Ukulu ya Gamboshi - (Ufalme chini ya Ardhi)

Ukulu ya Gamboshi - (Ufalme chini ya Ardhi)

Basi tulipofika getini walitushusha na kutuambia mnaweza kwenda sasa.
Ilikuwa yapata saa kumi za usiku, tuliporejea kutoka chini ya ardhi. Kusema kweli nilipofika juu ya ardhi nilihisi utofauti mkubwa mno, maana nilianza kupigwa na baridi kali, hali ya hewa nzito na changamoto nyingi tu.

Basi Misoji akaniambia unaweza kwenda nyumbani sasa, usimwambie mtu jambo uliloliona kwa sasa maana wanaweza kuanza kuniita mimi mchawi. Ndio maana huwa tunakuja huku usiku watu wasiweze kutuona. Ufahamu wa watu wengi umefingwa ni vigumu sana kukuelewa. Mpaka utakapopata mafunzo kadha wa kadha ndio utaweza kufungua geti hilo hata mchana.

Kisha akaniambia unatakiwa sasa ujiandae, kwaajili ya kuanza mafunzo. Kumbuka ulichoambiwa usisahaau hata kimoja.

Tuliweza kuagana nami nikarejea nyumbani kwetu na yeye akarejea kwao.

Asubuhi tuliamka nikiwa natafakari sana, kwamba kile kilichotokea ni ndoto au ni uhalisia? Maana kwenye ule mbuyu hakuna hata dalili yoyote ya kuwa na mlango. Hali yangu ya kila siku ikaendelea kuwa vilevile. Nikawa nawaza kwanini sasa asingeniacha tu huko? Nilikuwa na mawazo mengi sana. Na mawazo hayo ilibidi nikae nayo ndani ya moyo wangu maana hakuna mtu wa kuweza kumuelezea isipokuwa huyo Misoji tu.

Yapata kama saa kumi hivi kulikuwa na mashindano ya mpira wa miguu hapa kijijini kwetu, timu ya Amaboko na timu ya Amagulu zilikuwa zinashindana. Nilijisogeza pale ili anagalau kupunga upepo na kupunguza mawazo mengi ndani ya kichwa changu.

Nilimuona Misoji kwa mbali akiwa na wasichana wenzake wakiwa na furaha, wakipiga soga za hapa na pale. Wao walikuwa wakiishangilia timu ya Amagulu wakati mimi nilikuwa ni mpenzi wa timu ya Amaboko. Timu ya Amagulu walikuwa na mshambuliaji mmoja hatari aliyejulikana kwa jina la Klementi. Huyu jamaa alikuwa na uwezo wa kupiga mpira kwa kutumia miguu yote.

Klementi alikuwa na miguu yenye matege, ni mrefu kiasi fulani na pia alikuwa na kichwa kikubwa. Watu wengi sana walikuwa wanampenda maana alikuwa anajua kupiga chenga na kufunga. Klementi akiukamata mpira ni vigumu sana kumnyang'anya. Timu ya Amagulu ilikua hatari sana kutokana na huyo jamaa. Ndio maana wanawake wengi walikuwa wakiishabikia timu hiyo.

Amaboko ni timu ya muda mrefu ilikuwa na utamaduni wa kushangili kwa kupiga ngoma kubwa kubwa. Ngoma hizo zilikuwa zikipigwa watu wa vijiji vingine waliweza kuzisikia. Vijana wa maridadi, wanaojua kucheza ngoma, walikuwa wakinengua huku midundo ya ngoma hizo zikipigwa.
Amaboko iliweza kujizolea mashabiki wengi kutokana na aina ya upekee wao wa kushangilia. Mimi mwenyewe nilijikuta ni mshabiki wa Amaboko.

Siku hiyo akili zangu hazikuwepo kabisa kwenye shindano. Hata ile hamu ya kuimba nyimbo zetu za Amaboko kwa pamoja sikuwa nayo. Lengo langu lilikuwa japo kidogo niende kuonana na Misoji tuweze kuongea mawili matatu hivi. Kichwa changu kimejaa mawazo nataka kujua hivi yale yaliyotokea ni ndoto au ni kweli? Kwanini Misoji yupo na furaha hivyo! Yeye hawazi?
 
