Ulazima wa Kiingereza cha Rais Samia ziarani nchini Kenya

Kafie huko Kama juju Kiingereza shauri zako. Kiswahili ni Cha waarabu, heri ya Kiingereza kuliko kiswahili
 
Jiwe alielekea kuleta shida nchi hii. Nyerere wakati anang'atuka alisema "msikidharau English, kwa kuwa ni Kiswahili cha dunia". Sasa leo mtu anazuka na hoja ya ajabu. Kwani huko Kenya Rais Samia alikuwa anaenda kuwahutubia waTz ?!. Ujinga mtupu
 
Hii lugha ya kiswahili haina soko. Kwasabb ilipaswa kubeba teknolojia/maarifa ambayo ndiyo yangevutia watu kujifunza kiswahili
Magufuli kawaharibu wengi unaona eh! Science yote ni English Sasa usipojua Kiingereza unajidanganya làbda Kama huhitaji Kiingereza sawa.
 
Audience ya Uganda ukitumia Kiswahili utakua unaongea na sehemu ndogo sana ya population ila kwa Kenya, jamii kubwa sana wanaweza kuelewa Kiswahili.
 
Kenya medium of instruction ni Kiingereza, Sasa aatafanyaje? Mkalimani? Haya twende
 
kiingereza ni lugha ya kimataifa, lugha ya biashara .
Hata Kiswahili ni lugha ya kimataifa na ya kibiashara pia.

Kenya, Uganda, Rwanda, Congo... huko kote tunawasiliana nao na kufanya nao biashara kwa lugha ya Kiswahili.

Kwahiyo, kwa muktadha huo, Kiswahili kinakidhi sifa ya kuwa lugha ya Kimataifa na Kibiashara.

Ni vile tu ulishakaririshwa kwenye shule ya kata uliyosomea kwamba, ili kitu chochote kiwe cha "kimataifa" lazima kihusishe Ulaya.
 
Kuchanganya elimu na siasa ndio kumetufikisha hapa,hadi mtu anasema kila'' msomi anajisikia fahari kuongea Kiingereza''ndio maana yake ndio lugha aliyoitumia kwenye elimu yake yote ya juu usipoweza kuzungumza kwa ufasaha halafu unajiita Dkt basi shida ipo tena kubwa tena nadhani ni hapa kwetu tu,kiingereza unakikwepea wapi lugha ya kiswahili kinyakyusa na zinginezo ni za kuvunia mipunga na tu na kuchungia ng'ombe.
 
Umeandika kwa kisirani kikubwa! Haifai!
Ungeweza kuwasilisha hoja yako kwa kuzingatia ustaarabu wa nchi yetu ungeeleweka vema, lakini kwa namna ulivyowasilisha unaonekana una msongo wa mawazo wa kutoifahamu vizuri lugha ya Malkia!
 
Kenya medium of instruction ni Kiingereza, Sasa aatafanyaje? Mkalimani? Haya twende
Twende wapi kwa mfano?

Kamanda una mihemko sana, vipi uko mwezini nini?

Hata Tanzania "medium of instruction" ni Kiingereza pia. Lakini tunazungumza Kiswahili kama ilivyo Kenya.

Kwani we unaishi wapi Kamanda? Ulaya?
 
Duuuh Rais wetu anajua cha kufanya hahitaji nguvu nyingi kumweleza cha kufanya kama mwendazake kilimshinda basi Rais msimpangie cha kufanya. Ni aibu kuwa na Rias asieweza kuwasiliana kwa kiingereza fasaha kwa nchi inayofundisha kwa lugha ya kiingereza na kwa faida ya nani. Unaweza kukuta wanao wapo english medium huku unasema Rais azungumze kiswahili.
 
Meko, umefufuka nini?
 
Umeamua kumuua kabisa!
 
"Atakavyojitutumua na viingereza vyake uchwara" mkuu umekosea sana kuandika hii sentensi kwani kakukosea nini?
Uzi wako umeubadirisha kutoka ushauri hadi kejeli.
 
Commonwealth ipi wewee, wacha kujitutumua hapa.

Nina uhakika hata maana tu ya "Commonwealth" huijui.

Haya kamanda, hebu tueleze... "Commonwealth" ni kitu gani?
Duh, yaani niandike hoja inayohusu Commonwealth halafu nisijuwe Commonwealth ni nini? Umenidharau Sana kwa kweli!
Siwezi kukujibu swali lako
 
Duh, yaani niandike hoja inayohusu Commonwealth halafu nisijuwe Commonwealth ni nini? Umenidharau Sana kwa kweli!
Siwezi kukujibu swali lako
Commonwealth ni kitu gani?

Hebu tueleze, wacha kujibaraguza kamanda.
 
Wewe jamaa ni mjinga.Umeanza lini kumkejeli mh.raisi acheni dharau zakishamba uku kwenye mitandao.Mama ataona mwenyewe kipi kinamfaa kulingana na kilichompeleka uko sasa wewe ni nani hadi ujifanye mshauri wa raisi tena kwa kukejeli.acha ulimbukeni.
 
Kuandika kwenyewe hujui.

Basi ni vile tu hii mitandao inazoa every "tom and dick" — na wao wanajifanya wajuzi.

Sasa wewe bwana mdogo, kuandika tu hujui, halafu unalilia viingereza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…