Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
.
Ami, mjadala huu ni bahari ya kina kirefu, ila kwa maneno haya "lakini kwa nyinyi hamna jipya na mimi sasa naingia kwa kishindo kuwaumbua ili wana ukumbi wawaone ujinga wenu katika huu mjadala.Kwa kweli sasa nina hasira kwa ujinga wenu", nadhani utaishia kuzama bure, maana waonekana kama mvuvi kinda unaingia kwa kishindo bahari kuu kushindana na wazoefu!, eti uje kuwaumbua? haya tunakusubiria tuone hizo hasira zako, karibu!.
Nafurahi kwamba nawe Pasco umeingia kuwasaidia wenzio.Tunahitaji nguvu mpya ili tendelee kwa sababu wenzako wameshindwa sana kutoa hoja za kutetea nukta zao.Kwa upande mwengine wameonesha udhaifu ambao kama wangeufanya mbele ya mashabiki wao basi wangepigiwa kelele Kaa chini!,au kocha angeambiwa Toa huyoo!.

Angalia mfano:
Fundi Mchundo na Lole mara nyingi wamemshutumu Mohammed kwamba katika utafiti wake amekuwa akikwepa kutaja majina ya wapigania uhuru ambao ni wakristo.Katika kutaka kuthibitisha hilo Fundi Mchundo akaleta ushahidi wa majina ya wakristo kama yalivyotajwa na Mwakikagile.Maskini hakujua kuwa uandishi wa Mwakikagile ni nakili ya Mohammed.
Kuthibitisha hilo ni kulitaja jina la William Mwanjisi badala ya Wilbard Mwanjisi.Hili William baada ya Mohammed kupata malalamiko kwa ndugu wa Wilbard alikuwa tayari amelirekebisha katika toleo lake la Kiswahili.
Hapa kuna vitu viwili kwanza ndugu zako wamepwaya na hoja yao kuwa Wakristo hawajatajwa.Isingekuwa busara kutajwa kwa zaidi ya walichofanya kinyume na wenzao waislamu.Jengine ni kuwa kwa kutokuleta kinyume chake baada ya kuzindushwa hivyo ni kuwa wamekubali kuwa hawana hiyo historia iliyo madhubuti ya kutetea hoja zao.Ndugu wa Wilbard hawakukanusha au hawakutaka zaidi ya alivyotajwa mhusika kinyume na nyinyi na Nyerere wenu munaotaka kuhodhi hata vya wenzenu.Walichotaka ni usahihi wa jina tu.

Pamoja na wewe kuingia kwenye huu mjadala sina hofu na wewe hata kidogo, kwani kwa dharau zako za kuiita paper ya Mohammed Said kwenye hadhara ya Kenyatta University kuwa ni hadithi nzuri tu unayopenda kuisikiliza, na wala si presentation mbele ya wasomi,najua utaangukia huko huko walikoishia wenzako.
Tunakusubiri !.
 
Mohamed Said,

..umebainisha kwamba hakuna uwiano mzuri bungeni kati ya Waislamu na Wakristo.

..lakini ubunge ni suala la hiari na utashi wa mhusika kugombea au la. hata upigaji kura nao ni suala la utashi wa mtu.

..je, Waislamu wanaonewa, au wanahujumiwa, au ni kwamba hawana interest na mwamko wa kugombea nafasi za ubunge?
 
JK: Hapo ndipo patamu. Vipi TANU kilichokuwa chama kilichokuwa kimedhibitiwa barabara na Waislamu katika miaka ya 1950 kikianza mikutano yake kwa kusoma Qur'an na ukombozi wote ukachukua sura hiyo leo chama kina sura nyingine kabisa na itakuwa kiroja kama utasema tuanzeni mkutano kwa kusoma Surat Fat'ha? Palitokea nini hadi ikawa hali imepinduka kiasi hata historia ya TANU inaandikwa waanzilishi wa harakati hizo hawamo ndani ya kitabu? Vipi Nyerere anatoa medali 3979 za watu walifanya makubwa nchi hii Waislam hawapo? Kuna kubwa kuliko kupigania ukombozi wa nchi yako? Inakuwa vipi leo tumamjadili marehemu Abdulwahid Sykes chimbuko la TANU na baadhi ya watu wanamkataa kama kweli aliasisi TANU? Hapa ndipo patamu. Vipi Mohamed Said anaandika makala (Africa Events March/April 1987) ya kuwatukuza mashujaa wa uhuru magazeti yanakusanywa na kuchomwa moto? Huu ni mkono wa nani unofanya haya yote? Nini kinaogopwa na nani anaeogopwa?

