Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 7,799
- 14,215
- Thread starter
-
- #81
Asanteni mkuu kwa ushauri murua kabisa.Anza sehemu muhimu kama chumba na choo kuweka sawa, unahamia. sehemu nyingine unamalizia ukiwa humo humo ndani taratibu bila stress.
Hakika mkuu.Washikaji kama hao wamebaki wachache sana, ni rahisi kushinda bahati nasibu kuliko kupata waaminifu kama hao
Ushauri wako ni mzuri na uliloongea ni kweli. Mtu pekee ambae hata akila hela yako hautakuuma sana na mara nyingi huwa hawali ni wazazi tu, ila waliobaki uaminifu ni mdogo mno.Msaidiane na mke wako kuisimamia, project kama hiyo kumpa ndugu ni kutafutiana lawama tuu labda awe milionea na awe na muda, mtu pekee katika ndugu naweza kumuamini ni mama yangu tuu na hata akila inaweza isiniume sana
Dah mkuu maneno yako yamenigusa sana, utafikiri ni mke wang ndio alienambia hivyo.Mtu anaeamini ndugu zaidi ya ubavu wake anaolala nao na kuamka nao, ukiumwa hoi anakuogesha uchi aiseee lazima kikukute kitu. Hivyo we kazana tu na ujenz wako
Kule kwa Kaburu ni Jandoni utapaweza!!? Siyo unaambiwa uwende mkapige Mchomoko alafu unaanza kumbwelambwela!?Mkuu tupe connection huko kaburu, passport zipo tayari. Niandae kiasi gani ili niweze kufika nakusaka tonge huko?
Siku nyingine ujenge ukiwa likizo, utapata kichaa bure, hivi hiyo design ndo uliichagua? Mbona bati hilo kama litapauka? Anyway poleePesa yako tu hata wiki mbili unahamia. Kuna mafundi huwa wanafanya kazi usiku na mchana. Wanaweka kambi hapo
Nadhani sio ndugu na sio ndugo wote ila wengi wao hata marafiki japo nao sio wote lakini wengi tu, Tz shida kubwa maneno matamu kama asali ila wao huwa wanafikiria kwanza nitapigaje hapa nifaidike huwa maslahi yao wanaweka mbele lakini angalizo tu ukiona rafiki au ndugu au yoyote anatumia nguvu nyingi za ushawishi juu yako basi kimbia haraka ogopa mimi nakushauri ukitaka kufanya kwa haraka tumia fundi unayemuamini aweke gharama za umaliziaji na za kazi yake halafu wewe simamia manunuzi mbona siku hizi Mobile pesa zipo unaweza kufanya hata huko uliko kama step by step hili utaepuka kugombana na ndugu au marafiki bora ugombane na mafundi.Ya ulichoongea ni ukweli mtupu mkuu, ila umbali na mishe zetu ndo zinanishinda kuja kusimamia.
Ndugu ndio watu wanaoongoza kwa kurudishana nyuma, hata ukiwa mwema kiasi gani.
Ukisimamia mwenyewe ndo hautajiibia hata wake wanawaibia waume zao, mara nyingi nimeona wake wakiwadalalia waume zao bei za materialsHabari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.
Ndugu wanajamii forum wenzangu, unapokuwa nje ya nchi mara nyingi unakumbana na changamoto nyingi kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki uliyowaacha nyumbani.
Hii ni kutokana na wao kuona, au kuamini kwamba unao uwezo wa kufanya kila kitu kwao. Na kibaya zaidi hata utapojaribu kufanya baadhi ya vile unavyoweza kufanya bado utaendelea kubebeshwa lawama tu, ili mradi wahakikishe kuwa wew hauwezi ukaishi bila lawama zao.
Mwaka 2019 before corona nilikwenda bongo nikanunua kiji eneo maeneo ya salasala. Mpaka hapo tayari nilikuwa na eneo langu lingine ambalo tayari nimeshajenga kule Kigamboni, sehemu fulan inaitwa yebo yebo. Ila mimi binafsi nilipojaribu kupalinganisha Kigamboni na Salasala maeneo niliyonunua mimi, niliona kwamba Salasala ndio panafaa kuwa makazi yang ya kudumu pindi ntaporudi kuishi bongo mpaka pale muumba ataponichukua.
Kwahiyo nilivyorudi kaburu ikabidi nianze jitihada za ujenzi kule Salasala ili nishushe mjengo nitakaoishi mimi na familia yangu afu ile nyumba ya Kigamboni nitaipangisha. Kwa sasa kule yebo yebo Kigamboni anaishi brother wangu ambae na yey ana kiwanja chake huko huko Kigamboni anajenga, kwahiyo wakati namalizia mjengo wangu wa Kigamboni aliniomba akae kwanza kwa muda ili awe karibu na shughuli yake ya ujenzi afu nyumba yake ikishaisha ndo atapohama na kuniachia nyumba yangu nipangishe, nkasema haina noma bro.
Sasa basi ujenzi wa Salasala niliuanza mwaka 2020 nikitarajia kuwa katikati ya mwaka huu wa 2022 niwe nimeshamaliza afu ikiwezekana mwezi wa 12 nikienda bongo likizo iwe ndo kimoja nisirudi tena Kaburu. Cha kushangaza pamoja na jitihada zote nlizofanya lkn wanaosimamia mjengo wangu ndio wananikwamisha. Nyumba inaenda kimdondo sana mpaka inanikatisha tamaa kama ninaweza kuihamia mwishoni mwa mwaka huu.
Kabla ya kuanza ujenzi huu kuna watu walinishauri kwamba ni bora nimtume mama watoto aende kukaa bongo ili awe anasimamia shughuli za ujenzi kuliko kuwaamini ndugu tu pekee, mimi nikakaidi kwa kuona kuwa kamwe siwezi kumuweka mke wangu mbele ya ndugu zangu.
Sasa matokeo yake majuto ni mjukuu. Na mimi kuhamia Kigamboni staki naona kumenikalia kushoto sana aisee. Wana JF wenzangu mnaonaje, hivi mjengo huu unaweza kuisha kwa mwezi mmoja uliobaki kweli?
Maanake kuishi mbali na nyumbani kwa muda mrefu nako kunachosha.
View attachment 2400496View attachment 2400497
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]nacheka kama mazuri.Nimekuja hapa kupata ushauri na kupunguza stress baada ya kutuma zingine afu mabadiliko ya ujenzi au muendelezo ni zero.
Ndg nao wanaloga sana siku hizi! Utatumaa tu hata ukilalamika uko pembeni!![emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]nacheka kama mazuri.
Sasa nguvu ya kuwatumia zingine unaitoa wapi?
Au ndio mambo ya damu nzito.....
Dah ningekuwa na mawazo kama haya ya kwako, wala yasingenipata haya yalionipata.Kwakuwa ulisha nunua kiwanja ungechagua kati ya:
1. Kujenga kwa kutumia mkandarasi ambaye mnasaini mkataba na mnalipana kwa hatua ya ujenzi ulipofika. Hii ni nzuiri haina usumbufu wa kina fundi maiko ila ina gharama zaidi.
2. Ukusanye fedha uweke kwenye akaunti ukirudi upange maeneo jirani na site yako usimamie ujenzi mwenyewe ukiwa umesharudi tayari. Nyumba utakayoishi inauhitaji wa ww kuisimamia na kufanya maaumuzi.
3. Mkeo asimamie kama ulivyosema.
Fedha haina undugu sana sana utagombana na nduguzo kwa kuwapima imani ya kuwapa fedha za ujenzi.
Sijui kwanini tanzania hakuna developers wengi wa nyumba kama nchi nyingine ambapo suala la mtu mmoja mmoja kujenga halipo sana bali ni kununua tu nyumba au apartment iliyokamilika.
Dah sina hamu na mlichonifanyia aisee 😂😂Unakuja kutuanika humu na picha ya nyumba umeweka,ww tumekusaidia mangap?
Yan mambo mengi yamekwenda ndivyo sivyo. Ila sasa nimejifunza kutokana na makosa best angu.Siku nyingine ujenge ukiwa likizo, utapata kichaa bure, hivi hiyo design ndo uliichagua? Mbona bati hilo kama litapauka? Anyway polee
Kweli mkuu ushauri wako mzuri sana. Na kwa vile nimeshajua wapi nilipokosea, basi siwezi tena kurudia kosa.Nadhani sio ndugu na sio ndugo wote ila wengi wao hata marafiki japo nao sio wote lakini wengi tu, Tz shida kubwa maneno matamu kama asali ila wao huwa wanafikiria kwanza nitapigaje hapa nifaidike huwa maslahi yao wanaweka mbele lakini angalizo tu ukiona rafiki au ndugu au yoyote anatumia nguvu nyingi za ushawishi juu yako basi kimbia haraka ogopa mimi nakushauri ukitaka kufanya kwa haraka tumia fundi unayemuamini aweke gharama za umaliziaji na za kazi yake halafu wewe simamia manunuzi mbona siku hizi Mobile pesa zipo unaweza kufanya hata huko uliko kama step by step hili utaepuka kugombana na ndugu au marafiki bora ugombane na mafundi.