Uchaguzi 2020 Ukweli mchungu kwa Lissu, sio kila mtu anaweza kuwa Rais wa JMT

Uchaguzi 2020 Ukweli mchungu kwa Lissu, sio kila mtu anaweza kuwa Rais wa JMT

Ni hivi, mgombea wetu upinzani ni huyo huyo Lissu, hivyo vyombo vya dola vitake, visitake lakini habari ndio hiyo.
Sema mgombea wako sio wenu.Kifupi jiandae tu kisaikolojia Lisu ndani ya chadema hapitishwi.Mark my words
 
Hakuna mwenye uhakika na hilo.System ipi?Vyombo vya dola?Nafasi ya wananchi kuchagua viongozi wao iko wapi?Lolote linaweza kutokea,usiwe na uhakika sana
Mimi pia sina uhakika sana

faida za kutokukubalika na hivyo vyombo ulvovitaja i hope unazijua
 
Tatizo watu wa Lumumba hawaelewi kuwa urais ni taasisi. Vyombo vya ulinzi na usalama ni sehemu mojawapo ya vyombo vinavyotumiwa na taasisi hiyo. Havihusiki kikatiba ku-influence nani awe kiongozi wa taasisi hiyo. Wanaofanya hivyo ni wananchi kupitia sanduku la kura. Kwa hiyo, yeyote yule anayechaguliwa na watu ndiye anayekuwa rais na vyombo husika sharti vimtii. Kwa hiyo hakuna pingamizi lolote kikatiba kwa TL kuwa rais.
Soma post#25
 
Lisu akuna wakuweza kumzuia kugombea isipokua chama chake.
nani aljua ccm ingempitisha JPM na sio lowasa au membe?
tuelewane pale linapokuja swala la kiinchi lazima watu wenyeakili na walopewa mandates kusimama Ustawi wa nchi wafanye uhakiki hii aijalishi mgombea anatoka wapi.

Hao waliopewa mandate wamepewa na nani? Chaguzi zetu sasa hivi zimetawaliwa na ushenzi, ukatili na uhayawani wa wazi, hao waliopewa mandate inaonekana ndio hao wanaoagiza huo uchafu. Haiwezekani wenye mandate wapewe na hao hao wanaopaswa kushindana, kwa vyovyote watawabeba wanaowachagua ili waendelee kulinda maslahi yao binafsi.

Hao wenye mandate unaowasema, ni wahuni fulani wasioweza kujitegemea, hivyo wako sehemu wanamteua mtu atakayewapa ulaji. Hicho kikundi cha wahuni wanaojiita wenye mandate, ndio huingiza nchi kwenye machafuko kwa ajili ya maslahi yao. Fahamu ya kuwa ccm sio chama cha kizazi hiki, ndio maana kinatumia mabavu, ukatili na unyama, ili kuendelea kukaa madarakani kwa shuruti bila ridhaa ya wananchi walio wengi. Sasa hivi watu hawataki kujitokeza tena kupiga kura, kisa kuna wahuni fulani wanaojifanya wana mandate, kwa kulazimisha kukiweka madarakani chama kisichokubalika na kizazi hiki.
 
Mimi pia sina uhakika sana

faida za kutokukubalika na hivyo vyombo ulvovitaja i hope unazijua

Kutokubalika na “baadhi yawatu ndani ya vyombo vya dola”.Taarifa alizokuwa anapata naamini kuna watu ndani ya system wanampenda pia.Ideally,binadamu huwa Na wasiwasi na “kinachokuja “kuliko kile kilichopo.Hiyo ni hali ya kawaida.
 
Atagombea kama mgombea binafsi? Maana wamiliki wa CDM wanachaguo lao tayari, Nyalandu. Ni mtu ambaye wanaamini hatowasumbua kwenye kampeni financially

Wapiga kura hatumkubali Nyalandu. Hao wenye chama wanajua msimamo wetu, na mapendekezo yetu yako bayana kuwa, mgombea wetu ni Tundu Lissu fullstop.
 
Sema mgombea wako sio wenu.Kifupi jiandae tu kisaikolojia Lisu ndani ya chadema hapitishwi.Mark my words

Hatuna tatizo, apitishwe asipitishwe, huyo ndio chaguo letu wapiga kura tunaojitambua. Akipitishwa Mbowe, Nyalandu, sijui Msigwa nk, watakula jeuri yao. Akipitishwa Lissu, tutampigia kura hata mkiwa mmemfunga jela.
 
Wakuu nawasalimu,
naomba muelewe kitu kimoja kuwa sio kila mtu anaweza kuwa raisi wa JMT hili mliweke akilini. Kwa ufupi tuu hata kama Lissu akishinda uchaguzi na CCM kuamua kukubali kushindwa na ku backdown 'system haiwezi kumkubali Lissu abadani... vyovyote itavyokua.
hatuwezi kuongozwa na Raisi mbeambea, Rais asieweza kusimama peke yake katika maamuzi.
Unachosema akishinda mtampindua. Haitoshi kuna waliojaribu kumuua. Kwa hiyo mko radhi nchi iingie kwenye machafuko ili tu kama Lissu akishinda asitawale. Hapo mwisho ulipoandika "hatuwezi kuongozwa na Raisi mbeambea, Rais asieweza kusimama peke yake katika maamuzi" inaonyesha wazi humfahamu TL. Jiulize kwa nini walijaribu kumuua? Hivi kweli hiyo system haina kazi bali kufukuzana na mbea na asie na misimamo ya peke yake? Tafakari tena.
 
Imani hiyo anaweza kuwa nayo mganga tu.Unataka niamini bila facts zozote ulizoweka mezani.
Subiri facts Lisu anazo ndio maana anahaha mitandaoni wenzie hawako mitandaoni wako na wajumbe wafanya maamuzi ndani ya chadema yeye Yuko ulaya zake anajinadi mitandaoni kwetu sisi ambao sio chadema na hatuna maamuzi ndani ya Chadema kumteua mgombea!!!

Watia Nia wenzie wako silent wanajua agenda ya Sasa Ni kuteuliwa ndani ya Chadema .Lisu anahangaika kuteuliwa mitandaoni Kama mgombea Uraisi wa muungano .Uteuzi wa mgombea Chadema haufanywi mitandaoni Ni kwenye chama!!!

Wapambe wa Lisu akili hawana.Ona wagombea watia Nia wengine wanajua mitaondaoni sio Sasa kwa Sasa ni kutafuta uteuzi tu ndani ya Chadema kwa hiyo efforts zote wameelekeza huko moja kwa moja sio humu

Kuruka ruka ohh nafaa uraisi wa muungano wakati kiunzi tu Cha uteuzi ndani ya Chama hujakiruka Ni wehu anajua facts zake zote kuwa hatataeuliwa anatafuta sympathy za mitandaoni !!!
 
Hao waliopewa mandate wamepewa na nani? Chaguzi zetu sasa hivi zimetawaliwa na ushenzi, ukatili na uhayawani wa wazi, hao waliopewa mandate inaonekana ndio hao wanaoagiza huo uchafu. Haiwezekani wenye mandate wapewe na hao hao wanaopaswa kushindana, kwa vyovyote watawabeba wanaowachagua ili waendelee kulinda maslahi yao binafsi.

Hao wenye mandate unaowasema, ni wahuni fulani wasioweza kujitegemea, hivyo wako sehemu wanamteua mtu atakayewapa ulaji. Hicho kikundi cha wahuni wanaojiita wenye mandate, ndio huingiza nchi kwenye machafuko kwa ajili ya maslahi yao. Fahamu ya kuwa ccm sio chama cha kizazi hiki, ndio maana kinatumia mabavu, ukatili na unyama, ili kuendelea kukaa madarakani kwa shuruti bila ridhaa ya wananchi walio wengi. Sasa hivi watu hawataki kujitokeza tena kupiga kura, kisa kuna wahuni fulani wanaojifanya wana mandate, kwa kulazimisha kukiweka madarakani chama kisichokubalika na kizazi hiki.
sijui nikujibu nini sjaielewa point yako.
Ila naomba niwape ushauri wapinzani ANDAENI WANACHAMA WENU kuwa na sifa nzuri kuweza kugombea uraisi
 
Kutokubalika na “baadhi yawatu ndani ya vyombo vya dola”.Taarifa alizokuwa anapata naamini kuna watu ndani ya system wanampenda pia.Ideally,binadamu huwa Na wasiwasi na “kinachokuja “kuliko kile kilichopo.Hiyo ni hali ya kawaida.
tatizo mm mvivu wa kutyp ila OK
 
Unachosema akishinda mtampindua. Haitoshi kuna waliojaribu kumuua. Kwa hiyo mko radhi nchi iingie kwenye machafuko ili tu kama Lissu akishinda asitawale. Hapo mwisho ulipoandika "hatuwezi kuongozwa na Raisi mbeambea, Rais asieweza kusimama peke yake katika maamuzi" inaonyesha wazi humfahamu TL. Jiulize kwa nini walijaribu kumuua? Hivi kweli hiyo system haina kazi bali kufukuzana na mbea na asie na misimamo ya peke yake? Tafakari tena.
😁😁😁😁😁
 
sijui nikujibu nini sjaielewa point yako.
Ila naomba niwape ushauri wapinzani ANDAENI WANACHAMA WENU kuwa na sifa nzuri kuweza kugombea uraisi

Sifa nzuri sio za kuwaridhisha hao wenye mandate wasiofahamika. Labda ungesema wazi hao wenye mandate ni kina nani, na wanachaguliwaje. Sisi tunajua mtu anapigiwa kura na wananchi, anayeongoza kwa kura ndio mshindi. Na hivyo ndio inavyopaswa kuwa, na sio kwa maamuzi ya kikundi kisichofahamika uwepo wake. Kama tatizo la hicho kikundi ni Tundu Lisu. 2010 alikuwa Slaa, mbona hicho kikundi hakikumtangaza? Ni kwanini hicho kikundi kiipendelee tu CCM, na Sio kinyume chake?
 
Lumumba project kazini. Na mtaanzisha thread nyingi sana mwaka huu, ila ndo ivyo Tundu Antipas Lisse ni chaguo la wananchi na kama Mungu alivyomuepusha na kifo kwenye hila zenu mbaya ndivyo hivyo anaenda kumpa uraisi mwaka huu wa Tanzania.

Eti system haiwezi kukubali!! Hao vijana wenu mnaowatoa uvccm na kuwaingiza usalama wa Taifa ndo mnasema system.

Eti kuna misimamo ya Taifa,Magufuli mwenyewe kaenda tofauti na msimamo wa CCM na Sera zake kaiunga mkono Morroco ambao walipingwa na CCM na Baba wa Taifa miaka yote.

Sikiliza nikwambie mtu yeyote anaweza kuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano kikubwa akidhi matakwa tu ya watanzania na katika hili TUNDU ANTIPAS LISSU amekidhi vigezo vyote.
 
Back
Top Bottom