Sasa mimi sitaki kutoa jibu. Hebu na nyie wanaukumbi angaisheni bongo zenu lau kama kidogo niwasikie. Nawawekea kipande hiki kuwaamsha fikra zenu:

'Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa, katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa. Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo. Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima. Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu. Dossa Aziz, wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa mtu maarufu, mwenye nafasi, na kujiweza sana. Sasa Dossa baada ya miaka kupita hakuwa akifahamika tena na ule umaarufu na utajiri wake ulikuwa umetoweka. Alikuwa akiishi maisha ya kawaida kijijini Mlandizi, maili chache nje ya Dar es Salaam. Katika sherehe ya faragha Nyerere alimtunukia medali Dossa Aziz, rafiki yake wa zamani.'

Kwa nini Nyerere ampe Dossa medali amnyime, Abdulwahid na Ally Sykes, Mshume Kiyate, Jumbe Tambaza, Mwinjuma Mwinyikambi, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Zuberi Mtemvu, Said Chamwenyewe na wengineo? Kipi alichofanya Dossa ambacho hao wengine hawakufanya? Au alikuwa anatoa ngoma juani? John Malecela alimuuliza Nyerere, "Hivi Mwalimu ulipofika Dar es Salaam wewe hukuwa na wenyeji waliokupokea? Mbona umewasahau?

Wanaukumbi nakuulizeni mgependa kupata jibu alotoa Nyerere?
 
Nafurahi kwamba nawe Pasco umeingia kuwasaidia wenzio.Tunahitaji nguvu mpya ili tendelee kwa sababu wenzako wameshindwa sana kutoa hoja za kutetea nukta zao.Kwa upande mwengine wameonesha udhaifu ambao kama wangeufanya mbele ya mashabiki wao basi wangepigiwa kelele Kaa chini!,au kocha angeambiwa Toa huyoo!.

Angalia mfano:
Fundi Mchundo na Lole mara nyingi wamemshutumu Mohammed kwamba katika utafiti wake amekuwa akikwepa kutaja majina ya wapigania uhuru ambao ni wakristo.Katika kutaka kuthibitisha hilo Fundi Mchundo akaleta ushahidi wa majina ya wakristo kama yalivyotajwa na Mwakikagile.Maskini hakujua kuwa uandishi wa Mwakikagile ni nakili ya Mohammed.
Kuthibitisha hilo ni kulitaja jina la William Mwanjisi badala ya Wilbard Mwanjisi.Hili William baada ya Mohammed kupata malalamiko kwa ndugu wa Wilbard alikuwa tayari amelirekebisha katika toleo lake la Kiswahili.
Hapa kuna vitu viwili kwanza ndugu zako wamepwaya na hoja yao kuwa Wakristo hawajatajwa.Isingekuwa busara kutajwa kwa zaidi ya walichofanya kinyume na wenzao waislamu.Jengine ni kuwa kwa kutokuleta kinyume chake baada ya kuzindushwa hivyo ni kuwa wamekubali kuwa hawana hiyo historia iliyo madhubuti ya kutetea hoja zao.Ndugu wa Wilbard hawakukanusha au hawakutaka zaidi ya alivyotajwa mhusika kinyume na nyinyi na Nyerere wenu munaotaka kuhodhi hata vya wenzenu.Walichotaka ni usahihi wa jina tu.

Pamoja na wewe kuingia kwenye huu mjadala sina hofu na wewe hata kidogo, kwani kwa dharau zako za kuiita paper ya Mohammed Said kwenye hadhara ya Kenyatta University kuwa ni hadithi nzuri tu unayopenda kuisikiliza, na wala si presentation mbele ya wasomi,najua utaangukia huko huko walikoishia wenzako.
Tunakusubiri !.

AMI: Ahsante sana.
 
mimi ndipo mnaponiacha hoi ndugu zangu wenye imani tofauti na uislam hasa wasomi , ndio maana tz maskini hivi kutoakana na mawazo potofu ya baadhi ya wasomi wa kikiristo
Hapo umeshatukana. Hata dakika mbili hazijapita tangu maalim Mohammed Said akusihi tujadiliane kwa uungwana.
 
Vipi Nyerere anatoa medali 3979 za watu walifanya makubwa nchi hii Waislam hawapo? Kuna kubwa kuliko kupigania ukombozi wa nchi yako? Inakuwa vipi leo tumamjadili marehemu Abdulwahid Sykes chimbuko la TANU na baadhi ya watu wanamkataa kama kweli aliasisi TANU? Hapa ndipo patamu. Vipi Mohamed Said anaandika makala (Africa Events March/April 1987) ya kuwatukuza mashujaa wa uhuru magazeti yanakusanywa na kuchomwa moto? Huu ni mkono wa nani unofanya haya yote? Nini kinaogopwa na nani anaeogopwa?

Sasa mimi sitaki kutoa jibu. Hebu na nyie wanaukumbi angaisheni bongo zenu lau kama kidogo niwasikie. Nawawekea kipande hiki kuwaamsha fikra zenu:

'Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa, katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa. Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo. Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima. Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu. Dossa Aziz, wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa mtu maarufu, mwenye nafasi, na kujiweza sana. Sasa Dossa baada ya miaka kupita hakuwa akifahamika tena na ule umaarufu na utajiri wake ulikuwa umetoweka. Alikuwa akiishi maisha ya kawaida kijijini Mlandizi, maili chache nje ya Dar es Salaam. Katika sherehe ya faragha Nyerere alimtunukia medali Dossa Aziz, rafiki yake wa zamani.'

