Ukulu ya Gamboshi - (Ufalme chini ya Ardhi)

Ukulu ya Gamboshi - (Ufalme chini ya Ardhi)

Venus Star

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
26,519
Reaction score
78,311
Nimawasalimia wana JF wote.
Leo nimeona niweze kuelezea mambo muhimu sana ya nchi niliyoweza kuyapata miaka ya 90s.

Miaka hiyo nilitokea kumpenda mtoto mmoja wa kike jina lake akiitwa Misoji. Kusema kweli mwanamke huyo sitamsahau katika maisha yangu. Yeye ndiye aliyenifundisha mambo mengi sana kuhusu Ulimwengu wa Nuru na ulimwengu wa Giza. Japo kuwa nilikuwa muumini mzuri na nilikuwa nasoma vitabu vya dini na kukariri maandiko. Baada ya kukutana na Misoji niliweza kujifunza mambo mengi sana.

Siku moja baada ya kukutana na Misoji aliniuliza swali, Nikikuonesha vitu vizito vya dunia hii utakuwa na uwezo wa kustahimili? Ili kuonesha uanaume wangu nilisema Mpenzi hakuna kitu chochote utanionesha nikatetemeka.

Basi Misoji kwa jicho la upole na mahaba akatikisa kichwa na kusema basi naomba ukae siku mbili kwa kutafakari kisha baada ya hapo tuje kuonana saa sita usiku kwenye mbuyu uliokuwa unajulikwana kwa jina la Lyabatogwa. Bila kufikria sana nikasema sawa mpenzi wangu.

Siku hizo mbili nilizingojea kwa hamu sana, maana nilikuwa bado sijaonja tunda lake. Nilikuwa fika najua siku hiyo ndiyo siku muhimu sana ya kwenda kupata moto moto. Saa ilipofika nilijisogeza mpaka kwenye mbuyu ule. Eneo hilo lilikuwa limetulia sana na nilikuwa pekee yangu yapata kama dakika thelasini. Baadaye baridi ikaanza kuniyemelea kidogo kidogo, huku mbu wa hapa na pale wakijivinjari kwenye mwili wangu.

Muda kidogo kwa nyuma yangu nilisikia sauti ya Misoji ikiniita jina langu, Hanga! Hanga! Hanga! upo tayari, Niligeuka na kukutana na Misoji akiwa ameambatana na wasichana wengine wawili. Niliitikia ndio nipo tayari.

Basi yule msichana mmoja akauliza je, Misoji unauhakika huyu atafaa kweli? Misoji akasema ndio ninaouhakika kabisa. Basi! sikuelewa walikuwa na maana gani.

Walichora ardhini dura huku pembeni wakaweka vitu vyenye rangi nyeupe. Wakaniambia ingia kwenye hii duara. Huku nacheka cheka, huku moyoni ninajisemea hivi vitoto vya kike vinaleta michezo ya kitoto ngoja niingie kwenye duara nivifurahishe. Sikuchelewa nikaingia katikati ya duara. Baadaye wakaniweka katikati wakiwa wamesimama kwenye kingo za duara. Kila mmoja aliwasha moto na kushirikilia kupitia vijiti walivyokuwa wamevishikiria.
Wakaanza kuongea maneno. Kwakweli lugha ile sikuifahamu walikuwa wanaongea lugha gani.

Waliendelea kuonge maneno hayo kama dakika kumi hivi. Nilianza kusikia sauti za watu wakiongea, sauti za kiume na sauti za kike. Kila mmoja anasema "huyu amekuja huku ataweza?", Wengine wanasema tumpe muda na tumfanyie mafunzo maana ndio leo kafika.

Ghafla kuna mwanga mkali ulitokea mbele yangu mithili ya mlango ukifunguliwa na ndani ya mlango huo kuna taa kali. Baadae Misoji aliniambia twende. Tuliongozana na wasichana hao watatu kuingia kupitia lango hilo.

Nilipigwa bumbuwazi baada ya kuingia na kuona kuwa ni mji uliojengeka sana, nilianza kushaanga magari yanapishana, watu wengi wakinunua na kuuza. Watu wamevalia mavazi yenye thamani kubwa. Nikamuuliza Misoji, hapa ni wapi? Alisema sasa tumeingia dunia iliyochini ya Ardhi, hapa ulipo ni nchi inayoitwa Gamboshi. "Niliposikia neno Gamboshi nilianza kutetemeka nikajua fika sasa hawa wasichana wamenichukua niwe msukule". Nilijikaza kisabuni, huku ndani nateketea taratibu.

Tukakutana na mama mmoja aliyekuwa anatusubiri akasema Misoji njooni huku mwenyekiti wa hapa anataka kijana huyu aandikishwe.

Nimeitwa mara moja na boss. nitaendelea......
 
