Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
Si ukatoliki Tu,hata usabato nao Una makandokando kibao.
 
Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
Mkuu, katika kipande cha kanuni ya imani, inasema Yesu aliteswa kwa mamlaka ya Mrumi Ponsio Pilato na wala siyo kwa kupitia shinikizo ambalo alilopewa na makuhani na wazee wa Kiyahudi, ambao nao walitaka kumfitinisha na mamlaka yake ya uajiri wake ipale walipodai kuwa Yesu anajifanya kuwa ndiye mfalme wao, wakati wao mfalme wao ni Kaizari! Hivyo anastahili adhabu ya kifo kwa tuhuma za uhaini!

Kuwepo kwa mamlaka ya dola la Rumi katika kanuni hii na kuijumuisha na mamlaka ya kimbingu huenda ndiyo ikawa ndiyo chanzo lkikuu cha Wasabato kuja na "counter attack" dhidi ya Dhehebu Mama la Kikatoliki ndani ya dini ya Kikristo, na pia na mamlaka nzima ya dola ya Rumi.

Nafikiri pengine hiyo ndiyo sehemu ambayo ilimpa ukakasi mwingi Mama Hellen White, kiasi kwamba "fan base" yake haikubaliani na madai au mantiki iliyopo nyuma ya kanuni hii, na hasa ikizingatowa ndiyo tafakari kuu ya kipindi hiki cha Pasaka iliyoletwa na wale wajulikanao kama mababa wa imani waliokutana Rumi kwa wito wa Kaisari Kstaontino (mtaguso), ambao ndio hasa waliitamua siku ya Bwana kama Jumapili na wala siyo Sabato halisi na ya awali kuendana na maandiko matakatifu.
 
Usidhani kanisa katoliki ni mapadre tu na maaskofu na masista.

Kanisa ni pamoja na wewe yaani kila aliyebatizwa na hivyo kila mmoja ana duty ya kulilinda kanisa.

Hivyo mjibu huyo muhubiri usisubiri askofu au padre.
Inaonekana hata yeye mwenyewe hana anachojua,
 
Hakuna mkatoliki aliyesomea biblia, wamesoma canon law tu, wanatumikia taifa la rumi chini ya taasisi yao ya Vatican
Hakuna mkatoliki aliyesomea biblia, wamesoma canon law tu, wanatumikia taifa la rumi chini ya taasisi yao ya Vatican
Huna ulijuwalo, wewe hujui theolojia ni nini.

Wa katoliki wamesoma zaidi ya Biblia mpaka injili inayoitwa Apocrypha ambayo vitabu vyake havimo kwenye Biblia.

Kanisa Katoliki ndio Universal church la mitume.
 
Wakatoliki, wapentecoste, waprostent na vikundi vya mitume na manabii mnasali jumapili lkn mnafundishana maagizo ya wanadamu. Nyie ndo mnashika pasaka, kristmass, mnacheza disco kwenye ibada zenu, mnapiga miziki, mnashindana style na diamond. Ni maagizo ya wanadamu.

Wakristo tunasali jumapili, hatuna music, hatupigi music, tuna ibada kama zilivyo elekezwa na Kristo au mitume wake waliopokea ujumbe kwa Yesu au roho mtakatifu. Tunasali jumapili sababu:-

1. Yesu alifufuka jumapili. Leo mmesoma maandiko mengi yanayothibitisha hayo.

2. Wakristo wa kanisa la karne ya kwanza, walifanya ibada siku ya kwanza ya juma ya juma. Soma mdo 20:7 na 1kor 17:1-2

3. Jumamos siyo siku ya ibada, ni siku ya kupumzika. Kufanya ibada ni kazi, siyo mapumziko. Wanaofanya ibada jumamos hawana andiko linapowaagiza.

4. Siku ya kwanza imetamkwa tangu kutoka 12

Wakatoliki nyie ndiyo mmeharibu injili, mna mafundisho yenu ya uongo mmejitungia wenyewe
Kwa mjibu wa biblia, siku ya ibada ni ipi?
 
Kanisa la Mungu ni lipi? Kwa hbr ya upotofu, wakati katoliki imepotoka kwa asilimia 95%, Kakobe amepotoka kwa 50% ana nafuu japo wote ni wakosefu.

Punguza u much know. Na utambue fika mimi ni Mkatoliki nisiye sikia kelele zozote zile kutoka kwa wapita njia kama wewe.
 
