Ukweli usiopingika: Miaka 47 tangu CCM izaliwe lakini haijatendea haki watanzania kwa kuleta maendeleo stahiki.

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Angalia maziwa ,mito na vyanzo vya maji vinavyopatikana hapa nchini. Alafu kuna watanzania wanakosa maji safi salama ya kunywa. Kodi na vyanzo kibao vya mapato vipo.

Angalia madini kama Tanzanite, almas na hata ruby pia Alexandrite. Madini haya yanatosha kabisa kuwa chanzo cha mapato kwa taifa letu.

Leo hii miaka 47 tangu CCM iwe izaliwe. Lakini huduma za afya ni changamoto kwa raia maskini. Akina mama wanakosa dawa, raia masikini wananyimwa miili ya ndugu zao wakifia mahospitalini. Dawa nyingi raia maskini wanananunua kwa pesa zao.

Huko vijijini mabarabara hayapitiki kwa mwaka mzima. Mvua zikinyesha kila kila kitu tabu.

Sasa miaka 47 CCM wamekwama wapi?
 
Uliacha kuisapoti?
 
Ccm wenzio watakupopoa mawe
 
Ccm ukiwa mjinga tu ndio utaipenda vinginevyo uwe mpigaji kama wao.
 
Philosopher Plato aliwahi sema sio kila mtu anapaswa kuwa kiongozi,ndio maana Kuna mabwana na watwana.

Kwa kuangalia muono wa Plato ni ukweli ulio wazi kwamba "Mwafrika anatakiwa kuwa mtawaliwa tu na watu weupe wawe viongozi".Hili hata Kaburu Botha aliliona na kusema ukweli "mwafrika hawezi kujitawala" ndio maana hata katika mipango ya maendeleo ya Taifa la Afrika kusini hawakushilikishwa.

Ni muda tukubali tu,waje Wazungu,Wachina,wakorea,wajapan,wasingapore nk kutuongoza,sisi ngozi nyeusi hatawezi.
 
Siyo sahihi hata aje Biden hataweza, kinachotutesa ni mifumo ovu
 
Nchi hii chini ya sisiyemu haiwezi kuendelea hata siku moja viongozi hawako serious na maendeleo yetu wanaendesha comedy tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…