Waje wakupopoe...

waJF hawapendi neno itaendelea

kuna umbea mwingi wa kufuatilia😅😅
 
Mmh uongo huu, uongo mkubwa usio na mipaka nipo gamboshi hayo mambo hamna, gomboshi ni pazuri Tu huduma za Msingi Zipo, watu wa uku ni wakulima na wafugaji, pia wafanyaniashara wapo hayo mambo unayoyasema hayapo usiogopeshe watu, natunaishi kwa Amani kubwa tu
 
Story yako iko poa.

Sizani kama ulikusudia iwe kwenye jukwaa la entertainment au wameamisha uzi wako kuuleta huku.
 
NIlipelekwa mpaka kwa mwenyekiti. Wakati tunaelekea huko kuna watu nilikuwa nawaona sura zao kama nazifahama, wengine ni viongozi wakubwa kabisa. Lakini ilinibidi nikae kimya maana sikui kitu gani kinafuata.

Mwenyekiti, akafungua kitabu cheusi kikubwa akaanza kuniuliza Jina, umri wangu na maswali kadha wa kadha yanayoniuhusu mimi. Kisha akasema kuna sifa tumezipata kupitia kwa Misoji ngoja tutakujaribu tuone kama kweli sifa hizo ni za kwako.

Baada ya hapo tukaambiwa mnaweza kuendelea sasa maana tumeshamuweka kwenye kumbukumbu zetu.

Ngoja nielezee maeneo tulio kuwa tunapita:-
Jamani maenoe tuliyokuwa tunapita yalikuwa yananukia vizuri sana, barabra zikuwa za lami safi na hakuna takataka hata moja. Magari yalikuwa yakipita kwa mpangilio. Mauwa mazuri yalikuwa ya mepandwa kwenye kingo na katikati ya barabara. Pembezoni mwa barabara kulikuwa na mabomba tofauti tofauti. Mabomba mengine yaikuwa yakitoa maziwa, na mabomba mengine yakitoa vinywaji vingine.
Nilishindwa kijuzuia ikabidi niulize, hayo mambomba kazi yake ni nini? Misoji akaniambia usiongope tutakueleza kila kitu. Hayo mabomba unayoyaona ni mamboya ya kuwahudumia wakazi wa huku. Unajua sisi tunaokaa juu ya ardhi kuna mabomba mengi sana tunashindwa kufanya kutokana na kutaka sifa ambazo hazina hata manufaa. Vilevile ubinafsi umetujaa.

Lakin huku watu wanafanya vitu vyote kwaajili ya jamii. Mimi baada ya miaka 20 nitakuwa raia wa kudumu wa huku Gamboshi. Watu wa huku wanaishi umri wa miaka mingi sana. Unakuta kijana tu ana miaka mia mbili. Huku watu wanaoa na kuolewa. Lakini ili uwe raia wa huku kuna masharti mengi sana unatakiwa kuyafuata.

Kuna mabomba ya maji, mvinyo, maziwa na vinywaji vingine vingi tu vizuri. Ukikubaliwa kuwa mmoja wa raia wanaotazamiwa kuna mafundisho mengi utapitia. Sasa hivi mimi nina mika kumi nakuja huku. Watu wa huku wameniamini sana. Na nipo na marafiki zangu huku. Kuna wakati huwa tunaenda juu ya ardhi kwa pamoja. Huwa wanaiuliza namna mateso tunayoyapata kutokana na joto kali, baridi kari, magonjwa na watu kupigana na kumwaga damu.

Unajua sisi juu ya ardhi huwa tunashindania vitu vingi sana, siasa, pesa na mengine mengi kiasi kwamba tunauana, tunapigana na tunafanya mambo mengi sana ya ajabu.

Lakini huku watu wapo na upendo, wanalima mazao mazuri, wanafuga wanyama wa kila aina. Kuna mazao na wanyama wengine hawapatikani kabisa kule juu ya ardhi. Nipo na mabo mengi sana ya kukuambia kwa kuwa leo ni siku ya kwanza na umeingia huku utajifunza mengi. Na ukiwa mwepesi wa kuelewa utafanya mambo makubwa.

Watu wa huku wanapenda sana waongozwe na watu waliotoka juu ya ardhi.
 
NIlipelekwa mpaka kwa mwenyekiti. Wakati tunaelekea huko kuna watu nilikuwa nawaona sura zao kama nazifahama, wengine ni viongozi wakubwa kabisa. Lakini ilinibidi nikae kimya maana sikui kitu gani kinafuata.

Mwenyekiti, akafungua kitabu cheusi kikubwa akaanza kuniuliza Jina, umri wangu na maswali kadha wa kadha yanayoniuhusu mimi. Kisha akasema kuna sifa tumezipata kupitia kwa Misoji ngoja tutakujaribu tuone kama kweli sifa hizo ni za kwako.

