Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Kinana ni mtendaji makini zaidi ya makatibu wakuu wote wa vyama njaa akina slaa na utendaji wake unajulikana ndiyo maana chadema wanahaha na mambo ya meno ya tembo hivi ukiwa na basi ukapakia abilia akiwa na bangi kwenye begi lake ile bangi ikikamatwa wewe mwenye gari unahusika vipi? Mbona kuna viongozi wa upinzani ni wachafu wauaji lakini mnawasifia kila siku mfano mbowe alihusika na mauaji ya chacha wangwe na legia mtema na amezaa na esta matika lakini munamuna mungu wenu kwa sababu ya ujinga na uelewa wenu unao lingana na kuku wa kienyeji! Pole sana kinana atawanyosha mwaka huu hadi mkome.
 
Tunakushukuru mleta uzi kwa uzi huu nadhani ili upigane vita kwa uhakika ni lazima ujue uwezo na udhaifu wa adui yako kwa haya tunazidi kumjua kinana na kubuni mbinu mbadala za kupambana nae. Pamoja na sifa zote lakini bado kitu kimoja umeacha kuzungumza kuhusu udhaifu wa kinana. Hata hivyo pamoja na sifa zote ulizompamba lazima pia ukubali kwamba saliweza kufanikiwa kisiasa katika kipindi ambacho Watanzania wengi tulikuwa bado tumelala usingizi kwenye siasa za nche hii. Kumbuka kuwa kwa sasa kumekuwa na mabadiliko makubwa sana kuhusu siasa za nchi hii ambazo kwa vyovyote vile Kinana si mzoefu wa siasa za sasa. Lakini pengine kubawa zaidi ni kwamba, tofauti na miaka ya nyuma kizazi hiki ni cha tofauti sana kukubali siasa za kina Kinana. Hiki ni Kizazi ambacho mi nakiita Critical generation. Kinana hana uzoefu na kizazi hiki na nina uhakika kwamba anafahamu kuwa siasa za sasa ni changamoto kubwa kwa sasa. Vijana wanakwambia fashion ya sasa ya siasa ni CDM. M4C ndio story ya mjini ndio maana kwenye mikutano yake anaishia kubeba wamama kwenye malory baada ya kuwalipa elfu mbilimbili. Na hili halihitaji Ph.D Fanya personal observation utana ni akina nani wanahudhuria mikutano ya CCM na CDM. Mi nakaa na vijana vijiweni vyuoni wanakwambia CCM ya sasa unaona aibu kuizungumzia mbele ya watu au kuhudhuria mkutano wao labda unywe kidogo uende kama mwenda wazimu. Kwa mazingira kama haya Kinana ana kazi ya ziada kuivusha CCM 2015 na anaweza akajikuta anafail zaidi ya mtangulizi wake. Unajua CCM walizoea vyama vya msimu, Sasa CDM imewashika pabaya ndio maana mpaka wanachanganyikiwa wabunge wao wanaomba maandamano yafutwe, na wanasahau kama waliyaweka wao kikatiba kama haki, haya yote ni kauli za mfa maji, wanatapatapa CCM hoi. Nawasilisha
Kinana anakubalika mijini na vijijini. Waache chadema wahangaike na mijini ambako hata huko pia hawakubaliki
 
Hii thread ni makala ya Absalomu Kibanda ambayo ilishaprove kinyume na maudhui yake. Kwa muda aliokaa Kinana na cheo hicho sijaona lolote la maana mpaka sasa alilofanya zaidi ya Mukama. Kama ni kuzomewa wote wamezomewa na kama ni kuhonga wapinzani uchwara ili wajiunge na kununua kadi Kinana vivyo hivyo na mengine.... Nami na nasema ni mpuuzi tu anayeeendelea kuamini maudhui ya makala hii ya zamani, kwa wakati huu tulio nao.
Utakuja kuona kazi ya kinana baada ya uchaguzi mkuu wa 2015
 
Yaliondikwa yote hakuna asiyeyajua, ni sawa na mtu ambaye tokea shule ya msingi hadi anamaliza PHD amekua anafauru kwa marks za juu and may be amekua akirushwa hata baadhi ya madarasa (kama Dr. Daudi Balali) lakini linapokuja suala la uzalendo kwa nchi yake amekua akitumia akili yake kuangamiza nchi na vizazi vijavyo, hapa hatutaki kusikia uzuri wa historia ya mtu, tunaangali utendaji wa mtu na sio vinginevyo! Kajipange upya, twambie aliiba na kuua Tembo wetu au hakuua, hilo tu.
 
...ndiye aliyemuongoza Benjamin Mkapa katika mapambano makali ya kisiasa mwaka 1995, zama Augustine Mrema alipokuwa tishio la kwanza la kweli dhidi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu.

Je mahusiano yake na Gen. Imran Husein Kombe mbona huweki...?????
 
Yaani hii makala imejaa upotoshaji hebu someni historia ya Kinana:

Born in the Arusha region in October 1951, Kinana did his primary and secondary studies in that city, before attending the Old Moshi Secondary School.

He was one of those responsible for the TANU party youth organization in the Korogwe district between 1971 and 1972, before following the teachings of the Kivukoni Ideological College in 1973.

From 1974 to 1985, he undertook a long career as a political commissar in several military schools, and from 1984 to 1985, at the 20th division of the Tanzania Peoples Defence Force (TPDF).

In the meantime, in 1984, he had graduated from the university of Ljubljana in Yugoslavia.
 
Kinana ni mwanajeshi amelitumikia jeshi kwa kipindi kirefu kwa cheo cha kanali...si mtu wa kupuuzwa

Mimi Nampuuza, kwa kuwa hajajibu shutuma na wala serikali haijamwomba mtoa hoja atoe ushahidi. Tumwamini nani hapo bila ushahidi?
 
Hii imefanana na makala ya Kibanda ambayo niliwahi kuisoma kwenye gazeti la Tanzania Daima

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hakuna la maana hapa....kama angemudu kusafisha mafisadi wote ndani ya chama ningeelewa, lakini katu hawezi kuthubutu...anaetetea uovu nae ni mwovu tu. Pia si ana tuhuma za ujangili, kwahiyo uadilifu wake una mashaka makubwa. Labda awe ni hodari wa mikakati/mbinu ovu kwa ajili ya kuua upinzani lakini si kwa hoja.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa chama cha mapinduzi ccm ni chama ambcho kimeundwa na magenge ya wezi, majambazi wahujumu uchumi na watesji. Hii ndio taswiras kama ulikuwa haujui mtanzaqnia mwenzangu.
 
ziara yake moja tu ya mkoa wa Morogoro imezua tafrani nchi nzima

Ziara au alikuwa kwenye fiesta la chama kuweni wakweli jamani mkiitisha mikutano basi booking za maroli na mabasi zote zinafutwa ili myatumie kusomba watu na mpunga mnawapikia..kuweni wakweli acheni kujidanganya angekuwa mtu makini msingetumia mbinu za kusomba watu kwenye mikutano yenu ikiongozwa na kinana mwenyewe
 
Kinana anakubalika mijini na vijijini. Waache chadema wahangaike na mijini ambako hata huko pia hawakubaliki
Mkuu naona wewe huna hoja ila unazungumza ushabiki lakini labda nisijibu huenda ukweli unaujua au basi umepita kwa bahati mbaya hapa jamvini wewe hujui siasa za Nchi hii. Ukitaka kujua kama CDM wanakubalika au hawakubaliki nenda kawaulize akina kinana, Kikwete, Nape, wasira na hata Makinda watakwambia.
 
