Ukweli usio mchungu: Serikali ya awamu ya tano imejitahidi kupambana na ufisadi na ubadhilifu

Ukweli usio mchungu: Serikali ya awamu ya tano imejitahidi kupambana na ufisadi na ubadhilifu

Imefanya yote hayo lakini kuna vitu haviko sawa hapo.

Ukitaka kunielewa twende pamoja mpaka 2025.
 
Umegusa penyewe..

Hizi senema tumezoea. Mwaka ulee movie ilikuwa vichwa vya treni tena vyenye lebo TRC...

Leo eti vijisenti 900m lkn CEO hapo haguswi.
Hapo hapo mafuta ya mabilioni yanapigwa kisses sawa na husikii lolote...

Huyo Kokoko hapo yupo kwa maslahi ya nani ??

Vyanzo vya ufisadi huwa ni miradi mikubwa, iwe ya ujenzi, manunuzi au mikataba ya aina yoyote.
Leo ukiulizwa ndege imenunuliwa kwa sh ngapi hujui, mradi wa Stiglers unajengwa kwa fedha zipi hujui, SGR inajengwa kwa fedha zipi hujui. Mikataba ya madini iliyofanyiwa marekebisho bado yana utata mtupu...
 
Hongera sana kwa wote waliompinga mleta mada!

Rushwa/ ufisadi! Eti hizisimethibitiwa?

Na nani??? Huwezi ukajithibiti mwenyewe!

Serikali ganinafungakila mtu mdomo ili hata mtu akisikia trilion 2.4 hazionekani zilipo, hakuna hata moja anayeruhusiwa kuomgea ukweli huo! Au kuuliza?

Utajuaje ukweli kama watu hawana uhuru wa kutafiti na kusema ukwel???
 
Kivipi? Twende pamoja?
Yaani watu wanalia ajira huku.
Harafu ukiangalia ada kubwa, wengine wanadaiwa mikopo hawajui watarudi lini huku hawana ajira.
Wakiamua kujiajiri watengeneze walau simu wapate pakutoa hela, serikali inawaambia wawe wamesoma VETA au DIT.
Twende pamoja utanielewa
 
Yaani watu wanalia ajira huku.
Harafu ukiangalia ada kubwa, wengine wanadaiwa mikopo hawajui watarudi lini huku hawana ajira.
Wakiamua kujiajiri watengeneze walau simu wapate pakutoa hela, serikali inawaambia wawe wamesoma VETA au DIT.
Twende pamoja utanielewa
Haya uliyaeleza yanahusiana vipi na mapambano dhidi ya ufisadi?
 
Umegusa penyewe..

Hizi senema tumezoea. Mwaka ulee movie ilikuwa vichwa vya treni tena vyenye lebo TRC...

Leo eti vijisenti 900m lkn CEO hapo haguswi.
Hapo hapo mafuta ya mabilioni yanapigwa kisses sawa na husikii lolote...

Huyo Kokoko hapo yupo kwa maslahi ya nani ??
Nadhani Kiki na scandals za black brained people( wasanii) zilisolve tatzo la ufuatiliaj
 
Vyanzo vya ufisadi huwa ni miradi mikubwa, iwe ya ujenzi, manunuzi au mikataba ya aina yoyote.
Leo ukiulizwa ndege imenunuliwa kwa sh ngapi hujui, mradi wa Stiglers unajengwa kwa fedha zipi hujui, SGR inajengwa kwa fedha zipi hujui. Mikataba ya madini iliyofanyiwa marekebisho bado yana utata mtupu.

Ufisadi huwa unafichuliwa na Vyombo huru vya habari, Wapinzani walio huru kufanya shughuli zao za kisiasa pamoja na Wanaharakati ambao haki zao zinaheshimiwa na kulindwa. Katika utawala huu hakuna chombo hata kimoja kati ya hivi ambavyo vipo huru kusema. Huwezi sema hakuna ufisadi eti kisa rais wako anasema anapambana na Majizi.

Mfano kwenye suala la e- passports, John Heche alizungumza kuwa kuna ufisadi ulifanyika katika uingiaji wa Zabuni lakini kilichofuata ni yeye kutishiwa maisha badala ya kuambiwa atoe ushahidi na uchunguzi ufanyike.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Ndugu Abbas ambaye pasina shaka alionekana kutimiza wajibu wake kwa maadili makubwa aliondolewa kwa sababu za kutengeneza. Unatoa wapi huo udhubutu wa kusema serikali ni safi hii.

Kama umeanzisha mada kwa lengo la kuingiza siku basi najutia muda wangu niliotumia kukujibu, ila kama ulianzisha kulingana na uelewa na upeo wako basi tumia majibu yangu kutafakari maoni yako.
Mleta mada anaikwepa kabisa hii comment!
 
Moja kwa moja kwenye mada husika wadau wa Jf.

Huko nyuma ilikiwa ni aibu maana watu walikuwa hawafanyi ufisadi bali ni kujichotea na kujijazia. Fikiria skendo la Escrow watu walichota bil of Tsh kama wanachukua sh mia mbil ya kula karanga.

Alichofichua leo waziri mkuu ni ushahidi tosha kuwa kuna madiliko makubwa, tulizoea kusikia watu wakichota bil 60+,bil 150+ na ilikuwa kama watu wanajichotea karanga kwenye mfuko wa bibi.Vipi kama ingekuwa kama enzi za Kagoda,Epa na Meremeta. Ilikuwa ni aibu sana. Najua kila mtu anakubali kuna mabadiliko makubwa.

Leo hii wanaopiga Mil 900 wanadakwa na kushughulikiwa! Maana yake ni kuwa hata upigaji wa dili kubwa zilizosababisha tukashindwa kujenga hospita za wilaya,vituo vya afya na zahanati umebanwa.

Najua kuna wabongo wenye roho za korosho dhidi ya Ccm na serikali yake watasema hamna mabadiliko.

Nyankurungu@ Buzirayombo on the way to Chato on vacation.
Sema awamu hii wanaopiga ni wachache sn, tuambie utajiri wa Makonda na Mnyeti wa kupindukia walifanya biashara gani?
 
Back
Top Bottom