Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
OLGAH: Baba yangu alisoma Al Jamiatul Islamiyya sina uhakika wa khasa ni mwaka gani lakini nikihesabu kwa kuanza shule na miaka saba na yeye kazaliwa 1924 itakuwa kaanza darasa la kwanza mwaka 1931. Alisoma darasa moja na Abdulwahid Sykes na vijana wengine wa Dar es Salaam ya wakati huo. Kitu alichokuwa akinieleza ni kuwa Abdulwahid alikuwa na akili sana alitangulia kumaliza kusoma mas'haf yote kabla ya wenzake wote na mwalimu akiwa hajaja darasani yeye Abdu anasimama mbele anawafunza wenzake. Alioongoza hivyo hadi alipomaliza darasa la kumi Kitchwele na kupasi wa kwanza mtihani wa kuingia Makerere. Hapo Vita Kuu ya Pili akawa-conscripted katika jeshi KAR na kupelekwa Burma 1942. Abdulwahid Sykes alitoka jeshini na cheo kikubwa ambacho Mwafrika angeliweza kupewa katika jeshi la Waingereza na alitunukiwa medali kadhaa.
 
Bwana Mohamed Said

Kwa kuwa umefanya utafiti bila shaka miaka mingi kuliko mimi, bila shaka umetumia mara nyingi dhana ya 'hypothesis testing' (niwie radhi nimekosa neno la kiswahili). Katika sakata hili la Nyerere, TANU na uislam, baada ya kusoma maandishi yako nimeweza kupata hypotheses mbili ambazo kama ulishazifanyia kazi naomba majibu yake, kama bado basi nakushauri ukazifanyie kazi.

Ya kwanza: Nyerere alikosana na wazee unaowataja kwenye maandishi yako kwa sababu za kisiasa. Una hoja za kuthibitisha kuwa ndivyo au sivyo ilivyotokea?
Ya pili: Nyerere alikosana na wazee uliowataja kwa sababu ya dini yao. Hii ndiyo unayoisimamia, lakini ushahidi unaotoa haukidhi hata kidogo conclusion kama hiyo. Hili lingekuwa la kweli, Nyerere asingekosana na wakristo wenzake ambao pia aliwaweka kizuizini kwa miaka mingi bila kuwapa nafasi ya kujitetea mahakamani, na nimekutajia majina yao hapo kabla. Pia hili lingekuwa kweli, Nyerere asingekuwa na washirika waislam katika serikali yake, na nimekutajia majina ya wale maarufu, miongoni mwao hayati Mzee Rashidi Kawawa ambaye haswa alikuwa ndiye mtekelezaji mkuu wa sera za Mwalimu Nyerere. Na baadaye tumepata marais waislamu waliolelewa na Mwalimu Nyerere. Kwa hiyo hujaweza kuthibitisha kuwa ni tofauti za kidini zilizofanya hao waasisi wa TANU uliowataja watendewe vibaya kama hivyo ulivyotueleza.

Ushauri wangu kwako, hebu nenda katafiti ukitumia sababu nyingine, test hiyo hypothesis nyingine, je kuna ushahidi gani kuwa si tofauti za kisiasa zilizowafanya wazee wako hao waasisi wa TANU yakawafika hayo yaliyowafika?
 
'Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa, katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa. Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo. Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima. Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu. Dossa Aziz, wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa mtu maarufu, mwenye nafasi, na kujiweza sana. Sasa Dossa baada ya miaka kupita hakuwa akifahamika tena na ule umaarufu na utajiri wake ulikuwa umetoweka. Alikuwa akiishi maisha ya kawaida kijijini Mlandizi, maili chache nje ya Dar es Salaam. Katika sherehe ya faragha Nyerere alimtunukia medali Dossa Aziz, rafiki yake wa zamani.'[/SIZE][/FONT]
SIZE][/FONT]
Mkuu Mohamed Said, nadhani ukosoaji wa kimantic kwenye upande wa data. Nafanyia kajiresearch kadogo hii hesebu ya 3,979 waliopatiwa nishani na Nyerere, Mwislamu alikuwa ni mmoja tuu!. No research, no right to speak, and no right to critisize. Kwa vile wewe umefanya research, umekuja na jina la Muislamu mmoja tuu kati yao, nakufanyia kaji counter reseach ili nipate right to speak and to criticise.

Ika kwa kutumia just comon sense, Watunukiwa hao 3,979 walipewa nishani katika makundi matatu
1. Nishani ya Utumishi wa Muda Mrefu
2. Nishani ya Utumishi Uliotukuka
3. Nishani ya Utumishi Uliotukuka na Tabia Njema.

Waliopewa nishani hizi, wengi wao ni watumishi wa umma. Kundi la Kwanza, ni watumishi wote wa umma waliokuwepo serikali siku tunapata uhuru, na bado walikuwepo kwenye utumishi wa umma mpaka hiyo 1985 walipata ile nishani ya kwanza ya Utumishi wa muda mrefu. Sitaki kuamini eti Waislamu wote waliokuwepo serikali, walibaguliwa, wakapewa Wakristu tuu, wala sitaki kuamini, ni Wakristu tuu ndio waliokuwepo serikalini na kuendelea kuwepo mpaka mwaka huo 1985!.

Waliopewa Nishani ya Utumishi uliotukuka ni watumishi wote wa umma, walikuwa serikali tangu 1961 mpaka 1985 ambao walifikia ngazi ya Uofisa. Na wale waliopatiwa Nishani ya Utumishi Uliotukuka na Tabia Njema, ni wale wote ambao walikuwa Maofisa wa Juu, ma loyalist to Nyerere.

