KERO Ukosefu wa huduma muhimu ya maji na intaneti hosteli za UDSM za wanafunzi wa Masters na PhD ni mateso makubwa

KERO Ukosefu wa huduma muhimu ya maji na intaneti hosteli za UDSM za wanafunzi wa Masters na PhD ni mateso makubwa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Hostel ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam tawi la Ubungo kuna matatizo mengi yanawakumba wanafunzi.

Moja kati ya matatizo hayo ni upatikanaji wa maji. Hostel ya Ubungo licha ya kukaa zaidi wanafunzi wa master na PhD lakini tatizo la upatikanaji wa maji unasumbua sana.

Maji yanayopatikana hapo ni ya Serikali ambapo yanatoka kwa wiki siku 2 au siku 3 jambo ambalo wanaoishi hapo wanaishi kwa shida.

Matanki ya kuhifadhia maji ni madogo mno na yanawafanya wakazi wa hapo kutembea na ndoo wanapokwenda na kurudi vyooni kama wakazi Kinyangara ya juu huko Tabora.

Vyoo ni vichafu sana na vinanuka sana kwa sababu hakuna maji. Jambo la kufanya ni kuchimbwa kisima ili maji masaa 24 katika mabomba ya vyooni yanapatikana na sio kama hivi sasa ukienda chooni ubebee ndoo.

Jambo la pili ni internet. Jengo halina internet kabisa na wanafunzi wanaoishi hapa wanafanya tafiti na wengine na wanataka kujisomea.

Jengo limekosa kabisa huduma hiyo ambapo maisha yamekuwa magumu. Makazi haya hayapo Iringa milimani, yapo mjini kabisa karibu kabisa na Ubungo Plaza.

Kwa leo ni hayo tu
Pesa zinaliwa
 
Mwanafunzi wa PhD analalamikia upatikanaji wa internet! Wasomi mnasomaga Nini Kama mpaka level hiyo Bado hamuwrzi hata kubuni mbinu mbadala ya internet
 
Na kweli wewe mshamba haswa. Nchi gani duniani ambako hakuna hostel za wanafunzi wa post-graduate? au ukisikia hostel unakuwa na picha gani kichwani?
Nilikwenda kusoma mahali. Kulikuwa na graduate students village. Nikawa najisemea dah nakwenda kukaa bwenini. Kuingia ni two bedrooms halafu viko full furnished utafikiri hotelini. Kila kitu kipo ndo nikajua hawa watu wapo siriazi na mambo yao aisee.

Hivi kwa nini sisi hata mambo madogo tu hatuwezi? Inakuwaje vigumu kuhakikisha kwamba kuna maji ya kutosha katika hosteli za graduate students? Hapo ukute fungu lilishatolewa mtu akapita nalo.

Halafu wanafunzi wa PhD wanalalamika vyoo kunuka huku wakisingizia ukosefu wa maji. Ukienda kuangalia si ajabu ukakuta kumejazwa magazeti na makorokocho mengine. Na hawa ni wanafunzi wa PhD!

Sisi kusema kweli bado! 🚶🏿‍♂️🚶🏿‍♂️🚶🏿‍♂️
 
Hostel ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam tawi la Ubungo kuna matatizo mengi yanawakumba wanafunzi.

Moja kati ya matatizo hayo ni upatikanaji wa maji. Hostel ya Ubungo licha ya kukaa zaidi wanafunzi wa master na PhD lakini tatizo la upatikanaji wa maji unasumbua sana.

Maji yanayopatikana hapo ni ya Serikali ambapo yanatoka kwa wiki siku 2 au siku 3 jambo ambalo wanaoishi hapo wanaishi kwa shida.

Matanki ya kuhifadhia maji ni madogo mno na yanawafanya wakazi wa hapo kutembea na ndoo wanapokwenda na kurudi vyooni kama wakazi Kinyangara ya juu huko Tabora.

Vyoo ni vichafu sana na vinanuka sana kwa sababu hakuna maji. Jambo la kufanya ni kuchimbwa kisima ili maji masaa 24 katika mabomba ya vyooni yanapatikana na sio kama hivi sasa ukienda chooni ubebee ndoo.

Jambo la pili ni internet. Jengo halina internet kabisa na wanafunzi wanaoishi hapa wanafanya tafiti na wengine na wanataka kujisomea.

Jengo limekosa kabisa huduma hiyo ambapo maisha yamekuwa magumu. Makazi haya hayapo Iringa milimani, yapo mjini kabisa karibu kabisa na Ubungo Plaza.

Kwa leo ni hayo tu
Shalom ya vyoo kwa UDSM ni kubwa sana…..

Kuna vyoo Vipo pale Nkrumah,SR’s,Theaters etc. kiukweli hali ya vile vyoo ni mbaya sana

Kuna muda unaenda chooni unakuta vinyesi vya watu wazima,wamejisaidia halafu wakashindwa kuflash kwa sababu maji hakuna na vyoo vinatoa harufu kali sana Kama vyoo vya soko

UDSM vyoo ni vya pale maktaba mpya(japo na vyenyewe vinakwenda kuharibika soon kutokana na uangalizi hafifu)na kule Confucius institute pekee
 
Hahaaaaa, siku hizi hata kuchakata data zenu mnazozipika imekuwa rahisi sana. 😀😃😄😁 kila kitu kinafanyika mtandaoni.

Ukishamaliza kupika data za uongo na kuokoteza material mtandaoni na kupewa cheti chako cha Master's njoo kwenye "utendaji ni zero". Master's inatakiwa ireflect utendaji wako ila hadi huruma. Mtu ana Master's ila kujieleza kiswahili hawezi wala kiingereza hawezi. Mtu ana Master's ila kuandika taarifa na reports za hata page 1 hawezi. Tunao maofisini, tunao mitaani inasikitisha sana. Mungu awasaidie.
Hilo la competency ya wahitimu wetu pengine halina uhusiano kabisa na kuwepo kwa intaneti. Linaweza kuwa limesababishwa na mitaala yetu na namna tunavyowaandaa na kuwatunza walimu wetu kwa ngazi zote. Aliyeleta hii mada ana hoja ya msingi sana na ambayo haikwepeki kabisa, uwepo wa huduma za internet za uhakika na ambazo watu wataweza kuzimudu.
Kwa taasisi za elimu ya juu na taasisi zingine zote bila ya kusahau umma kwa ujumla wake, huduma ya intaneti ni ya lazima na ya muhimu sana, vinginevyo tuendelee kupiga ramli chonganishi tu.
 
Hostel ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam tawi la Ubungo kuna matatizo mengi yanawakumba wanafunzi.

Moja kati ya matatizo hayo ni upatikanaji wa maji. Hostel ya Ubungo licha ya kukaa zaidi wanafunzi wa master na PhD lakini tatizo la upatikanaji wa maji unasumbua sana.

Maji yanayopatikana hapo ni ya Serikali ambapo yanatoka kwa wiki siku 2 au siku 3 jambo ambalo wanaoishi hapo wanaishi kwa shida.

Matanki ya kuhifadhia maji ni madogo mno na yanawafanya wakazi wa hapo kutembea na ndoo wanapokwenda na kurudi vyooni kama wakazi Kinyangara ya juu huko Tabora.

Vyoo ni vichafu sana na vinanuka sana kwa sababu hakuna maji. Jambo la kufanya ni kuchimbwa kisima ili maji masaa 24 katika mabomba ya vyooni yanapatikana na sio kama hivi sasa ukienda chooni ubebee ndoo.

Jambo la pili ni internet. Jengo halina internet kabisa na wanafunzi wanaoishi hapa wanafanya tafiti na wengine na wanataka kujisomea.

Jengo limekosa kabisa huduma hiyo ambapo maisha yamekuwa magumu. Makazi haya hayapo Iringa milimani, yapo mjini kabisa karibu kabisa na Ubungo Plaza.

Kwa leo ni hayo tu
PhD na Master m akaa chuo. Hapana kapangeni mjifunze Maisha.
 
Hahaaaaa sasa wanalilia Internet mkuu. Kila kitu kinakuwa copied toka mtandaoni.

Juzi kuna mmoja kaja ofisini kwangu akaomba anihoji kama mzimamizi wa Ofisi anafanya utafiti wake, akaniambia "research title yake" nikamwambia mbona hii Tittle yako kuna mmoja alishakuja hapa na Title hii hii na akanihoji toka chuo fulani na akanihoji maswali kama haya yako na aligraduate mwaka jana? Akajingatangata nikamuonea huruma na kumruhusu anihoji atajua mwenyewe huko.

Wakija maofisini mbwembwe nyingiiii nina Master's na blah blah ila mwambie asimame ajielezee. Utaona aibu.
Mpaka mwenye PhD hawezi kujieleza
 
Sijaelewa vzr mkuu,, unalalamika kwa sababu hakuna huduma tajwa au kwa kuwa hiyo huduma wanaokosa ni wanafunzii wa uzamivu na uzamiri
 
Zinasaidia nini kwenye masomo hizo huduma za internet. Mbona sisi tuliosoma Msc kipindi hiko SUA wakati hakukuwa na internet tulisoma vizuri tu.

Internet zinawadumaza nkuwafanya wawe vilaza hao wanafunzi wa kisasa. Wanashindwa kununua bundle binafsi? Hizo WiFi ndio wanatumia kuangalia video za ngono na kudownload movie tu hakuna lolote.
Hayo labda ndo matumizi yako ukipata internet.
Kwa Dunia ya sasa hata hostel za undergraduate zilifaa ziwe na internet.
Kuitumia kujijenga au kujibomoa ni maamuzi ya mtu binafsi.
 
PhD anakaa hostel!?mbona mnadeka sana PhD
PhD na masters inatakiwa unakaa mahali kwenye ka apartment hata ka laki na nusu mahali ila hostel tena hapa mjini hapana.
Anyway ushauri wako wa kuchimba kisima ni mzuri
sasa unataka akakae baa? Tatizo la watz ndio hivyo, akipata kimaster chake anajiona hawezi kukaa hostel. Nchi zilizoendelea hayo mambo yapo, hujatembea ndio maana unasema .
 
Hahaaaaa, siku hizi hata kuchakata data zenu mnazozipika imekuwa rahisi sana. 😀😃😄😁 kila kitu kinafanyika mtandaoni.

Ukishamaliza kupika data za uongo na kuokoteza material mtandaoni na kupewa cheti chako cha Master's njoo kwenye "utendaji ni zero". Master's inatakiwa ireflect utendaji wako ila hadi huruma. Mtu ana Master's ila kujieleza kiswahili hawezi wala kiingereza hawezi. Mtu ana Master's ila kuandika taarifa na reports za hata page 1 hawezi. Tunao maofisini, tunao mitaani inasikitisha sana. Mungu awasaidie.
Watakuwa wa st J hao, wa MUM wapo vizuri
 
PhD bado unalia shida ya makazi na unataka internet ya bure? kazi ipo hapo jalalani..
 
Back
Top Bottom