Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Pundit,
You are the man. This is what I was looking for. Thanks a million
 
wakuu nadhani sasa ndio tunaelekea mkondo wa thread.
nawashukuru wote kwa michango yenu makini.

swali kwako mfes. umalawi wa kambona ukoje hapo? kijiji cha kambona si kipo tanzania?

nje ya mada: mbona kuna tetesi pia kwamba karume nae anaasili ya malawi? kama ni kweli (i hope si kweli) mbona alichukua nchi?

shukurani wakuu tuendelee kupeana shule katika hili.
 
Wakuu,
Nimerudi kuangalia vitu viwili vitatu inaonekana ni kweli Kambona alikuwa anataka umaarufu wa haraka. Kutoa mfano, nina ripoti moja inahusu ishu moja ya "alleged" forged documents kuhusu Marekani kutaka kupindua nchi kwa ushirikiano na wareno mwishoni wa 1964. Serikali ilipata document moja iliyokuwa inaonyesha mipango ya siri ya kupindua nchi. Kambona aliharakisha kukimbia kutoa habari OAU na vyombo vya habari kwamba Wamarekani wanapanga kupindua nchi kwa kutumia mercenaries. Wamarekani wakaleta mtaalamu wao achunguze hiyo paper, balozi wa marekani akaande moja kwa moja kwa mwalimu kumwonyesha ushahidi kwamba ni feki.

Balozi anaripoti Nyerere alishika kichwa na mikono miwili. Akamwambia balozi, and I quote: "I don't know what Kambona is doing"? Wamarekani walitaka Nyerere aseme publicly kwamba ilikuwa ni uongo. Yeye akakataa kwasababu ishu ilishafika mbali sana. It was a major diplomatic dissaster and very embarassing to Mwalimu.

Hii haikuwa mara ya kwanza au ya pili Kambona kukurupuka na kuharibu mambo. Kuna mifano mingine. Nyingine ilitokea 1960 wakati Nyerere amesafiri. Kambona aliwaambia wakoloni tunataka uhuru sasa hivi na alikuwa anaoongea kama mmoja wa viongozi wa chama. Huo ulikuwa wakati Nyerere ana-negotiate na U.K. kuhusu uhuru. Ikaja kuleta matatizo mengi. Kwa ujumla ni kwamba Kambona alikuwa anakosea stepu wakati mwingine. Na nakubaliana nanyi kwamba inaonekana alikuwa anataka umaarufu.

Hii ripoti ninayo. Kinachonisikitisha ni kwamba Bongo hizi ripoti wanaficha, lakini ulaya na kwengine zinapatikana. Mengi wasiyotaka kuongelea yapo kwenye ripoti za nje. Siwalaumu sana, lakina kuna mengi mazuri nchi yetu ilifanya lakini ni vigumu sana kupata access ya data na kuandika hizo historia. Matokeo yake ni kwamba tunaachwa kwenye giza.

Maswali:

Sina source yoyote kuhusu mambo ya 60s. Lakini mwaka 1964, kulikuwa na matukio matatu makubwa. Kwanza kulikuwa na maasi ya wanajeshi wa Tanganyika ambazo sababu zake mpaka sasa kwa watanzania wengi ni kitendawili kwa sababu usiri wa serikali yetu.

Sababu ya pili kulikuwa na mapinduzi ya kuondoa utawala wa ki-Sultani huko Zanzibar. Baada ya kuingia kwa mataifa yenye nguvu afrika mashariki (ujerumani na uingereza), utawala wa sultani ulishindwa kulinda himaya yake zilizopo Kenya na Tanganyika. Hili kulinda alichobakiwa nacho ilibidi aingie mikataba ya ulinzi na uingereza miaka ya 1880.

