Najua kuwa hapa wanasoma wengi ndio maana nasema kuwa "simulizi" zako hazina mshiko kwa maana haujazifanyia utafiti wa kutosha na hii inafanya conclusions zako ziwe na walakin. Unachukua maneno ya upande mmoja na kutaka sote tuamini kuwa ndivyo ilivyokuwa kwa sababu tu ya uhusiano wako nao kijamii au kidini. Kwa mfano kuna mahali ulidai kuwa waliokuwa nyuma ya mgogoro wa ardhi ya wameru walikuwa waislamu wakina Kandoro na Sykes bile kumtaja mkristu Japhet Kirilo. Nilipokuuliza na kukwambia kuwa, hapana, mtu aliyeenda New York kusimamia kesi ya mgogro huo alikuwa Kirilo na ni yeye ndiye aliyezunguka nchi nzima pamoja na hao uliowataja, ukasema kuwa ulienda Arusha kumtafuta Kirilo ukiongozana na Abduu na kunitajia mpaka gari mlilopanda kwenda kule lakini hamkumkuta maana alikuwa ameenda Nairobi. Mtafiti mahairi anayetaka ukweli angerudi tena au hata kumtafuta Mzee Kirilo kwa simu! Umetusimulia hotuba ya Kighoma Malima halafu ukadai kuwa ndiye yeye aliyeleta taratibu ya kutumia namba katika mitihani ya darasa la saba ili kuzuia ubaladhuli wa wakristu. Ulipopingwa na kuelezwa kuwa wengi tu wamefanya mitihani hiyo KABLA ya Kighoma Malima kuwa waziri, umekaa kimya. Nilitumaini ungetuambia kama wewe katika mtihanio wako wa darasa la saba (au nane) uliandika jina lako na sio namba na kwa sababu hiyo wakristu waovu walikufelisha! Umetoa statistics zikionyesha uwiano wa dini katika bunge letu na kudai kuwa zinaonyesha kuwawabunge wakatoliki ni 75% ya bunge. Nilipochukuwa statistics zako na kukuonyesha kuwa tofauti na unavyosema, zinaonyesha kuwa wislamu ni majority katika hilo bunge , umekaa kimya! Na mifano kama hii iko mingi. Unapobanwa unachukuwa kurasa nzima hata kama haiendani na kilichoulizwa na kuibandika hapa. Au unatupa hadithi ambayo unatuambia ulisimuliwa peke yako. Hadithi hizo ni nzuri na zinafurahisha lakini hazitoshi.
Mwenye dharau ni wewe, Mkuu. Umezoea kusifiwa na watu kupokea kila unachosema kama vile wewe ni malaika fulani. Unapopingwa unadai kuwa ati unadharauliwa na lugha ya kukejeliwa. Wewe kama umewahi kufanya presentation katika midahalo ya kimataifa ambayo ni diverse na sio ya waislamu wenzako, ungetambua kuwa vigorous criticism ni course for par! Ukiweka kitu hadharani ni lazima atatokeza mtu kupinga na kudai uthibitisha na kuonyesha mapungufu yake. Ni kama vile wewe unavyochambua historia iliyoandikwa na watu wa Kivukoni basi na wewe vile vile kitabu chako kitachambuliwa. Ndivyo ilivyo. Wewe unaonyesha dharau kubwa kwa kutufanya kama watoto wadogo ambao umekuja kutufungulia macho!
Mimi naona kwa mtu ambae anajifanya kuwa ni mnyenyekevu suala la umaarufu umeliweka mbele mno. Kuwa wewe ni mtoto wa mjini, kuwa wewe ni ndugu wa watu maarufu, kuwa wewe unakaribishwa na vyuo vikuu vikubwa vikubwa ( nilikuhoji kuhusu hili na mpaka sasa haujanijibu) n.k. n.k. Yote hayo hayana maana hapa. Hapa tunaangalia hizo video zako na maandishi ayako unayoyaweka na tunayajibu ipasavyo. Mimi nimekulia Dar es Salaam na mbona sikujui? Au umaarufu wako ni kwa wenzako wenye dini yako tu?
Umezoea kusifiwa na hao wanaokuomba uwapedarasa bila kupingwa au kuambiwa u-substantiate allegations zako.
Mimi sijui kama una shida ya pesa au la. lakini hii kusisitiza kuwa hauwezi kujadiliana na mtu hadi huyo mtu asome kitabu chako kunanitia wasiwasi. Unataka kuniambia kuwa unapoenda kwenye hizo kongamano za kimataifa, haumjibu mtu mpaka akuhakikishie kuwa amesoma kitabu chako? Si mara nyingi unajibiwa kwa yale unayowaelezea? Kitabu chako si msahafu kiasi kuwa bila kukisoma basi mtu hauwezi kujua ukweli wa historia yetu. Ni kitabu kimoja tu katika vingi.
Wewe ( sio mimi ) ndiye uliyemuita Sykes THE Founder of Political Movements. Au haujui maana yakutumia neno "THE"? Kama ulijua kuwa alikuwepo mwingine, hata mmoja tu usingetumia neno hilo. Huu ni uthibitisho mwingine wa upotoshaji wa makusudi unaoufanya. Kama ulijua kuwa Chief Kidaha Makwaia alihusika pia katika kuanzisha TANU ( kitu ambacho si kweli, maana hawakuwa peke yao hawa) kwa nini basi ulimuita Sykes THE FOUNDER ... kama vile alikuwa peke yake barabarani akielekea Damascus?
Kumbe aliliia akimkumbuka rafiki yake kipenzi! Hivi mlitaka Nyerere afanye nini? Yeye hakuandika kile kitabu mnachodai kuwa kimedharau Sykes. Sijawahi kumsikia Nyerere hata siku moja akikipigia debe kitabu hicho. Mzee Rashad kama mtu mwiingine yeyote alikuwa na haki ya kufanya ulichofanya wewe, kusahihisha mapungufu hayo kwa kuandika kitabu. Kulia kwake hakusaidii kitu bali kuandika kwake kungetusaidia wote.
Hivi wewe ambae umechukua jukumu la kutuandikia masahihisho hayo, kitabu chako kimepigwa marufuku? Umewahi kutiwa ndani kutokana na maandishi yako?
Hakuna mtu anayekukataza kuwaenzi wazee wako kwa kandika waliyokusimulia. Tatizo ni pale unapotaka kutulazimisha kuwa simulizi zao ni ukweli wetu sote. Hii haikubalik hata kidogo. Ndiyo maana umeambiwa kuwa ulichoandika hakiendani na title ya kitabu chako.
Amandla........