Ukweli ni upi katika kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA?

Ukweli ni upi katika kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Katika gazeti la Hoja (Ijumaa, Novemba 15 – 21, 2019), kuna makala ‘’Mufti Zubeir alivyoikarabati BAKWATA,'' iliyoandikwa na Hemed Kimwanga.

Makala hii ingepita kama makala nyingine yeyote ile endapo makala isingekuwa na mambo ambayo si kweli kuhusu kuundwa kwa BAKWATA.

Imekuwa kawaida sana hasa katika miaka ya hivi karibuni kwa kusemwa na kuandikwa mengi ambayo si ya kweli kuhusu asili ya BAKWATA.

Kimwanga anasema na hapa najitahidi kunukuu kwa uchache yale aliyoandika.

Kimwanga anamuhusisha Julius Nyerere kwa kuvunjwa EAMWS na kuundwa kwa BAKWATA.

Kimwanga anasema, ‘’...uongozi wa Mufti umekidhi matumaini yaliyokuwa moyoni mwa Mwalimu Julius Nyerere kwa kushauri mpaka kuiva kwa ndoto zake za kuiona Tanzania ikiwa na Baraza lake la Kiislam ambalo litakuwa huru katika mashirikiano na vyombo vingine vya mlengo huo ndani na nje ya nchi.’’

Kimwanga anaandika anasema East African Muslim Welfare Society ilikuwa, ‘’chini ya uongozi na utawala wa Prince Aga Khan wa Uingereza...’’

Kimwanga anaendelea, ‘’...kuna mantiki ndogo sana ambayo ilifanya serikali ya Mwalimu Nyerere kuivunja EAMWS.

Alitaka Waislam wa Tanzania wajiongoze wenyewe.
Siyo kupokea maagizo kutoka London kwa Prince Aga Khan kupitia Nairobi...’’

Historia ya BAKWATA hivi sasa inafanana na historia ya TANU kwani historia ya BAKWATA kama ilivyo historia ya TANU imekuwa ikijaza hofu kwa baadhi ya watu kiasi ya kupelekea kusemwa uongo mwingi kwa kuogopa ukweli.

Haikunichukua muda wakati naisoma makala hii kutambua kuwa Kimwanga anaandika kitu ambacho yeye kwa kweli kabisa hakijui.

Sheikh Mohamed Ayub alikuwa heshi kuwausia wanafunzi wake kwa kuwaaambia kuwa popote linapokuwa jambo kuhusu Uislam wafike ili ikiwa patakuwa na jambo ambalo haliko sawa watanlieleza kwa ukweli wake.

Sheikh Mohamed Ayub akiwaambia wanafunzi wake kuwa, "Semeni, msiposema, hayo wasemayo yasio kweli, yataonekana ni kweli."

Ingekuwa kweli Mwalimu Nyerere anataka Waislam wasipokee amri kutoka London basi angelianza na kanisa lake mwenyewe, Kanisa Katoliki na kuishughulikia Vatican iliyokuwa na uwakilishi Tanzania nzima kama ifuatavyo:

White Fathers (Tabora), Karema, Kigoma, Mbeya, Mwanza na Bukoba; Holy Ghost Fathers (Morogoro na Kilimanjaro), Benedictine Fathers (Peramiho na Ndanda) Capuchin Fathers (Dar es Salaam) Consolata Fathers (Iringa na Meru), Passionist Fathers (Dodoma) Pallotine Fathers (Mbulu), Maryknoll Fathers (Musoma), na Rosmillian Fathers (Iringa).

Kimwanga kaandika mengi ambayo sijaona kama iko haja ya kuyasemea hapa na ningependa kueleza kuwa historia ya BAKWATA inafahamika na sababu za kupigwa marufuku EAMWS pia zinafahamika.

EAMWS imevunjwa wakati tayari ilikuwa na mipango ya kuwainua Waislam katika elimu na walikuwa wanajenga Chuo Kikuu Cha Waislam mradi ambao ulikuwa unakwenda sambamba na ujenzi wa shule Tanzania nzima.

Hapo yalipo Makao Makuu ya BAKWATA pamoja na shule hiyo ya Kinondoni imejengwa na EAMWS.