Kwa upande wa Sultani, mapinduzi ya 1964 yalitokea kwa sababu watu aliopatana nao (uingereza) waliondoa majeshi yao. Na kwa mtaji huu, Sultani alikuwa hayupo katika nafasi ya kuunda jeshi la maana katika kipindi cha muda ufupi. Na ambacho angeweza kukifanya ni kuingia mikataba ya ulinzi na Marekani ambayo ilikuwa inatafuta vituo vya majeshi dunia.

Na wanamapinduzi nao walikuwa hawana jeshi la kulinda nchi na walichofanya ni kuomba majeshi ya Tanganyika na kusababisha tukio la tatu-Muungano.

Kwa maoni yangu, kulikuwa na sababu nyingi muhimu za kuipindua serikali ya Tanzania kufikia mwishoni mwa 1964.

Vilevile mapinduzi yakusaidiwa na marekani mara nyingi yanafanywa na jumuia ya kijasusi ya Marekani. Hawa jamaa ni wasiri na document zao kuzipata inashukua miaka. Ni miaka kama mitano iliyopita wametoa document zilizotolewa kuonyesha walihusika na kuchochea mapinduzi ya kumuondoa Kwame Nkrumah.

Vilevile balozi wa marekani kuleta makaratasi ku-prove kuwa kulikuwa hakuna njama ni sawa na Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani kwenda umoja wa mataifa na kuonyesha kuwa Iraq ina silaha za kuangamisha mamilioni ya watu kwa muda mfupi.

Kwanini mtuhumiwa aunde tume ya kuchunguza tuhuma zake?

Kuhusu kutaka uhuru wakati Nyerere yupo uingereza mwaka 1960 sioni kwamba Kambona alichemsha. Mpaka 1958, Nyerere alikuwa kiongozi wa upinzani bungeni. Kufikia mwaka 1960, Nyerere alikuwa waziri kiongozi na madaraka ya ndani tulikuwa nayo. Hivyo aliyosema Kambona yalikuwa in-line na kipindi kilichokuwepo.
 
swali kwako mfes. umalawi wa kambona ukoje hapo? kijiji cha kambona si kipo tanzania?

Mkuu marehemu Chiume, alisoma bongo na kuwa waziri wa Malawi, Nyirenda na Kambona, walikuwa ni wa-Malawi, lakini ninaaamini kuwa wanavyo vijiji bongo!
 
Mkuu marehemu Chiume, alisoma bongo na kuwa waziri wa Malawi, Nyirenda na Kambona, walikuwa ni wa-Malawi, lakini ninaaamini kuwa wanavyo vijiji bongo![/QUOTE]

Mbona Lusinde na Cigweyemisi wanadaiwa vilevile kuwa ni Wamalawi.

Babu/Baba yao alikuja Mvumi kama Mmisionari.
 
Nasikia yournameisMINE pia mmalawi..........so what??.
 
Mkuu marehemu Chiume, alisoma bongo na kuwa waziri wa Malawi, Nyirenda na Kambona, walikuwa ni wa-Malawi, lakini ninaaamini kuwa wanavyo vijiji bongo

Mbona Lusinde na Cigweyemisi wanadaiwa vilevile kuwa ni Wamalawi.

Babu/Baba yao alikuja Mvumi kama Mmisionari. !

Ukienda nyuma kidogo utasema Wangoni ni Wazulu, Nyerere ni Mtutsi etc etc

Kwa mtaji huu wabantu wote Wa-Nigeria /Cameroon, si wametokea nyanda za Jos huko?

Wakina Cigwiyemisi walizaliwa na kukulia Dodoma, baba yao alikuwa anakaa karibu sana na Chief Mazengo.It doesn't get any more authentic than that.
 
Pamoja na mapungufu yake ya kibinadamu kama aliyokuwa nayo Nyerere, mimi bado ninaamini kabisa kuwa vision ya Kambona kuhusu uchumi ilikuwa ni sahihi. Tatizo lake alishindwa kuondoa tofauti zilzokuwapo bana yake na Nyerere. Wakati vision ya Nyerere kuhusu usawa katika jamii ilikuwa sahihi, kilicohotakiwa ni kuunganisha vision ya Nyerere kuhusu ujenzi wa jamii ya usawa na vision ya Kambona kuhusu ujenzi wa uchumi kitaifa. Nchi yetu ingekuwa mbali sana leo na wala tusngekuja kupata hawa wanasiasa uchwara wa leo wanauza nchi yetu kama haina wenyewe.
 
