Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Chukia sana had utapike nyongo[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Ndugu yangu kasome vzr amri.kumi za Mungu. Au nyie katoliki.mmeziedit kwa biblia yenu

Kwa nini akasome, wewe kam unaijua hiyo Amri si uiweke hapa ili umthibitishie Otorong'ong'o kuwa ni muongo yeye na "Biblia yake ya Kikatoliki"
Vinginevyo utabaki na kusema yeye anasoma kwenye Biblia Tofauti, weka hiyo Amri kaka

kichakaa man saidia pia kuleta hiyo Amri kutoka kwenye Biblia inayokataza kusiwepo na Masanamu mAkanisani na mahekaluni
 

Kaka kuna shida kubwa ya Elimu ya Dini ya Ukatoliki kwa wasio wakatoliki,
Huwezi kuamini hili-hakuna Dhehebu linalofata misingi ya ibada iliyomo ndani ya Biblia kama Wakatoliki nasema tena Huwezi amini hilo

Maada ya issue ya Sanamu imeongelewa sana humu,
Kwa kifupi Wakatoliki hawaabudu sanamu, na kama umewahi kumuona Mkatoliki anaabudu na kuitumikia sanamu basi huyo amekufuru na amefanya shiriki kubwa kwa Mungu wetu mwenye wivu,

Kuabudu sanamu ni kuitumainia kuwa inaweza kufanya lolote unaloliomba, hivyo unaitolea Sadaka na kuitumainia, je kweli kazi ya mikono ya binadamu inaweza kutoa msaada, haisikii, haioni, haisemi nk

Sanamu ziko kwenye makanisa ya Kikatoliki kama kumbukumbu ya uwepo wa watakatifu na wafia dini mbalimbali, hivyo ni sanamu za kuangalia na kukumbuka uwepo wao (Bikira Maria, Yesu, Joseph nk )na Sanamu zote zilizopo ni za watu waliowahi kuwepo hapa Duniani, HAKUNA KANISA LA KIKATOLIKI LENYE SANAMU YA MUNGU BABA, kwa sababu hakuna aliyemuona

Stay blessed na uwe na Amani, hakuna muabudu sanamu ndani ya Ukatoliki
 
Kwanza mnamwabudu Maria kama nani? mnamwomba kama nani? maana biblia inasema tuombe kupitia jina la Yesu.hakuna mahala neno limesema muombeni Maria.sasa uje ukemee pepo kwa jina la Maria uone litakavyokufanya

Hakuna Mkatoliki anayemuabudu Maria
 
MUHIMILI WA UKRISTO DUNIANI NI KANISA KATOLIKI.
.......
HAYA YOTE YANAJARIBU KUBADILISHA HISIA YA MWANADAMU NA KUMLETA KARIBU ZAIDI NA TUKIO. WATU WANATOFAUTINA SANA KWA HISIA, UELEWA, KUMBUKUMBU N.K.
Kwa nini RC hawajachonga sanamu ya Bibi yake "mungu"? Au Mababu wa Mungu (Wazazi wa Maria)?

Mimi sikujua kwamba "mungu" ana mama.

Moses alifundisha nini kuhusu Mungu?
Nini Moses aliwaambia wale waliochonga "Golden Calf"?

Utata umebaki pale pale?
Inakuwaje wanaojiita wakristo wanamwabudu binadamu mwenzao?
Wanawezaje kujifanya hawana habari na Mungu aliyemuumba binadamu wanayemwabudu?

John 17:3 Now this is eternal life: that they know you, the only true God, and Jesus Christ, whom you have sent.

Link http://www.riadnachef.org/index.php...laha-illallah&catid=35:english-text&Itemid=56


Link Association of Islamic Charitable Projects » How Does One Become a Muslim?
 
biblia ina lugha karibu zote duniani na zaidi ya 99% ya watumiaji wa jf wanaelewa lugha ya kiswahili ungetumia kwa kiswahili ingeeleweka zaidi.
 