Hizi hazikuwa nishani za Mashujaa wa Taifa, Wapigania Uhuru, Wanachama waaminifu wa TANU, au Watanzania wa kawaida, hizi zilikuwa nishani kwa watumishi wa umma, wakiwemo wanajeshi wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama. Siamini kuto huko hakukuwa na waislamu. Nalifanyia kazi hizi, nipo nikurudie Mkuu Mohamed Said, na ikitokea ikawa kweli, Muslamu alikuwa mmoja tuu, kati ya hawa 3,979, nakuhakikishia Mzimu wa Nyerere, utaamka kutoka kaburini pale Mwitongo, na utawaomba msamaha Waislamu kwa such an omission!.
 
MALARIA SUGU: Sheikh Muhammad Ayubu akisema ilm ni amana na aliyokuwanayo sharti aitoe inapobidi kama vile mtu kawekeza kitu chake kwako siku akijakitaka huna budi kumpa. Nami ninayo historia ya wazee wangu ambayo hawa wenzetu hawakuwa wanaijua ni wajibu wangu kuwafahamisha ikiwa watataka. Hili nimejitahidi sana kulifanya usiku na mchana.
 
KITHUKU: Ahsante kwa ushauri wako lakini kabla sijakupa jibu nami nina swali. Ushasoma kitabu changu?
 
SAFRE: Kitabu kinaitwa: The Life aand Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press, London, 1998. Kinapatikana WH Smith Bookshops London na Africa House, London.

Hapa nyumbani utapata cha Kiswahili Ibn Hazim Bookshop, Msikiti wa Mtoro - Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...Phoenix Publishers, Nairobi.
 
WANAUKUMBI: Nimeulizwa swali vipi Nyerere ampe medali Zuberi Mmanga Mwinshehe Mtemvu na yeye alitoka TANU? Niltoa jibu mashine ikakorofisha jibu limepotea. Sasa naeleza mambo yalivyokuwa kabla ya mtafaruku wa 1958 kupelekea wana TANU maarufu kama Ramadhani Mashado Plantan, Saleh Muhsin, Said Chamwenyewe, Zuberi Mtemvu na wengineo kujitoa TANU wengine kuanzisha Congress na wengine AMNUT.

Ramadhani Mashado Plantan kabla ya TANU alikuwa TAA na ndiyo alikuwa "mouthpiece" yao kupitia gazeti lake "Dunia" wakati wa Vita vya Pili na kupitia "Zuhra" baada ya vita. Watu walimsoma Nyerere kwa mara ya kwanza katika "Zuhra" kupitia kalamu ya Mashado Plantan kufuatilia mkutano wa kwanza wa TANU uliofanyika Ukumbi wa Arnatouglo Dar es Salaam Agosti 1954. Mashado aliandika makala na kuwajuvya wananchi nini kilikuwa kinafanyika Tanganyika. Kazi hii aliifanya hadi pale TANU ilipoweza kuwa na gazeti lake "Sauti ya TANU" mwaka wa 1956. Mashado kafanya mengi katika propaganda za TANU. Katika kitabu nimeeleza kwa urefu wake. Kwa hili anastahili medali lau kama alijitoa TANU na kuanzisha AMNUT.

Said Chamwenyewe yeye alikuwa TAA na mwaka 1951 Kamati ya Udhamini ya UNO ilipotembelea Tanganyika yeye ndiye alikuwa msemaji mkuu. Ilipokuja TANU 1954 wakoloni walikataa kutoa tasjila kwa kisingizio kuwa TANU haina wanachama. Abdulwahid Sykes alimpa kazi Said Chamwenyewe ya kutafuta wanachama. Said Chamwenyewe alikwenda Rufiji ambako ndiko kwao na kuleta orodha ndefu ya wanachama. Alikuwa akienda Rufiji kwa baiskeli akipita kila kijiji kuuza kadi za TANU na fedha akikabidhi Makao Makuu, New Street. Ukienda kutazama nyaraka za TANU wanachama wa mwanzo utakuta majina ya kina Mbonde na saini ya Said Chamwenyewe katika kadi hizo. Alifanya mengi katika TANU hadi ulipotokea mtafaruku wa 1958 yeye na Mtemvu wakenda kuunda Congress. Said Chamwenyewe kwa uzalendo aloonesha alistahili medali.

Mtemvu yeye ndiye aliyemshawishi Ali Mwinyi Tambwe wakati ule katibu wa Al Jamiatul Islamiyya ajiunge na TANU. Al Jamiatul Islamiyya ilikuwa na fedha nyingi za Waislam na zilitumika sana katika shughuli za TANU. Mtemvu ndiye alikuwa katibu wa TANU wa kwanza na sifa yake kubwa ilikuwa uhamasishaji na kufanya mikutano bila kibali. Mtemvu ndiyo aliyoiingiza Mafia katika TANU.

Mifano ni mingi na michango ya hawa mashujaa nimeieleza kwa kirefu katika kitabu changu.

Saleh Muhsin alikuwa anatoka katika ukoo tajiri na walikuwa na hodhi kubwa Kurasini. Ghorofa lao hadi leo lipo Mtaa wa Kirk Street (sasa Lindi) na Nyamwezi. Watu kama hawa ndiyo walioifadhili TANU katika siku zile ngumu za shida kati ya 1954 - 1958.

Kwa hayo waliyotenda walistahili kabisa kukumbukwa na kuenziwa. Hiyo ni haki yao. Kufanya kinyume ya hivyo ni dhulma kubwa.