Kwa nini Nyerere ampe Dossa medali amnyime, Abdulwahid na Ally Sykes, Mshume Kiyate, Jumbe Tambaza, Mwinjuma Mwinyikambi, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Zuberi Mtemvu, Said Chamwenyewe na wengineo? Kipi alichofanya Dossa ambacho hao wengine hawakufanya? Au alikuwa anatoa ngoma juani? John Malecela alimuuliza Nyerere, "Hivi Mwalimu ulipofika Dar es Salaam wewe hukuwa na wenyeji waliokupokea? Mbona umewasahau?

Wanaukumbi nakuulizeni mgependa kupata jibu alotoa Nyerere?

Bwana Mohamed Said unatuchanganya na hizi makala zako za kibaguzi. Nimesoma hii thread tangu mwanzo na ninachoona ni ubaguzi mtupu, na mbaguzi mwenyewe ni wewe unayetulazimisha tuamini kuwa waislamu wamebaguliwa katika nchi hii, yaani unachofanya ni uhandisi wa habari, si uandishi. Kama hapo juu umelalamika kuwa waislamu hawakuwemo katika orodha hiyo kubwa ya waliopewa medali za heshima, lakini ndani ya habari hiyohiyo unatutajia jina la sheikh Abdallah Idi Chaurembo aliyepewa medali, sijui huyo alikuwa sheikh wa dini gani?

Tatizo lako ninaloliona ni kuwa unatoa sababu ya uongo kuelezea matukio ya kweli. Inafaa urudi tena kwenye utafiti utafute sababu za matukio hayo unayoelezea. Inawezekana ni kweli kuwa Mwalimu Nyerere aliwatendea isivyopasa watu hao uliowataja, lakini siamini kuwa sababu ya kuwatendea hivyo ni uislamu wao. Wapo wengi wakristo waliotofautiana na Mwalimu Nyerere enzi za utawala wake, nao aliwatenda hivyohivyo, na kwenye historia tukaambiwa walikuwa wasaliti, maadui wa ujamaa nk, mifano akina Christopher Kasanga Tumbo, Joseph Kasela Bantu, James Mapalala, Oscar Kambona, nk orodha ni ndefu.

Narudia. Rudi kachunguze tena katika utafiti, ni kwa nini hao watu wako yaliwafika hayo. Nina uhakika si kwa sababu ya Uislamu kama unavyodai. Ingekuwa kweli uislamu basi Mzee Rashidi Kawawa, Sheikh Kaluta Amri Abeid na baadae kina Salim Ahmed Salim, Ali Hassan Mwinyi wasingefikia kiwango hicho cha heshima ya kuitumikia nchi hii kupitia kwa huohuo mfumo wa Mwalimu Nyerere ambao wewe unalaumu ati ulikandamiza waislamu.

Mimi nafahamu kuwa Mwalimu Nyerere kweli aliwatenda watu fulanifulani katika namna unayoweza kuita ukandamizaji kutokana na kutofautiana nao, lakini nina uhakika alilotofautiana na watu hao halikuwa dini bali misimamo na mitazamo ya kisiasa. Acha kupotosha historia.
 
Kithuku: Karibu ndugu yangu. Hapana silazimishi mtu kuamini nisemayo sina sababu wala uwezo wa kufanya hivyo. Ninachokifanya mimi ni kuiweka sawa historia ya wazee wangu. Si zaidi si pungufu.

Katika Kiswahili ukisema kama nilivyosema hakuna hata Waislam wakati yuko Muislam mmoja ni sawa. Maana ndiyo hiyo kuwa hawapo. Kama uniamini mimi waulize Waswahili wengine wenye lugha yao watakufahamisha vizuri. Katika orodha ile alikuwapo Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo peke yake. Muislam mmoja.

Tatizo lako nalifahamu na ndiyo tatizo la wengi. Hamuijui Dar es Salaam ya 1950s hadi 1960s wala historia ya kudai uhuru. Kama haki ingepitika medali hiyo basi angepewa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir maana yeye kafanya makubwa katika ukombozi kuliko Sheikh Chaurembo ambae alikuwa mwanafunzi wake.

Juu ya hayo yote sikulaumu kwa kutoijua historia hii kwani si yako. Ni wajibu wetu sisi wenye wazee wetu walioshiriki mapambano yale na Muingereza tukuelezeni.

Hivi kama hivyo ndivyo, basi unapouliza swali au kutoa mchango tulia na uliza kwa utaratibu. Utafaidika hata kama hutokubaliana na mimi.

Sasa alopotosha historia nani? Wale Kivukoni College walioandika kitabu kizima cha Historia ya TANU wakaacha kuwataja wahusika wakuu au mie nilieandika kitabu na kueleza yale ninayoyajua na kuwataja takriban wazalendo wote?

