Ulaya yakataa kununua gesi ya Urusi kwa sarafu ya taifa hilo

Ulaya yakataa kununua gesi ya Urusi kwa sarafu ya taifa hilo

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amepuuzilia mbali takwa la rais wa Urusi, Vladimir Putin la kuyataka mataifa ya Ulaya kununua gesi kwa sarafu ya Kirusi, huku akimshutumu rais huyo kuwa mwenye nia ya kutaka kuvikwepa vikwazo alivyowekewa kutokana na uvamizi wake wa Ukraine.

Macron aliwaambia waandishi wa habari baada ya Mkutano wa Kilele wa Umoja wa Ulaya wa mjini Brussels kwamba hatua ya Urusi haipo katika makubaliano na haoni sababu ya kutekelezwa kwa jambo hilo. Rais Putin alitoa takwa hilo juma hili katikia kipindi hiki ambacho serikali yake inakabiliwa na vikwazo vikali vinavyoathiri uchumi wa taifa hilo, kutokana na hatua yake ya kuingia kijeshi nchini Ukraine.
61243721_303.jpg

Source: DW
 
Hii ngoma bado mbichi Putin anapiga kwenye moyo vizuri Sana ,ngoja tuone mwisho wake

Hata hajui anachofanya putin, hata Govana wake wa central bank ambae amesoma Yale universit pale marekan anafahamu, anajitekenya tuu reserve yake yoote iko kwenye form of $ nan ataenda kwe ruble[emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amepuuzilia mbali takwa la rais wa Urusi, Vladimir Putin la kuyataka mataifa ya Ulaya kununua gesi kwa sarafu ya Kirusi, huku akimshutumu rais huyo kuwa mwenye nia ya kutaka kuvikwepa vikwazo alivyowekewa kutokana na uvamizi wake wa Ukraine.

Macron aliwaambia waandishi wa habari baada ya Mkutano wa Kilele wa Umoja wa Ulaya wa mjini Brussels kwamba hatua ya Urusi haipo katika makubaliano na haoni sababu ya kutekelezwa kwa jambo hilo. Rais Putin alitoa takwa hilo juma hili katikia kipindi hiki ambacho serikali yake inakabiliwa na vikwazo vikali vinavyoathiri uchumi wa taifa hilo, kutokana na hatua yake ya kuingia kijeshi nchini Ukraine.
View attachment 2164574
Source: DW

Walioweka vikwazo hawataki wawekewe vikwazo [emoji16][emoji16]
 
Urusi hawezi kushindana na dunia
Qatar karudia kusema ni uamuzi wa kijinga kuachana na gesi ya Urusi kwa nchi za ulaya na zaidi ni kitu kisichowezekana kufidia gepu la 40℅ ya gesi kwenye soko la dunia si kwa Leo wala kesho HAIWEZEKANI.

Putin ni simba mwenda Pole, uchumi wa dunia unaenda kutikiswa kwa kiwango kisicho elezeka.
 
Russia lazima iheshimu terms of contract ambayo inasema malipo yatafanywa kwa sarafu za dola/euro/pound, period hayo mambo ya sijui ruble yanatoka wapi tena.

Kama anavunja mkataba kuna gharama yake vilevile ya kulipa damages for the breach of contract gharama ambayo kwa hali yao ya sasa hawawezi kumudu kulipa.

Putin anajaribu bila mafanikio kuokoa sarafu yake isiporomoke lkn hana jinsi kwani ameshashika mavi lazima awe mpole, uchumi lazima uporomoke tu.
 
Qatar karudia kusema ni uamuzi wa kijinga kuachana na gesi ya Urusi kwa nchi za ulaya na zaidi ni kitu kisichowezekana kufidia gepu la 40℅ ya gesi kwenye soko la dunia si kwa Leo wala kesho HAIWEZEKANI.

Putin ni simba mwenda Pole, uchumi wa dunia unaenda kutikiswa kwa kiwango kisicho elezeka.
Watu sasa ndio wanaongeza kasi ya kuwekeza kwenye Renewable Energy ambaye bado ameweka akili yake kwenye Fossil Fuels atabaki gizani akipigwa baridi.

Hydrocarbons have no future in our modern world 🌎
 
Russia lazima iheshimu terms of contract ambayo inasema malipo yatafanywa kwa sarafu za dola/euro/pound, period hayo mambo ya sijui ruble yanatoka wapi tena.

Kama anavunja mkataba kuna gharama yake vilevile ya kulipa damages for the breach of contract gharama ambayo kwa hali yao ya sasa hawawezi kumudu kulipa.

Putin anajaribu bila mafanikio kuokoa sarafu yake isiporomoke lkn hana jinsi kwani ameshashika mavi lazima awe mpole, uchumi lazima uporomoke tu.
Umenena vyema, russia kutaka malipo yawe kwa ruble maana yake anataka aipe thamani pesa yake ktk uchumi ambae anaona mbele utamsumbua zaidi na sio kwamba anaikomoa NATO.

Mambo yakienda hivi, uchumi wa NATO na Russia utatetereka mno apo mbeleni, sijui kwanini Africa hasa TZ tusitazame hizi fursa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom