Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Kumbe Mkuu haukujua kuwa huko walikotokea wakina Dr. William Mwanjisi, Mzee John Mwakangale, Mzee Japhet Kirilo aliyesimamia kidete kesi ya mgogoro wa adhi wa wameru. Na wengine waliotoka nje ya mikoa unayoijua wewe ni wakina Mzee Joseph Kimalando kutoka Moshi ambaye amehusika katika harakati za kupinga ukoloni toka miaka ya 1930s akiwa ameajiriwa kwenye shirika la reli Tanganyika, mhehe Julius Mwasanyaji, mhindi Amir Jamal kutoka Morogoro, Frank Humplick na dada zake Mary na Regina ambao nyimbo zao ndizo zilitumika kuhamasisha wana TANU. Hata huko Tanga kwenye waislamu wengi, mchango wa Stephen Mhando na mdogo wake Peter Mhando katika kuhamasisha wabondei hauwezi kudharauliwa! ( kutoka " Nyerere and Africa: End of an era cha Godfrey Mwakikagile"). Na hawa ni sehemu ndogo tu ya waliohusika katika mapambano hayo. Ukweli nikuwa sehemu za pwani bila kuungwa mkono na sehemu nyingine za Tanganyika zisingefua dafu mbele ya mkoloni. Wote walihusika, tofauti na unavyotaka kutuaminisha.
Amandla.........
FM: Pole sana ndugu yangu. Mwakikagile amenakili kazi yangu. Ungesoma kitabu changu ungestaajabu na kusema mbona hii kama inatoka kitabu cha Mohamed Said? Ndiyo maana nikikusisitizia kuwa soma kwanza kitabu ndipo utakuwa katika hali nzuri ya kufanya majadiliano. Mwakikagile si wa kwanza kufanya hivyo watu wengi sana wanatumia kazi zangu kama zao na mimi ninafuata mila ya Kiislam kuwa elimu na taalamu haviuzwi kwa hiyo hata mtu akichukua kazi yangu akaitumia huwa kwangu si kitu hata kama hakunitaja.