Ukweli Mchungu: Hakuna biashara Serikali inaweza kufanya kwa ufanisi

Ukweli Mchungu: Hakuna biashara Serikali inaweza kufanya kwa ufanisi

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Nimepanda treni ya Kigoma - Dar mwaka 2021, na nilijisemea sitakuja kupanda tena kwa namna treni hii ilivyo na huduma mbovu na za aibu.

Ninatumia usafiri wa ndege Air Tanzania mara kwa mara kwa safari zangu za ndani ya Tanzania. Kuna kipindi hata namba zao za huduma kwa mteja hazipatikani, umekata ticket ya Dar ila unapiga no ya simu ya ofisi ya Dar haipatikani inabidi upige namba ya Arusha au Mwanza wakati wewe ofisi inayopaswa kukuhudumia ni ya Dar.

Nimetumia usafiri wa Tazara mara kadhaa miaka ya nyuma, kote huko huduma ni mbovu kiufupi zipo hoehahe.

Nimekuwa mtumiaji wa mabasi ya mwendokasi tangu yalipoanza na kusema kweli wakati tunakata ticket kielectronic kipindi cha Max Malipo wengi tuliojaaliwa kufika America na Ulaya tulianza kuufananisha mfumo huu wa usafiri na mfumo uliyopo maeneo ya Ulaya na Marekani. Ila alipoingia Jiwe muharibifu aliwaondoa Max Malipo na mwisho kukawa hakuna tofauti kati ya daladala na mabasi ya mwendokasi. Huo ukawa mwisho wangu kupanda magari ya mwendokasi.

Sasa tunaenda kwenye SGR. Walewale TRC wanaoendesha usafiri wa kwenda mwanza na kigoma ndo wanaenda kuendesha SGR. Itachakaa vibaya sana kwa huduma mbovu kabla hata ya miaka 5.

Ifike kipindi tuseme ukweli, serikali zetu Afrika hasa Tanzania haziwezi kufanya biashara. Masuala ya biashara wawaachie tu sekta binafsi ambao wao kutokana na kuwa na akili ya kupata faida kulingana na ubora wa huduma wataweza kuendesha hizi sekta zetu kwa faida na pia kwa kuzingatia ubora wa huduma.

Sekta za huduma za biashara serikali iachane nazo tu, hatuziwezi. Serikali hawajali ubora wa huduma, hawajali maintenance and repair, wao wanajali tu kuingiza pesa na watu kupata mishahara na kupiga.
 
Kwa namna serikali inavyohangaika na huu mradi wa SGR, hiyo siku utakapokamilika naamini itakuwa ni sherehe, sidhani kama watakuja kuuchezea huko mbele ya safari.

Muhimu ni kujipanga tu, ufuatiliaji wa reli na mabehewa yake uwe wa karibu, pawepo na vituo vya ukaguzi kila baada ya mwendo fulani, 24 hrs, ikibidi waajiriwe watu wa kufuatilia reli na vifaa vyake, ili kuifanya idumu.

Wasiwasi wangu sekta binafsi kupewa huo mradi wanaweza kuweka viwango vikubwa vya nauli, ambavyo mtanzania wa kawaida atashindwa kuvimudu, matokeo yake hiyo reli itakuwa ya wachache wanaojimudu kiuchumi, hivyo kutotimiza lengo la kuanzishwa kwake.

Binafsi ningependa viwango vya nauli viwe vya kati, sio juu sana au chini sana, vinavyoeleweka kwa wengi, ili kutimiza lengo la kupunguza adha ya usafiri kwa wale wanaoenda mikoa ya mbali hasa Mwanza na Kagera.

NB.
Kama hauuamini uwezo wa watu wako, ni vyema ukawapa wazungu na serikali yote waiendeshe kabisa, kuliko kutoa vitu nusu nusu inakuwa haina maana, hakuna kitu kibaya kisaikolojia kama kujidharau, hii nayo ni mental slavery of a certain kind.
 
Yale yale.
Kuwa Serikali za Waafrika haziwezi kufanya biashara.

Mabeberu wamo Kazini. Wanataka turudi kuuule, yaani Serikali zinapewa mikopo, wanawezeshwa, wanatumia nguvu za dola, kama vile kuwahamisha watu bila malipo stahiki na kutunga sheria zinazoipa nguvu "Shirika"....

Uwongo unatengenezwa, kuwa mashirika yanashindwa kuleta faida na hivyo basi yauzwe kwa mabeberu-kumbuka kuna kishinikizo cha kulipa deni ambalo riba yake inaendelea kupanda na kufanya deni liwe gumu kulipa.

Kinafuatia na kuuzWa Shirika kwa bei ya chini kwa kigezo kuwa wao "mabeberu" wanarithi deni, pamoja na kutaka/kuomba msamaha wa kodi/tozo n.k kwa miaka ambayo wanakuwa wanalipa deni au mpaka pale wakianza kupata faida. Wakati huo wanachagua wapi wanaweza kupata faida, kwa mfano wanaweza sema wao watakuwa wanakatisha tiketi, wanalisha wasafiri n.k watauza majengo n.k huku Serikali ikiendelea kuyatengeneza/maintanance vifaa hapa kama mabehewa na reli

yaani ni mchezo mchafu. Kwa mgongo wa mwananchi.

Ni Uwongo mtupu kuwa Serikali, hususani za Waafrika haziwezi kufanya biashara kifanisi.

Tutapinga uwongo kama huu. Nani kasema vita ya uchumi viliisha baada Jiwe kuondoka!!!

ALUTA CONTINUA
 
Nimepanda treni ya Kigoma - Dar mwaka 2021, na nilijisemea sitakuja kupanda tena kwa namna treni hii ilivyo na huduma mbovu na za aibu...

Ukitaka kujua huko serekalini kumejaa uozo, utakuta wakaguzi wa serikali kwenye huduma za jamii, mfano shule, hospitali nk wanakomalia huduma ziwe na kila kitu kwenye biashara za watu binafsi na penalti juu, lakini ingia kwenye hospitali au shule za serikali, nyingine hata choo hakuna na huduma haifungwi!

Wakati magufuli anajitapa kujenga SGR nilisema nitampima kwenye huduma ya mwendo kasi, maana wakati anaingia madarakani ndio huo usafiri ulikuwa umeanza. Nilichokiona nilijua fika hata mradi wa SGR itakuwa ni uchafu kama uchafu mwingine.
 
Mkuu inapaswa ujibu hoja,tueleze ni mradi gani wa serikali ambao unaendeshwa kwa ufanisi!
 
Yale yale.
Kuwa Serikali za Waafrika haziwezi kufanya biashara.

...Mabeberu wamo Kazini. Wanataka turudi kuuule, yaani Serikali zinapewa mikopo, wanawezeshwa, wanatumia nguvu za dola, kama vile kuwahamisha watu bila malipo stahiki na kutunga sheria zinazoipa nguvu "Shirika"...
Tueleze mradi gani wa serikali unaendeshwa kwa ufanisi? Umeshawai hata panda treni kutoka Dar kwenda kigoma au kigoma kwenda Dar?
 
Yale yale.
Kuwa Serikali za Waafrika haziwezi kufanya biashara.

...Mabeberu wamo Kazini. Wanataka turudi kuuule, yaani Serikali zinapewa mikopo, wanawezeshwa, wanatumia nguvu za dola, kama vile kuwahamisha watu bila malipo stahiki na kutunga sheria zinazoipa nguvu "Shirika"...

Mmhhh, yaani hata sielewi unaongea nini. Tuje kwenye mfano halisi wa mashirika ya umma mfano TTCL, shirika hili la simu lilishindwa kutoa huduma kwa ufanisi tena likiwa halina ushindani. Yamekuja makampuni ya simu tena kukiwa na ushindani, na yanapata faida kibao, huku yakifikisha huduma kila kona ya nchi.

Sasa hayo maelezo sijui wazungu sijui nini unayatoa wapi? Ni mzungu gani ana muda wa kuhangaika na watu tulioko kwenye hatua ya elimu ya kunawa mikono ukitoka chooni?
 
Mmhhh, yaani hata sielewi unaongea nini. Tuje kwenye mfano halisi wa mashirika ya umma mfano TTCL, shirika hili la simu lilishindwa kutoa huduma kwa ufanisi tena likiwa halina ushindani. Yamekuja makampuni ya simu tena kukiwa na ushindani, na yanapata faida kibao, huku yakifikisha huduma kila kona ya nchi.

Sasa hayo maelezo sijui wazungu sijui nini unayatoa wapi? Ni mzungu gani ana muda wa kuhangaika na watu tulioko kwenye hatua ya elimu ya kunawa mikono ukitoka chooni?
Hajielewi huyo
 
Nimepanda treni ya Kigoma - Dar mwaka 2021, na nilijisemea sitakuja kupanda tena kwa namna treni hii ilivyo na huduma mbovu na za aibu...
Wataalamu wa kuendesha STATE OWNERSHIP/ STATE OWNED ENTERPRISES / STATE COMPANIES hapa duniani ni CHINA asilimia 60%-70% ya makampuni ya China ni ya serikali na yanafanya vizuri ndani ya China na duniani kote.

Tanzania tukajifunze China kuendesha haya mashirika katika ubora au tuajiri wataalamu kutoka China watuendeshee haya mashirika yetu kwa miaka 10+
 
Mmhhh, yaani hata sielewi unaongea nini.
Umenielewa hutaki tu kukubali Ukweli.
Tuje kwenye mfano halisi wa mashirika ya umma mfano TTCL, shirika hili la simu lilishindwa kutoa huduma kwa ufanisi tena likiwa halina ushindani. Yamekuja makampuni ya simu tena kukiwa na ushindani, na yanapata faida kibao, huku yakifikisha huduma kila kona ya nchi.
Tunajua, walisema, Kuwa rushwa ilikithiri sana katika mashirika ya Umma na hiyo ilikuwa kati ya sababu kuu za Kushindwa kuyaendeleza. Kikubwa ni Waajiriwa, pamoja na wakuu wa hayo makampuni wanaojiona hawashikiki(hakuna accountability) akiharibu anapelekwa kwingine badala ya kushitakiwa kwa kufilisi.
Sasa hayo maelezo sijui wazungu sijui nini unayatoa wapi? Ni mzungu gani ana muda wa kuhangaika na watu tulioko kwenye hatua ya elimu ya kunawa mikono ukitoka chooni?
Sasa na wewe tindo, sikusema sijui wazungu, nawajua, ni wezi tu.
Na sio lazima mabeberu wawe ni wazungu.
Hiyo elimu unayodai, mpaka leo hii ukienda nchi za ngambo unakutaka kuna notisi chooni inayosema "wanawe" mikono kabla ya kurudi kazini....wewe unafikiri hilo ni kwanini?

Hulka za kibinadamu lakini mnadai ni waafrika tu ndio wanaojamba na kunya!
 
Tueleze mradi gani wa serikali unaendeshwa kwa ufanisi? Umeshawai hata panda treni kutoka Dar kwenda kigoma au kigoma kwenda Dar?
Kwani kupanda treni ndio kujua nani wanapanga kuja kutuhada???
Hapana. Hadaa za wazungu zinajulikana. Sihitaji kupanda treni kuelewa unataka kuweka taswira gani.

Hayo ulioeleza ni mbinu moja yapo yakujaza akili za watu kuwa shirika halifanyi vizuri. Mbadala wake ni nini? Ati kupanda treni.
 
Hasira za Ukweli hizo Naelewa Wazungu(mabeberu) ni wezi tu.

Ww utakuwa ni mzee lazima. Wazee ndio wana akili hizi. Mkoloni kaondoka 60yrs ago, ni kipi bado kinasimamiwa na mzungu hapa kwetu. Miradi mingi mikubwa sasa hivi tunawapa wachina. Wazungu wanatokea wapi hapa kwetu? Kama ni uhitaji sisi ndio tunawaomba misaada wao.

Tutajie shughuli yoyote ambayo wazungu wametuzuia kufanya, au raslimali yoyote wanayochukua bila kuingia mikataba na viongozi wetu. Ingekuwa wametuwekea vikwazo vya kiuchumi hapo ungekuwa na hoja.
 
Ww utakuwa ni mzee lazima. Wazee ndio wana akili hizi. Mkoloni kaondoka 60yrs ago, ni kipi bado kinasimamiwa na mzungu hapa kwetu. Miradi mingi mikubwa sasa hivi tunawapa wachina. Wazungu wanatokea wapi hapa kwetu? Kama ni uhitaji sisi ndio tunawaomba misaada wao.

Tutajie shughuli yoyote ambayo wazungu wametuzuia kufanya, au raslimali yoyote wanayochukua bila kuingia mikataba na viongozi wetu. Ingekuwa wametuwekea vikwazo vya kiuchumi hapo ungekuwa na hoja.
Nimesema ni wezi tu! ndio hoja yenyewe, nimesema wanatuhadaa tu ndio hoja yenyewe.
Sasa huo mbadala uwe vipi?
Auziwe GSM??? au unataka kusema nini.
 
Back
Top Bottom