Hebu nifafanulie kidogo sijaelewa Salim Ahmed, Rashid Kawawa na Kaluta Amri Abeid wameingiaje katika mjadala huu?

Au ndio yale ya mfa maji anakamata hata unyasi? Mimi nakushangaa wewe vipi hushangai kwa nini Nyerere hakutoa medali kwa waliopigania uhuru wa Tanganyika kwa mali na nafsi zao. Wewe hili halikushangazi? Ajabu.

Ikiwa mimi muongo ukweli ndiyo huo wa Kivukoni College? Huyo mkweli ni nani na yu wapi?
 
Mkuu kitabu ulichoandika kinaitwaje na kinapatikana wapi
 
JK: Hapo ndipo patamu. Vipi TANU kilichokuwa chama kilichokuwa kimedhibitiwa barabara na Waislamu katika miaka ya 1950 kikianza mikutano yake kwa kusoma Qur'an na ukombozi wote ukachukua sura hiyo leo chama kina sura nyingine kabisa na itakuwa kiroja kama utasema tuanzeni mkutano kwa kusoma Surat Fat'ha? Palitokea nini hadi ikawa hali imepinduka kiasi hata historia ya TANU inaandikwa waanzilishi wa harakati hizo hawamo ndani ya kitabu? Vipi Nyerere anatoa medali 3979 za watu walifanya makubwa nchi hii Waislam hawapo? Kuna kubwa kuliko kupigania ukombozi wa nchi yako? Inakuwa vipi leo tumamjadili marehemu Abdulwahid Sykes chimbuko la TANU na baadhi ya watu wanamkataa kama kweli aliasisi TANU? Hapa ndipo patamu. Vipi Mohamed Said anaandika makala (Africa Events March/April 1987) ya kuwatukuza mashujaa wa uhuru magazeti yanakusanywa na kuchomwa moto? Huu ni mkono wa nani unofanya haya yote? Nini kinaogopwa na nani anaeogopwa?

Sasa mimi sitaki kutoa jibu. Hebu na nyie wanaukumbi angaisheni bongo zenu lau kama kidogo niwasikie. Nawawekea kipande hiki kuwaamsha fikra zenu:

'Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa, katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa. Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo. Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima. Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu. Dossa Aziz, wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa mtu maarufu, mwenye nafasi, na kujiweza sana. Sasa Dossa baada ya miaka kupita hakuwa akifahamika tena na ule umaarufu na utajiri wake ulikuwa umetoweka. Alikuwa akiishi maisha ya kawaida kijijini Mlandizi, maili chache nje ya Dar es Salaam. Katika sherehe ya faragha Nyerere alimtunukia medali Dossa Aziz, rafiki yake wa zamani.'

Kwa nini Nyerere ampe Dossa medali amnyime, Abdulwahid na Ally Sykes, Mshume Kiyate, Jumbe Tambaza, Mwinjuma Mwinyikambi, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Zuberi Mtemvu, Said Chamwenyewe na wengineo? Kipi alichofanya Dossa ambacho hao wengine hawakufanya? Au alikuwa anatoa ngoma juani? John Malecela alimuuliza Nyerere, "Hivi Mwalimu ulipofika Dar es Salaam wewe hukuwa na wenyeji waliokupokea? Mbona umewasahau?

Wanaukumbi nakuulizeni mgependa kupata jibu alotoa Nyerere?

Mkuu tatizo la kuzamia kwenye udini ndio unakufanya kukosa mizania ya ukweli.
Sasa tujiulize kibinadamu Nyerere angempaje nishani mtu kama Zuberi Mtemvu ambaye alijitoa TANU kwa HIARI YAKE. Treni ya kisiasa ikamuacha na akatokomea kusiko julikana.
Ni minor observations kama hizo ambazo zinaifanya rejea zako kukosa uzito. Na je utafiti wako woote umeona hao tu waliokosa nishani?
Nimeona unalalamika kuwa kitabu chako kipo UDSM library lakini lecturers wamewakataza wanafunzi kurefer!!!
Huu ndio ushauri sasa nakupa in black and white, unaweza kuandika kitu chochote under the sun, lakini kama maandiko yako yanaleta trafrani katika jamii kwa udini hayatapata umaarufu unaotegemea.Zaidi ya hapo maadiko yako yako subjective na hayana critical analysis ya sweeping statements zako.
Matamshi mengi hayako based na facts ,ukiachia mbali reference za akina Sykes.Hivyo basi maandishi yako ni partisan writings na si mazuri sana kuwa an authority for reference.
Kama unaandika historical fact ni LAZIMA uwe na independet refence inayoweza ku validate yale unayoyaweka.
Na huo ndio asili ya kutofautiana kwetu katika matumizi ya "inasemekana" na maneno mengine kama hayo yaayo fanya maandiko yako kuwa hadithi za kuambiwa.
 
