HIBISCUS 80
JF-Expert Member
- Jun 18, 2020
- 1,058
- 1,218
Pole Sana na hali ngumu unayopitiaHuu ndio ukweli unaofahamika kila mahali , Mifano ya waliokuwa wana CHADEMA na kusaliti chama chao waliodhalilika baada ya uamuzi wao huo ni mingi mno, hatuna haja ya kuirudia, ni kweli kwamba kuna waliopewa vyeo baada ya usaliti huo lakini heshima yao mbele ya jamii imepukutika mithili ya majivu kwenye upepo mkali.
Kwahiyo wanachopaswa kutambua wasaliti wapya na wajao ni kwamba usaliti wao utawagharimu heshima na utu wao mbele ya jamii kama ilivyowagharimu wasaliti waliopita ambao sasa wamepoteza kila kitu mbele ya Jamii, japo wamepata hela baada ya kununuliwa, hawaheshimiki na yeyote na wamedharauliwa moja kwa moja.
Muda utaongea .....
Ila tu tunakukaribisha CCM
achana na hao watu utazeeka siku so zako