hii profile yako naloliga hurita inanifanya nisiamini sana uliyoandika, lakini pia mtu makini kama unavyotuaminisha asingetumia zaidi ya nusu saa kuiongerea cdm morogoro kana kwamba ndicho jk alichomuwekea hapo. Siasa zinabadilika na hata Mzee Makamba alikuwa luteni lakini wanasema ndiye kadhoofisha chama na hata hizo siku unazoongelea sijui mwaka 1972 akina Mnyika, Lissu, Zitto na hata Filikunjombe walikuwa hawajainuka.
Kajipange upya na kama ni mchango wake upo basi historia itautendea haki wala usiwe na hofu
Join Date : 22nd April 2013

Posts : 84

Rep Power : 318
Likes Received10
Likes Given21
 
Ni mtu asiyejali au mpuuzi asiyezijua vyema siasa za Tanzania anayeweza akasimama na kuudharau uteuzi uliofanywa na Rais Kikwete ambaye baada ya kushindwa mara kadhaa hatimaye amefanikiwa kumshawishi, mmoja wa wanasiasa makini na wakongwe, mtumishi wa umma wa muda mrefu, mwanadiplomasia na Kanali Mstaafu wa Jeshi, Abdulrahaman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM.

Kwa muktadha huo na kwa kuzingatia nafasi kuu ya utendaji aliyopewa, nitazungumzia kwa sehemu tu wasifu wa Kinana, mtu ambaye naamini anapaswa kuangaliwa kwa jicho la karibu na wakati mwingine kudhibitiwa ili kasi yake ya kukijenga chama alichopewa dhamana ya kukinusuru isije ikasababisha kuyumba kama si mauti ya kisiasa kwa baadhi ya vyama vya upinzani.

Ni wazi kwamba, kuteuliwa kwa Kinana kuwa Mtendaji Mkuu wa CCM Taifa, akirithi mikoba iliyomshinda, Wilson Mukama, kumetutia ganzi baadhi yetu ambao kwa muda mrefu tumekuwa ‘mashabiki’ au waumini wa kuchagiza kwa njia ya kalamu na wakati mwingine katika mijadala ya wazi kwamba, taifa lilikuwa na haja ya kutafuta mabadiliko ya uongozi kutoka nje ya chama tawala.

Sitaki kuwa miongoni mwa wapenda mabadiliko ambao kwa njia za kujifariji au za kujipa matumaini hewa wameingia katika mkumbo wa jumla jumla wa kumbeza Kinana kwa namna wanayotaka kuuaminisha umma wa Watanzania kwamba, mtu huyo anaweza akasukumwa kirahisi kwa namna ile ile ilivyopata kuwa kwa watangulizi wake kadhaa waliopata kushika wadhifa huo.

siku zote nilikuwa nikiamini kwamba, ukatibu mkuu kwa Kinana ilikuwa ni silaha moja ya maangamizi kwa vyama vya upinzani ambavyo naamini vinapaswa kuendelea kupewa fursa ya kuaminiwa na kukomaa.

Kinana anaendelea kubakia kuwa tishio kubwa kwa ustawi wa upinzani ambao ni rutuba muhimu kwa maendeleo ya demokrasia na misingi ya utawala bora.

Hili ndilo ambalo naamini wapinzani wanapaswa kulitazama na kulitafakari nyakati hizi wanapoendesha harakati zao za kukabiliana na maguvu ya dola na haya mapya ya hoja ambazo aghalab zitaongozwa na Kinana nyakati hizi taifa linapojiandaa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa miaka mitatu ijayo.

Haitoshi kwa kina Freeman Mbowe, Profesa Ibrahim Lipumba, James Mbatia, Dk. Willibrod Slaa na Zitto Kabwe kumbeza Kinana na timu ya watendaji wake eti kwa hoja nyepesi na zisizo na mashiko za ufisadi au uchafu wa jumla jumla wa CCM.