[/B][/I]
Ukienda nyuma kidogo utasema Wangoni ni Wazulu, Nyerere ni Mtutsi etc etc

Kwa mtaji huu wabantu wote Wa-Nigeria /Cameroon, si wametokea nyanda za Jos huko?

Wakina Cigwiyemisi walizaliwa na kukulia Dodoma, baba yao alikuwa anakaa karibu sana na Chief Mazengo.It doesn't get any more authentic than that.

Ni mipaka iliyowekwa na wakoloni ndio iliyotenganisha watu wa kijiji kimoja, kabila au familia moja.

Hivi sheria ya uraia wakati tunapata uhuru ilikuwa vipi? Nchi nyingine uraia ulitolewa kwa mtu yoyote aliyekuwepo wakati nchi inapata uhuru.
 
Ipo haja ya kujiuliza juu ya ushiriki na uwepo wa Wa-Malawi wengi wakati wa kugombea na baada ya kupatikana kwa uhuru. Was it a mere coincidence, fate, or a planned event.

Hili linawahusu kina Banda, Mtawali, Kamaliza, Chiume, Shaba etc.

Kuna theory inayodai kuwa Waingereza hawakutaka Tz ipate uhuru hadi mwaka 1974. Ilionekana kuwa kipindi hicho kingeweza kutoa muda wa kupatikana watanzania Waanglikana wengi wa kuweza kuongoza serikali pamoja na organs zake. Hawakutaka nchi hii iongozwe na wakatoliki.

Hivyo basi, kwa vile kanisa la Kianglikana lilikuwa limejikita zaidi Malawi ambapo kulikuwa na wasomi wengi kwa kipindi hicho, ilionekana ni vyema kuwaleta Tz kama mkakati mkubwa wa maandalizi hayo.
Haya yanasemwa, ila sina uhakika na uhalali wake!
 
Wakuu,
Hii thread inakataa kona nyingi. Nafikiri itakuwa jambo la busara kama tukifungua thread nyingine ya 1964 Army Mutiny. Je Kambona alihusika vipi na maasi hayo? Sina uhakika kwa kweli. Lakini nikiangalia data nilizoweza kupata, siwezi ku-speculate kwamba Kambona alikuwa na mipango yake mwenyewe. Ndio kuna maswali bado sijapata majibu yake. Lakini kwa sasa naacha hivyo mpaka pale nitapopata ushahidi zaidi.

Kurudi kwa Kambona, kuna article nimeandika lakini siwezi kuweka hapa mpaka ikichapishwa. Kuna mengi ningependa kusema lakini kwa sasa nitasema machache tuu.

Kulikuwa na power struggle kati ya Nyerere, Kambona, na Kawawa. Nyerere na Kawawa walikuwa pamoja. Hiyo struggle ilianza pale Kambona alivyorudi kutoka London. Alirudi baada ya kufeli mtihani wake wa mwisho kule. Katika mvutano wa power, Kambona akawa na kikundi chake kilichojulikani kama vijana "radicals." Hawa walikuwa wanataka mabadiliko makubwa ya haraka. Kuna baadhi ya mawazo yao yalikuwa mbali, lakini mengine walikuwa wanalazimisha haraka. Hilo lilimtia Kambona katika matatizo na wazee wa TANU. Nyerere hakuwa pekee kupingana na Kambona. Aliyekuwa anafanya mipango mingi ya kumtoa Kambona alikuwa ni Kawawa. Yeye alikuwa anaongea na wazee ambao wakawa tayari kumtoa Kambona. Na Kambona kwa upende wake, alifanya makosa mengi ambayo yaliwapa sababu adui zake kumtoa.

