Ulianzaje kukaa gheto?

Nilipomaliza chuo 2018 nlirud nyumban lakin wazaz wangu walikuw hawakai hapo waliish mkoa mwngne kikazi...

Nilipofka kwa ndugu zake mzee nlifkia kwa shangaz.

Nilishndwa maisha ya kwa aunt kwasbabu ikifika saa2 ucku hujarud mlango unafungwa nkaona aya maisha sio kabsa nkaamua kushare ghetto moja na washkaj wawil jumla watatu lakin mmilik wa ilo ghetto mmoja tu mi na mwenzang tulipga kitonga...

Cku zlivyoenda yule mweny ghetto akatuambia anatka kuoa ikabdi tuchek utaratbu wa kuhama.

Mwenzang ambae pia hakuw mmilik wa lile ghetto akaachiwa chumba na mjomba ake kwa mda usiojulkana maana alienda nje ya nchi...

Tukahamia apo na mshikaj,,, mara mshkaj akampa ujauzito dem X wazaz wa mwanamk wakamwambia jamaa akae na mwanamke had atakapojfungua mamb mengne yatafuata...

Kichwa kikaanza kuwaka moto, wap niende kwasas??? Lakin kwa wakat huo nilikuw najshughulisha na biashar ndog ndog..

Aisee wazee wakubet mpo??? Cku iyo nkaweka mkeka wa elfu 1000 tu nkachagua timu 11 zenye odds mbili na point, mungu akaniona ukatiki nakumbuka nilipata laki 5 na elf 35....

Nkatafuta chumba maisha yakaendlea nam nnaghetto saiz
 
1st time nasoma hii thread nilikua nakaa kwa bro baada ya kumaliza chuo (2018),nilikua intern kwenye moja ya processing plants huko Geita.

2019 mwishoni bro akawa anavuta jiko hivo kwa kunionea huruma akaniachia baadhi ya vitu kama kitanda na sofa moja la watu wawil na tv 24",ila asikwambie mtu unapiga intern hulipwi cha maana zaidi ya nauli na kuambulia kula hapo kazini,mambo yakawa tight kinoma kodi ikaanza kupiga chenga,nikiwaza kurudisha mpira kwa kipa naona jau,nikaamua kupambana hivo kwa msaada wa bro(kumpiga vizinga vya hapa na pale)

Mungu mkubwa 2021 mwanzoni nikawa nimeitiwa kijinafasi cha kujishkuza kwenye moja ya machimbo mikoa ya kusini,hapo ni mimi na kibegi changu cha mgongonj shuka la kimasai la kujifunika,PC yangu na simu nokia kitochi maana hata Samsung niliotoka nayo chuo nilishauza kwa wakati huo kupunguza ukali wa msoto.

Hapo machimboni nilikua naishi kibishi sana,unalala sehemu wanaziita matanda (watu wa migodinj wanaelewa),nimeweka turubai na kuzungushia kibanda mianzi,afu godoro la sufi nilinunua Nachingwea town Tsh 15k.Sikuwahi hata siku moja kujikweza na kujionaa labda m ni graduate nna ki degree,sasa katika kufahimana na watu,nikaanza kupata deals za kuchenjua (ndio taaluma yangu) kwenye processing plant kama mkemia.Hela ya kwanza ya maana kupata nikapanga chumba Nachingwea mjini,nikanunua smart ili nirudi mjini maana mambo nowadays yako digitalized,godoro na mkeka na kiredio cha bluetooth life likaanza.


Kupitia hio nafasi hapo machimboni niliweza pia kujuana na watu wengi sana na kupitia hao watu nikafanikiwa kupata kazi (yenye maslahi mazuri kwa upande wangu) na kwa sasa walau nauona mwanga,nipo ghetto napambania kombe taratibu,weekends kama hivi unashinda unacheza games plus movies maana msimu wa football ndo umeishia hivo.

NB:Kukata tamaa na kurudisha mpira kwa kipa haipaswi kua option yako no 1.Jah Bless


 
CONGLATULATION BRO
 
Hongera
 
Tunafanana hivyo najiachiaga na mito yangu

Kuna clip ya mdau nilisikiliza jana aisee nikakukumbuka ujue[emoji23][emoji23][emoji23]
Wee mlongo n clip gani huyo?? Hebu nidokezee bas jomoneeeh
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Niienda mbeya,nikarudi nikaelekea tunduru

Nililalaga songea[emoji23]

Yaani niliambiwa boda kutoka stend ya zamani hadi luhuwiko ni sh,15000[emoji23]
Khaaaah wee, mbna hatareee hii, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wayback 2003
Sina life ,Mimi ndiyo mtoto wa kiume ukizingatia bi mkubwa Hana maisha.
Anaishi chumba kimoja.
Ikabidi ni drop kwa bibi ambaye hakuwa ndugu zaidi ya ubibi wa dar haha SI mnaujua ulee wa bibi bibiii.

Nikawa na chill pale ki bishi bishi, siku nyingine nikienda mara mlango umefungwa mara naambiwa nirudi nilipotoka hahaha walikuwa wanalala saa 1. Na Mimi muda huo ndo nakuwa natafuta Dala za kugeukia home .

[emoji16]Siku 1 kama kawaida, nimerudi kwa bibi wa kubatizwa, nikadandia dirisha na kuanza kumuita dogo anifungulie dogo akaropokaa "ahah jamaa unazingua bhna, hapa hakuna mkeo ulitumwa uzaliwe masikini[emoji57]"

Haha mwamba yale maneno yakanichoma, kesho yake mapema nikaamsha kusiko julikana.

Piga sana kazi za mitaro mixer kubeba vifusi nikawa sichagui kazi. Ndani ya mwezi nikaingia ghetto.[emoji16]

Unyama ukawa mwingi likawa siyo ghetto Bali sehemu ya kuchinjia wanafunzi.

Manzi alipewa mimba,piraa likatimba skani tukasombwa wote..
Ile siku selo niliumia sana!!

Kesi nikawa Sina,maana me niliwapa wadau tu ghetto wawe wanalitumia kuchinjia.

Nikaona hapa msala nikahama mkoa mwengine.
Piga sana saidia fundi. Nikawa fundi njaa.
Jah aka bless nikawa na ghetto langu na Mimi official.
Jina likakuwa nikawa na Kila aina ya material ndani ya ghetto. Hamu ikasogea ya kuwa na chumba nasebu. Nikaona uduwanzi hiyo pesa nikaidundulia nikanunua kiwanja.

Material natolea wapi wakati me fundi maiko bhna.
Ndani ya miezi 4 nikawa nachumba mixer sebu ya kishkaji fundi mwenyewe material nimeokoteza site.

[emoji16]cut story.
Dogo aliyenifukuza kwa bibi yake Ali ni inspire sanaa n Nina mshukuru Hadi kesho namuona kama malaika wangu ambaye alitumwa kuniamsha toka kwenye usingzii wa kubweteka.
Kulipa fadhira dogo nilimsomesha na nikamuingiza kwenye kampuni yangu ya ujenzi.

Hadi leo hajuhi KWANINI namjali na kumpenda Sanaa na hiyo sababu sijawah kumpa zaidi ya wife tu.
 
Aahaa we jamaa una moyo mweupe sana.

Yaani dogo alikutamkia maneno mbofu, ila wewe ukayachukulia "in a positive way".

Ndivyo inavyotakiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…