Baada ya hapo tukaambiwa mnaweza kuendelea sasa maana tumeshamuweka kwenye kumbukumbu zetu.

Ngoja nielezee maeneo tulio kuwa tunapita:-
Jamani maenoe tuliyokuwa tunapita yalikuwa yananukia vizuri sana, barabra zikuwa za lami safi na hakuna takataka hata moja. Magari yalikuwa yakipita kwa mpangilio. Mauwa mazuri yalikuwa ya mepandwa kwenye kingo na katikati ya barabara. Pembezoni mwa barabara kulikuwa na mambomba tofauti tofauti. Mambomba mengine yaikuwa yakitoa maziwa, na mambomba mengine yakitoa vinywaji vingine.
Nilishindwa kijuzuia ikabidi niulize, hayo mambomba kazi yake ni nini? Misoji akaniambia usiongope tutakueleza kila kitu. Hayo mambomba unayoyaona ni mamboya ya kuwahudumia wakazi wa huku. Unajua sisi tunaokaa juu ya ardhi kuna mambo mengi sana tunashindwa kufanya kutokana na kutaka sifa ambazo hazina hata manufaa. Vilevile ubinafsi umetujaa.

Lakin huku watu wanafanya vitu vyote kwaajili ya jamii. Mimi baada ya miaka 20 nitakuwa raia wa kudumu wa huku Gamboshi. Watu wa huku wanaishi umri wa miaka mingi sana. Unakuta kijana tu ana miaka mia mbili. Huku watu wanaoa na kuolewa. Lakini ili uwe raia wa huku kuna masharti mengi sana unatakiwa kuyafuata.

Kuna mambomba ya maji, mvinyo, maziwa na vinywaji vingine vingi tu vizuri. Ukikubaliwa kuwa mmoja wa raia wanaotazamiwa kuna mafundisho mengi utapitia. Sasa hivi mimi nina mika kumi nakuja huku. Watu wa huku wameniamini sana. Na nipo na marafiki zangu huku. Kuna wakati huwa tunaenda juu ya ardhi kwa pamoja. Huwa wanaiuliza namna mateso tunayoyapata kutokana na joto kali, baridi kari, magonjwa na watu kupigana na kumwaga damu.

Unajua sisi juu ya ardhi huwa tunashindania vitu vingi sana, siasa, pesa na mengine mengi kiasi kwamba tunauana, tunapigana na tunafanya mambo mengi sana ya ajabu.

Lakini huku watu wapo na upendo, walima mazao mazuri, wanafuga wanyama wa kila aina. Kuna mazao na wanyama wengine hawapatikani kabisa kule juu ya ardhi. Nipo na mabo mengi sana ya kukuambia kwa kuwa leo ni siku ya kwanza na umeingia huku utajifunza mengi. Na ukiwa mwepesi wa kuelewa utafanya mambo makubwa.

Watu wa huku wanapenda sana waongozwe na watu waliotoka juu ya ardhi.
Nimeishia kwenye MAMBOMBA, MAMBOMBA, MAMBOMBA
 
Wakati anaendelea kunielezea, wasiwasi wangu ukaanza kuisha na kurudi katika hali yangu ya kawaida. Basi ilinibidi nilulize swali jingine. Kwanini sasa umeamua kunileta huku? Misoji aliendelea kueleza, Kwanza niliona namna ulivyo na moyo wa kipekee. Na kwamba unanipenda kweli kweli. Nilitaka uweze kuanza kujifunza elimu ya ulimwengu na watu wake. Maana ulikuwa unajifunza vitu vingi sana na vingine huwezi hata kuvifanyia kazi.

Nilikuwa nakuonea huruma sana, maana kuna wakati mwingine ulikuwa unatumia nguvu kubwa wenye vitu ambavyo havihitaji hata kutumia nguvu. Tokea mwanzo nilikuwa natamani sana kukueleza mambo mengi. Lakini wewe ulikuwa mjuaji sana kila kitu ulikuwa utajifanya kukijua. Lakin baada ya kukuliza kuwa utakuwa tayari na ukakubali, nikaona ndio muda sahihi sasa wa kuanza kukufundisha ulimwengu waulivyo.

Kwanza kabisa najua wewe unauwezo wa kufanya mambo mengi tu. Ngoja nikueleze kitu hapa "Hakuna muujiza wowote" Muujiza ni jambo ambalo linatokea nje ya uwezo wako wa kufikiri. Lakini ukipata elimu ya juu sana utaona kuwa hakuna muujiza. Sisi tunaokaa juu ya ardhi wengi tunakuwa na macho lakini hatuoni. Lakini huku chini ya ardhi unajifunza mambo mengi na elimu ya huku ni ya kiwango cha juu sana.

Ninajua utakapo jifunza mambo huku utaenda kuisaidia Tanzania na dunia kwa ujumla.