Waislam hawakuwa na ujinga kuivunja EAMWS wakati inajenga Chuo Kikuu na shule kuwainua Waislam ambao ukoloni uliwanyima elimu na kutoa uwanja mpana kwa makanisa kuhodhi elimu ambayo waliitoa kwa ubaguzi kwa waumini wao kwa kipindi cha zaidi ya miaka 100.

Kimwanga asome historia ya kweli ya Tanganyika atafahamu kwa nini EAMWS ilivunjwa na sababu haikuwa kupokea amri kutoka kwa Prince Aga Khan wa Uingereza (sic).

Aga Khan hakuwa London bali akiishi Paris na mgogoro wa EAMWS ulipokuwa umepamba moto alijiuzulu nafasi yake ya Patron kutoka Paris.
 
Hii nchi hii ina mfumo Kristo wallah dhulma dhidi ya Waislam wa Tanganyika haitaliacha Kanisa salama na wallah tunaumia kwa haya yanayotokea , Allah amjalie sheikh wetu ilunga Pepo ya juu in sha Allah ameacha athari kubwa sn kwa kizazi cha leo maneno yake bado yanaishi japo watu wasema vijana punguzeni jazba wallah hatutapunguza mpk hizza yetu itakaporudi bi idhniLlaah.
 
Mkuu, hiyo EAMWS imeshavunjwa siku nyingi, sasa hivi iko BAKWATA, huoni maneno yako yanachochea chuki kwa waislamu dhidi ya BAKWATA?
 
mkuu, hiyo EAMWS imeshavunjwa siku nyingi, sasa hivi iko BAKWATA, huoni maneno yako yanachochea chuki kwa waislamu dhidi ya BAKWATA?
Laki...
Chuki na uchochezi katika kusema kweli?

Unataka vizazi vijavyo viamini kuwa Waislam walikuwa watu wapumbavu kiasi waliivunja EAMWS wakati wanajenga shule na Chuo Kikuu?

Tuna wajibu wa kueleza ukweli na kupinga proaganda za watu kama Kimwanga.
Unajua kuwa hadi leo historia ya Auschwitz bado inasomeshwa?
 
Hii nchi hii ina mfumo kristo wallah dhulma dhidi ya Waislam wa tanganyika haitaliacha kanisa salama na wallah tunaumia kwa haya yanayotokea , Allah amjalie sheikh wetu ilunga Pepo ya juu in sha Allah ameacha athari kubwa sn kwa kizazi cha leo maneno yake bado yanaishi japo watu wasema vijana punguzeni jazba wallah hatutapunguza mpk hizza yetu itakaporudi bi idhniLlaah
Ameacha athari kubwa sana ipi na inatija gani hiyo athari?

Mimi nachoweza kusema ni kuwa Allah amsemehe kwa fikra chafu alizoziacha kwa vijana wa kiislamu wasio taka kujifunza dini yao.
 
Religion is the opium of the people!

Kuna haja gani sasa ya kuwa na Serikali kama Taasisi ya kidini ilitakiwa kufanya yote hayo? Kama ni hivyo si Waislamu wangeomba tu nchi yao? I mean kama huyo A.Khan alitaka kuwa na Shule, Vyuo vikuu Hospitali n.k. kwa Waislamu basi angeanzisha pia nchi yake ya Waislamu, kama unasema nia yake ilikuwa kuwainua Waislamu Kielimu, je Waislamu siyo raia wa JMTZ? Na mwisho wa siku wangekuwa watiifu kwa Aga Khan au kwa Serikali ya JMTZ?

BTW siyo fan wa Shule, Hospitali Vyuo vikuu vya Kikristo pia, lkn angalau ziko neutral kuhudumia kila binadamu.
 
mkuu, hiyo EAMWS imeshavunjwa siku nyingi, sasa hivi iko BAKWATA, huoni maneno yako yanachochea chuki kwa waislamu dhidi ya BAKWATA?
Nenda kamsome Mzee Ben katika My life My purpose kisha utafakari uhalali wa hiki ulicho andika
 
Religion is the opium of the people!

Kuna haja gani sasa ya kuwa na Serikali kama Taasisi ya kidini ilitakiwa kufanya yote hayo? Kama ni hivyo si Waislamu wangeomba tu nchi yao? I mean kama huyo A.Khan alitaka kuwa na Shule, Vyuo vikuu Hospitali n.k. kwa Waislamu basi angeanzisha pia nchi yake ya Waislamu, kama unasema nia yake ilikuwa kuwainua Waislamu Kielimu, je Waislamu siyo raia wa JMTZ? Na Na mwisho wa siku wangekuwa watiifu kwa Aga Khan au kwa Serikali ya JMTZ?

BTW siyo fan wa Shule, Hospitali Vyuo vikuu vya Kikristo pia, lkn angalau ziko neutral kuhudumia kila binadamu.
Barbarosa,
Waislam waliathirika sana na ukoloni na ndiyo maana ukirejea katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika utakutana nao kila utakapoweka mguu wako.

Waislam walijua kuwa kwa kuwa nchi washaikomboa na iko huru sasa wajibu wao ni kupigania maendeleo yao kwani walijua serikali haina uwezo wa kufanya kila kitu.

Hii ndiyo sababu mwaka wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akatangaza kuwa anajiuzulu siasa na anaunda jumuia Daawat Islamiyya (Wito Kwa Waislam) ili ashughulike na elimu kwa Waislam, elimu ambayo ilikuwa inatolewa kwa ubaguzi wakati wa ukoloni.

Huenda ukashangaa kwani naamini hujapatapo kusoma wala kusikia kuwa kulikuwa na mpigania uhuru jina lake Sheikh Hassan bin Ameir na ndiye aliyekuwa Mufti wa Tanganyika wakati wa EAMWS.

Mwaka huo wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akaitisha Muslim Congress ya Kwanza na katika maazimio yaliyopitishwa ni EAMWS kuweka umuhimu wa juu kabisa katika suala la elimu.

Mwaka wa 1963 ikaitisha Muslim Congress ya Pili.

Nadhani umeelewa.

La kama maelezo haya bado hujayafahamu nifahamishe nitazidi kukusomesha historia ya Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika na matarajio yao uhuru ukipatikana.

Haikuwa mategemeo yao kabisa kuwa watakuja kupambana na matatizo katika elimu katika nchi huru waliyoikomboa kutoka makucha ya ukoloni.
 
Barbarosa,
Waislam waliathirika sana na ukoloni na ndiyo maana ukirejea katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika utakutana nao kila utakapoweka mguu wako.

Waislam walijua kuwa kwa kuwa nchi washaikomboa na iko huru sasa wajibu wao ni kupigania maendeleo yao kwani walijua serikali haina uwezo wa kufanya kila kitu.

Hii ndiyo sababu mwaka wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akatangaza kuwa anajiuzulu siasa na anaunda jumuia Daawat Islamiyya (Wito Kwa Waislam) ili ashughulike na elimu kwa Waislam, elimu ambayo ilikuwa inatolewa kwa ubaguzi wakati wa ukoloni.

Huenda ukashangaa kwani naamini hujapatapo kusoma wala kusikia kuwa kulikuwa na mpigania uhuru jina lake Sheikh Hassan bin Ameir na ndiye aliyekuwa Mufti wa Tanganyika wakati wa EAMWS.

Mwaka huo wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akaitisha Muslim Congress ya Kwanza na katika maazimio yaliyopitishwa ni EAMWS kuweka umuhimu wa juu kabisa katika suala la elimu.

Mwaka wa 1963 ikaitisha Muslim Congress ya Pili.

Nadhani umeelewa.

La kama maelezo haya bado hujayafahamu nifahamishe nitazidi kukusomesha historia ya Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika na matarajio yao uhuru ukipatikana.

Haikuwa mategemeo yao kabisa kuwa watakuja kupambana na matatizo katika elimu katika nchi huru waliyoikomboa kutoka makucha ya ukoloni.

Hakuna ambaye hakuathirika kwa Ukoloni, tuliuzwa utumwa, tulibebeshwa pembe za ndovu ktk Kigoma hadi Pwani kwa miguu karavani, tulifanyishwa kazi bila ya ujira au ujira mdogo sana kwenye mashamba ya Wakokoni huko Tanga, Zanzibar, Tabora Kigoma na kwingineko.