Abbas Mtemvu mtoto wa Zuberi Mtemvu alimuoa Aziza bint Muhsin (sasa ni marehemu Mungu amlaze pema peponi), mjukuu wa Saleh Muhsin. Siku ya harusi watu wamekusanyika Mzee Saleh akasimama akawanadia watu huku akicheka kwa furaha akasema, "Sikizeni jamani mimi nilimwambia Zuberi bwana usivunje hii Congress yetu huu ni mwamba tuendelee na mapambano dhidi ya TANU yeye akakataa sasa presiedent akiondoka kuna nini tena. Haya chama akakivunja lakini nikamwambia, "Zuberi wewe utarudi hapa kwangu." Leo si huyu hapa mnamuona hapa kwangu?" Pakaanguka kicheko kikubwa sana. Mzee Mtemvu yuko katika kanzu kaegemea ukuta anafuta machozi na kitambaa cheupe. Saleh Muhsin alikuwa kamkumbusha mbali sana.

Siku hiyo watu wa Dar es Salaam tulikuwa tumekutana kufarahia harusi na katika mikusanyiko kama hiyo ndipo hukumbushana historia yetu na ya mji wetu. Hapo tulipokuwa tumekaa nyumba ya Mashado Plantan unaiona ile pale na ikiwa utasimama na kutazama upande wa Mnazi Mmoja unaiona nyumba ya Abdulwahid Sykes. Na hapo tulipokuwa tumekaa tunasubiri biriani mtaa wa mbele na sawasawa na nyumba ya Mzee Saleh Muhsin ndipo nilipozaliwa mimi Mtaa wa Kipata (sasa Kleist Sykes). Nyumba hizo zote nilizozitaja zilikuwa uwanja wangu wa mchezo nilipokuwa mtoto mimi na rafiki zangu tukiingia na kutoka wakati wowote bila ya kipingamizi chochote.

Muhali mkubwa sana mimi kuona historia hii ya wazee wangu inapotoshwa na mimi nikae kimya. Kwa hili sina stahamala na yeyote.

Wataniwia radhi.
 
WANAUKUMBI: Nimeulizwa swali vipi Nyerere ampe medali Zuberi Mmanga Mwinshehe Mtemvu na yeye alitoka TANU? Niltoa jibu mashine ikakorofisha jibu limepotea. Sasa naeleza mambo yalivyokuwa kabla ya mtafaruku wa 1958 kupelekea wana TANU maarufu kama Ramadhani Mashado Plantan, Saleh Muhsin, Said Chamwenyewe, Zuberi Mtemvu na wengineo kujitoa TANU wengine kuanzisha Congress na wengine AMNUT.

Ramadhani Mashado Plantan kabla ya TANU alikuwa TAA na ndiyo alikuwa "mouthpiece" yao kupitia gazeti lake "Dunia" wakati wa Vita vya Pili na kupitia "Zuhra" baada ya vita. Watu walimsoma Nyerere kwa mara ya kwanza katika "Zuhra" kupitia kalamu ya Mashado Plantan kufuatilia mkutano wa kwanza wa TANU uliofanyika Ukumbi wa Arnatouglo Dar es Salaam Agosti 1954. Mashado aliandika makala na kuwajuvya wananchi nini kilikuwa kinafanyika Tanganyika. Kazi hii aliifanya hadi pale TANU ilipoweza kuwa na gazeti lake "Sauti ya TANU" mwaka wa 1956. Mashado kafanya mengi katika propaganda za TANU. Katika kitabu nimeeleza kwa urefu wake. Kwa hili anastahili medali lau kama alijitoa TANU na kuanzisha AMNUT.

Said Chamwenyewe yeye alikuwa TAA na mwaka 1951 Kamati ya Udhamini ya UNO ilipotembelea Tanganyika yeye ndiye alikuwa msemaji mkuu. Ilipokuja TANU 1954 wakoloni walikataa kutoa tasjila kwa kisingizio kuwa TANU haina wanachama. Abdulwahid Sykes alimpa kazi Said Chamwenyewe ya kutafuta wanachama. Said Chamwenyewe alikwenda Rufiji ambako ndiko kwao na kuleta orodha ndefu ya wanachama. Alikuwa akienda Rufiji kwa baiskeli akipita kila kijiji kuuza kadi za TANU na fedha akikabidhi Makao Makuu, New Street. Ukienda kutazama nyaraka za TANU wanachama wa mwanzo utakuta majina ya kina Mbonde na saini ya Said Chamwenyewe katika kadi hizo. Alifanya mengi katika TANU hadi ulipotokea mtafaruku wa 1958 yeye na Mtemvu wakenda kuunda Congress. Said Chamwenyewe kwa uzalendo aloonesha alistahili medali.

Mtemvu yeye ndiye aliyemshawishi Ali Mwinyi Tambwe wakati ule katibu wa Al Jamiatul Islamiyya ajiunge na TANU. Al Jamiatul Islamiyya ilikuwa na fedha nyingi za Waislam na zilitumika sana katika shughuli za TANU. Mtemvu ndiye alikuwa katibu wa TANU wa kwanza na sifa yake kubwa ilikuwa uhamasishaji na kufanya mikutano bila kibali. Mtemvu ndiyo aliyoiingiza Mafia katika TANU.

Mifano ni mingi na michango ya hawa mashujaa nimeieleza kwa kirefu katika kitabu changu.

Saleh Muhsin alikuwa anatoka katika ukoo tajiri na walikuwa na hodhi kubwa Kurasini. Ghorofa lao hadi leo lipo Mtaa wa Kirk Street (sasa Lindi) na Nyamwezi. Watu kama hawa ndiyo walioifadhili TANU katika siku zile ngumu za shida kati ya 1954 - 1958.