Tuliendelea kusonga mbele huku nikifikiria mambo mengi sana. Nikawa natamani sana kama angekuwepo rafiki yangu Ayubu aweze kuona haya ninayoyaona maana huyu jamaa ni mbishi sana. Akianza kubisha lazima umletee uthibitisho ndio akubali. La sivyo jamaa, mtakesha.

Kwanza hebu niweze kuelezea kidogo huko Gamboshi kukoje,
Kusema kweli watu wa huko Gamboshi wameendelea sana maana hakuna jua wala mwezi lakini wanalima na kufuga. Tukiweza kufungua geti la kuingia kule na kufanya makubaliana hata walimu wachache waje kutufundisha teknolojia ya kilimo hakika tutapiga hatua sana.

Kuna nchi nyingi sana hapa duniani wameweza kusaini makubaliano na Gamboshi ndio maana wanakuwa na teknolojia kubwa sana. Kwa mfano Nchi ya china viongozi wa nchi hiyo wameweza kukubaliana na Gamboshi ndio maana hawa jamaa wanajifunza mambo mengi sana.

Kule hakuna mvua wanategemea umwagiliaji kutokana na mito mbalimbali na mingine wameitengeneza wao. Kwa sasa mimi nimejuana na viongozi wengi sana wa huko Gamboshi na baada ya miaka kadha wa kadha nitaweza kuwa raia wa huko. Nimeweza kufanya mafunzo mengi sana ya huko Gamboshi na ninajua sheria za huko namna ya kufungua geti la kuingia gamboshi ninajua na mambo mengi tu.
 
Tuliweza kufika kwenye jumba moja zuri sana, tukakaribishwa ndani kisha Misoji na wale wasichana wawili na yule mama wakaingia chumbani. Wakaniambia nisubiri kisha watakuja. Walikaa kule yapata dakika kumi na tano hivi. Kisha wale wasichana wawili na yule mama wakatoka. Misoji alibaki kule ndani. Aliniambia niingie mle ndani.

Nilipoingia ndani nikakutana na watu wanne wamekaa kwenye meza mithili ya watu wakiwa kwenye kikao na mmoja wao akionekana kama kiongozi akiwa amekalia kiti kimoja kikubwa. Huku Misoji akiwa amekaa kwenye kiti kingine pembeni. Nikaoneshwa kiti cha kukaa nami sikuvunga niliketi katika kiti nilichooneshwa.

Basi mmoja aliniuliza maswali ya hapa na pale, nami niliyajibu kwa ufasaha bila kuongopa. Baada yule aliyekuwa amekaa kwenye kiti kikubwa alijitambulishwa kuwa jina lake ni Admtilar kwamba yeye anajihusisha na mafunzo ya awali ya Gamboshi. Akanieleza kuwa tayari Misoji aliwaeleza kuwa wewe utakuwa ni mwaminifu na utaanza mafunzo hivi karibuni. Kwa kweli mimi sikuwa na cha kuongeza zaidi ya kutikisa kichwa kuonesha kwamba nimekubali.

Waliandika jina langu na kisha nikapewa kitambulisho, huku Misoji akiwa anatabasamu. Nikaelezwa kwamba sasa ninatakiwa nikae huko juu ya ardhi muda wa mwezi mmoja huku Misoji akikabidhiwa anielekeze mambo kadha wa kadha ya kuanzia.

Baadae tuliangwa Mimi na Misoji tulianza kurejea kuelekea kwenye lile lango tuliloingilia. Tulisindikizwa kwa usafiri wa gari moja zuri sana.

Hebu ngoja nilielezee hilo gari:-
Kusema kweli gari la namna hilo sijawahi kuliona hata kwenye movie tunazooneshwa na wamarekani. Ndania ya hilo gari kuna hewa safi, gali hilo haligusi chini linaenda kama vile linapaa lakini kwa chini mno. Hilo gari nilajua kama kunasehemu kuna maamuvi, kuna vifaavinagusa na kuonesha rangi nyekundu.

Misoji akaniuliza unataka unyoshwe kwenye maumivu? Nami nikasema ndio. Basi kuna sehemu ya kumbonyeza. Nilianza kuguswa na kunyoshwa kila sehemu kwenye maumivu mwilini. Shingo iliwekwa sawa, miguu, mgongo nk. Nikawa nawaza sana wazee wenye matatizo ya Misilu na Mifupa wangepanda gari hilo hakika magonjwa hayo yangeweza kutoweka.

Lakini tusiwe na wasiwasi maana tayari kwa sasa nipo na mahusiano mazuri na Gamboshi tunaweza kusaidiana nao.
 
Kwa hiyo wachina wanatoka china, wanakuja Gamboshi TZ Kufuata teknolojia? Anyway ni story nzuri, tupo tunaifuatilia.
 
Back
Top Bottom