Kambona alikuwa on top wakati alipokuwa Chairman wa ALC, na alipofanya mipango ya kusaidia mapinduzi ya Zanzibar na muungano. Alimtumia rafiki yake Harue Tambwe, Commissioner wa Tanga, kuongea na Hanga baada ya mapinduzi. Hanga alikuwa roommate wa Kambona London wakati anasoma. Na pia alikuwa on top wakati wa maasi ya jeshi. Aliweza kuongea na wanajeshi akawapooza mpaka pale Nyerere alipopata nafasi ya kuwaita waingereza kuzima hayo maasi. Pamoja na kwamba yeye alisaidia kusuluhisha hilo tatizo kama Minister of Defense, naona intelligence system yote ili-fail; yeye, Lusinde, C. Mzena na wengine walikuwa gizani, lakini pia kuna baadhi ya ripoti ambazo zingewapa clues wali-ignore. Zaidi ya hapo sijaona ushahidi wowote. Siwezi kutoa speculations.

Januari 22, Nyerere alitembelea sehemu zilizoshambuliwa na wanajeshi. Alikuwa na mke wake na Lusinde. Tukumbuke hiyo ilikuwa baada ya maasi kuanza. Wakati huo Nyerere alikuwa analala State House. Kwa siku mbili, kuanzia January 20 mpaka 22, Nyerere hakuwa mafichoni. Kama kulikuwa na mpango wa kumuua nafikiri wangemuua. Ila ni kweli kwamba situation ilikuwa inazidi ku-deteriorate. Hata kabla Nyerere hajaomba msaada wa jeshi la waingereza, according to the National Military Command Center, Joint Chief of Staff report, balozi wa uingereza alishaomba jeshi lao liwe karibu kuokoa maisha ya raia wao na wamarekani.

Kusema kweli hawa wanajeshi wa TNG wasingefika mbali. Waingereza na Wamarekani walishaanza kuleta majeshi yao kuzima maasi. Waingereza waliita vikosi vyao viliyokuwa Kenya on January 20 vije karibu na Dar: 4940 regular soldiers, 3230 Gurkas and Colonials, na walikuwa na 5 Beverly type aircraft, 6 Twin Pioneers. Kwa wamarekani, USS Manley ilkuwa 1000 miles northeast of Dar es Salaam. State Department ikaomba ipelekwe Dar on Jan 20 ikutane na British HMS Rhyl ambayo tayari ilikuwa maeneo ya Dar. Top Secret American document "CINSTRIKE/USCINCMEAFSA OPLAN" inasema ifuatavyo: "purpose-to provide for either US assistance to UN sponsored action in Tanganyika or U.S. unilateral action in conjunction with friendly forces in Tanganyika, to restore order and maintain or re-establish the legitimate government. Mission: conduct operations to neutralize or destroy dissident forces, to prevent entry or seizure by Communist or other forces, to restore order and to assist in maintain or re-establishing the legitimate government of Tanganyika." Kama waingereza wasingekuja, wamarekani wangekuja. Na tukumbuke jeshi la Tanganyika likuwa dogo sana wakati huo. Sio zaidi ya 1000 kama sijakosea. Kwa wale wanao-speculate kwamba Kambona alikuwa na mipango mingine, inawezekana alikuwa anafahamu kwamba west ililikuwa tayari kutumia nguvu kurudisha serikali.

Baada ya kufikia apex ya power na popularity January-April 1964, Kambona akaanza kuporomoka pole pole. Hii inaweza kuwa na sababu tofauti. Pengine alioona yupo juu sana na akawa anafanya maamuzi makubwa ya serikali bila kujadili na wakubwa wengine; pili kuna uwezekano wakubwa wenzake walimwonea wivu baada ya maasi na wakawa wanamtafutia sababu ya kutoa.