Kwa hayo waliyotenda walistahili kabisa kukumbukwa na kuenziwa. Hiyo ni haki yao. Kufanya kinyume ya hivyo ni dhulma kubwa.

Abbas Mtemvu mtoto wa Zuberi Mtemvu alimuoa Aziza bint Muhsin (sasa ni marehemu Mungu amlaze pema peponi), mjukuu wa Saleh Muhsin. Siku ya harusi watu wamekusanyika Mzee Saleh akasimama akawanadia watu huku akicheka kwa furaha akasema, "Sikizeni jamani mimi nilimwambia Zuberi bwana usivunje hii Congress yetu huu ni mwamba tuendelee na mapambano dhidi ya TANU yeye akakataa sasa presiedent akiondoka kuna nini tena. Haya chama akakivunja lakini nikamwambia, "Zuberi wewe utarudi hapa kwangu." Leo si huyu hapa mnamuona hapa kwangu?" Pakaanguka kicheko kikubwa sana. Mzee Mtemvu yuko katika kanzu kaegemea ukuta anafuta machozi na kitambaa cheupe. Saleh Muhsin alikuwa kamkumbusha mbali sana.

Siku hiyo watu wa Dar es Salaam tulikuwa tumekutana kufarahia harusi na katika mikusanyiko kama hiyo ndipo hukumbushana historia yetu na ya mji wetu. Hapo tulipokuwa tumekaa nyumba ya Mashado Plantan unaiona ile pale na ikiwa utasimama na kutazama upande wa Mnazi Mmoja unaiona nyumba ya Abdulwahid Sykes. Na hapo tulipokuwa tumekaa tunasubiri biriani mtaa wa mbele na sawasawa na nyumba ya Mzee Saleh Muhsin ndipo nilipozaliwa mimi Mtaa wa Kipata (sasa Kleist Sykes). Nyumba hizo zote nilizozitaja zilikuwa uwanja wangu wa mchezo nilipokuwa mtoto mimi na rafiki zangu tukiingia na kutoka wakati wowote bila ya kipingamizi chochote.

Muhali mkubwa sana mimi kuona historia hii ya wazee wangu inapotoshwa na mimi nikae kimya. Kwa hili sina stahamala na yeyote.

Wataniwia radhi.

Na hapo ndo tunatofautiana Mkuu Mohammed Said.
Hiyo historia unayoelezea inawezekana ina ukweli ndani yake , hilo hatu pingi.
Sasa hapo kilichopotoshwa nini?
Unakuwa nonstalgic katika kuelezea historia hii.
Ingawa hatusemi, mimi nikekua na hao kina Abbas, ni wadogo zangu.Tumekaa karibu toka Temeke hadi Masaki.Ni watu wastaarabu na tumeishi nao vizuri tu, hata mke wake Abbas tuna wafahamu sana.
Historia huwa haina aibu wala huruma.Kitendo cha baba yao Mzee Zuberi Mtemvu kupingana na Nyerere kisiasa kabla ya uhuru ni kama kila mtu alichukua njia yake ya kisiasa.
Sote tunajua kilichowatokea wale WOTE waliopingana na Nyerere kimawazo.
Unawakumbuka kina Anangisye na TYL? Kina Kambona je?
Hapo hakuna suala la Uislamu bali siasa.
 
LG: Wewe umekuwa na Abbas toka Temeke nami nakufahamisha kuwa Bi Siti Kilungo mama yake Abbas na mama yangu Baya bint Mohamed walikuwa mashoga toka ujana wao Bi Siti akiishi Kirk Street nyumba ya baba yake Mzee Kilungo na sisi tuko Kipata. Nikakutana na Bi Siti Masaki nilipoanza kazi sasa mimi kijana.

Mimi sina tatizo na yeyote awaye yule ninachofanya ni kuweka sawa historia ya wazee wangu. Naamini kabisa endapo mimi ningejifanya naijua historia ya Tindahimba au Bukoba vijijini wenyewe wangelikuja juu na kuniuliza wewe Mswahili mno utayajuaje yaliyotokea kwetu?

Ama kuwa "nostalgic" hilo khasa na ndicho kilichonifanya ninyanyue kalamu kuandika historia ya kweli kupigania uhuru wa Tanganyika. Hawa watu wanaishi ndani yangu.

Babu yangu akisema, "Nyerere hakutukuta tunalea mikono, katukuta katika mapambano dhidi ya ukoloni." Marehemu Abdulwahid kasema, "Let him be. Let him take the credit." Lakini soma orbirtuary ya Brendon Grimshaw aliyekuwa mhariri wa Tanganyika Standard katika Sunday News (sikumbuki tarehe) utapata jibu.
 