Walinzi walikuwa wakipita na kutangaza, kabla ya mechi kuanza tunataka mashabiki wa Amaboko muende mashariki mwa uwanja, halafu mashabiki wa Amagulu muende Magharibi mwa uwanja.
Mashabiki wote wa Amaboko tulifuata maelekezo ya walinzi na kuelekea Mashariki. Lakini upande ule jua lilikuwa linatupiga machoni. Hatuwezi kuona vizuri. Mimi wala sikujali maana lengo langu la kuja hapo kwenye mpira ni kuonana na Misoji.

Mpira ulianza kuchezwa, niliona kama dakika haziendi, maana lengo langu lilikuwa; baada ya mpira kuisha niweze kuonana na Misoji aweze kuondoa wasiwasi wangu. Baada ya mpira kuisha nilienda haraka kwenye jukwaa lao na Mungu saidia niliweza kumuona Misoji.

Nilimuita pembeni, nikamwambia Misoji hakika ninataka kuwa na maongezi na wewe. Basi akasema sawa, wakati anaelekea nyumbani tutaenda wote na nitamueleza shida yangu. Kwa sasa anataka kuwaaga marafiki zake na atapita dukani kununua vitu vya kupeleke nyumbani. Moyo wangu ulitulia. Basi nilianza kumfuatilia kwamba kila kona anazopita Misoji. Siku hiyo nilikuwa kama shushushu, sikutaka kabisa aweze kupotea nisimuone akielekea nyumbani. Japo kuwa kulikuwa na wa wengi; jicho langu halikuweza kukauka kumtaza Misoji. Kila hatua aliyokuwa akikanyaga jicho langu lilitua pale. Marafiki zake waliendelea kupiga soga, huku wakienda naye kwenye maduka, nami kwa mbali najongea kama chui akiwa kwenye mawindo.

Sikutaka kabisa siku hiyo rafiki yangu Ayubu anione. Maana huyu jamaa yupo na mdomo mrefu sana.

Baadae Misoji aliagana na wasichana wenzake na akabaki pekee yake. Nilikuwa kama kipanga nilienda kwa kasi ya hatari sana!! pale alipo. Nikamuita aligeuka na kuniangalia usoni. Kisha alitabasamu na kuniambia Hanga haukuwa kwenye ndoto ni uhalisia nakusihi uwe mtulivu. Kuna mengi sana utajifunza. Ndani ya moyo wangu nilihisi kama wembe umechana chwaa!!!

Basi niliongozana naye kuelekea nyumbani kwao huku akinieleza mambo ya kufanya kwaajili ya kujiandaa na mafunzo ya awali. Alinieleza kuwa mafunzo ya awali ni namna ya kufungua geti na kuingia kule.

Baada ya kukaribia kwao niliweza kumuaga na mimi nikarejea nyumbani kwetu
 
sibishi nilitaka tu ufafanuzi maana najua china wana tamaduni zao na mungu wao wanayemtegemea kwny mambo yao ya siri na sidhani kama wanategemea huko gamboshi
Hewa, Air, Aeras, Aire.

Ulicho kisema ni sawa na: Najua binadamu wote tunahitaji hewa ili tuweze kuishi, ila sidhani kama waswahili tunahitaji air ili tuweze kuishi.
 
Nimekuwa na changamoto ya kuendelea. Lakini leo nitaendelea kuwaeleza yale ya Gamboshi
 
Kwamba Kuna nchi ipo chini ya ardhi na kuna watu ambao wanapatikana kule ila walikuwa huku au ni kule na huku au walipotea huku wakaenda kuishi kule!
Wakati umeenda kule je huku Duniani au ardhini ulikuwepo pia au ulienda jumla
 
Mkuu kula tunda kwanza ndio akufundishe ayo mambo ya chini ya ardhi..
 
Back
Top Bottom