Kwa upande wangu naona turning point ilikuwa jinsi alivyo-handle "Western Plot" Novemba 1964. TANU National Executive Council ilikutana Desemba 16-18, 1964 kukawa na motion ya kum-discipline Kambona kwa jinsi alivyo handle "Western Plot." Sina uhakika nani aliweka hiyo motion, lakini nafikiri ni Peter Siyovelwa (1970s alikuwa minister responsible for Usalama). Motion ya kum-censure Kambona ikapita. Baada ya hayo yote, aliachiwa aendelee na kazi yake. Lakini mambo yalikuwa hayajaisha. Machi 5-8, 1965 TANU Annual Conference, wazee wa TANU wakaja juu. Wali-recommend Nyerere amtoe Kambona kwa jinsi alivyo deal na "Western Plot." Behind the scene engineer alikuwa Kawawa.

Stormy Cabinet meeting ikafanyika March 9-10, 1965. Usiku wa March 10, mkutano wenye mvutano ukaendelea; kikundi kimoja kilikuwa na Nyerere, Kawawa na wengine na upande mwingine Kambona, Lusinde, Babu, Kamaliza, Maswanya na wengine. Mwishoni upande wa Nyerere ukashinda. Uamuzi ukawekwa Kambona atolewe na aingizwe Sijaona. Baada ya yote hayo, Nyerere hakumtoa Kambona. Babu aliweza kumshawishi Karume amwambie Nyerere huu sio wakati wakubadilisha serikali na kama atafanya hivyo atahatarisha muungano.

Kambona alikuwa na maadui wengi TANU. Wazee wa TANU walitaka atolewa tangu 1964 na Nyerere alikataa mpaka 1966 walipoanza kushtuka na kukutaa Kambona alikuwa na 50,000Sterling pounds akaunti yake pale Tanzania. Serikali ika-freeze hiyo akaunti wakati Kambona yuko Holland akipata matibabu na wao wakifanya uchunguzi. Sikubali kwamba Kambona hakuwa na pesa. Hata kama aliishi kimaskini Uingereza. Sources zinasema alikuwa na cash nyingi sana Nairobi baada ya kutoroka 1966. Nimeona barua aliyoandika Kambona anamtumia Kwame Nkrumah pesa Guinea 1968. Na 1969, Kambona alimwonyesha P.K. Leballo $70,000 cash ambazo alikuwa anatakaa kutumia kwa mipango yake ya kupindua nchi. Mzena alitoa ushahidi huo alipoenda mahakama wakati wa kesi ya 1970.

Kwa ujumla wengi waliokuwa katika kikundi cha "radicals" hawakufika mbali. Wote walikwisha. K. Geugeu, Eli Enangisye, Michael Kamaliza, Chipaka brothers, Gray Mataka, Bibi Titi Mohamed, Hanga, Babu, Tambwe, Major Herman, Colonel Chacha, wote walikuja ku-losti. Mpaka Director of CID, Akena, alitiwa ndani kwa kum-tip Kambona kuhusu arrest warrant. I.M. B. Munanka nae alikuwa suspect kwa sababu ya uhusiano wake na Kambona. UCLA trained Dr. Wilbert A. Klerruu alipewa posti nzuri 1966, ingawa alikuwa upande wa Kambona. Aliuliwa baadaye katika hali ya utatanishi 1973. Inasemekana mkulima aliyemuua Dr. Klerruu alikuwa mmoja wa watu wakwanza kunyongwa na serikali.

Kuna mengi ya kuendelea, lakini ngoja niishie hapo. Kambona aliharibu sana pale alipotaka kujaribu kupindua nchi pamoja na kuwa na mawazo mengine mazuri. Kwa hilo alichemsha sana. NO EXCUSE FOR THAT!
 
Bin Maryam,
Nimejaribu sana kusoma kuhusu mapinduzi ya Zanzibar na maasi ya 1964. Sijaona jipya lililosemwa hapa.

Hebu tuambie: kulikuwa na sababu gani ya kupindua serikali 1964? Ulikuwa unataka tutawaliwe na Sultani nini?

Ni kweli Marekani ilifanya mambo mengi ya kijasusi Afrika kipindi kifupi 1960-66, ikiwa ni pamoja na kumtoa Nkrumah. Kuhusu "Western Plot" ya 1964, nimeona documents nyingi, na nime-conclude kwamba haikuwa na ukweli. Kwanza, Top Secret document niliyo quote hapo juu ya wamarekani inaonyesha walikuwa tayari kutumia jeshi lao kurudisha serikali mapema 1964. Katika vita baridi, Nyerere aliweza kuwamuda east/west vizuri. Pili, viongozi wa serikali, including Nyerere, walikuja kusema documents zilikuwa feki. Lukumbuzya, alimpa balozi wa marekani barua ya serikali kumaliza hiyo ishu ya plot Novemba 1964. Wakasema wanaomba mambo yaishe. Wamarekani wakataka Nyerere aseme publicly, yeye akakataa. Tatizo likaamka tena Desemba 9 UN wakati Permanent Representative wa TZ aliposema "plot" ilikuwa kweli. Mchana wa Desemba 9, ikabidi Nyerere aongelee tena hiyo ishu kwenye speech yake ya independence rally. Akasema serikali imetuma barua US na "these exchanges will be the end of this thing."

Kama una data, sio speculations, sema tujifunze.

1960 Kambona alichemsha. Nyerere alikuwa ana-negotiate details za uhuru, na yeye akaweka demands bila kujadili na viongozi wa TANU. Statement yake ika-complicate negotiations za uhuru.
 
Bin Maryam,
Nimejaribu sana kusoma kuhusu mapinduzi ya Zanzibar na maasi ya 1964. Sijaona jipya lililosemwa hapa.

Hebu tuambie: kulikuwa na sababu gani ya kupindua serikali 1964? Ulikuwa unataka tutawaliwe na Sultani nini?

Ni kweli Marekani ilifanya mambo mengi ya kijasusi Afrika kipindi kifupi 1960-66, ikiwa ni pamoja na kumtoa Nkrumah. Kuhusu “Western Plot” ya 1964, nimeona documents nyingi, na nime-conclude kwamba haikuwa na ukweli. Kwanza, Top Secret document niliyo quote hapo juu ya wamarekani inaonyesha walikuwa tayari kutumia jeshi lao kurudisha serikali mapema 1964. Katika vita baridi, Nyerere aliweza kuwamuda east/west vizuri. Pili, viongozi wa serikali, including Nyerere, walikuja kusema documents zilikuwa feki. Lukumbuzya, alimpa balozi wa marekani barua ya serikali kumaliza hiyo ishu ya plot Novemba 1964. Wakasema wanaomba mambo yaishe. Wamarekani wakataka Nyerere aseme publicly, yeye akakataa. Tatizo likaamka tena Desemba 9 UN wakati Permanent Representative wa TZ aliposema “plot” ilikuwa kweli. Mchana wa Desemba 9, ikabidi Nyerere aongelee tena hiyo ishu kwenye speech yake ya independence rally. Akasema serikali imetuma barua US na “these exchanges will be the end of this thing.”

Kama una data, sio speculations, sema tujifunze.

1960 Kambona alichemsha. Nyerere alikuwa ana-negotiate details za uhuru, na yeye akaweka demands bila kujadili na viongozi wa TANU. Statement yake ika-complicate negotiations za uhuru.

Soma posti yangu vizuri. Nimeweka issues ambazo zingefanya serikali ipinduliwe mwaka 1964. Nilisema sina source yoyote lakini kulikuwa na matukio muhimu ambayo yangefanya mapinduzi yatokee.

Nyie wenye vyanzo, mnatuletea taarifa ili wasomaji tuamini kuwa kilichopo kwenye makaratasi mliyosoma ni ukweli mtupu. Wakati wa kusoma na kuamini kilichoandikwa umepitwa.

