Ukraine yaiomba Ujerumani silaha za kujilinda dhidi ya Urusi

Ukraine yaiomba Ujerumani silaha za kujilinda dhidi ya Urusi

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Ukraine imetuma ombirasmi kwa serikali ya Ujerumani kwa ajili ya msaada wa "silaha za kujihami", kwa mujibu wa ripoti ya gazeti.

Katika barua iliyonukuliwa na Gazeti la Ujerumani la Süddeutsche Zeitung, ubalozi wa Ukraine umeiomba Berlin kutoa jibu la haraka, kutokana na hali tete ya kiusalama na kitisho cha uvamizi wa Urusi.

Moscow imepeleka maelfu ya wanajeshi kwenye mpaka wa Ukraine, na kusababisha hofu kwamba inapanga kumvamia jirani yake huyo mdogo. Jumuiya ya kujihami ya mataifa ya magharibi NATO, pia imeonya juu ya idadi kubwa ya wanajeshi wa Urusi wanaopelekwa nchini Belarus.

Urusi inakanusha kupanga uvamizi. Imedai uhakikisho kadhaa wa kiusalama kutoka mataifa ya magharibi, ikiwemo kwamba Ukraine kamwe haitajiunga na NATO na kwamba muungano huo wa kijeshi uondoe vikosi vyake kutoka eneo la Ulaya Mashariki.

Katika kujibu matakwa ya Urusi, NATO na Marekani zimesema madai yote mawili hayana mashiko na badala yake zimependekeza mazungumzo zaidi kuhusu makombora na kupunguza kwa wanajeshi.

Katika barua iliyonukuliwa na Süddeutsche Zeitung, Ukraine inatoa maombo kadhaa makhsusi ya vifaa vya kujilinda, ikiwemo mifumo ya makombora ya masafa ya kati ya kudungua ndege, bunduki za kudungua ndege zisizotumia rubani, kamera za uchunguzi, mifumo ya ufuatiliaji ya kielektroniki, vifaa vya kuona usiku na risasi.

Kyiv inatafuta "msaada wa mara moja katika upatikanaji wa haraka wa mifumo ya silaha za aina ya kujihami," inasema barua hiyo, kwa mujibu wa Gazeti la Süddeutsche Zeitung.
 
Katika barua iliyonukuliwa na Süddeutsche Zeitung, Ukraine inatoa maombo kadhaa makhsusi ya vifaa vya kujilinda, ikiwemo mifumo ya makombora ya masafa ya kati ya kudungua ndege, bunduki za kudungua ndege zisizotumia rubani, kamera za uchunguzi, mifumo ya ufuatiliaji ya kielektroniki, vifaa vya kuona usiku na risasi.
Noma sana hivi vifaa..... binadamu wanahangaika sana
 
Mjerumani anawabania jamaaa hadi NATO wenzie wameanza kujiuliza jamaa wana ajenda gani maana wameombwa silaha muda sana ila wanajizungusha tu ..................isije baadae ikafanywa suprise matata
 
Kwani maamuzi ya nchi moja kujiunga na kingine si maamuzi ya nchi husika? Inakuaje Ukraine izuiliewe na Urusi kujiunga na NATO?
Ukraine wao watie sahihi tu, hayo Mambo mengine yatafuata baadae .....unyonge ni ujinga
 
Mjerumani anawabania jamaaa hadi NATO wenzie wameanza kujiuliza jamaa wana ajenda gani maana wameombwa silaha muda sana ila wanajizungusha tu ..................isije baadae ikafanywa suprise matata
German anakumbuka maumivu ya vita ya pili ya dunia hataki kujiingiza kichwa kichwa hii vita mwenye maslai nayo ni marekani na UK tu wengine ni Sawa na chamboo apoo nchi zao zitaaribiwa warudi nyuma kimaendeleo Germany anataka kufanya kile alichofanya USA kwenye vita ya kwanza ya dunia na ndyo ichoicho atakachofanya China vita vikiaanza
 
Mjerumani anawabania jamaaa hadi NATO wenzie wameanza kujiuliza jamaa wana ajenda gani maana wameombwa silaha muda sana ila wanajizungusha tu ..................isije baadae ikafanywa suprise matata
Ujerumani ni kama Japan. Hawapendi vita hata kidogo maana wanajua wao ndio walianzisha vita ya pili ya dunia. Tena huyo Ujerumani hata ya kwanza aliilazimisha iwe kubwa yeye
 
Ujerumani kwenye WW1 ndio ilihangaisha Waingereza na Wafaransa kwenye trench warfare, Warusi waliteseka nayo. WW2 Ujerumani ikaua Warusi milioni 20, Wayahudi milioni 6 na wazungu wengine. Kwenye cold war Ujerumani ikatengwa na ikawa kati ya power projection ya Eastern and Western blocks.

Wajerumani ni wapiganaji wazuri wa modern world ila hawataki vita kwa hali yoyote. Hata Nord Stream 2 hawataki kuiacha, hawaoni sababu chuki na migogoro itaisha kwa vita. Hawaoni sababu ya kuachana na uchumi kuingia kwenye vita.

Wana experience kihistoria hivyo hawabahatishi. Wamezuia hata nchi kama Estonia ambazo zina licence production ya silaha zao wasiuze kwa Ukraine.

Hata Israel imesema haitouza silaha kwa Ukraine, hii sio kama ilivyokuwa Syria pale Urusi alikuwa anajitolea. Uturuki ana drones uko ila sijajua kama ataendelea. Uhakika wa silaha ni kutoka Uingereza na Marekani.
 
Mwanaume anaye jilinda kwa silaha ni muoga wa maisha

Muda utaongeya tu ila silaha sio kitu cha kuogopa kabisa kwanza ni useless

Wenzao siku hizi tumekuja na technologie ya radi sio tena silaha tukipiga moja takatifu tunangamiza inch mzima
 
Ujerumani kwenye WW1 ndio ilihangaisha Waingereza na Wafaransa kwenye trench warfare, Warusi waliteseka nayo. WW2 Ujerumani ikaua Warusi milioni 20, Wayahudi milioni 6 na wazungu wengine. Kwenye cold war Ujerumani ikatengwa na ikawa kati ya power projection ya Eastern and Western blocks.

Wajerumani ni wapiganaji wazuri wa modern world ila hawataki vita kwa hali yoyote. Hata Nord Stream 2 hawataki kuiacha, hawaoni sababu chuki na migogoro itaisha kwa vita. Hawaoni sababu ya kuachana na uchumi kuingia kwenye vita.

Wana experience kihistoria hivyo hawabahatishi. Wamezuia hata nchi kama Estonia ambazo zina licence production ya silaha zao wasiuze kwa Ukraine.

Hata Israel imesema haitouza silaha kwa Ukraine, hii sio kama ilivyokuwa Syria pale Urusi alikuwa anajitolea. Uturuki ana drones uko ila sijajua kama ataendelea. Uhakika wa silaha ni kutoka Uingereza na Marekani.
Ndo kwanza jamaa anafanya yake
Screenshot_20220206-190317_Samsung Internet.jpg
 
Back
Top Bottom