sheikh mahammed said, nashukuru sana kuuukuta mjadala huu ukiendelea. mimi ni nilifungiwa one 1 month hadi jana kwa kosa nililaombiwa ni mdini.
dini kwa hivyo najua wazi endapo utajaribu kuipa umbele dini yako ktk jamii hii utaonekana wewe ni mtu hatari. nakumbuka nilipokuwa chuo, nilipokuwa najaribu kufanya ibada chumbani kwangu , kwa bahati bnilikuwa nakaa na iamni tofauti na dini yangu nilikuw anpata shida fulani. kitu kilichonisaidia kwamba nilikuwa sikubali kuwekwa dini yangu daraja la pili. ndipo niliposhinda hao wasomi wetu.
kwa hivyo nakupa pole sana najua mengi wenye dini tofauti na wewe watakavyokuijbu.
lkn najua wewe umshib malezi ya kiislam yaani amani na Upendo utatoa darsa kubwa humu
Assalaam alaykum wa ahlan wa sahlan yaa Malaria Sugu!.Pole sana.
Nashukuru kukuona tena.Nilikuwa nakutafuta sana.Matatizo yako niliyakisia kwani niliwahi kukutafuta kila jukwaa humu nikakukosa.Allaahu akbar!,nilikuwa niko karibu sana kukutolea mfano kwa Mohammed Said kuhusiana na post yake moja huko nyuma aliposema "nisije nikafukuzwa humu".Nilitaka nimthibitishie kuwa kweli kufukuzwa kupo hapa.
Nachukua fursa hii kukutambulisha kwa maalim Mohammed ambaye nataraji hakufahamu.Nyinyi wawili munafanana sana kwa kutokuwa na hasira.Tofauti na mimi.Hata hivyo kwa kuangalia ninavyowapiga mweleka hawa jamaa,mutaelewa kuwa hasira zangu si za mkizi,za kujirusha kwenye mtumbwi wa wavuvi,bali nina hasira za kutetea ukweli.
Baada ya kuingia akina sisi mara nyingi nimesikia malalamiko ya baadhi ya wana JF kuwa hili jukwaa sasa limevamiwa.Sidhani kwamba ni uvamizi bali ni hofu tu.Huko nyuma walikuwa na mijadala yao ya kucheka cheka tu.Huu mjadala nataraji ni wa mwanzo ambao ni wa ki-intelligence na watu wanafaidika na teknolojia kweli.
Nimefurahi umerudi na ile ile T-shirt yako waliyokufukuza nayo.Naomba nielekeze wapi pa kuipata ili nimnunulie mwanangu.Ulipoondoka yumkin nilikuwa bado sijaanza kubeba hilo bango unaloliona hapo.Nilikuwa bado nimevaa yale mavazi ya waanzilishi wa chemistry,nakusudia kilemba.Nitakivaa tena baadae kikishakauka.
 
Muongo njia yake fupi. Hapa hao unaowa/quote wenyewe wanasema walioagiza waislamu wapigwe Mwembechai ni waislamu wenzao! Badala ya kuegemea nyuma ya mgongo wa huyo Dk. Lwaitama, ungetuambia Kadinali Pengo aliunga vipi mauaji yaliyofanyika Mwembechai. Tuambie ni wapi na lini ambapo Kadinali huyo alisema kuwa tendo la kuwaua waislamu lilikuwa sawa.

Hao wote hapo juu ( akiwemo mkristu), hakuna aliyeongelea vurugu za Mwembechai zilianzaje bali wanalaani heavy handed approach ya serikali. Kwenye kitabu chake Njonzi anadai serikali iliitikia wito wa padri Camillius Lwambano wa parokia ya Mburahati( Njozi, uk.15)! Huyu padri ndiye aliyewafanya viongozi wa serikali ambao walikuwa waislamu wawaagize polisi kwenda kuua waislamu wenzao! Na mnapozungumzia kuuawa na kujeruhiwa kwa waislamu, mnasahau kuwa wakristu kibao nao waliumizwa katika vurugu zile! Wauza mitumba na wafanya biashara ndogo ndogo wengi tu waliathirika bila kujali imani yao. Mnasahau atmosphere iliyojaa chuki kati ya uongozi wa zamani na vijana wa kiislamu wa msikiti huo. Mnasahau kuwa vijana hao ambao mnasema walifunzwa heshima katika dini yao hawakusita kuvamia na kuwacharaza bakora watu ambao waliwazidi umri! Mnasahau, conveniently, kuwa baadhi ya vijana hao walikuwa na silaha na waliisha-apa kupigana kidete kutetea uislamu! Nyinyi wenzetu, historia yenu inaanzia pale ambapo polisi walivamia msikiti na mnakataa kabisa kuangalia mchango wenu uliopelekea hali ile kutokea!

Kitendo cha polisi kuwapiga risasi na hata virungu raia wenzao kinatakiwa kilaaniwe na kila mtu. Lakini kudai kuwa polisi hao walifanya hivyo kwa sababu tu waislamu walihusika ni makosa. Polisi hao wamekuwa wakiwapiga bila huruma wanafunzi wake kwa waume wanaodiriki kuandamana kudai haki zao. Baadhi ya hao mapolisi wamesikika wakijivunia na kufurahia kuwa wamepata fursa ya kuwashikisha adabu wasomi! Kutokana na ukweli huu basi mtataka kutuambia kuwa serikali inabagua wasomi? Hata kama hao viongozi wa serikali ni wasomi!

Amandla.......

Ulipokuwa unamjibu Yaya no.907 ulikozesha majibu yake pale aliposema "Lakini lililomshangaza zaidi alisema ni kuona wanaoshutumu Waislamu na kutuma polisi wawapige ni viongozi ambao ni Waislamu. Dk. Lwaitama alionesha kusikitishwa kwake kwa hatua ya Kadinali Pengo kuunga mkono mauaji."
.....................................................................................................................................................................
Katika kumjibu Yaya ndipo ukasema hapo juu "ungetuambia Kadinali Pengo aliunga vipi mauaji yaliyofanyika Mwembechai. Tuambie ni wapi na lini ambapo Kadinali huyo alisema kuwa tendo la kuwaua waislamu lilikuwa sawa"
Kauli halisi aliyotumia kardinali Pengo kuhalalisha mauwaji ni pale alipotoa kisa cha Daud na Goliath kuhalalisha mauaji ya Waislamu pale Mwembechai,kwa kusema na jiwe nalo huwa linaua pia.Kauli hii ilikuwa ni kuwatetea polisi kwa kutumia risasi za moto dhidi ya vijana waliowauwa.
Hapo juu umesema "Mnasahau, conveniently, kuwa baadhi ya vijana hao walikuwa na silaha na waliisha-apa kupigana kidete kutetea uislamu!".
Naomba tutajie ni silaha zipi walizokuwa nazo hao vijana?.
 
AMI: Ahsante sana. Hawa ni ndugu zetu na tunawajibu wa kuwaeleza kwa utaratibu yale ambayo sisi tunayajua kuhusu historia ya wazee wetu. Hawa wengi wao hawaijui historia ya wazee wetu na juhudi walizotia katika kupigania uhuru wa nchi hii. Wazee wetu walitoa nyumba zo kuwa ofisi za TANU, walitembea nyumba kwa nyumba kuchangisha fedha kwa ajili ya TANU nk. Marehemu Abduwahid Sykes mwisho biashara yake ya petrol station pale Ilala Boma ikafilisika fedha zote zinakwenda kwenye harakati. Ikabidi aweke nyumba yake rehani kwa Karimjee ili aifufue. Kila ikitokea shida TANU yeye na Dossa na Mzee Rupia wako mbele kuchangishana. Dossa yeye kafa masikini Mlandizi pale. Mimi nimefika kwake na niliiona hali yake. Hawa wenzetu haya hawayajui wanakuja na kitabu cha historia ya TANU wazee wetu hawamo. Hivi kweli ndiyo tukae kimya? Wajibu ni kuwaeleza kuwa mlichoandika sicho hiyo siyo historia ya TANU. Mbona fulani na fulani hawamo humu? Sasa unawaweka kitako unawaeleza. Khiyari yao kukubali au kukataa. Muhimu sana na hili nalirudia tena na tena, wasitukataze kuwarehemu wazee wetu na TANU yao. Bila shaka na wao wazee wao walifanya mambo huko sehemu za Tindahimba na Bukoba vijijini itakuwa bora na wao wakaandika michango ya wazee wao ili historia ikamilike lakini si kutukataza sisi kueleza habari za wazee wetu tena kwa kejeli ati tunaandika hadithi. Hivi sio sawa.
 
KITHUKU: Ahsante kwa ushauri wako lakini kabla sijakupa jibu nami nina swali. Ushasoma kitabu changu?

Kitabu chako nimekinunua Dar na kukisoma chote, sijapata jibu la hilo nililokuuliza, yaani je hao walitendewa hivyo kutokana na tofauti ya kidini ama ya kisiasa? Hilo hukulijibu katika kitabu chako.
 
MALARIA SUGU: Baba yangu akiijua sana historia ya Dar es Salaam. Tukitembea njiani akikutana na mtu basi atanambia huyu mdogo wake Dossa unajua alikuwa na dada yake akiitwa fulani huyu alikuja olewa na fulani nk. tunakwenda njiani gumzo linanoga. Tena ajabu hakuna utakaemtaja yeye akawa hamjui. Hivi nami nikaja jua mengi sana kuhusu mji wa Dar es Salaam na historia yake.

Sikiza kihoja hiki: Mwaka 1988 nikamshauri Bwana Ally Sykes nikamwambia tumfanyie Bwana Abdu kumbukumbu katika magazeti tununue nafasi mimi nitaandika kitu. Wakati ule bado kitabu chake sijamaliza. Mwaka 1988 marehenu Abdu alikuwa anatimiza miaka 20 toka kufariki. Basi nikaandika kumbukumbu na kuipeleka Daily News na Uhuru. Katika kumbukumbu ile nimesema Abdu ndiyo muasisi wa TANU na kadi yake no. 3. Kadi No. 1 Julius Kambarage Nyerere, No. 2 Ally Kleist Sykes na Kadi No. 3 Abdulwahid Kleist Sykes. Kisha nikasherehesha na mengi alofanya katika jamii kama kuwa katika Aga Khan Education Committee, Baraza la Kiswahili nk. Daily News alikuwako Reginald Mhango yeye akifahamiana na Kleist (mtoto wa Abdu Sykes) walisoma wote Aga Khan School. Reginald Mhango akampigia simu Kleist usiku akitaka radhi kuwa hatoweza kutoa ile kumbukumbu ya baba yake hadi apate idhini kutoka ngazi za juu. Kleist akauliza kwanini iwe hivyo? Jibu alotowa Mhango ni kuwa, "Historia ya baba yako inagusa historia ya Tanzania kwa hiyo sitoweza kuitoa mpaka nipate idhini."

Siku ya pili ile kumbukumbu kwa bahati nzuri ilitoka katika Daily News na katika gazeti la Uhuru lakini yale yote maneno muhimu katika historia ya Abdu Sykes na mchango wake katika TAA hadi TANU yalifutwa. Ikawa ile kumbukumbu ni sawa na kumbukumbu ya mtu yoyote yule.

Mimi nikawa najiuliza hivi kinachoogopwa khasa ni nini?
 
KIthuku: KIla mtu ana uwezo wake wa kutafakari na kuchambua mambo. Siwezi kukulazimisha hii ndiyo silka yetu binadamu kila mtu ana namna yake ya kuliona jambo. Nakushukuru kwa ushauri wako.
 