Nilichofanya ni kuonyesha matukio ya 1964 na uwezekano wa mapinduzi kuwepo. Huwezi kumlaumu Kambona wakati kuna sababu za kimsingi kuamini kuwa serikali ingeweza kupinduliwa.

Hizo data ulizotoa ni historical documents na kwa kipindi cha sasa hatutakiwi kabisa kuzisoma na kuwa na mtazamo wa 1964.

Uhuru ulipatikana 1961 na mpaka 1964, Tanzania haikuwa na vyombo vya maana vya kikachero au vya kiulinzi. Hivyo hata kama documents zilikuwa feki mwandishi hakuwa Kambona na hakuna sababu ya kumlaumu kwa kile alichoamini.

Collin Powell alitumia documents kuonyesha baraza la umoja wa mataifa kuwa Iraq bado inayo WMD. Collin Powell hana lawama zozote kwa kusoma taarifa alizopewa. Hivyo Kambona asipewe lawama kwa taarifa za kijasusi ambazo yeye hakuziandika.

Kuhusu Kambona kuchemsha na details za uhuru sioni umuhimu wake. Tanzania ilikuwa chini ya umoja wa mataifa na uhuru wetu tulikuwa tunadai New York na sio London na mwaka 1960 Nyerere alikuwa waziri kiongozi, hivyo kulikuwa hakuna details zozote za uhuru. Na katika kipindi hicho Nyerere alikuwa tayari kusogeza mbele uhuru wetu hili Kenya, Uganda na Tanganyika zipate uhuru siku moja.

Kambona alikuwa mwanachama wa TANU lakini alikuwa na uhuru wa kuzungumza mawazo yake kitu ambacho viongozi wengi wa sasa hawana. Kuzungumza mawazo yako sio kuchemsha.
 
Wengi wetu hapa tz ni watu wa kujipendekeza kutokana na hali ya umaskini tuliyonayo.Mtu kuzungumza waziwazi mawazo yako unaogopa kwa sababu ya kuja kutengwa au kuonekana si mwenzetu.hofu pia inaingia moyoni hasa kutoka na malezi ya baba wa taifa hili ya kutisha na kuwaweka watu ndani bila kusikilizwa,kitu ambacho kinachangia fikra za wananchi wengi hadi leo kuwa duni.
Mimi naunga mkono kwa hapo tu.Kuhusu Kambona na Nyerere ni dhahiri kuwa Nyerere alikuwa alimuogopa Kambona na kwa hiyo alishirikiana na mtu ambaye hana iq nzuri yaani Kawawa na walifanikiwa kumwondoa na madarakani na akaenda zake UK.Rafiki yake aliyerudi kwa kuahidiwa msamaha hakusamehewa badala yake aliuawa kwa nyundo akatiwa ndani ya pipa lenye zege la kuzamishwa Indian Ocean maana hadi leo maiti yake haijapatikana.Mchonga alijua hilo maana kabla yake alimdhalilisha mbele ya umati wa watu hapo Mnazi Mmoja na kumuita malaya mkubwa etc etc..kabla hajamkabidhi kwa wauaji wake.
Kama Kambona alikuwa na makosa ni pale alipokataa kuchukua mamlaka ya nchi hii katika yale maasi ya wanajeshi ya 1964.

Mchonga alikimbia na kujificha kwa woga wakati Oscar alikuwa shujaa aliyejitokeza ku negotiate na askari walioasi.

Ninayosema sikuyasoma bali nilikuwa ni kijana mkubwa tu niliyejua nini kilichoendelea wakati huo.
 
[/B][/I]
Ukienda nyuma kidogo utasema Wangoni ni Wazulu, Nyerere ni Mtutsi etc etc

Kwa mtaji huu wabantu wote Wa-Nigeria /Cameroon, si wametokea nyanda za Jos huko?

Wakina Cigwiyemisi walizaliwa na kukulia Dodoma, baba yao alikuwa anakaa karibu sana na Chief Mazengo.It doesn't get any more authentic than that.

sasa u-malawi wa kambona unatoka wapi?
kambona kijiji chake kinaitwa kwambe katika wilaya ya
mbinga, mkoa wa ruvuma. baba yake alikuwa padre wa kianglikana
hapo kijijini na mpaka leo ukoo wake upo hapo kijijini.
 
Alnadaby,
Watanzania si watu wenye fikra duni kama unavyotaka tuamini. Na hii ya kumpakazia Mzee wa watu Mchonga kuwa ndiye alitufanya tuwe na fikra duni, miaka 22 tangu aachie ngazi na miaka nane tangu afariki ni kuashiria kwamba hata wajukuu zetu watakuwa watu wa fikra duni. Na kwa mantiki hiyo Watanzania wataendelea kuwa watu wa fikra duni. I am not buying that.
 
Alnadaby,
Watanzania si watu wenye fikra duni kama unavyotaka tuamini. Na hii ya kumpakazia Mzee wa watu Mchonga kuwa ndiye alitufanya tuwe na fikra duni, miaka 22 tangu aachie ngazi na miaka nane tangu afariki ni kuashiria kwamba hata wajukuu zetu watakuwa watu wa fikra duni. Na kwa mantiki hiyo Watanzania wataendelea kuwa watu wa fikra duni. I am not buying that.

Mie nakubaliana na alnadaby, na katika mjadala huu tumeongelea sana kuwa Nyerere ni problem tena sana(hai na ndani ya umarehemu wake). Hatua ya kwanza kwenda mbele ni kukubali kwamba huyu bwana(mchonga) hakuwa saint, anything short of that, we're doomed!!!!!!!!!!!!!!.Huwezi kukumbatia legacy ya Nyerere na ukategemea mabadiliko Tanzania, ni sawa nakumpaka lipsticks guruwe ukamvisha na gauni halafu ukasema ati si guruwe tena, wakati ni guruwe with lipsticks na gauni!.
 
Bin Maryam,
Kuna system ya kuchambua data kutafuta ukweli. Kwa mfano, fani ya Political Science ina methodology yake ya kuchambua data; hilo ni kweli kuhusu fani zote nyingi. Unaposema wakati wa kusoma makaratasi umepitwa, sijui unataka nini sasa? Data zipo, na kuna njia ya kuchambua hizo data kutafuta ukweli. Unaposema haitakiwa kusoma data sasa hivi na kuwa na mtazamo wa zamani, mimi ningependa kukutaarifu kwamba unaposoma data za zamani ni lazima uziangalie kwa mtazamo wa kipindi unachoongelea. Naona sasa tunacheza sarakasi na maneno tuu. Hamna cha msingi kinachosemwa.

Alnadaby,
Kusema watu wanajipendekeza kutokana na umaskini sio kweli. Tanzania ni nchi maskini. Lakini ukumbuke sisi hatuko pekee. Nchi gani Afrika iliendelea sana kipindi cha 1960s na 70s? Wengine wanasema maskini wakati wanamapesa ya mafuta. Whatever you say about Nyerere's handling of the mutiny, he came on top when its all said and done.

YournameisMINE,
Bila kuangalia Nchi zote za Africa zili-fair vipi kwenye hicho kipindi na kuchambua umaskini wa bara zima, hatutaweza kuendelea kamwe. Tanzania haikuwa pekee. Jiulize kwanini? Kuna matatizo ambayo nchi zote za Afrika zimepitia na zinaendelea kupitia leo. Wale waliokuwa wanadai u-capitalist mbona hawajaendelea? Sera za Nyerere pekee sio sababu hatujaendelea. Neither socialist nor capitalist leaning African states have developed when compared to the rest of the world. Put it in a larger context and lets begin to analyze "why" and "how"
 
Back
Top Bottom