Bwana Mohamed Said unatuchanganya na hizi makala zako za kibaguzi. Nimesoma hii thread tangu mwanzo na ninachoona ni ubaguzi mtupu, na mbaguzi mwenyewe ni wewe unayetulazimisha tuamini kuwa waislamu wamebaguliwa katika nchi hii, yaani unachofanya ni uhandisi wa habari, si uandishi. Kama hapo juu umelalamika kuwa waislamu hawakuwemo katika orodha hiyo kubwa ya waliopewa medali za heshima, lakini ndani ya habari hiyohiyo unatutajia jina la sheikh Abdallah Idi Chaurembo aliyepewa medali, sijui huyo alikuwa sheikh wa dini gani?

Tatizo lako ninaloliona ni kuwa unatoa sababu ya uongo kuelezea matukio ya kweli. Inafaa urudi tena kwenye utafiti utafute sababu za matukio hayo unayoelezea. Inawezekana ni kweli kuwa Mwalimu Nyerere aliwatendea isivyopasa watu hao uliowataja, lakini siamini kuwa sababu ya kuwatendea hivyo ni uislamu wao. Wapo wengi wakristo waliotofautiana na Mwalimu Nyerere enzi za utawala wake, nao aliwatenda hivyohivyo, na kwenye historia tukaambiwa walikuwa wasaliti, maadui wa ujamaa nk, mifano akina Christopher Kasanga Tumbo, Joseph Kasela Bantu, James Mapalala, Oscar Kambona, nk orodha ni ndefu.

Narudia. Rudi kachunguze tena katika utafiti, ni kwa nini hao watu wako yaliwafika hayo. Nina uhakika si kwa sababu ya Uislamu kama unavyodai. Ingekuwa kweli uislamu basi Mzee Rashidi Kawawa, Sheikh Kaluta Amri Abeid na baadae kina Salim Ahmed Salim, Ali Hassan Mwinyi wasingefikia kiwango hicho cha heshima ya kuitumikia nchi hii kupitia kwa huohuo mfumo wa Mwalimu Nyerere ambao wewe unalaumu ati ulikandamiza waislamu.

Mimi nafahamu kuwa Mwalimu Nyerere kweli aliwatenda watu fulanifulani katika namna unayoweza kuita ukandamizaji kutokana na kutofautiana nao, lakini nina uhakika alilotofautiana na watu hao halikuwa dini bali misimamo na mitazamo ya kisiasa. Acha kupotosha historia.

Mkuu Kithuku umenena.
Udini ulivyokaba koo ndugu yetu hajitambui.
Angeishia kuandika habari za mchango wa wazee wake katika kuleta uhuru mimi mmoja wapo ningemuelwa. Ni wazi kuwa kundi lile llilioanzisha TANU si lile lilionedndelea katika serikali ya Tanganyika na hatimae Tanzania na kuendelea.
Katika siasa misuguano ipo na ni lazima iwepo ama sivyo hitakuwa siasa bali aidha msikitini au kanisani.
Lakini humu kwenye hii mada tumesoma mambo ya ajabu,
hadithi za,
Christian lobby
Nyerere aliwakandamiza waislamu(sio mababa zake Mohammed Said bali wasilamu kwa ujumla)
Mabwana na watwana
Uhuru uliletwa na waislamu
Waislamu hawatendewi haki
Mashule wanapendelewa waKristo
N.K.
Vitu hivyo vyote Mohammed Said amevikuza na kujaribu kuonyesha kuwa kuna mapambano kati ya Ukristo na Uislamu, mapambano ya kudhania.
N a linalosikitisha ni kuonyesha kuwa walioleta uhuru hapa Tanganyika ni watu wa pwani tu, kwa vile TANU ilianzia TAA.
Kuna matatizo mengi sana ya kimaendeleo nchini, na kati ya sehemu hizo zingine hata waIslamu hawapo kabisa , kuna matatizo makubwa ya umasikini, hapo sijui wameonewa na Nyerere yupi.
Mbaya zaidi ni maandiko ya kudhania kudhutu kujaribu kuhalalisha kile mtu anachofikiri na kuhisi kuwa ndio mwanzo wa matatizo ya maendeleo yake.
Napata faraja kuona watu wengi zaidi wanaomuelekeza ndugu yetu Mohammed Said kuwa tatizo la umasikini si la waIslamu peke yao, kuna matatizo sehemu nyingi nchini.
 
Kwa nini Nyerere ampe Dossa medali amnyime, Abdulwahid na Ally Sykes, Mshume Kiyate, Jumbe Tambaza, Mwinjuma Mwinyikambi, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Zuberi Mtemvu, Said Chamwenyewe na wengineo? Kipi alichofanya Dossa ambacho hao wengine hawakufanya? Au alikuwa anatoa ngoma juani? John Malecela alimuuliza Nyerere, "Hivi Mwalimu ulipofika Dar es Salaam wewe hukuwa na wenyeji waliokupokea? Mbona umewasahau?

