Ulianzaje kukaa gheto?

Ulianzaje kukaa gheto?

Dah nikaona kama harakati za kutafuta mtaji nifungue biashara ili Nikae geto kama inakwama basi nikasema nisubiri sensa. Ikaja nikaaply vzr dah siku ya interview nikafika. Matokeo holla.
Wakuu nikalala ndani siku nzima stress.
Kuna mwana jirani akanipa pole akanipanga ya kuwa kuna eneo lao la familia ila yeye kapewa kipande anataka apande miti so kuna miti pori so nifanye kuchoma mkaa. Fresh nikapiga gunia saba hivi.
Hiyo ni mwezi wa nane mwishoni. Ikanibidi pia nirudi kijijini kuvuna mahindi yangu. Nikiwa kule bimkubwa anaona kijana jobless ikawa jau. Yaani watoto wote mimi sina issue. Unaweza fanya kazi siku tano then jmos ukaamua kupumzika ila siku hiyo utawakiwa kama mbwa.

Inauma aisee. Kuna bro angu akanitumia siku tangazo la kazi mahali fulani hvi. Nikaaply nikaitwa interview.
Baada aya week mbili niko Bush ninapiga kibarua cha kupiga ngano napigiwa simu na Hr ya kuwa nimepita. Imagine kati ya watu 400 nimepita. Tuliopita ni 70 na kitu.
Basi nikaripoti sign mkataba. Hivi jana ndio nimepanga geto la vyumba viwili na nimetengeneza mwenyewe my dream bed.

Nimefupisha stry kuonesha hamu ya vijana wanaomaliza vyuo na wengine pia wakiwa na hamu ya kujitegemea. Tuschague kazi ilimradi haikuvui utu. Displine mazee inahajika sana mpk tutakapopata makazi yetu ya kudumu.
Long live jf.

Jana ndio nimeingia rasmi kwenye getho langu rasmi.
Hongera mkuu
 
Yote haya ya nn? Siwezi ishi nyumba yenye watu zaidi ya wa 4. Full stop.
Afu sipendi uswahili mie.
Nina rafiki yangu anaishi nyumba ina wapangaji wawili tu yeye yupo single yule mwenzie ni mzanzibari anafamilia yaani anapanga masharti kwenye ile nyumba kama yeye ndo father house jamaa akiingiza dem ni shidah yaani full kufuatiliwa
 
Getho bila shughuli ya kuingiza pesa jau mazee. Bora ubaki kwenu usiwe ombaomba kama huna moyo wa kufanya kazi ya kuingiza kipato na kulipa bills. Nimeingia leo getho madirisha wazi. Mwenye nyumba ndio anafunga shata.


Nakupenda jamii forums. Walec una akili sana
Afu pia cocastic sitaki uniponde sijapanga room kali ndio naanza life.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] naomba niwe mgeni wakooo.
 
Nina rafiki yangu anaishi nyumba ina wapangaji wawili tu yeye yupo single yule mwenzie ni mzanzibari anafamilia yaani anapanga masharti kwenye ile nyumba kama yeye ndo father house jamaa akiingiza dem ni shidah yaani full kufuatiliwa
Khaaaaah si amchane makavu, lol. Kodi analipiwa au?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Leo nimeambiwa hapa mtaani ninapokaa kuna mnada wa vitu mbalimbali vya matumizi ya nyumbani so naenda Kuhemea vitu. Nataka leo nianze kutoa vitu mwenyewe. Kuanzia juzi hela ya kula imekwenda nyingi sana.
 
Kizuri,hongera
Ahsante. Nilikitengeneza mwenyewe kwa ku Google. Nikakisafirisha hadi huku bush ila watu majirani wakawa wanshangaa ni nini hiki. Ila dadeki kuna work mate alikipenda tu kabla sijakipanga na kukihamishia hapa. Jumapili nimemtengeneza nae nimekula efu ishirini. Hakina mbwembe nyingi ila ukikipangilia ni hatari fire.
IMG_20221204_160115.jpg
hapa ni wakati niko namtengenezea work mate
IMG_20220616_133115.jpg
hiki hapa ndio nilikuwa natengeneza cha kwangu..
 
Ooooh hapo sasa si mpo watu na business zenu, tunsemea wale wa vyumba na choo ndan, au chumba tupu choo cha kushare watu wote, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hata ikiwa hivyo kama huna maneno mengi mbona unaishi tu. Tatizo la nyumba za hivyo kunakuwa na uswahili.

Sipendi sehemu ambazo watu hufungulia subwoofers Kama wanashindana.

Hapa nilipo unaweza hisi hakuna binadamu
 
Back
Top Bottom