Hivi hii hali ya kuiweka historia ya Tanzania mikononi mwa Nyerere as if alipambana peke yake ndiyo sababu ya project nyingi kupewa jina lake?. mara, Mwl Nyerere International Airport, Mara Viwanja vya sabasaba vya Mwalimu Nyerere, nasikia kitajengwa chuo kikuu kingine cha kilimo na kitaitwa Mwalimu Nyerere, barabara ya mwalimu nyerere, na pale Kigamboni navy kuna something Mwalimu Nyerere...., hivi hakuna wazalendo wengine wapigania Uhuru wa kupewa heshima hizi?. watu kama abdulwahid sykes, John Rupia, AbdulRahmani Babu, Vedastus Kyaruzi?. why most of things Nyerere?.
kuna hadi siku ya Nyerere ya mapumziko (wakaweka na ya karume ili kuwatuliza wazanzibari), pamoja na uchumi wetu mdogo bado tunaafford kutokwenda makazini katika siku hizi mbili.

namkubali sana Nyerere lakini, tuwe fair kwa historia ya nchi yetu na wale waliopambana kwa hali na mali lazima tuwatambue, na si kwa majina ya vijimitaa, ni vyema project kubwa kama mabarabara makubwa, majengo makubwa, hata picha zao kwenye noti za pesa, stempu,n.k , wakumbukwe watu hawa.
 
Na hapo ndo tunatofautiana Mkuu Mohammed Said.
Hiyo historia unayoelezea inawezekana ina ukweli ndani yake , hilo hatu pingi.
Sasa hapo kilichopotoshwa nini?
Unakuwa nonstalgic katika kuelezea historia hii.
Ingawa hatusemi, mimi nikekua na hao kina Abbas, ni wadogo zangu.Tumekaa karibu toka Temeke hadi Masaki.Ni watu wastaarabu na tumeishi nao vizuri tu, hata mke wake Abbas tuna wafahamu sana.
Historia huwa haina aibu wala huruma.Kitendo cha baba yao Mzee Zuberi Mtemvu kupingana na Nyerere kisiasa kabla ya uhuru ni kama kila mtu alichukua njia yake ya kisiasa.
Sote tunajua kilichowatokea wale WOTE waliopingana na Nyerere kimawazo.
Unawakumbuka kina Anangisye na TYL? Kina Kambona je?
Hapo hakuna suala la Uislamu bali siasa.

Mkuu Lole inaonekana maudhui muhimu sana ya mada hii umeisahau, naomba nikukumbushe. Kwanza nashkuru sana kama umeanza kukubali kuwa hiyo historia inayoitoa Mohamed Said ina ukweli ndani yake.

Kinachopotoshwa ni kuwa Historia ya nchi hii imeandikwa tofauti na alivyoiandika Mohamed Said na katika kupotoshwa huku ndiko kunapozua maswali mengi ya msingi ambayo Mohamed Said anajaribu kuyafafanunua.

Cha muhimu zaidi kama hukubaliani na Historia aliyoandika Mohamed Said unatakiwa uje na ushahidi wa kumkosoa na ueleze wewe Historia yako unavyoifahamu.

Naomba kila tunapochangia tusisahau maudhui muhimu ya mada hii kuwa Historia ya nchi yetu iliyoandikwa na inayofundishwa mashuleni imepotoshwa na kuna watu muhimu sana katika Historia ya nchii hii wamesahauliwa.

Tuendelee kujadiliana ili kupata elimu na faida kwa watu wote.
 
LG: Wewe umekuwa na Abbas toka Temeke nami nakufahamisha kuwa Bi Siti Kilungo mama yake Abbas na mama yangu Baya bint Mohamed walikuwa mashoga toka ujana wao Bi Siti akiishi Kirk Street nyumba ya baba yake Mzee Kilungo na sisi tuko Kipata. Nikakutana na Bi Siti Masaki nilipoanza kazi sasa mimi kijana.

Mimi sina tatizo na yeyote awaye yule ninachofanya ni kuweka sawa historia ya wazee wangu. Naamini kabisa endapo mimi ningejifanya naijua historia ya Tindahimba au Bukoba vijijini wenyewe wangelikuja juu na kuniuliza wewe Mswahili mno utayajuaje yaliyotokea kwetu?

Ama kuwa "nostalgic" hilo khasa na ndicho kilichonifanya ninyanyue kalamu kuandika historia ya kweli kupigania uhuru wa Tanganyika. Hawa watu wanaishi ndani yangu.

Babu yangu akisema, "Nyerere hakutukuta tunalea mikono, katukuta katika mapambano dhidi ya ukoloni." Marehemu Abdulwahid kasema, "Let him be. Let him take the credit." Lakini soma orbirtuary ya Brendon Grimshaw aliyekuwa mhariri wa Tanganyika Standard katika Sunday News (sikumbuki tarehe) utapata jibu.

Naona Mkuu we might have a common area baada ya mabishano ya muda mrefu.
Mabishano haya yanatokana na maono tofauti ya kule tutokako na kule tuendako.
Na ndio suala ambalo nimekuwa niki advocate toka mwanzo juu ya ushirikiano wa waTanzania toka wakati wa uhuru.
Familia hii ya Abbas Mtemvu naifahamu toka utoto na tumekua pamoja pamoja kwamba Abbas ni mdogo kwangu. Hatukuwa na aina yoyote ya utengano wa kimawazo miaka hiyo ya 60 hadi 80's na nadiriki kusema hata kufuturu nimeshiriki kwao baada ya mfungo wa Ramadhan pale Masaki. Na wao tumeshirikiana pamoja na hata mtoto mdogo wa kiume wa Abbas ameshiriki kwangu nyakati za Krismas.
Hiyo ni familia ya kistaarabu pamoja na mama yao ambaye ni mcheshi sana. Maalim Mohammed Said , sisi kama waTanzania tumekua hivyo na huu ni mfano mmoja tu ya undugu unao jumuisha watu wa dini zote.
 
