwafanya wafanyabiashara wawe matajiri
Siku zote nasema uganga ungekuwa hivyo basi hadi leo kusingekuwa na kazi ya uganga tena usingekuwa na soko, hivi mkuu wewe ulishawahi kwenda kwa mganga au umeshawahi kushuhudia rafiki au ndugu yako kwenda kwa mganga ili utupe mfano halisi kwa hayo unayoyasema?
 
NIshafikiria kuwa biblia takatifu haipo
binafsi navitambua na kuviheshimu vitabu vinavyodhaniwa vitakatifu kwa dhana moja tu kwamba ni mkusanyiko wa mafundisho yenye hekma na historia za kweli na kufikirika kwa nyakati hizo.
Ili kuvipa nguvu ya kuheshimika na kufwatwa ilibidi itumike mbinu ya ni ...Neno la Mungu
Kinachothibisha Mungu hajawai kuwa na sifa ya kujihusisha na mambo hayo ya kibinadam moja kwa moja, ni uwepo wa vitabu vilivyokinzana hadi kufutwa!
Kwa upande mwingine ni Neno la Mungu kwa misingi ni ujumbe wenyewe kuwa mwema katika kuleta na kujenga mahusiano mazuri kati ya Mungu na viumbe wake wote!
Nikimaanisha hata mafundisho mema ya mila na desturi zetu ni Neno la Mungu
Tofauti ni tu wengine kufanya coding
Ninachokataa ni habari ya Mungu kushusha amri kwenye bango wala kumkabidhi mtume Quran!
Mungu ni simply WEMA kama ambavyo shetani ni simply UBAYA
 
Back
Top Bottom