Ukraine yafanikiwa kurudisha Maji na Umeme Kiev

Ukraine yafanikiwa kurudisha Maji na Umeme Kiev

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Baada ya Urusi kupiga miundo mbinu ya maji na umeme huko Kiev. Maengineer na Mafundi wa Ukraine wanefanikiwa kurudisha umeme na Maji katika mji mzima wa Kiev.

Hayo yamesemwa na Mayor wa jiji la Kiev.

Wakati huohuo Ukraine imesema imefanikiwa kudondosha Drone 8 za Urusi ilizopewa na Iran(Shahed-136) jana zilizokuwa zimetumwa zikapige miundo mbinu ya Kiraia

Hii inafuatia baada ya Ukraine kuongeza ulinzi wa anga kutokana na mitambo mbalimbali ya Ulinzi wa Anga iliyopata kutoka kwa washirika wake wa Magharibi. Ujerumani imeipa Ukraine mtambo wake wa Gepard unaodungua ndege na drone na pia Marekani imeipa Ukraine mitambo ya ulinzi wa anga ya NASAM miwili na imesema itapeleka mingine nane.

Kwa upande wa uwanja wa vita, Urusi imeondoa mamlaka yake ya kiutawala kutoka Mji wa Kherson na kuuhamishia kusini karibu na Crimea, na wakati huohuo imekuwa ikiendesha operesheni ya kuondoa raia huko Kherson baada ya pressure ya kijeshi kutoka Ukraine kuwa kubwa.
 
Fashisti kashindwa kupambana front line kahamishia hasira zake kwenye miundombinu..,huko front mambo ni magumu sana kwa urusi..,siku ya jumamosi alipoteza asikari zaidi ya 1000..hii ni idadi kubwa ya asikari kuwahi kuuwawa ndani ya siku Moja tangu uvamizi uanze[emoji848]
 
Fashisti kashindwa kupambana front line kahamishia hasira zake kwenye miundombinu..,huko front mambo ni magumu sana kwa urusi..,siku ya jumamosi alipoteza asikari zaidi ya 1000..hii ni idadi kubwa ya asikari kuwahi kuuwawa ndani ya siku Moja tangu uvamizi uanze[emoji848]
Source ni Aljezeera!?au BBC, CNN au!!?
 
Juzi nimetoka kuongea kuwa Ukraine sio Congo au Burundi hawa ni watu wa dunia ya Kwanza hata iweje Ukraine hawatakufa Kwa baridi au njaa...
Maisha ya kuishi gizani na kukosa maji Safi ya kunywa tutabaki nayo Sisi huku bongo
 
Ukombozi wa Crimea lazima...,Ili siku nyingine ajiulize mara mbili mbili kabla ya kufanya uvamizi dhidi ya nchi nyingine [emoji848]
Ndiyo nawaambia wasishabikie Ukraine kuanguka maana hujui lengo la putin

Maana ameishavamia na kunyanyasa karibia kila jirani yake..

Vipi kwa usalama wa dunia??
 
Source ni Aljezeera!?au BBC, CNN au!!?

Hizo heavy duty transformers wamezipata wapi, pump kubwa za kusukumia maji kukidhi wakazi wote wa jiji la Kiev wamezinunua na kuzifunga lini, umeme na miundo mbinu zote za uzalishaji na usafirishaji umeme wamezirudisha lini??

Au zinarudi adithi zile zile za kusema jeshi la Ukraine limelipua kifaru kimoja cha Urusi na kuuwa wanajeshi 1,000 (elfu moja) wa Urusi kwa mpigo au hili la kudai kwamba missiles 50 zilizo vurumishwa huko Ukraine 48 kati ya hizo zilitunguliwa na air defense systems za Zelensky, jeshi la Ukraine likihojiwa ilikuwaje tena, mbona karibu miji yote ya Ukraine ilishambuliwa na kuchakazwa na missiles ikiwemo Kiev yenyewe hii inamaanisha nini kwamba kila missile iloyokuwa inatunguliwa baadae inakuja kufufuka kimiujiza na kuzalisha missiles nyingine tatu za kwenda kushambulia miji mingine na vituo vingine nyeti nchini Ukraine??

Bottom line ni kwamba: jeshi la Zelensky ni mabingwa sana katika nyanja za usanii wa kusema uongo.
 
9720f514-50b1-46e7-bd2a-c7f3458097fa.jpg
 
Mnachekesha! Marekani na Nato yake hakuna atakayeshinda Vita vinavyoendelea.
 
Zelensky asema kuwa kitu cha kwanza atakachofanya baada ya ushindi ni kwenda Crimea kuona bahari😀

Ilianzia Crimea, Itaishia Crimea

 
Hizo heavy duty transformers wamezipata wapi, pump kubwa za kusukumia maji kukidhi wakazi wote wa jiji la Kiev wamezinunua na kuzifunga lini, umeme na miundo mbinu zote za uzalishaji na usafirishaji umeme wamezirudisha lini??

Au zinarudi adithi zile zile za kusema jeshi la Ukraine limelipua kifaru kimoja cha Urusi na kuuwa wanajeshi 1,000 (elfu moja) wa Urusi kwa mpigo au hili la kudai kwamba missiles 50 zilizo vurumishwa huko Ukraine 48 kati ya hizo zilitunguliwa na air defense systems za Zelensky, jeshi la Ukraine likihojiwa ilikuwaje tena, mbona karibu miji yote ya Ukraine ilishambuliwa na kuchakazwa na missiles ikiwemo Kiev yenyewe hii inamaanisha nini kwamba kila missile iloyokuwa inatunguliwa baadae inakuja kufufuka kimiujiza na kuzalisha missiles nyingine tatu za kwenda kushambulia miji mingine na vituo vingine nyeti nchini Ukraine??

Bottom line ni kwamba: jeshi la Zelensky ni mabingwa sana katika nyanja za usanii wa kusema uongo.
ayo maswali unge muuliza meya wa kiev maana ndie alie toa hizo taarifa ww uko mchamba wima uko una uliza pump za kusukuma maji na generator wame zitoa wap nyie vijamaa vya usoviet mko na shida mahali sio bure
 
ayo maswali unge muuliza meya wa kiev maana ndie alie toa hizo taarifa ww uko mchamba wima uko una uliza pump za kusukuma maji na generator wame zitoa wap nyie vijamaa vya usoviet mko na shida mahali sio bure

Nimeuliza maswali ya msingi kabisa na yenye mshiko, wewe utaona ni swali la ajabu kutokana na background yako kielimu lakini kwa wale wenye hand on experience katika masuala haya wala hawezi kuleta mambo ya kukejeri kejeri members wenzao, ataleta maoni mbadala ili watu wamsikilize - unaposema watu sijui wanatoka mchamba wima kwa sababu wana maoni tofauti na ya kwako - hilo tu speaks volume about your personna!!!
 
Back
Top Bottom