Wanaukumbi nakuulizeni mgependa kupata jibu alotoa Nyerere?
Endelea na hadithi Mohamed Said, endeleza simulizi hizi za fasihi simulizi katika fasihi andishi.
Nadhani post hii itakuwa ni ya 900 au 901!, hivyo mimi ni miongoni mwa waliosoma posti zote, na kwa vile ni mpenzi wa hadithi za kale, niko nawe hata posti 1000!
Asante.
 
Mkuu Kithuku umenena.
Udini ulivyokaba koo ndugu yetu hajitambui.
Angeishia kuandika habari za mchango wa wazee wake katika kuleta uhuru mimi mmoja wapo ningemuelwa. Ni wazi kuwa kundi lile llilioanzisha TANU si lile lilionedndelea katika serikali ya Tanganyika na hatimae Tanzania na kuendelea.
Katika siasa misuguano ipo na ni lazima iwepo ama sivyo hitakuwa siasa bali aidha msikitini au kanisani.
Lakini humu kwenye hii mada tumesoma mambo ya ajabu,
hadithi za,
Christian lobby
Nyerere aliwakandamiza waislamu(sio mababa zake Mohammed Said bali wasilamu kwa ujumla)
Mabwana na watwana
Uhuru uliletwa na waislamu
Waislamu hawatendewi haki
Mashule wanapendelewa waKristo
N.K.
Vitu hivyo vyote Mohammed Said amevikuza na kujaribu kuonyesha kuwa kuna mapambano kati ya Ukristo na Uislamu, mapambano ya kudhania.
Kuna matatizo mengi sana nchi na sehemu zingine ambazo hata waIlamu hawapo kabisa , kuna matatizo makubwa ya umasikini, hapo sijui wameonewa na Nyerere yupi.
Mbaya zaidi ni maandiko ya kudhania kudhutu kujaribu kuhalalisha kile mtu anachofikiri na kuhisi kuwa ndio mwanzo wa matatizo ya maendeleo yake.
Napata faraja kuona watu wengi zaidi wanaomuelekeza ndugu yetu Mohammed Said kuwa tatizo la umasikini si la waIslamu peke yao, kuna matatizo sehemu nyingi nchini.
Lole Gwakisa, mnyonge, mnyongeni, haki yake mpeni, huyu jamaa ni msimulizi mzuri wa hadithi na ana kipaji kikubwa cha kuhifadhi kumbukumbu, which is a plus, na kati ya sifa zake kubwa kwenye mjadala huu ni spinar mzuri, kwa kuspin humshindi, kila akiulizwa swali, sio tuu hukwepa kutoa majibu, bali huja na simulizi mpya zenye kutoa maswali zaidi, hivyo bila majibu, posts zinaendelea tuu,

Mimi ni mpenda hadithi sana, hii thread naiona kama wale wadada wawili, Shahazrade na Dinazrade, mbele ya Khalifa Mkuu, Harun El Rashid,
Hadithi ziendelee...
 
Endelea na hadithi Mohamed Said, endeleza simulizi hizi za fasihi simulizi katika fasihi andishi.
Nadhani post hii itakuwa ni ya 900 au 901!, hivyo mimi ni miongoni mwa waliosoma posti zote, na kwa vile ni mpenzi wa hadithi za kale, niko nawe hata posti 1000!
Asante.

....hahah najiuliza kuhus mazingira wakati huo JSM anamuuliza JKN hilo swali...............nani alikuwepo.........just trying to get a picture...........sasa ni Mkristo anamuuliza Mkristo mwenzie..............nilidhani hawa lao moja hawa!............
 
Ukisiskiliza hizo clip zilizowekwa hapo juu utamsikia MS akisema kuhus shule moja kuwa ilikuwa ofisi za waasisi na sasa ni shule...........na akasema baba yake alisoma pale.............bado natafakari baba yake alisoma pale mwaka gani............
 
Lole Gwakisa, mnyonge, mnyongeni, haki yake mpeni, huyu jamaa ni msimulizi mzuri wa hadithi na ana kipaji kikubwa cha kuhifadhi kumbukumbu, which is a plus, na kati ya sifa zake kubwa kwenye mjadala huu ni spinar mzuri, kwa kuspin humshindi, kila akiulizwa swali, sio tuu hukwepa kutoa majibu, bali huja na simulizi mpya zenye kutoa maswali zaidi, hivyo bila majibu, posts zinaendelea tuu,

Mimi ni mpenda hadithi sana, hii thread naiona kama wale wadada wawili, Shahazrade na Dinazrade, mbele ya Khalifa Mkuu, Harun El Rashid,
Hadithi ziendelee...

Mkuu Pasco mbona hilo la kuwa jamaa i.e. MS kafanya utafiti watu wanali-acknowledge na kazi yake haiwezi kupuuzwa, jambo ambalo linapingwa hapa si kazi yake ya kurekebisha historia bali ni HISIA ZAKE ZA UDINI na kwamba Waislamu wako nyuma kiamendeleo kwa sababu Mkatoliki/Wakristo wame/liwa sideline Waislamu.................

