Ukraine: Iron Dome ya Israel haiwezi mudu kuzuia makombora ya Urusi, Iron Dome imeundwa kuzuia makombora dhaifu yatengenezwayo gereji kwa tech duni

Sikirimimimasikini

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
2,926
Reaction score
15,634
Waziri wa Ulinzi wa Ukraine amesema kuwa mfumo wa Ulinzi wa anga wa Israel maarufu kwa jina la Iron Dome hauwezi kuhimili kuzuia makombora ya Urusi nchini Ukraine.

Waziri huyo aliyeshuhudia na kutesti nguvu ya makombora ya Urusi anasema kuwa mfumo huo wa Iron Dome umeundwa kwa ajili ya kuzuia makombora yaendayo kwa kasi ndogo, yarukayo kimo cha chini na yasiyo na nguvu kubwa (yenye nguvu hafifu) ambayo kimsingi makombora hayo hutengenezwa gereji. Iron Dome haina uwezo wa kukinga anga dhidi ya makombora ya kruizi na balistiki yanayomiminwa na Urusi yenye kasi kubwa na nguvu (impact) kubwa zaidi, yatengenezwayo kwenye viwanda maalumu kwa teknolojia ya juu zaidi, hata mengine yakawekewa 'decoys' za kuidanganya/kuikwepa mifumo ya ulinzi wa anga imara zaidi ya hiyo Iron Dome.

Ngoja nisubiri Povu toka kwa Waisrael wa Kibaigwa, uzuri wa bahati habari hii imeletwa na The Jerusalem Post.
====

 
Yaani viongozi wa kijeshi na kiraia was Ukraine kila day wao Ni kulialia. Kwa Hali ya kawaida Israel haiwezi kutoa silaha Kama Iron Dome itumike dhidi ya Russia.

Israel katika mgogoro huu Yuko Neutral ili kujihakikishia usalama wa ardhi na watu wake. Iko wazi kwa Israel Kwamba kuwa against Russia katika ulaya dhidi ya Ukraine Ni kujiandaa kua na unrest ya ndege zake katika anga la Syria.

Israel Ni mjanja Sana . Ally namba moja was US lakini asiyejali kabisa maslahi ya US ulaya.
Nb. Nani aliyemdanganya waziri kua Iron Done zinaweza kutolewa Kama sadaka katika occupied Ukraine?
 
Baada ya hii vita nchi nyingi zitajikita kutengeneza siraha tofauti tofauti zenye uwezo zenye Teknolojia ya juu,
Israel kaipa hio protector jina kubwa tofauti na jinsi ilivyo fanya kazi, muda huu ndio wa kajaribu siraha kila mmoja alizotengeneza.
 
Baada ya hii vita nchi nyingi zitajikita kutengeneza siraha tofauti tofauti zenye uwezo zenye Teknolojia ya juu,
Israel kaipa hio protector jina kubwa tofauti na jinsi ilivyo fanya kazi, muda huu ndio wa kajaribu siraha kila mmoja alizotengeneza.
Na wakati huo mrusi akiendelea kuwa piga gap mbaya,kwani anlisha ya jua mabeberu ya ulaya na America kuwa ni zaidi ya mashetani🦞
 
... huyo waziri wa Ukraine ana asili ya kiyahudi; ameongea hivyo na amenukuliwa na gazeti la kiyahudi - The Jerusalem Post kwa sababu maalumu. Kwa akili yako mithili ya punje ya haradali huwezi kuelewa kwanini.
 

Hio S-400 kuiweka hapo No.1 roho inawauma sana sema ndo aibu. Nakumbuka pale syria US alirusha sana kombora na zote zikawa intercepted na zinadunguliwa na S-400 mpaka akasanda mwenyewe.

Hio S-400 tu hatujaweka S-500 na 550
 
Hio S-400 kuiweka hapo No.1 roho inawauma sana sema ndo aibu. Nakumbuka pale syria US alirusha sana kombora na zote zikawa intercepted na zinadunguliwa na S-400 mpaka akasanda mwenyewe.

Hio S-400 tu hatujaweka S-500 na 550
Hivi hii mifumo ya ulinzi wa anga inafanya kazi ya kuintercept makombora ya adui tu au na yenyewe ina uwezo wa kushambulia?
T14 Armata
 
Tuliyokua hatuyajui mwaka huu tutayajua tu mtake msitake.
 
Mrusi kaamua kuichukua Ukraine mdogo mdogo,alianza kujimegea Crimea 2014 sasa hivi kaimega Donbass kifika 2025 atakuwa keshaitwaa kyiv kimchezo mchezo huku akina Biden wakiwa wanaanguka hovyo kama walevi

Ikumbukwe kufika 2024 akina Boris,Macron na wale makiherehere watakuwa wameshakimbizwa Ikulu kama kule Sri-Lanka
 
Hivi hii mifumo ya ulinzi wa anga inafanya kazi ya kuintercept makombora ya adui tu au na yenyewe ina uwezo wa kushambulia?
T14 Armata
Hizo surface to air missiles ni za gharama zaidi kuliko makombora ya kawaida. Zimetengenezwa na booster au engines za kasi kubwa na manouvres, sensors na radar ngumu ndio maana nchi chache zinaweza tengeneza hizi. Kwanza kombora hili halina warhead kubwa, kiujumla haliwezi tumika kushambulia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…