OLGAH: Baba yangu alisoma Al Jamiatul Islamiyya sina uhakika wa khasa ni mwaka gani lakini nikihesabu kwa kuanza shule na miaka saba na yeye kazaliwa 1924 itakuwa kaanza darasa la kwanza mwaka 1931. Alisoma darasa moja na Abdulwahid Sykes na vijana wengine wa Dar es Salaam ya wakati huo. Kitu alichokuwa akinieleza ni kuwa Abdulwahid alikuwa na akili sana alitangulia kumaliza kusoma mas'haf yote kabla ya wenzake wote na mwalimu akiwa hajaja darasani yeye Abdu anasimama mbele anawafunza wenzake. Alioongoza hivyo hadi alipomaliza darasa la kumi Kitchwele na kupasi wa kwanza mtihani wa kuingia Makerere. Hapo Vita Kuu ya Pili akawa-conscripted katika jeshi KAR na kupelekwa Burma 1942. Abdulwahid Sykes alitoka jeshini na cheo kikubwa ambacho Mwafrika angeliweza kupewa katika jeshi la Waingereza na alitunukiwa medali kadhaa.[/QUOTE]

Mimi hapa ndipo unaponikatisha tamaa! Hicho cheo kikubwa alichokuwa nacho Abdulwahid Sykes ni kipi? Hizo medali ni zipi? Inakuwaje wewe ambae umeamua kuvaa joho la historian wa ukoo wa akina Sykes halafu unamung'unyamung'unya maneno! Hizo hadithi kuhusu akili za Abduu ndio hizo hizo tunazosikia kutoka kwa wapambe wa Nyerere. Kwetu sisi hazina tija. Tunachoangalia na kupima ni nini walifanya wakati wa kugombea uhuru. Hakuna mtu mpaka sasa aliyekana mchango mkubwa wa hao ndugu wawili. Tunachokataa ni hiyo spin yako kuwa hawakupewa hiyo heshima unayoona wanastahili kutokana na ukatoliki uliokithiri wa Mwalimu Nyerere! Inawezekana hawakupewa vyeo vya kisiasa lakini Nyerere hata wakati wa kilele cha siasa ya ujamaa hakudiriki kuingilia biashara zao! Si lazima mtu uwe waziri ndio uone umeheshimiwa!

Amandla......
 
Mkuu Lole inaonekana maudhui muhimu sana ya mada hii umeisahau, naomba nikukumbushe. Kwanza nashkuru sana kama umeanza kukubali kuwa hiyo historia inayoitoa Mohamed Said ina ukweli ndani yake.

Kinachopotoshwa ni kuwa Historia ya nchi hii imeandikwa tofauti na alivyoiandika Mohamed Said na katika kupotoshwa huku ndiko kunapozua maswali mengi ya msingi ambayo Mohamed Said anajaribu kuyafafanunua.

Cha muhimu zaidi kama hukubaliani na Historia aliyoandika Mohamed Said unatakiwa uje na ushahidi wa kumkosoa na ueleze wewe Historia yako unavyoifahamu.

Naomba kila tunapochangia tusisahau maudhui muhimu ya mada hii kuwa Historia ya nchi yetu iliyoandikwa na inayofundishwa mashuleni imepotoshwa na kuna watu muhimu sana katika Historia ya nchii hii wamesahauliwa.

Tuendelee kujadiliana ili kupata elimu na faida kwa watu wote.

Hakuna nchi yenye historia iliyokamilika. Historia ni dynamic na siyo static. Ndio maana kila wakati panatokea tafsiri tofauti ya yaliojiri. Hata katika nchi kama Marekani mpaka hivi leo historia yake inaangaliwa upya kujaribu kuwaingiza wale ambao inaonekana waliachwa. Kama Mohamed Said, angebakia kwenye kukumbushia umuhimu wa wale ambao anaona wameachwa katika historia tunayoijua, wote tungemshukuru. Kwa watu kama mimi, dosari kubwa ya simulizi yake ni kuchukua kwake ushahidi uliopo (ambao mara nyingi yeye mwenyewe anauelezea ) na kujaribu kuleta picha tofauti. Kwa mfano, anapotoa mfano wa babu yake kuwekwa kizuizini kama uthibitisho wa chuki za Mwalimu kwa waislamu ni kutufanya wengine hatuna akili. Ninasema hivi maana wengi wetu tunajua kuwa Nyerere alitupa Lupango watu kibao bila kujali dini! Kusema kuwa Nyerere aliifungia EAMWS kwa sabau ati ilitaka kujenga Chuo Kikuu ni uongo mwingine maana yeye mwenyewe anajua thika kuwa mtu wa kwanza kunyang'anya mali za EAMWS alikuwa Sheikh Abeid Amani Karume. Anajua vile vile kuwa pingamizi kubwa dhidi ya EAMWS halikutoka kwa Nyerere bali waislamu ndani ya TANU ambao walikiona kama chombo cha waarabu na wahindi na kuwa kinaenda tofauti na malengo ya kijamaa ya TANU. Yeye kama anaona kuwa kuna upotoshaji wa historia yetu, ni haki yake kuandika tafsiri yake ya hiyo historia. Lakini asitegemee kuwa kwa vile tu ataachiwa kama atarudia makosa yaleyale ambayo ana washutumu wenzake kuyafanya!

Amandla......
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom