Ukiwa unampa sana mama yako pesa, anahisi kuwa wewe unazo sana. Hata kama umejitoa tu ili mama yako asipate shida

Ukiwa unampa sana mama yako pesa, anahisi kuwa wewe unazo sana. Hata kama umejitoa tu ili mama yako asipate shida

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,158
Reaction score
5,626
Ukiwa unampa sana mama yako pesa, anahisi kuwa wewe unazo sana. Hata kama umejitoa tu ili mama yako asipate shida, kuna namna anaamini kuwa huyu mtoto wangu anacho tu!

Hivyo, mara nyingi anachukua matatizo ya ndugu wengine na kukuletea! Ndiyo maana ndugu wengi sana watamfuata kumuomba msaada wakijua atakuomba wewe na wao kufaidi, bila kujali kama mambo yako yanaendelea vizuri au la!

Hivyo, kama unampenda mama yako kweli, kabla ya kumpa pesa, hebu jiulize: je, hiki kitu anakihitaji kweli? Je, kiasi hiki cha pesa na matumizi yake ni sahihi?

Ndugu hawataki kukuomba wewe moja kwa moja wakijua utakataa kwa sababu vitu wanavyoomba ni vya kijinga au si vyalazima.

Mfano, anataka kumalizia nyumba wakati wewe huna hata kiwanja, anamwomba mama yako akijifanya anaumwa ili mama yako akuombe umpe pesa.

Ukweli ni kwamba, hata ukitoa, bado watakuona una roho mbaya. Kuwa na kipimo!
 
Sijutii kumpa mama yangu chochote atakachotaka kikiwa ndani ya uwezo wangu.
Asante yake ni dua kubwa kwangu.

Na najua fika hawezi niomba kitu ikiwa hana uhitaji nacho.
 
Mi niliona isiwe tabu nikamjengea mama yangu nyumba za kupangisha ili aiswe ananisunbua
 
Mama yangu;
Nikiwa nazo anajua
Nikiwa sina anajua
Nikiwa sina ila najitutumua kumsaidia anajua
Mama yangu amenizaa kanilea tangu nikiwa kinda hadi sasa nimejitegemea. Ananijua vizuri. Uwa hahisi. Anajua.
 
Ukiwa unampa sana mama yako pesa, anahisi kuwa wewe unazo sana. Hata kama umejitoa tu ili mama yako asipate shida, kuna namna anaamini kuwa huyu mtoto wangu anacho tu!

Hivyo, mara nyingi anachukua matatizo ya ndugu wengine na kukuletea! Ndiyo maana ndugu wengi sana watamfuata kumuomba msaada wakijua atakuomba wewe na wao kufaidi, bila kujali kama mambo yako yanaendelea vizuri au la!

Hivyo, kama unampenda mama yako kweli, kabla ya kumpa pesa, hebu jiulize: je, hiki kitu anakihitaji kweli? Je, kiasi hiki cha pesa na matumizi yake ni sahihi?

Ndugu hawataki kukuomba wewe moja kwa moja wakijua utakataa kwa sababu vitu wanavyoomba ni vya kijinga au si vyalazima.

Mfano, anataka kumalizia nyumba wakati wewe huna hata kiwanja, anamwomba mama yako akijifanya anaumwa ili mama yako akuombe umpe pesa.

Ukweli ni kwamba, hata ukitoa, bado watakuona una roho mbaya. Kuwa na kipimo!
Huyo mama yako ni mpuuzi na ni wa hovyo sana kwasababu kazaa mtoto tikiti maji kama wewe...hivi wewe ni dini gani? Unakuja kumsema mama yako ambae ndie binadamu anaekupenda na kukutakia heri kuliko yeyote yule kwetu sisi ambao hautujui?
 
Back
Top Bottom