Uliambiwa nini ukiwa Mtoto lakini baada ya kukua ukagundua ni Uongo?

Uliambiwa nini ukiwa Mtoto lakini baada ya kukua ukagundua ni Uongo?

mapipando

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
2,922
Reaction score
3,559
Habari wanajamvi,

Kumekuwa na desturi ya watoto kudanganywa aidha na watu wazima ama na watoto wenzao kwa malengo tofauti tofauti. Mfano kuogopeshwa tu au kutotakiwa kufanya jambo fulani.

Mimi nilidanganywa kuwa
1. Eti kama mvua inanyesha halafu ukawa unakimbia basi maji yote ya bahari yatakuja na kujaa mahala pote kiasi kwamba nyumba zitasombwa.(Dar)

2. Wanajeshi ama polisi wa kike kazi yao ni kuwapikia wanajeshi ama polisi wa kiume.

3. Mwanaume ukila chakula kwenye chungu ama sufuria utachelewa kuoa ama hutooa kabisa


Wewe ulidanganywa nini?
 
Mama alishawahi kunambia mdgo wangu alonifata kamnunua sehem......kipindi hcho nlikua sijui kama mpka kuzaliwa ni lazma mkwich kwich.....
 
Nilidanganywa vingi...
Nilikuwa napenda sana kulia lia hovyo pengine kitu kidogo nalia,niliambiwa nkilia usiku ni kuita wachawi na wataondoka na sauti yangu nitakuwa bubu. Nikaacha habari za kujiliza Liza na madeko.

Kingine kula muhindi unaambiwa njoo nikuwekee njia ya kwenda kwenu (wanatamka origin yako huko kwenu)
 
Mama alinambia hivi "nilikununua hospital, niliona watt weeengi ila nilipofika kwako tuu,ukanichekeaaa nami nikafurahi na kukuchekea pia,nikakuchua ukawa mwanagu mzuuuri hadi Leo"... Looh niliamini eti nimenunuliwa hospital mpaka nipokuja kujua hahahhaha so funny

Ukimchungulia MTU mzima unapofuka macho[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] n.k
 
Nikifaulu kila mtihani nikiwa wa kwanza afisa usalama watakuja kunirecruit kimya kimya nami nipige hizo mission hii ilinifanya nijitahidi kufanikisha hilo na kila nikipanda darasa nao hawatokei tu na haikutokea hadi nilipojua uongo ila ilinipa msingi mzuri.
 
Back
Top Bottom