Wee unaelewaje Kutoka 20 : 4 - 8
Hicho kitabu unatakiwa ukisome ukiwa umetuliza sana akili. Na ukisome na vitabu au vifungu vingine alafu uje kwenye uhalisia pengine utaweza kuelewa zaidi!
Siku ukijua maana halisi ya Sanamu kuwa ni ishara au taswira au hisia au alama au kitu chochote kinachochukua nafasi kwenye mawazo na maisha yetu hakika utajua kuwa sanamu na ibada ya Sanamu inayokatazwa ni ipi.
Fedha ni Sanamu
Simu yako ni Sanamu
Nyumba yako ni Sanamu
Gari lako ni Sanamu
Picha za ni Sanamu
Nguo zako ni Sanamu
Samani zako za ndani zote ni Sanamu!
Tamaa... Dharau... Kiburi... Majivuno... Ufisadi... vyote hivyo ni sanamu
Tamaa, urahibu uliopitiliza wa vitu hivyo na vikakufanya umsahau MUNGU wako hiyo ndo inakua ibada kamili ya masanamu.

Hao wakatoliki mnadai wanaabudu Sanamu si kweli. Katika macho ya imani wanatumia zile ishara kuimarisha imani yao. Ishara ya msalaba! Mapicha yao kanisani vyote vinawaelekeza kuabudu Utatu Mtakatifu.
Kuna watu na makanisa wanathamini fedha na vitu vya anasa na starehe. Hawa ndo mngewafikiria kama waabudio masanamu!
 
Kanisa la Mungu ni lipi? Kwa hbr ya upotofu, wakati katoliki imepotoka kwa asilimia 95%, Kakobe amepotoka kwa 50% ana nafuu japo wote ni wakosefu.
MUNGU ni nani?
Mtu ni nani?
Dini ni nini?
Kanisa ni nini?
Ukatoliki ni nini?
Kupotoka ni nini?
Nani anajua fulani kapotoka fulani yupo sawa?
Naomba majibu
 
Katoliki siyo kanisa, ni dhehebu lililohusika kupotoa kanisa la Yesu. Mathayo 16:17-18. Kujiita kanisa, ni kujifungamanisha na Mungu wkt mmetangaza kumwasi.

Mt 15:8-9 SUV
Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.
Dhehebu ni nyie mliotoka kwenye uasi wa Luther 1517. Kanisa lilikuwa ni moja tu aliloacha Yesu chini ya Petro.
 
Dah! kubabake hii ilikuwa ID yangu ya kwanza kabisa JF badae nikaitelekeza 😀😀😀.
 
Hicho kitabu unatakiwa ukisome ukiwa umetuliza sana akili. Na ukisome na vitabu au vifungu vingine alafu uje kwenye uhalisia pengine utaweza kuelewa zaidi!
Siku ukijua maana halisi ya Sanamu kuwa ni ishara au taswira au hisia au alama au kitu chochote kinachochukua nafasi kwenye mawazo na maisha yetu hakika utajua kuwa sanamu na ibada ya Sanamu inayokatazwa ni ipi.
Fedha ni Sanamu
Simu yako ni Sanamu
Nyumba yako ni Sanamu
Gari lako ni Sanamu
Picha za ni Sanamu
Nguo zako ni Sanamu
Samani zako za ndani zote ni Sanamu!
Tamaa... Dharau... Kiburi... Majivuno... Ufisadi... vyote hivyo ni sanamu
Tamaa, urahibu uliopitiliza wa vitu hivyo na vikakufanya umsahau MUNGU wako hiyo ndo inakua ibada kamili ya masanamu.

Hao wakatoliki mnadai wanaabudu Sanamu si kweli. Katika macho ya imani wanatumia zile ishara kuimarisha imani yao. Ishara ya msalaba! Mapicha yao kanisani vyote vinawaelekeza kuabudu Utatu Mtakatifu.
Kuna watu na makanisa wanathamini fedha na vitu vya anasa na starehe. Hawa ndo mngewafikiria kama waabudio masanamu!
Mkuu hakika umeshuka kisawasawa!
 
Hakuna mkatoliki aliyesomea biblia, wamesoma canon law tu, wanatumikia taifa la rumi chini ya taasisi yao ya Vatican
Unaongea utadhani unajua lolote. Cannon law msingi wake ni bibilia. Alafu sisi kila kitu katika ibada msingi wake ni bibilia. Alafu we kiazi kasome historia ya bibilia, hujui kitu unaharisha tu. Jipe muda wa kutafiti sio kuropoka tu kwa akili za kuambiwa
 
hakuna dhehebu nnalolichukia kama waroma...na hayo madude wanayaabudu na kwenda kinyume na amri za Mungu.
imeandikwa usijifanyie sanamu ya kuchonga wala kitu chochote kilicho mfano mbinguni, baharini, nchi kavu etc... na kukiabudu.
lakini hawa ndo kwanza ukiingia unakuta kila kona wamechonga masanamu ya maria mtakatifu... masanamu ya Yesu... hivi mliwah kuwaona? nyie ndio kwanza mmekazana na rozari mnabusu na zina sanamu ya Yesu...ni wazima nyie?
mnachefua.
Usichokiamini Kinakuchefua vipi.
 
hakuna dhehebu nnalolichukia kama waroma...na hayo madude wanayaabudu na kwenda kinyume na amri za Mungu.
imeandikwa usijifanyie sanamu ya kuchonga wala kitu chochote kilicho mfano mbinguni, baharini, nchi kavu etc... na kukiabudu.
lakini hawa ndo kwanza ukiingia unakuta kila kona wamechonga masanamu ya maria mtakatifu... masanamu ya Yesu... hivi mliwah kuwaona? nyie ndio kwanza mmekazana na rozari mnabusu na zina sanamu ya Yesu...ni wazima nyie?
mnachefua.
Unawashwa, hakuna dhehebu linaitwa roma kwanza, unatuchefua wewe usie na akili wala lolote ulijualo, sanamu ni zetu, hazikuhusu, na hatuzitoi kamwe. Chukia upasuke au ufe kabisa.
 
Hata wanaoabudu ng'ombe Mungu ameruhusu wawepo?
Upo sahihi.

Maisha yangu yote ndani ya Kanisa Katoliki sijawahi kumsikia kiongozi yeyote wa Kanisa akihubiri kulisema vibaya kanisa lolote au Uislam au dini yeyote.

Mimi ninachoamini ni kwamba kila ambaye yupo hapa Duniani ni kwa sababu Mungu ameruhusu. Imani yoyote ambayo ipo hapa Duniani naamini Mungu ameruhusu. Asipotaka, hawezi kushindwa kuifuta.

Wakati yetu akiwa na mitume wake, wapo mitume waliomlalamikia Yesu kuwa kuna watu wengine ambao siyo.miongoni mwao, nao wanahubiri habari ya Mungu na habari zake. Lakini siyo Yesu aliwakanya na kusema kuwa kama kuna yeyote ananena neno la Mungu, hata kama hayupo nao, basi yupo upande wao. Lile ni fundisho kubwa sana.

Muislam anaposema wizi ni dhambi, watu msiibe. Anaposema hivyo, hawezi kuwa adui wa ukristo badala yake anazidi kueneza ujumbe wa Kristo. Yeyote anayeeneza chuki dhidi ya wanaoeneza ujumbe wa Mungu, bila ya kujali dhehebu au dini, anafanya kazi ya shetani. Azidi kuombewa.
 
Kuna wakati, nilipokuwa nimemaliza masomo yangu ya kidato cha 6, ikiwa ni pamoja na masomo ya biblia, nilialikwa kwenye mkutano wa wasabato. Nilienda huko nikiwa sijui kuwa ningepewa nafasi ya kuongea.

Cha ajabu, nikawekwa kama mtu wa kujibu maswali waliyokuwa wakiyaelekeza kwa Kanisa Katoliki. Nilijibu, kwa kadiri Roho alivyoniongoza.

Wote wakawa kimya kabisa. Nilishangaa mwishowe kufuatwa na viongozi wao kuwa eti wananiomba nijiunge nao na kisha niwe mchungaji wa Kanisa lao. Nilishangaa sana, nikawauliza kuwa tangu mwanzo wamelituhumu Kanisa Katoliki kuwa limepotoka, inakuwaje tena mimi Mkatoliki naweza kuwa kiongozi wao? Hawakuwa na jibu.

Nilivyomaliza masomo yangu ya shahada ya pili, nilipofika Dar, nikaalikwa na jamaa mmoja, aliwahi kuwa mtu mkubwa kwenye ngazi ya kitaifa kwenye Serikali. Yeye ni muislam. Nikaitikia mwaliko, nikaenda. Kufika huko nikashangaa walikuwa wamejaa wasomi wa dini ya Kiislam. Pekee yangu nilitengewe kiti, huku wao wote wakiwa wameketi kwenye majamvi. Nikaanza kuulizwa mambo ya Ukristo. Sikuwa nimejipanga kwa hilo. Lakini kwa utulivu niliwajibu kadiri nilivyoweza, hata wakaishiwa swali lolote.

Nilitafakari sana kwa nini niliitwa mimi, lakini baadaye nilikuja kutambua kuwa kuna ndugu zangu, nao walikuwa wasomi wazuri kwenye elimu ya Dunia, lakini hawakuwa vizuri sana kwenye mafundisho ya kiimani. Na kuna watu walitaka kuwabadilisha wale ndugu zangu kwenda uislam, na ikaelezwa kwamba kikwazo ilikuwa mimi. Hivyo wakinibadilisha mimi, basi wale wengine watanifuata.

Nashukuru mpaka leo wote tupo katika imani yetu.

Na neno la mwisho nililowaambia wale wasomi wa dini ya Kiislam ni kwamba sisi katika Ukristo tunaamini sana katika neema. Na neema hiyo inaweza kumwangukia yeyote, na ukashangaa aliyekuwa imamu au hata mpagani, siku nyingine anaweza kuja kuwa mkristo, tena kukuzidi hata wewe uliyedhania unaujua zaidi ukristo, akawa mwalimu wako.

Kwa hiyo usighadhabike Kanisa likinenewa vibaya. Kristo pamoja na ukuu wote, na mamlaka yote, alidhalilishwa, alitukanwa, alipigwa, alivuliwa nguo, alitemewa mate, hakuhangaika na waliomtendea hayo. Alipofufuka neno lake la kwanza lilikuwa Shalom, yaani muwe na amani, nimekamilisha, msiwe na mashaka. Mkristo unatakiwa kuyaiga maisha ya Kristo. Hatushindani katika kumjua au kumwabudu Mungu. Hata anayetusi, ujue Mungu ameruhusu, asipotaka, hawezi hata kuupanua mdomo wake.

Huo mkutano wa wasabato ulifanyika wapi?
Kanisani au nje ya kanisa?
Maswali uliyoulizwa na kuyajibu ni yapi ndugu
 
hakuna dhehebu nnalolichukia kama waroma...na hayo madude wanayaabudu na kwenda kinyume na amri za Mungu.
imeandikwa usijifanyie sanamu ya kuchonga wala kitu chochote kilicho mfano mbinguni, baharini, nchi kavu etc... na kukiabudu.
lakini hawa ndo kwanza ukiingia unakuta kila kona wamechonga masanamu ya maria mtakatifu... masanamu ya Yesu... hivi mliwah kuwaona? nyie ndio kwanza mmekazana na rozari mnabusu na zina sanamu ya Yesu...ni wazima nyie?
mnachefua.
Yaani kama unachukia Sanamu ya Yesu alafu unampenda Yesu wewe ni kilaza!
Bora anayetumia Sanamu ya Yesu na akawa na upendo kuliko aliyejichongea masanamu ya kiburi, dharau, chuki, fitina na yakamfanya aabudu fedha, magari, majengo, masengenyo, dharau, umimi na kujikwaza!
Someni Biblia zenu vizuri msiruke ruke kama bisi!
 
Mimi ni mkatoliki nisiyeunga mkono uwepo wa masanamu kanisani... Na ijumaa kuu huwa sijiangaishi kubusu msalaba. Sisali rozari kwakuwa naamini bikira Maria hawezi kusikia sala zangu...

Ntabakia mkatoliki kwa msimamo wangu.
Kukusaidia soma vizuri historia. Ingia pia kwenye hii link usome zaidi:
Watu mnataka mambo ya kiroho myafahamu kwa macho ya kimwili! Si rahisi hivyo! Go read your Bible!

 
Kujipa moyo tu. Haina maana kbs kusema ipo lakini haimaanishi kuabudiwa. Sasa ya nin mle ndani?!! Kubusu,kupiga ishara ya msalaba huku unaiangalia sanamu au picha nini maana yeke km sio kuabudu?! Heshima,mazoea,taratibu?!!
Mambo ya imani yana mengi ya kuhoji ila majibu yapo kwenye biblia
Go read the scriptures.
Ile kuchukia tu na kwadharau wengine ni ibada tosha ya masanamu! Mnajichongea masanamu na mnayaabudu bila kujijua!

 
Back
Top Bottom