Ulazima wa Kiingereza cha Rais Samia ziarani nchini Kenya

Ulazima wa Kiingereza cha Rais Samia ziarani nchini Kenya

Asije akaambatana na waziri Fulani Prof mwenye kumuhemuhe Cha kuongea kiingereza hasa na wachina wanaochelewesha kazi.
 
Wabongo bhana vitu vingi tunatumia vya mzungu ila kwenye lugha ya kimataifa ya biashara mnaona ni kusujudia...jamiiforum hii ipo hapa kwa ajili ya tekinolojia za mzungu ndio mimi na wewe tunasawaliana tumeacha hadi kupanda punda...
Wapi nimesema kusujudia?!

Kenya wanazungumza Kiswahili, Tanzania wanazungumza Kiswahili! Sasa unaweza kutaja sababu za msingi za kutaka kutumia Kiingereza badala ya Kiswahili?!
 
kingereza ni lugha ya biashara za kimataifa
Ulishakaririshwa kwenye shule ya kata uliyosomea kwamba, ili biashara iwe ya "kimataifa" lazima ihusishe ulaya ambapo kuna Kiingereza.

Biashara tunazofanya na somalia, Kenya Burundi na Rwanda, sio za "kimataifa" kwa kuwa tu hazihusishi ulaya na hazitumii Kiingereza.

Kwa kweli ningekuwa waziri wa elimu ningefunga shule zote za kata mpaka nipewe mwongozo unaosema vinginevyo!

Wewe nae umehitimu fom foo?
 
Uganda akiongea Kiingereza, sawa tu manake wale jamaa wana bifu na Kiswahili!!

Kenya, kwa kuwakomoa tu, anapaswa atumie Kiswahili manake Kiswahili wanakijua vizuri lakini kutokana na ulimbukeni wao wa kumsujudia Mzungu, wanajifanya hawakijui!!
Kwani Kivukoni hakufundishwi kiengereza??
 
Tumesikia Bi. Samia anaenda Kenya kwa ziara ya kikazi mnamo hapo kesho.

Ni matumaini yangu na fahari yangu kwamba atatumia Kiswahili katika shughuli zote atakazoalikwa kuzifanya.

Hivi majuzi tu alipoenda Uganda, tuliona anatumia kizungu kuhutubia.

Wengi wa wananchi wetu nina uhakika hawakuelewa hata anachozungumza.

Ifahamike kwamba, Kiswahili si lugha ngeni Afrika Mashariki. Tuachane na Viingereza pasipo na ulazima.

Sijui ni nani aliyewalaghai kwamba kuongea kizungu ni ufahari na usomi?

Hata katika mazingira yasiyohitaji kizungu, bado watu watajing'ang'aniza kuongea kizungu hata kama hawakiwezi na tunajua kwa hakika kwamba hawakiwezi.

Hebu tuachane na hizi "You Know You know ofcozi zea zea" mingi mingi. Tunajiaibisha na kujidunisha.

Tunayo lugha adhimu ya Kiswahili. Tuitumie hiyo.

Nasubiri kuona hiyo Kesho vile Bibi SASHA atakavyojitutumua na viingereza vyake uchwara.

Ashauriwe vyema. Maana shughuli za aina ile sio mahali pa kuonesha mbwembwe za kuzungumza kwa lafudhi bandia za kimalkia.

Tunahitaji kusikia "maswala" yakijadiliwa na kuzungumzwa. Hatuhitaji mikogo ya lafudhi bandia za Kizungu.
Wanajavi wenzangu kama Mama Atasoma speech zake zote kwa Kiingreza ni sawa tuu, Ila Mama anaongea Kiingereza cha kueleweka. Kuongea kwa ufasaha wa kujivunia lugha ya Kiingereza bado kidogo aongeze jitihada.
 
Kosa letu ni kuwaanzisha watoto wetu elimu ya msingi kwa lugha ya Kiswahili . Halafu tunabadika secondary watoto wakishakuwa na aibu ya kuongea broken English. Ni mpango wa ajabu sana
Hilo nalo ni tatizo!!!

Na kwa upande mwingine, na kwa uzoefu wangu, ni rahisi zaidi kukielewa Kiingereza (in fact, lugha yoyote ile) endapo unakifundisha kama lugha ya pili kuliko kukifundisha kama somo!!
 
Tumesikia Bi. Samia anaenda Kenya kwa ziara ya kikazi mnamo hapo kesho.

Ni matumaini yangu na fahari yangu kwamba atatumia Kiswahili katika shughuli zote atakazoalikwa kuzifanya.

Hivi majuzi tu alipoenda Uganda, tuliona anatumia kizungu kuhutubia.

Wengi wa wananchi wetu nina uhakika hawakuelewa hata anachozungumza.

Ifahamike kwamba, Kiswahili si lugha ngeni Afrika Mashariki. Tuachane na Viingereza pasipo na ulazima.

Sijui ni nani aliyewalaghai kwamba kuongea kizungu ni ufahari na usomi?

Hata katika mazingira yasiyohitaji kizungu, bado watu watajing'ang'aniza kuongea kizungu hata kama hawakiwezi na tunajua kwa hakika kwamba hawakiwezi.

Hebu tuachane na hizi "You Know You know ofcozi zea zea" mingi mingi. Tunajiaibisha na kujidunisha.

Tunayo lugha adhimu ya Kiswahili. Tuitumie hiyo.

Nasubiri kuona hiyo Kesho vile Bibi SASHA atakavyojitutumua na viingereza vyake uchwara.

Ashauriwe vyema. Maana shughuli za aina ile sio mahali pa kuonesha mbwembwe za kuzungumza kwa lafudhi bandia za kimalkia.

Tunahitaji kusikia "maswala" yakijadiliwa na kuzungumzwa. Hatuhitaji mikogo ya lafudhi bandia za Kizungu.
Wewe ndie mwenye kiingereza uchwara! Mama anatiririka sio wewe!
 
Kwani Kivukoni hakufundishwi kiengereza??
Kama Kivukoni ya akina Polepole, sina shaka wanakifundisha... huoni JPM alivyokuwa anabonga ung'eng'e huku akiwashangaa wale wanaosema hajui Kiingereza wakati amesoma "Uraya"!
 
Wanajavi wenzangu kama Mama Atasoma speech zake zote kwa Kiingreza ni sawa tuu, Ila Mama anaongea Kiingereza cha kueleweka. Kuongea kwa ufasaha wa kujivunia lugha ya Kiingereza bado kidogo aongeze jitihada.
Kuna ulazima gani kuhutubia kwa Kiingereza cha kusoma kwenye Karatasi wakati hadhira yote (ya Kenya na Tanzania) inakijua Kiswahili?

Na itakuwa ni ajabu sana, mwenyeji wake wa Kenya azungumze Kiswahili, halafu yeye mtanzania aanze kutusomea hotuba za Kizungu-butu!

Inawezekana kweli yeye ni mjuzi sana wa kusoma hotuba za kizungu, lakini mahala pale sio pa kufanya mbwembwe za ujuzi wa kusoma kizungu kwa mikogo ya lafudhi za kuigiza.

Wananchi wote wa Kenya na Tanzania wana kiu ya kusikia kinachozungumzwa (preferably kwa KISWAHILI).

Yale maudhui yanayotarajiwa kusikilizwa, ndicho hasa wananchi wanachokisubiri kwa hamu.

Sio mikogo ya kizungu-butu.
 
Kwa sasa Kiswahili kimepanuka karibu nusu nzima ya Afrika.

Somalia, Kenya, Sudan, DRC, Uganda, msumbiji, Uganda, Rwanda, Botswana, Malawi, Burundi, China, South Afrika...

Huko kote Kiswahili kinaenea kwa kasi.
Mbona unalazimisha watu, hata rais kufuata mawazo yako ya ajabu kabisa!!!

Kwani mh. Rais akiongea Kiingereza huko Kenya kutazuia Kiswahili kuendelea "kuenea kwa kasi", if at all it's true?
 
Mbona unalazimisha watu, hata rais kufuata mawazo yako ya ajabu kabisa!!!

Kwani mh. Rais akiongea Kiingereza huko Kenya kutazuia Kiswahili kuendelea "kuenea kwa kasi", if at all it's true?
Wewe huna japo uwezo mduchu wa kuelewa mtiririko wa majadiliano.

Umezoea ile midahalo ya sekondari ya maji ni bora kuliko chumvi.

Kama huwezi angalau kusoma na kuelewa, basi kaa kimya — usinipotezee WAKTI.
 
Wewe huna japo uwezo mduchu wa kuelewa mtiririko wa majadiliano.

Umezoea ile midahalo ya sekondari ya maji ni bora kuliko chumvi.

Kama huwezi angalau kusoma na kuelewa, basi kaa kimya — usinipotezee WAKTI.
Duh!
Mkuu, mbona una hasira kama za jiwe (R.i.p) ?!!!
 
Tumesikia Bi. Samia anaenda Kenya kwa ziara ya kikazi mnamo hapo kesho.

Ni matumaini yangu na fahari yangu kwamba atatumia Kiswahili katika shughuli zote atakazoalikwa kuzifanya...
Ukitaka kumfurahisha mgeni au mwenyeji wako zungumza lugha yake.

Pia ukitaka kumjua au kumshinda adui yako jifunze lugha yake.
 
Back
Top Bottom