Ukweli usio mchungu: Serikali ya awamu ya tano imejitahidi kupambana na ufisadi na ubadhilifu

Ukweli usio mchungu: Serikali ya awamu ya tano imejitahidi kupambana na ufisadi na ubadhilifu

Ni kweli ila imeshindwa kutenganisha kati ya ufisadi na biashara, na imesababisha uchumu wa watu kutetereka.
 
Huna hoja za kujadili na watu,umegeuka mganga mpiga ramli.
Mkuu, nilidhani umeanzisha uzi ili watu wajadili kwa mitazao mbalimbali, mingine kukubaliana, mingine kuweka nyongeza na mngine hata kupingana na maudhui ya mada yako. Lakini naona kama vile unapanic na kujibu kimipasho mipasho
 
Vyanzo vya ufisadi huwa ni miradi mikubwa, iwe ya ujenzi, manunuzi au mikataba ya aina yoyote.
Leo ukiulizwa ndege imenunuliwa kwa sh ngapi hujui, mradi wa Stiglers unajengwa kwa fedha zipi hujui, SGR inajengwa kwa fedha zipi hujui. Mikataba ya madini iliyofanyiwa marekebisho bado yana utata mtupu.

Ufisadi huwa unafichuliwa na Vyombo huru vya habari, Wapinzani walio huru kufanya shughuli zao za kisiasa pamoja na Wanaharakati ambao haki zao zinaheshimiwa na kulindwa. Katika utawala huu hakuna chombo hata kimoja kati ya hivi ambavyo vipo huru kusema. Huwezi sema hakuna ufisadi eti kisa rais wako anasema anapambana na Majizi.

Mfano kwenye suala la e- passports, John Heche alizungumza kuwa kuna ufisadi ulifanyika katika uingiaji wa Zabuni lakini kilichofuata ni yeye kutishiwa maisha badala ya kuambiwa atoe ushahidi na uchunguzi ufanyike.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Ndugu Abbas ambaye pasina shaka alionekana kutimiza wajibu wake kwa maadili makubwa aliondolewa kwa sababu za kutengeneza. Unatoa wapi huo udhubutu wa kusema serikali ni safi hii.

Kama umeanzisha mada kwa lengo la kuingiza siku basi najutia muda wangu niliotumia kukujibu, ila kama ulianzisha kulingana na uelewa na upeo wako basi tumia majibu yangu kutafakari maoni yako.
Asante sana mkuu.
 
Kuna upambanaji wa ufisadi au kupambana na matumizi ya neno fisadi? Huwezi kupambana na ufisadi huku ukiwa adui wa uhuru wa vyombo vya habari.
Ni CDM na ACT tu wanaopinga kwa makusudi juu ya jinsi Serikali inavyopambana na ufisadi - Dkt John Pombe Magufuli kwa kweli ni mwamba
 
Ni CDM na ACT tu wanaopinga kwa makusudi juu ya jinsi Serikali inavyopambana na ufisadi - Dkt John Pombe Magufuli kwa kweli ni mwamba

Hakuna upambanaji wa ufisadi, bali kuna vita dhidi ya matumizi ya neno fisadi.
 
Ni CDM na ACT tu wanaopinga kwa makusudi juu ya jinsi Serikali inavyopambana na ufisadi - Dkt John Pombe Magufuli kwa kweli ni mwamba
Ana umwamba gani yeye mwenyewe mwizi tu yule.
Alishiriki kuuza nyumba za umma kwa mahawala zake kina kabula wale alikuwa akiwafuata mabibo hostel usiku.
Alinunua nyumba za NIC Kwa shilingi laki 6 Kyle dodoma. Yani ghorofa linunuliwe kwa laki 6???
Alipora KOROSHO za WAKULIMA?
Aliita watengeneza ndege na kukaa nao akiagiza ndege atakazo vila kufuata sheria za manunuzi ya umma?
Huyo ndiyo mwamba wa kupambana na ufisadi?
 
Hakuna upambanaji wa ufisadi, bali kuna vita dhidi ya matumizi ya neno fisadi.
Labda ungejenga hoja hii kwa kutoa mifano - nachojua ni kwamba kipindi cha nyuma ukipita na gari zuri watu waliongea "ufisadi", mikataba mingi ilikuwa ten %, watu walihamisha fedha kinyemela nk

Utawala huu umedhibiti hali hii na kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za umma
 
Wakati huo ufisadi mkubwa unafanyika ni chama gani kilikuwa madarakani na discount ya ndege iko wapi na ni kiasi gani.

Kisha ule uwanja wa ndege wa Chato ulijengwa kwa fedha kiasi gani mbona imekuwa siri na fedha za covid-19 zilizotolewa na wazungu zilitumikaje.

Wakati unaandika usiandike kama vile unaandikia jukwaa la watoto wa chekechea.

Please be advised accordingly.
 
Labda ungejenga hoja hii kwa kutoa mifano - nachojua ni kwamba kipindi cha nyuma ukipita na gari zuri watu waliongea "ufisadi", mikataba mingi ilikuwa ten %, watu walihamisha fedha kinyemela nk

Utawala huu umedhibiti hali hii na kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za umma

Kinachokufanya uamini ufisadi umeisha ni kwakuwa vyombo vya habari haviko huru kuongea, na wapinzani ni marufuku kukosoa. Unapoondoa mfumo wa Open Government jua unapigwa mchana kweupe.

Wakati mwingine ni vyema ukakaa kimya tu, unafuatilia matumizi ya fedha za umma, huku serikali inafanya kazi barabarani kati ya Dodoma na Da! Jaribu kufuatilia uone pesa ya umma inavyopotea kwa safari zisizo na tija kwa viongozi kutoka Dar kwenda Dodoma na kinyume chake. Ni kweli miradi ilikuwa na 10%, je manunuzi ya hizi ndege unajua bei yake kwa uhalisia? Ujenzi wa bwawa la SG una uhakika na bei yake?
 
Manunuzi na ujenzi wa miundombinu watu wanapiga kama kama ila uwe kipenzi cha godfather
 
Hongera umeongea ukweli ambao mababeli wengi hawapendi kusikia, kwa sasa nchi ina nidhamu kubwa sana.
 
Neno fisadi limezaa mafisadi wanaopigwa nyundo. Hujapata majibu jinsi mafisadi wanavyobanwa?

Ukishafanya mambo kwa kificho huna uadilifu wa kubana mafisadi, sana sana utakachofanya ni uonevu wa kimadaraka.
 
Moja kwa moja kwenye mada husika wadau wa Jf.

Huko nyuma ilikiwa ni aibu maana watu walikuwa hawafanyi ufisadi bali ni kujichotea na kujijazia. Fikiria skendo la Escrow watu walichota bil of Tsh kama wanachukua sh mia mbil ya kula karanga.

Alichofichua leo waziri mkuu ni ushahidi tosha kuwa kuna madiliko makubwa, tulizoea kusikia watu wakichota bil 60+,bil 150+ na ilikuwa kama watu wanajichotea karanga kwenye mfuko wa bibi.Vipi kama ingekuwa kama enzi za Kagoda,Epa na Meremeta. Ilikuwa ni aibu sana. Najua kila mtu anakubali kuna mabadiliko makubwa.

Leo hii wanaopiga Mil 900 wanadakwa na kushughulikiwa! Maana yake ni kuwa hata upigaji wa dili kubwa zilizosababisha tukashindwa kujenga hospita za wilaya,vituo vya afya na zahanati umebanwa.

Najua kuna wabongo wenye roho za korosho dhidi ya Ccm na serikali yake watasema hamna mabadiliko.

Nyankurungu@ Buzirayombo on the way to Chato on vacation.
Aliyeshinda tenda ya ujenzi uwanja wa chato alishindanishwa na nani,tenda ilitangazwa lini,uligharimu kiasi gani?
Trilioni za Assad vipi?
Sare za polisi makontena na makontena ya Lugola zipo wapi?
Sanamu la Mwl.Nyerere lilitafuna kiasi gani?
Ununuzi wa ndege kwa cash mchakato wake ulifuata taratibu,upi?
Fedha za TRA Kisutu Branch ziko wapi na kiasi gani kimeshakusanywa hadi jana?

Watanzania siyo wajinga!
 
Nilijua tu mtajitokeza kupinga haya mafanikio. Unataka uhuru gani wa habari ambao unaakisi mapambano ya ufisadi?
Tuwe wakweli nidhamu imeboreka,wakati huo huo ufisadi na rushwa bado vinafanyika na vingine vinaonekana kawaida.Yafaa tujipangie madaraja kwa vipimo tutakavyo kubaliana mafanikio ni yapi na kushindwa ni kupi hii itatusaidia kama taifa.
 
Moja kwa moja kwenye mada husika wadau wa Jf.

Huko nyuma ilikiwa ni aibu maana watu walikuwa hawafanyi ufisadi bali ni kujichotea na kujijazia. Fikiria skendo la Escrow watu walichota bil of Tsh kama wanachukua sh mia mbil ya kula karanga.

Alichofichua leo waziri mkuu ni ushahidi tosha kuwa kuna madiliko makubwa, tulizoea kusikia watu wakichota bil 60+,bil 150+ na ilikuwa kama watu wanajichotea karanga kwenye mfuko wa bibi.Vipi kama ingekuwa kama enzi za Kagoda,Epa na Meremeta. Ilikuwa ni aibu sana. Najua kila mtu anakubali kuna mabadiliko makubwa.

Leo hii wanaopiga Mil 900 wanadakwa na kushughulikiwa! Maana yake ni kuwa hata upigaji wa dili kubwa zilizosababisha tukashindwa kujenga hospita za wilaya,vituo vya afya na zahanati umebanwa.

Najua kuna wabongo wenye roho za korosho dhidi ya Ccm na serikali yake watasema hamna mabadiliko.

Nyankurungu@ Buzirayombo on the way to Chato on vacation.
NIDA,kitwanga,Lugola,Bandari,x,y,z,,,,,,
nk!!!!!??
 
Back
Top Bottom