Ukweli usemwe: Aliyeharibu nchi hii ni Mwalimu Nyerere kwa kushindwa kuwapa Watanzania Elimu

Ukweli usemwe: Aliyeharibu nchi hii ni Mwalimu Nyerere kwa kushindwa kuwapa Watanzania Elimu

Kwa mada hii ndugu yangu yafaa Sasa tuwaite hata kenge waje JF kuchukua umember humu na watengeneze ID zao Kama vile Pluto star, Mercury star au Jupiter star! Maana mada Kama hii yako imekaa kikengekenge mnoo!

Ndio, kenge Hana Nidhamu, Kama ambavyo mada yako ilivyokosa Nidhamu kwa mzee wetu mwl Julius Kambarage Nyerere!

Jiulize kwanza Je, familia yako inapaswa kutegemea misingi iliyowekwa na babu yako, kwa ustawi wake?
Je, misingi ileile aliyoweka babu yako ndio ipasayo kuwaongoza wajukuu wako?

Acha ukenge ewe nyota ya Zuhura!
Mpe heshima Nyerere, na kila unapomkumbuka mhurumie kwa kazi mzito aliyofanya kujenga hili Taifa la wahuni Kama ninyi ambao Leo munaishia kumtukana matusi ya nguoni!

Kumbuka yule mzee aliongoza serikali maskini kuliko zote! Kipato Cha serikali yake kilikuwa duni mnoo, si Kama serikali tajiri za akina Kikwete!
Mapato ya miaka mitano ya serikali ya Kikwete, yalizidi mapato ya miaka 24 yote ya serikali ya Nyerere

Zingatia pesa ndogo aliyokuwa nayo, serikali yake iliwajibika kukidhi huduma zote za Jamii, Elimu, afya, maji, umeme, barabara, mishahara, ulinzi na usalama, na mengineyo!

Wewe umesimama na hoja ya miaka 24, vipi huangalii umaskini wa Taifa?
Alikuwa na vyanzo gani hasa kupata fedha lukuki kumwaga mashule Nchi mzima? Enzi zile hata waalimu hawakuwepo, hizo shule angefundisha Nani?

Nyakati zile raia walikataa shule, aliwaswaga wakae kwenye vijiji na aliwahimiza kujenga shule! Walioitika waliweza kukata miti na kujenga shule za udongo na waalimu wawili au watatu waliletwa, na shule ilianza!

Hivi unajua mzigo wa kusambaza vitabu mashuleni Nchi mzima? Hawa marais wako wa siku hizi bado wanashindwa kujaza vitabu mashuleni, ingawa wanaingia madarakani wanakuta shule Zina upungufu wa vitabu na Hadi wanaondoka madarakani wanaacha shule Zina upungufu wa vitabu!
Enzi za Nyerere vitabu vilijaa mashuleni, wanafunzi wanapewa daftari na peni, Elimu bure, si hii ya leo michango miiingi na tunaambiwa Elimu bure!

Mwache yule mzee apumzike!
Wewe na Mimi tulijenge hili Taifa Sasa!
Mambo aliyoanzisha yangedumishwa, Taifa hili lisingekuwa hivi lilivyo!

Watu eti munamlaumu katiba! Hivi Ni kweli? Tunashindwa kuunda katiba? Ule mchakato wa katiba ulisitishwa na Nyerere?
Hio Ni sawa kumlaumu baba yako hajanunua nguo za wewe kuvaa ujanani na uzeeni!
Baba ananunua nguo za utotoni tu, ukikua nunua mwenyewe!

Aliandaa katiba iliyompa uhalali wa vile alivyopenda atawale! Ameondoka hakuwashurutisha watanzania kuendelea kuifuata! Kwani bunge si mnalo? Unapomlaumu Nyerere, huoni unazuia wabunge kuwajibika?
Na ingewezekana vipi abadili katiba ili ang'atuke na kuwaachia marais wenzake msala?
Hilo Ni Jambo la kutekelezwa na wananchi, sikitika kwamba wananchi hawajaamka!

Mataifa mengi, yamebadili katiba, wamejenga uchumi na maendeleo ya Taifa bila kulalama eti Rais wa kwanza hajaweka misingi imara!

Nosense!







Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
You have nailed it,Hongera.Kweli nikikumbuka tuliosoma Shule za Serikali enzi za Nyerere Elimu Bure ilikuwa Bure kweli,kusafiri baada ya kufungwa shule unapewa warrant na masurufu( mkate ma orange squash etc) Ili kujikimu njiani,ukirudi toka likizo unakuwa refunded Nauli,Shule vitabu tele na Hata maabara zilikuwa na reagents siyo sayansi ya sikuhizi Shule nyingi ni mwendo wa kukariri tu.Hiyo Aridhi angeenda mwendo wa tamaa wa majirani zetu Kenya wa Familia Moja ya Kenyatta kumiliki 1/3 ya Aridhi ya nchi cjui wengine tungejenga wapi pa kujenga vibanda vyetu
Nyerere aliacha viwanda Kila Mkoa lakini vyote vimekuwa privatized bila tija yoyote,hapo napo pa kumlaumu Nyerere?
Nyerere tumpongeze alifanya kazi yake,na alipoachia inapaswa tuendelee kuchukua hatua na siyo kujiliza kama mfano wa watoto wa kiume wenye deko wanaomlaumu baba yao eti hakuwaachia nyumba za urithi,wakati wapo wengi ambao wamepewa elimu na kujijengea Maisha Yao bila kulilia urithi.
 
Nyerere unamuonea bure.

Nyerere amekuta nchi iko so disorganized, magonjwa, ujinga, umaskini wa kutupwa na ukabila

Nyerere alikua na mlima mrefu sana wa kupanda, kwanza kuhakikisha chembechembe za ukabila zinakufa na kuleta umoja, kupambana na ujinga, kuhakikisha watu wanajua hata kusoma na kuandika. Ulitaka awape elimu gani kama hata kusoma na kuandika hawajui? Ulitaka awape elimu ya uraia wakati hata kusoma hawajui?

Mwalimu kakuta pepopunda, surua, polio, kifua kikuu, kifaduro, kwashakoo na magonjwa mengine yametamalaki kwa watanzania, ulitaka awape alimu ya uraia huku akiwaacha wafe?

Mwalimu kakuta Watanzania ni mafukara wa kutupwa, hawana matumaini ya kesho, akaanzisha vijiji angalau wawe pamoja ili iwe rahisi kuwaletea maendeleo kwa sababu walikua so scattered and disorganized, akaanzisha mashamba ya ushirika ama sustainable farming, akahakikisha anapeleka watu shule wakasome waje wampokee ma kubadilisha nchi kina Chenge na wengine, matokeo yake, wamekua wezi.

Nyerere alipigana kuanzisha viwanda, mashamba ya vijiji, na mambo mengine mengi bila kuuza ardhi hata kipande kimoja kwa waarabu wala wazungu.

That man died poor, had nothing kwa kuwapigania Watanzania

Na alivyokua mwema yule bwana, alipotoka madarakani aliangalia nyuma, akaona failures zake na success zake, akakiri kwamba kweli kuna mahala alifeli, na sababu kubwa za failure za mwalimu zilikua nje ya uwezo wake, kumbuka oil crisis and financial crisis za 70s and 80's.

Yule jamaa alipoona he can continue failing, akajipumzikia yeye mwenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote. Angeweza kufia madarakani.

Tukubaliane kwamba CCM ndio ya kulaumiwa, ila kumpa Nyerere zigo la lawama ni kumuonea. Yule bwana aliachia hii nchi miaka zaidi ya 35 iliyopita, hao wengine waliofuata walifanya nini?
Nyerere hakupumzika kwa kupenda bali alifosiwa kupumzika,
 
Utakuta hata ukipewa uongoze mtaa , huwezi! Kuongoza Nchi mnadhani jambo Dogo.

Familia zenu mnashindwa kuziongoza.

Bure kabisa.
 
Utakuta hata ukipewa uongoze mtaa , huwezi! Kuongoza Nchi mnadhani jambo Dogo.

Familia zenu mnashindwa kuziongoza.

Bure kabisa.
Angola mbona wameweza? Walikuwa kwenye vita tangu 1975 mpaka 1991 lakini wanatuzidi uchumi kwa mbali.
 
Ndugu yangu Elimu ndio msingi muhimu wa kujenga taifa.

Katika kauli mbiu yake kuhusu maadui watatu wa taifa ilikuwaje akashindwa kuweka mikakati ya maana katika kufuta ujinga?

Hapa tunaongea reality. Nyerere ali fail kuwapatia watanzania elimu.
TATIZO KUBWA LA NCHI HII SIYO ELIMU.

Ni CENTRALIZATION ya KEKI ya Taifa na hivyo imezaa UCHAWA na UNAFIKI.

Watu wanajitoa akili kwa makusudi tu ili kutafuta UGALI.

Pili, kama maamuzi ya kisiasa ndio unayodhani ni sababu, issue ni kwamba ili kuleta mabadiliko kwa ob psychology unatakiwa ni aidha uunganishe watu kwa kutumia COMMON IDEOLOGY. Aidha DINI au KABILA.

Kenya UKABILA ndio nguvu ya kisiasa. Hata urais unategemea ziadi makabila makubwa mawili yaliyounganisha nguvu.

TZ, CUF sasa ni ACT inatumia sana nguvu ya dini kupata wafuasi.

CCM ya Magufuli ilitumia sana ukabila kuvuna kura za MWANZA na Shinyanga na hivyo hivyio Lowassa wa CHADEMA alitumia ukanda kuvuna kura za Arusha NA kILIMANJARO.

Kiuhalisia ingekuwa kila mtu anakula kwa jasho na watu hawapati vyeo kwa uchawa, AKILI ZA WATU WANGETUMIA VIZURI TU.

Hii iko proved.

KABUDI wa TUME ya WARIOBA ni tofauti na kabudi wa MAGUFULI. Same to KITILA MKUMBO, RIOBA (TBC) NK
 
Hilo sio kosa la Nyerere, ni kazi yenu kuitoa CCM sio mtu aliyeondoka 35yrs ago na kufariki over 20yrs ago. Hizo ni cheap excuses
Nimekuuliza njia unanijibu sio kosa la Nyerere . Unajitoa ufahamu ?
 
Kwahiyo unakiri hamna akili za kutatua changamoto zenu zaidi ya kutegemea akili za Nyerere tu? Sasa naelewa kwanini bandari inauzwa.
Hivi umeelewa swali kweli nililo kuuliza au unajitoa ufahamu ?
 
Walimu wako wote walikuwa na degree! Yet unachangina hoja na kwa dharau na tambo!!
Huna tofauti na Chenge na Mkapa, watu walisoma top universities, badala ya kuja kulisaidia taifa kwa elimu zao wakaja kuwa chanzo cha sera mbovu zinazoleta umasikini mkubwa hadi leo.
' Kwenye ulimwengu wa vipofu ,chongo huonekana mfalme" hoja zako zinazidi kuji manifest kwenye tatizo alilotuachia the late mwalimu, la kutunyima elimu bora , wachache waliopenya , badala ya kuwa msaada ndo wanakuja kuwa maadui na tambo..
Kungekuwa na elimu bora usingekuja kunitambia mimi st kayumba , kuwa umefundishwa na walimu wenye degree!

Hakuna tambo yeyote nimekuonesha ndugu, mimi nilikuwa nakuweka sawa uliposema eti mikataba mibovu ni kwaajili ya lugha, hivyo nilikuwa nakujulisha tu yakuwa, hapo Tanzania, kuna shule za serikali (Ilboru na nyingine za vipaji maalumu) na shule za dini na wana aina tofauti ya waalimu na secondari za kawaida.

Seminary za katoliki nyingi walimu ni mapadre na masister ambao hakuna asiye na degree ama zaidi. Kwahivyo, swala sio lugha.
 
Mimi naona kosa kubwa alilolifanya Nyerere ni utaifishaji wa mali za watu binafsi na kuzifanya za umma kisha kushindwa kuziendesha na hatimaye kufa.
 
Back
Top Bottom