Ukitaka kumuelewa vyema Ndugu MS msome pia HISTORIA YAKE na wazazi wake...............pia sikiliza vizuri hizo clips zake hapo juu...........
 
KUMBUKUMBU ZA MWEMBECHAI



Maprofesa walaani mauaji ya Mwembechai
  • Prof. Shivji asema malalamiko ya wanyonge yasipuuzwe
  • Prof. Chris Peter akemea mfululizo wa mauaji
  • Dk. Lwaitama asikitika Kardinali kuunga mkono mauaji
Hayo yamesemwa katika jopo lililoandaliwa na chama cha wanataaluma wa Sayansi ya Jamii Chuo Kikuu Dar es Salaam - University Political Science Association (DUPSA) kwa kushirikiana na taasisi ijulikanayo kama The Philosophical Club. Jopo hilo lililofanyika Aprili 17, katika ukumbi wa Nkrumah liliwajumuisha wazungumzaji watano ambo ni Dk. A.F. Lwaitama, Prof. Issa Shivji, Prof. Samwel Maghimbi, Prof. Haroub Othman na Dk. H.M. Njozi.

. Lakini lililomshangaza zaidi alisema ni kuona wanaoshutumu Waislamu na kutuma polisi wawapige ni viongozi ambao ni Waislamu. Dk. Lwaitama alionesha kusikitishwa kwake kwa hatua ya Kadinali Pengo kuunga mkono mauaji wakati Maaskofu duniani kote hupigania haki za binadamu.

Muongo njia yake fupi. Hapa hao unaowa/quote wenyewe wanasema walioagiza waislamu wapigwe Mwembechai ni waislamu wenzao! Badala ya kuegemea nyuma ya mgongo wa huyo Dk. Lwaitama, ungetuambia Kadinali Pengo aliunga vipi mauaji yaliyofanyika Mwembechai. Tuambie ni wapi na lini ambapo Kadinali huyo alisema kuwa tendo la kuwaua waislamu lilikuwa sawa.

Hao wote hapo juu ( akiwemo mkristu), hakuna aliyeongelea vurugu za Mwembechai zilianzaje bali wanalaani heavy handed approach ya serikali. Kwenye kitabu chake Njonzi anadai serikali iliitikia wito wa padri Camillius Lwambano wa parokia ya Mburahati( Njozi, uk.15)! Huyu padri ndiye aliyewafanya viongozi wa serikali ambao walikuwa waislamu wawaagize polisi kwenda kuua waislamu wenzao! Na mnapozungumzia kuuawa na kujeruhiwa kwa waislamu, mnasahau kuwa wakristu kibao nao waliumizwa katika vurugu zile! Wauza mitumba na wafanya biashara ndogo ndogo wengi tu waliathirika bila kujali imani yao. Mnasahau atmosphere iliyojaa chuki kati ya uongozi wa zamani na vijana wa kiislamu wa msikiti huo. Mnasahau kuwa vijana hao ambao mnasema walifunzwa heshima katika dini yao hawakusita kuvamia na kuwacharaza bakora watu ambao waliwazidi umri! Mnasahau, conveniently, kuwa baadhi ya vijana hao walikuwa na silaha na waliisha-apa kupigana kidete kutetea uislamu! Nyinyi wenzetu, historia yenu inaanzia pale ambapo polisi walivamia msikiti na mnakataa kabisa kuangalia mchango wenu uliopelekea hali ile kutokea!

Kitendo cha polisi kuwapiga risasi na hata virungu raia wenzao kinatakiwa kilaaniwe na kila mtu. Lakini kudai kuwa polisi hao walifanya hivyo kwa sababu tu waislamu walihusika ni makosa. Polisi hao wamekuwa wakiwapiga bila huruma wanafunzi wake kwa waume wanaodiriki kuandamana kudai haki zao. Baadhi ya hao mapolisi wamesikika wakijivunia na kufurahia kuwa wamepata fursa ya kuwashikisha adabu wasomi! Kutokana na ukweli huu basi mtataka kutuambia kuwa serikali inabagua wasomi? Hata kama hao viongozi wa serikali ni wasomi!

Amandla.......
 
Kama kweli Nyerere alitoa medali za heshima kwa watu hao wote kwa mchango wa nchi hii bila kuwapa Wazalendo Waanzilishi wa TANU kama vile kina Sykes kweli hapo kuna tatizo somewhere. tena tatizo lenyewe si dogo !!!!!!.