Wapinzani na wachambuzi wa mambo wanapaswa kujua na kutambua kwamba, Kinana ni mwanasiasa wa vitendo, msomaji mzuri wa vitabu, ripoti, taarifa, magazeti, msikilizaji na msikivu mzuri wa mambo mepesi na mazito kuliko alivyokuwa ‘utopia’ Mukama anayeamini na kuzitetea nadharia zisizotekelezeka.

Si hilo tu, wapinzani wanapaswa kutambua kwamba, historia yake ya uaskari alioutumikia miaka 20 hadi mwaka 1972 akifikia cheo halisi cha jeshi cha Kanali ikimhusisha na mafunzo mahususi ya kimkakati ni sehemu ya mambo ambayo yanatawala nidhamu ya kazi ya aina ya kipekee iliyomfanya Kinana akawa jemedari wa mapambano ya CCM tangu mwaka 1995 hadi leo.

Wachambuzi wa mambo, nikiwamo mimi mwenyewe ambao siku zote tumekuwa tukiiona CCM kuwa chama kinachokufa kwa maana ya kuchungulia kaburi, tunapaswa kuanza kutafakari upya mawazo yetu hayo, nyakati hizi Kinana alipopewa dhamana ya kuwa mtendaji wake mkuu.

Tutakuwa wendawazimu iwapo tutamlinganisha Kinana na Mukama na kusahau kwamba huyu aliye kilingeni leo ndiye aliyemuongoza Benjamin Mkapa katika mapambano makali ya kisiasa mwaka 1995, zama Augustine Mrema alipokuwa tishio la kwanza la kweli dhidi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu.

Alikuwa ni Kinana aliyefanya kazi kubwa katika kipindi chote cha kampeni akiratibu na kuongoza kampeni zote za Mkapa zilizomjumuisha pia Mwalimu Nyerere katika mazingira ambayo wengi walikuwa wakiamini CCM ilikuwa katika mwelekeo wa anguko la kihistoria.

Kinana ambaye kabla ya mwaka 1995 alikuwa tayari amepata kuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Waziri wa Ulinzi alitumia vyema mbinu za medani na zile za kidemokrasia na kidiplomasia kumjengea uhalali Mkapa ambaye wakati huo alikuwa mwanasiasa ambaye hakuwa akijulikana sana.

Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, siku chache tu baada ya kuingia Ikulu kwa mara ya kwanza mwaka 1995, kwa sababu ama ya ulevi wa madaraka au kwa kutingwa na kazi za kimamlaka, Mkapa alisahau kazi kubwa aliyofanyiwa na Kinana.

Ni katika kipindi hicho cha kati ya mwaka 1995 na 2000 ndipo nilipokutana kwa mara ya kwanza na mara kadhaa na Kinana nyumbani kwake Masaki, jijini Dar es Salaam ambako nilipata fursa ya kumsikiliza na kuufahamu upeo mkubwa wa kuona mambo aliokuwa nao mwanasiasa huyo.

Tangu wakati huo hadi wakati wa kampeni za mwisho za mwaka 2010, niliendelea kukutana kwa nyakati fupi fupi na Kinana na mara kadhaa nikawa mtu wa kufuatilia na kuzisikiliza kwa makini, habari zake kutoka ama kwa marafiki au maadui zake wa kisiasa.

Sikushangazwa hata kidogo niliposikia tena kwamba, Mkapa alilazimika kumuangukia tena Kinana na kumuomba aongoze tena kampeni zake mwaka 2000 kabla ya Kikwete naye hajafanya kile alichofanya mtangulizi wake alipomuomba mwanasiasa huyo adhibiti joto la kiti cha urais mwaka 2010.

Uwezo wake mkubwa wa kisiasa, umakini wake na upeo mkubwa alionao katika kuona na kuchambua masuala ya siasa, uchumi na jamii ndivyo vitu ambavyo kwanza kwa nyakati tofauti vimepata kumfanya Kinana awe Mbunge wa Jimbo la Arusha kwa miaka 10, Mbunge wa Afrika Mashariki na Spika wa Bunge hilo.

Si ajabu hata kidogo kwamba, hata kabla ya kufikia huko, ni Kinana huyo huyo ambaye alipata kuwa Mwakilishi wa Kidiplomasia wa Rais wa Tanzania katika eneo la Maziwa Makuu na kabla ya hapo akiwa Mwenyekiti wa Mawaziri wa Ulinzi wa Nchi za Kusini Mwa Afrika (SADC) zama akiwa Waziri wa Ulinzi katika Serikali ya Awamu ya Pili iliyokuwa ikiongozwa Rais Ali Hassan Mwinyi.

Uzoefu wake katika siasa za kiraia unaanzia mwaka 1972 wakati alipostaafu jeshi akiwa Kanali baada ya kulitumikia kwa miaka 20 ndiyo ambao amekuwa akiutumia kama silaha kubwa ya kukijua chama chake na pengine kumfanya awe mmoja kati ya watu wachache ambao wamepata kuwafanyia kazi marais wote wane wa Tanzania.

Anarithi mikoba ya Mukama akiwa mmoja wa wanasiasa wachache wa CCM wa rika ile ile la kina Kikwete ambaye alilikimbia na kulikana kundi la mtandao mwaka 2005 ambalo baadhi yetu tunaamini kuwa, ndilo lilisababisha kuzaliwa kwa siasa mpya za kupakana matope, kuzushiana na kuhujumiana ndani na nje ya CCM.

Lakini pengine kubwa katika yote hayo anaingia madarakani huku akiwa na hazina ya uzoefu mkubwa wa kuongoza mapambano dhidi ya vyama vya upinzani na kushinda katika mazingira ambayo aghalab yamekuwa yakiacha vidonda visivyopona kwa wapinzani tangu mwaka 1995. Huyu si mtu wa kumpuuza au kumbeza hata kidogo.
umechambua vizuri mno nami naafikiana nawe kuwa Kinana ni mtu wa kimkakati zaidi na haijalishi kuwa mkakati huo ni halali au ni haramu.
Jambo moja ambalo umesahau ni kuwa kwa sasa kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya CCM ukiwajumuisha watu ambao hawakuwepo 1995 na 2000,hili si jambo jepesi.
Pili ni kuwa kuna ujasiri mkubwa wa watu kuzungumza kuhusu viongozi na hata hili la meno ya tembo si ajabu nimeibuliwa na watu walioko ndani ya CCM.
Hatari ninayo iona ni kuwa anaweza akatumia mkakati uliopitwa na wakati na akatuingiza katika machafuko.
Nguvu kubwa iliyotumika kumtetea na ujanja wa kukwepa kuchukua ushahidi kutoka kwa wapinzani unanitia mashaka,nahisi kuna dalili ya ukweli katika hili.
 
Ukweli ukikuuma unaishia kutukana tu

siku zote mpaka nchi inaingia kwenye UFISADI na ujangili wa hali ya juu alikuwa wapi? Tatizo la CCM hawaangali hali halisi ya Watz kwa sasa tunakabiliwa na nini,
Ushindi wa CCM siku zote tangu kuingia mageuzi huwa ni wa Tume na wala si wa wapiga kura,
Hakuna cha Kinana wala nini ni Tume tu ndio inawaweka CCM madarakani
 
Ndio nyinyi wachumia tumbo mliotumwa kumsafisha???!!! Mbona hauzungumzii ufisadi na ujangiri wake kuanzia mashine za hospital,TALL na uchafu mwingine kibao ikiwemo meno ya tembo???!!

Endeleeni na ukuwadi wa mafisadi,sijui wajukuu na watukuu wenu watarithi mini zaidi ya historia na hasira dhidi ya waangamizi wa maslahi ya taifa!!!
 
Back
Top Bottom