Kaka sio issue ya Pombe tu, kadiri siku zinavyoenda wanaanza kuuona ukweli ambao Wakatoliki wameuanza karne na Karne
Walokole walikuwa wanasema hakuna kinachoweza kumsaidia mtu zaidi ya Yesu pekee, so walikuwa wanawacheka wakatoliki walipokuwa wanatumia Maji ya Baraka, Chumvi, Mafuta nk cha ajabu leo kila kanisa la kilokole linatumia Maji, chumvi na mafuta japo wanayatumia nje ya misingi sahihi, soon wataingia kwenye Masakrament
 

Hakuna Mkarismatic-Mkatoliki anayepingana na hivyo vitu, ukimuona huyo basi sio Mkatismatic-Mkatoliki, huyo atakuwa Mkarismatic-Mlokole
 
Wewe nonda ni mpinga kristo ni wa kupuuzwa umeanza kuleta hayo mavideo na malink yako ya kishetan, zile maada ya dini yako ya kiisilamu umezikimbia umekuja huku kwenye maada za iman za kikristo
 
Ni swala la muda..

Niliona Video ya Muhubiri wa Kipentekoste Benn Hinny akiisifia Sakrament Kuu ya Ekarist Takatifu

Hivyo ni muda tuu tunawapa....mbaya zaidi wakilogwa wasome Historia ya Xstianity na Church Fathers imekula kwao...
 
1)kwa utetezi wa amri ya pili"usijifanyie sanamu ya kuchonga na kuiabudu" kuwa ni muendelezo wa amri ya kwanza hii itapelekea catholcs kuwa naamri tisa badala ya kumi maana kwnye amri ya kumi (kumb 5;21) mliyoigawanya mara mbili inazungumzia kitu kimoja (kutaman mali ya mwingingine maana unaposema mke wake una maanisha anammliki yeye)
2)yesu hakubadil amri bal alizigawnya katika makund mawili 1)upendo kwa mungu 2)upendo kwa mwanadamu
3)kama ni mtu mwenye uelewa wa lugha unapoambiwa amri utaelewa maanayake huwezi ukaniambia usiabudu miungu mingine na usijifanyie sanamu ya kuchonga wala kuisujudia ni amri moja
 
ni kweli wanakosea lakini si vizuri kuwachukia maana kama raia wa yesu unatakiwa kuwapenda wote hata wanaokuudhi
 
Mimi ni mkatoliki nisiyeunga mkono uwepo wa masanamu kanisani... Na ijumaa kuu huwa sijiangaishi kubusu msalaba. Sisali rozari kwakuwa naamini bikira Maria hawezi kusikia sala zangu...

Ntabakia mkatoliki kwa msimamo wangu.
muhimu sio ucatholic muhimu ni kufanya mungu apendacho ikwamo kushika amri zake
 
1. Labda utata ni hili neno kuabudu. Maana ya kuabudu haswa ni ipi?!!
2. Mungu aliruhusu kwa nyakati flani kutengeneza sanamu,lakini mara zote yeye ndio alisema sanamu iwe ya kitu gani na wapi iwekwe.
3. Sasa sanamu za Bikira Maria,Yesu msalabani nani aliwapa mamlaka kutengeneza?!!
 
Ndio umefungua mjadala kabisa zile sanamu zinafanya nini mle ni mapambo usimuunganishe Mungu na sanamu na nyoka wa shaba wa jangwani Rafiki Biblia haijichanganyi kama wanadamu mnavyojichanganya usije kutafuta uhalali wa ibada yako ya masanamu mbele ya watu wa Mungu kama unayoyandika ni kweli nenda pale saint peters au joseph kigango cha mjini sijui ukamwambie paroko ayatoe yake masanamu pale kwa sababu wewe umeangaziwa nuru kwamba hayaabudiwi uone atakayokujibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…