Mohammed Saidi endelea kutupa darasa, usikatishwe Tamaa na wale wasiopenda kusikia upande wa pili wa shilingi. watu wanaoishi katika jamii ya kufikirika kwa kudhani kwamba eti hakuna ubaguzi wa kidini Tanzania. Udini upo!!. badala ya kutoa hoja za kitafiti wanaanza kupinga kwa kupin point vijimaneno vidogo na kuacha kontext nzima. unaweza Kupinga utafiti wa kisomi bila ya utafiti mbadala?. kejeli na dharau ndiyo ada ya msomi?. ila ninachofurahia ni kwamba pamoja na provocations zote Mohammed Said ametunza composure yake. maana lengo la wenye kejeli hizi ni kujaribu kumfunga mdomo Mohammed Saidi kwa kumkatisha tamaa, au kumfanya ahamaki ili kupoteza lengo ili aingie katika majibizano yasiyo na tija.
 
PASCO: Ahsante sana kwa mchango wako. Insha Allah nami nitaendelea kukufurahisha kwani kutia furaha katika nyoyo ya nduguyo nalo ni jambo jema.
 
Kama kweli Nyerere alitoa medali za heshima kwa watu hao wote kwa mchango wa nchi hii bila kuwapa Wazalendo Waanzilishi wa TANU kama vile kina Sykes kweli hapo kuna tatizo somewhere. tena tatizo lenyewe si dogo !!!!!!.

Mohammed Saidi endelea kutupa darasa, usikatishwe Tamaa na wale wasiopenda kusikia upande wa pili wa shilingi. watu wanaoishi katika jamii ya kufikirika kwa kudhani kwamba eti hakuna ubaguzi wa kidini Tanzania. Udini upo!!. badala ya kutoa hoja za kitafiti wanaanza kupinga kwa kupin point vijimaneno vidogo na kuacha kontext nzima. unaweza Kupinga utafiti wa kisomi bila ya utafiti mbadala?. kejeli na dharau ndiyo ada ya msomi?. ila ninachofurahia ni kwamba pamoja na provocations zote Mohammed Said ametunza composure yake. maana lengo la wenye kejeli hizi ni kujaribu kumfunga mdomo Mohammed Saidi kwa kumkatisha tamaa, au kumfanya ahamaki ili kupoteza lengo ili aingie katika majibizano yasiyo na tija.

GAMBA LA NYOKA:Ahsante kwa kunitia moyo na hima. Mimi siwezi kukasirika kwa kejeli na dharau kwani hizo naishi nazo kila uchao. Namshukuru mwalimu wangu Maalim Haruna (Mungu amlaze pema) kwa kunifunza adabu. Akisema, "Mtu akikutukana au kukukejeli wewe badala ya kukasirika nenda mbali zaidi ya hapo ujiuilize kwa nini huyu kawa na hulka mbaya? Jibu litakuja ni kuwa huenda hakupata malezi au mimi nimemuudhi. Sasa angalia ikiwa umemuudhi haraka sana mtake radhi." Maalim akawa anasema," Hilo ndilo kubwa. Lau hujamuudhi ila kakutusi kwa kibri chake tu basi wewe mtulize kwa maneno mazuri kwani huyu si kama wewe. Wewe umefunzwa kwenu huyu hakubahatika. Muhurumie." Huu ndiyo muongozo wangu.

Siwezi kumkejeli mtu kwa ajili ya kupishana fikra. Mimi napambana huko nje na watu wenye ilm zao kweli kweli. Mjadala moto kabisa mwisho wa siku ananipigia simu, "Mohamed could we have diner tonight I would like you to meet my family." Hapo urafiki unakujakuwa wa kudumu. Nikiwaaga na zawadi wananipa. Hapa kama zawadi ni hizi kejeli basi hiyo ndiyo majaaliwa yetu tushukuru ala kuli hali. Lakini nia khasa ni na hawa watu wa kejeli wawe waungwana ili wapendeze na kung'ara katika uwanja na ukumbi huu. Hii ndiyo dua yangu kwao.
 
Lole Gwakisa, mnyonge, mnyongeni, haki yake mpeni, huyu jamaa ni msimulizi mzuri wa hadithi na ana kipaji kikubwa cha kuhifadhi kumbukumbu, which is a plus, na kati ya sifa zake kubwa kwenye mjadala huu ni spinar mzuri, kwa kuspin humshindi, kila akiulizwa swali, sio tuu hukwepa kutoa majibu, bali huja na simulizi mpya zenye kutoa maswali zaidi, hivyo bila majibu, posts zinaendelea tuu,

Mimi ni mpenda hadithi sana, hii thread naiona kama wale wadada wawili, Shahazrade na Dinazrade, mbele ya Khalifa Mkuu, Harun El Rashid,
Hadithi ziendelee...

Mkuu mimi sina tatizo na spin, surely the gentleman is a spin doctor for his faith.
Nilikwisha msifia sana mkuu Mohammed Said kwa hadithi zake nzuri.
Tatizo langu ni hiyo observation ya pili, ukimbana jamaa kwa a direct question anaishia na hadithi ndefu yenye mvuto wa kukusahaulisha swali.
Tatizo kubwa na proposition yake ni uwezekano wa mtafaruku mkubwa kutokea huko mbeleni.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom