Kama umenisoma vizuri,retail price haitazidi TSh 1,500 kwa nchi nzima.
Hizi tofauti za bei za mkoa kwa mkoa huwa ni ndogo sana. Kwa mfano kama DSM diesel inauzwa Sh 3,200, kwa Mwanza itauzwa Sh 3,360. Tofauti hizi EWURA wangaliweza kuziondoa kwa kutafuta wastani wa bei kwa sehemu zote za nchi kama yanavyofanya makampuni ya bia na ya soda. Bei ya bia DSM na Morogoro ni ile ile.
Pia reli ingalitumika kusafirisha bidhaa hii muhimu badala ya malori ya tankers. Usafirishaji wa kutumia malori kwa bidhaa hii ni wa hatari sana, EWURA inapaswa kuupiga marufuku. Hii kwanza itaimarisha shirika letu la reli kiuchumi. Tatizo malori haya mengine ni ya vigogo serikalini, mama anapaswa kusimama imara. Usafirishaji kwa njia ya reli ni rahisi mara dufu ukilinganisha na wa barabara na SGR itakapokamilika, ni usafiri wa haraka zaidi kuliko wa barabara. SGR ya kutoka DSM hadi Morogoro itakapokamilika hivi punde. Hatutarajii hata kidogo kuona bidhaa hii ikisafirishwa kwa barabara kwenda Morogoro kutoka DSM baada ya hapo.