Kwanza ninaweza kusema Waislamu Waarabu, Wahindi na wengineo walinufaika zaidi na Ukoloni klk sisi Waafrika weusi kwani Waislamu Waarabu na Wahindi walikuwa daraja la pili baada ya Muzungu na sisi weusi tulikuwa daraja la tatu.

Kuna sababu kwa nini miji yote Mikubwa TZ kuna makazi yajulikanayo kama Uzunguni, Uhindini na Uswahilini, na Uswahilini ni kwetu sisi weusi na mweusi haikujalisha kama ulikuwa Muislamu au Mkristo, tulikuwa wote ni daraja la tatu.

Hivyo kusema kwamba Waislamu walionewa wakati wa Ukoloni sijui unamanisha nini na walionewa kwa kulinganisha na nani? Kama kulinganisha na Mwafrika mweusi, hapo nitakupinga.
 
Nenda kamsome Mzee Ben katika My life My purpose kisha utafakari uhalali wa hiki ulicho andika
Boywise,
Sijakisoma kitabu cha Rais Mkapa lakini naweza kutafakari bila ya kusoma kitabu kwa kuwa nimefanya utafiti wa kile kilichoitwa Mgogoro wa EAMWS.

Mgogoro huu ulikuwa mwaka wa 1968 na mgogoro ule Rais Mkapa anaujua vizuei sana kwa kuwa yeye alikuwa Mhariri wa The Nationalist na gazeti lake na RTD ikiwa chini ya Martin Kiama vilichangia sana katika kuikandamiza EAMWS na viongozi wake, Sheikh Hassan bin Ameir, Tewa Said Tewa, Bilal Rehani Waikela na Bi. Titi Mohamed waliopigania uhuru wa Tanganyka.

Nadhani unawajua hao hapo juu kuwa wote hao walikuwa viongozi wazalendo na waasisi wa TANU.

Nadhani baada ya kusoma haya sasa uko katika hali ya kutafakari uhalali wa hicho ulichoniandikia.
 
Hakuna ambaye hakuathirika kwa Ukoloni, tuliuzwa utumwa, tulibebeshwa pembe za ndovu ktk Kigoma hadi Pwani kwa miguu karavani, tulifanyishwa kazi bila ya ujira au ujira mdogo sana kwenye mashamba ya Wakokoni huko Tanga, Zanzibar, Tabora Kigoma na kwingineko.

Kwanza ninaweza kusema Waislamu Waarabu, Wahindi na wengineo walinufaika zaidi na Ukoloni klk sisi Waafrika weusi kwani Waislamu Waarabu na Wahindi walikuwa daraja la pili baada ya Muzungu na sisi weusi tulikuwa daraja la tatu.

Kuna sababu kwa nini miji yote Mikubwa TZ kuna makazi yajulikanayo kama Uzunguni, Uhindini na Uswahilini, na Uswahilini ni kwetu sisi weusi na mweusi haikujalisha kama ulikuwa Muislamu au Mkristo, tulikuwa wote ni daraja la tatu.

Hivyo kusema kwamba Waislamu walionewa wakati wa Ukoloni sijui unamanisha nini na walionewa kwa kulinganisha na nani? Kama kulinganisha na Mwafrika mweusi, hapo nitakupinga.
Barbarosa,
Nimekusoma.

Mimi si mtu wa kufanya ubishi niko hapa kufahamisha yale ambayo wengi hawayajui siko hapa kushinda mjadala na yoyote yule.
 
Barbarosa,
Nimekusoma.

Mimi si mtu wa kufanya ubishi niko hapa kufahamisha yale ambayo wengi hawayajui siko hapa kushinda mjadala na yoyote yule.


Sawa, lkn pia kila mtu ana haki pia ya kutoa maoni isitoshe mambo ya Historia ni magumu sana kwani hata wana Historia wenyewe pia huegemea upande ambao wanaona huwanufaisha, na hii ni Dunia nzima.

Mfano Wazungu wa AK wanasema wao walipokuja walikuta mapori wakafyeka na kujenga Miji kama Capetown baadaye Waafrika wakaja na kusema wamechukuwa ardhi yao lkn wao wanasema hawakukuta mtu bali mapori.

Hivyo Historia ni ngumu sana, na ndo maana cha muhimu kuangalia nchi tunayoishi sasa hivi tufanye nini ili tuishi kwa amani, umoja na haki baina yetu.
 
Boywise,
Sijakisoma kitabu cha Rais Mkapa lakini naweza kutafakari bila ya kusoma kitabu kwa kuwa nimefanya utafiti wa kile kilichoitwa Mgogoro wa EAMWS.

Mgogoro huu ulikuwa mwaka wa 1968 na mgogoro ule Rais Mkapa anaujua vizuei sana kwa kuwa yeye alikuwa Mhariri wa The Nationalist na gazeti lake na RTD ikiwa chini ya Martin Kiama vilichangia sana katika kuikandamiza EAMWS na viongozi wake, Sheikh Hassan bin Ameir, Tewa Said Tewa, Bilal Rehani Waikela na Bi. Titi Mohamed waliopigania uhuru wa Tanganyka.

Nadhani unawajua hao hapo juu kuwa wote hao walikuwa viongozi wazalendo na waasisi wa TANU.

Nadhani baada ya kusoma haya sasa uko katika hali ya kutafakari uhalali wa hicho ulichoniandikia.
[/QUOTE]
Nilikusudia kumjibu Laki Mzee wangu
 
Sawa, lkn pia kila mtu ana haki pia ya kutoa maoni isitoshe mambo ya Historia ni magumu sana kwani hata wana Historia wenyewe pia huegemea upande ambao wanaona huwanufaisha, na hii ni Dunia nzima.

Mfano Wazungu wa AK wanasema wao walipokuja walikuta mapori wakafyeka na kujenga Miji kama Capetown baadaye Waafrika wakaja na kusema wamechukuwa ardhi yao lkn wao wanasema hawakukuta mtu bali mapori.

Hivyo Historia ni ngumu sana, na ndo maana cha muhimu kuangalia nchi tunayoishi sasa hivi tufanye nini ili tuishi kwa amani, umoja na haki baina yetu.
Barbarosa,
Hii historia nikuekezayo haina ugumu wowote ni historia ambayo inawahusu wazee wangu nami nimeishi ndani ys historia hii.

Nawajua wazee wangu na historia ya uhuru wa Tanganyika toka walipounda African Association 1933 hadi kufika TANU na harakati za uhuru.

Wengine nimebahatika kuwaona kwa macho yangu na kuzungumzanao.

Na hawa ndiyo walionisomesha mimi historia hii na nikaandika kitabu kilichobadili historia yote ya uhuru wa Tanganyika.

Ndiyo maana hapa leo nakuelezeni historia ya wazalendo ambao hata siku moja hamkupata kuwasoma popote pale wala kusikia majina yao kutajwa na kuhusishwa na chama cha TANU ingawa wao ndiyo waliokiasisi.

Hii ndiyo kazi yangu mimi hapa.
Kukaa chini kitako na kusomesha.
 
Boywise,
Sijakisoma kitabu cha Rais Mkapa lakini naweza kutafakari bila ya kusoma kitabu kwa kuwa nimefanya utafiti wa kile kilichoitwa Mgogoro wa EAMWS.

Mgogoro huu ulikuwa mwaka wa 1968 na mgogoro ule Rais Mkapa anaujua vizuei sana kwa kuwa yeye alikuwa Mhariri wa The Nationalist na gazeti lake na RTD ikiwa chini ya Martin Kiama vilichangia sana katika kuikandamiza EAMWS na viongozi wake, Sheikh Hassan bin Ameir, Tewa Said Tewa, Bilal Rehani Waikela na Bi. Titi Mohamed waliopigania uhuru wa Tanganyka.

Nadhani unawajua hao hapo juu kuwa wote hao walikuwa viongozi wazalendo na waasisi wa TANU.

Nadhani baada ya kusoma haya sasa uko katika hali ya kutafakari uhalali wa hicho ulichoniandikia.
Nilikusudia kumjibu Laki Mzee wangu[/QUOTE]Boywise,
Tupo jamvini tunazungumza hapana neno.
 
Hakuna ambaye hakuathirika kwa Ukoloni, tuliuzwa utumwa, tulibebeshwa pembe za ndovu ktk Kigoma hadi Pwani kwa miguu karavani, tulifanyishwa kazi bila ya ujira au ujira mdogo sana kwenye mashamba ya Wakokoni huko Tanga, Zanzibar, Tabora Kigoma na kwingineko.

Kwanza ninaweza kusema Waislamu Waarabu, Wahindi na wengineo walinufaika zaidi na Ukoloni klk sisi Waafrika weusi kwani Waislamu Waarabu na Wahindi walikuwa daraja la pili baada ya Muzungu na sisi weusi tulikuwa daraja la tatu.

Kuna sababu kwa nini miji yote Mikubwa TZ kuna makazi yajulikanayo kama Uzunguni, Uhindini na Uswahilini, na Uswahilini ni kwetu sisi weusi na mweusi haikujalisha kama ulikuwa Muislamu au Mkristo, tulikuwa wote ni daraja la tatu.

Hivyo kusema kwamba Waislamu walionewa wakati wa Ukoloni sijui unamanisha nini na walionewa kwa kulinganisha na nani? Kama kulinganisha na Mwafrika mweusi, hapo nitakupinga.
Nafikiri hapa Mzee MS anamaanisha kuathirika Waislam dhidi ya Wakristo. Sasa hapo itabidi upate picha ni kwa namna gani Wakristo walifaidika sana na ukoloni na Waislamu wakiathirika.

Yaani unatakiwa ujue kwa mfano akina Mzee Sykes walioajiriwa na katika Serikali ya mkoloni walikuwa waathirika sana kuliko Mkristo muumini pale Ilala au Tanga
 
stormryder,

Huwa mimi sipati tabu ninaposoma maneno kama haya.

Huwa naangalia haya kwa nia njema kuwa asemae hajui bado hajapata kuelezwa haya sasa atajuaje?

Nilipokuwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam mwalimu anafundishi historia ya utaifa katika nchi za Afrika ya Mashariki anaeleza historia ya TANU lakini nagundua makosa mengi.

Nanyoosha mkono kumfahamisha kuwa TAA hakikuwa chama cha starehe na Mwalimu Nyerere hakuunda TANU.

Darasa zima linapigwa na butwaa pamoja na mwalimu wangu.
Mwalimu ananiomba ushahidi ''empiricism.''

Namweleza kama ameshapata kusikia jina la Abdulwahid Sykes na mdogo wake Ally na baba yao Kleist nataja hadi namba za kadi zao za TANU.

Namuuliza mwalimu wangu kama amepata kusikia jina la Sheikh Suleiman Takadir au Sheikh Hassan bin Ameir katika historia ya TANU.

Nawaambia kuwa babu yangu Salum Abdallah ni mmoja wa watu walioshuhudia hayo yote na ni muasisi wa TANU na kapigania uhuru wa Tanganyika kwa jasho lake na mali yake.

Wanadhani natania.

Sasa ikiwa wewe unanijua mimi kwa muda mrefu utakuwa unatambua kuwa najua mengi katika historia ya Tanganyka na sifanyi mzaha katika haya niandikayo.

Umesema, ''Waislam ni kama wanawake...''

1573921991522.png

Hiyo picha hapo juu ni safari ya Julius Nyerere UNO mwezi February 1955 huyo aliye mkono kulia kwa Mwalimu aliyavaa koti kanzu na tarbush jina lake ni Iddi Faizi Mafungo Mwekahazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Safari ya UNO ilipangwa na Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti Sheikh Suleiman Takadir na ndiyo walimpa Iddi Faizi jukumu lote la kukusanya fedha za safari ya Mwalimu Nyerere.

Naamini historia hii ni ngeni na mpya kwako.
Kama ulivyokuwa huyajui haya na hayo mengine ndivyo usivyoyajua.

Waswahili tuna msemo, ''Usilolijua msitu wa kiza.''

Kuwa na subira uliza maswali kwa adabu na heshima si kama hivyo hapo juu nitakufunza historia ya Tanganyika ya miaka 100 kurudi nyuma na utakuwa unajua na utafanya mjadala ukiwa una elimu ya kutosha katika somo hili.

1573923036882.png

Baraza la Wazee wa TANU 1954
 
Back
Top Bottom