Ulianzaje kukaa gheto?

Ulianzaje kukaa gheto?

Wadau wa ghetto hamjambo? Mimi nilianza maisha ya ghetto mwezi wa 5 mwaka huu.Naishi maeneo ya uswahilini sana.Sasa jana wakati narudi kutoka kwenye mishe zangu nikakuta nimeibiwa hela.Ni shilingi elfu hamsini tu, kiukweli ni hela ndogo sana lakini ninavyoipata kwa shida inasababisha iniume kwa kweli.Kitu kibaya zaidi wakati naanza maisha ya ghetto bi mkubwa alinionya sana kuweka hela cash chumbani nilipopanga .
Kuweka hela ndogondogo kwenye simu naona ni usumbufu haswa pale inapokatwa wakati wa kutoa. Inaniuma sana yani nimeingia kanisani huku nina kinyongo.
Muwe na Jumapili njema.
Kama chumba chako kina tiles, bandua moja vizuri bila kuacha alama, halafu tengeneza space ya kufanya bank. Hakuna mwizi hapo labda umwonyeshe demu wako maana Kuna watu viherehere sana.
 
Kama chumba chako kina tiles, bandua moja vizuri bila kuacha alama, halafu tengeneza space ya kufanya bank. Hakuna mwizi hapo labda umwonyeshe demu wako maana Kuna watu viherehere sana.
Sikuhizi kuna vibubu vya kidijitali ninampango ninunue hiki kibubu
-1872368921-20272586.jpg
 
Dah[emoji1787][emoji1787][emoji1787] nimeiona nicomment tu mkuu mbona umekaza sana Toka mda hutaki tulete mademu ghetto
[emoji23][emoji23][emoji23]sipendi............,,wengine wanamabalaa kaka yangu[emoji16]

Unapo lala na kuamka kwenda kusaka tonge inatakiwa upaheshimu sana.

Room kwako ingiza yule ambaye utaoa tu.


Wengine vichochoro vipo.
 
Uko sahihi Mkuu, kwanza hata issue ya kuwa na mahusiano mengi nayo haijakaa poa si tu kwa kijana mtafutaji ila hata kwa mtu yeyote yule. Ukiachilia mbali kwamba unaathiri uchumi wa huyu mtafutaji,pia kuna athari nyingi sana nyinginezo ni za kiroho pia.
Ukuyane na yote but si ya ki roho hii inakutafuna na utasema umelogwa,

Kuwa na mahusiano mengi wala si ujanja,
 
Kama chumba chako kina tiles, bandua moja vizuri bila kuacha alama, halafu tengeneza space ya kufanya bank. Hakuna mwizi hapo labda umwonyeshe demu wako maana Kuna watu viherehere sana.
Jamani unaanzaje kumuonyesha demu unapoweka pesa[emoji16]

Demu anaonyeshwa pahala inapokaa funguo.
 
Hii ni kwetu wanangu wa Maghetton!

Tusisahau kusave kila tunapopata mkwanja,hata kama umepata buku ten fanya saving walau ya buku sio mbaya. Jambo lingine na muhimu zaidi,ni kuwekeza katika kitu ambacho una ujuzi au ufahamu nacho kiundani,itapendeza zaidi kitu hicho kiwe kinagusa kwa namna moja au nyingine katika shughuli zako za kila siku.
Hapa namaanisha,mfano mimi msimamizi wa masuala ya mbao,basi mara moja moja nanunua miti kadhaa,au sometimes nanunua mbao kadhaa na kuziuza.
Kwa mfano ukiwa fundi katika workshop ya mtu,unaweza kununua hata MDF-Boards zako,au bawaba,handles,nob,n.k na kuwauzia baadhi ya mafundi wenzio.

Hivyo hivyo hata ukiwa dukani,kama bosi sio mkuda weka hata mzigo wako pale unapoona boss hajaleta mzigo kwasababu either kakwama au lah.
Muhimu ni pesa izunguke.

La mwisho na kubwa zaidi,usisahau kuwapa watu wenye uhitaji,toa msaada kwa watu wanaohitaji,mfano masikini,wazee,watoto yatima,n.k. Wakuu hii issue ya kutoa ni zaidi ya ndumba,milango mingi sana ya kimafanikio hufunguka. Mtu anaposhukuru kuna kitu kikubwa sana unapata. Mtumie hata Mshua, Mother au madogo chochote kile bila kujali uko katika hali gani.


NB: Pahala ambapo unaamka kila siku kwenda kusaka mkate wa kila siku ni pahala muhimu na nyeti sana.
So, Ghetto liheshimiwe,na si kila mtu anapaswa kulazwa ghetto kwako.

Tuendelee kupambana wanangu wa damu,JAH bless us![emoji109]
Umeongea ukwel saving ni muhimu sana na saving nzuri niile unayo iweke kwenye vitu vinavyo ingiza pesa au vitakuja kupanda thaman uko mbeleleni mfano ardhi , kingine tuwe na saving ya mambo ya emergency mfano ugonjwa na kutokuwa na mishe kwa mda flan.

Sent from my Nokia G10 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom