Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Watanzania wana akili nyepesi sana!

Binafsi naamini ni tatizo la upungufu wa mlo kamili ndio chanzo cha upeo mdogo wa watanzania wengi, mfano ni mleta mada.

Kwa akili ya kawaida kabisa, utagundua huyo mnafiki Msigwa kushadadia suala la Kinana kuwa ana husika na ujangili ni kutaka umaarufu wa bei rahisi.

Wenzake wakina Zitto na makamanda wengine walikuwa wakiibua masuala ya siri mno ya kulihujumu taifa yanayo fanywa na watendaji wasio waadilifu. Ndio maana mchango wa Zitto katika kukomboa raslimali za nchi hauwezi kubezwa na yeyote yule.

Hili suala la Kinana ni la tangu 2008 huko, na INTERPOL walichunguza wakabaini kuwa Kinana ahusiki, sasa kelele za Msigwa za nini hapa? Kwenye ili Msigwa asahau kuwa atatambulika miongoni mwa wabunge machachali kwenye medani za siasa hapa nchini.

Inabidi watanzania mshtuke nia ya huyu Msigwa kupeleka hotuba iliyojaa masimango, kashfa na uongo wa kupitiliza pale bungeni, nia kubwa ya Msigwa ni kumchafua Katibu Mkuu wa CCM taifa, wala hakuwa na maslahi mengine zaidi ya ili.

Ila kama ilivyo ada, njia ya muongo ni fupi, watanzania wazalendo na wafatiliaji wameujua ukweli, na malengo ya Msigwa hayajatimia katika juhudi zake za kumchafua Kinana.

Nikweli kabisa watanzania wana akili nyepesi ya kuelewa mambo ndo maana wanatoa malalamiko yao na hawatakubali kuona rasilimali zao zikichotwa na vigogo wachache. Tabia ya jangiri akikosa mnyama huanza ujambazi. Tembo wamesalia 70 elfu tu na kila siku majangiri hukwapua tembo 30 piga hesabu mwenyewe zimebaki siku ngapi waanze kututeka sisi wenyewe?
 
pale serikali? Kabila gani wewe?HUo uzushi utawafikisha wapi CDM? hata kama kungekuwa na ukweli, binafsi naona bora ujangili kuliko UGAIDi

Ukabila hauna nafasi hapa,hoja ni UJANGIRI wa ngugu zako unaliua taifa
 
ngonjera mingi bila kutaja meno ya tembo wetu hainogi. kajipange upya.
 
JANGILI la kisomali limeingia hadi jeshini na kupata cheo cha Kanali. Duh, TZ zaid ya uijuwavyo.
 
Kinana ni mwanajeshi amelitumikia jeshi kwa kipindi kirefu kwa cheo cha kanali...si mtu wa kupuuzwa
Kwa hiyo mtu akilitumikia jeshi kwa kipindi kirefu kwa cheo cha kanali basi huyo mtu si wa kupuuzwa?, hivi nyie watu wanawatoa wapi? maana hamuwezi kabisa kujenga hoja, Binafsi ninachokihofia kwa huyo kinana ni tembo wetu tu, na wala si kingine, kasi ya jamaa kwenye ujangili inatisha, fikiria meli nzima imejaza meno ya tembo, ni tembo wangapi wameuawa?, ni meli ngapi zimepita bila kugundulika?, huyu jamaa ni hatari, hatareee!, weka mbali na tembo.
 
Tembo wanajuta kuzaliwa TZ ya kinana.
Mkuu umenikumbusha kuna thread moja ya picha ya tembo akijaribu kumdhuru jamaa kwenye gari, mwana JF mmoja Baba V, akachangia namna ya kujinasua pale ni kuchukua simu, kisha unazuga kama unampigia kinana, eti tembo lazima atatimua mbio, nilicheka sana.
 
issue ya tembo haiwezi kumrudisha kinana nyuma,ni bora mngeacha nayo tu,ni kama issue ya slaa kukwiba mke wa mtu haiwezi kumrudisha nyuma!thats just the politics of character assasination a.k.a. siasa za maji chuki yaliyo na taka
 
hAMNA HAYA magaidi nyie ambao Ulimboka na Kibanda hatawasahau milele na roho ya Mwangosi inawalilia, je roho ya Prof Mwaikusa na Kolimba ama kweli CCM ni Chama Cha MAGAIDDI YALIYOKWISHA THIBITISHWA

ficha aibu zenu, kaangalie vizuri ile video ya gaidi mkuu lwakatare ndio urudi hapa
 
ni kinana gani unae mzungumzia wewe....ni huyu wa magamba au yule wa tembo......
 
Kinana is simple by looking, but firm and hard working in serious issues
 
Back
Top Bottom