Nimependa sana hii, inafikia hatua mnaweka tofauti zenu za ndani pembeni, hamna cha sijui chama hiki au kile, au Simba/Yanga au serikali au upinzani, inakua muda wa kutetea bendera ya nchi, kutetea ardhi, kutetea watoto wenu, vizazi vijavyo visiandike historia mbovu kuwahusu nyie wa leo.
Kila mmoja chukua silaha, bibi, babu, shangazi, mjomba, vijana wote wa kike au kiume, jaza chupa za petroli, tupigane kwenye vitongoji vyote, milimani, mashambani, kwenye mitaroni, nyumba kwa nyumba, mlango kwa mlango, mahandakini, mapangoni aisei hadi raha......
Ndio kilimkuta Marekani kule Vietnam, wanajeshi wake walikufa hadi akakimbia maana ilifikia hatua ikawa hajui adui ni yupi.