Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Kwema Wakuu!
Wakati wewe ulitumia mamilioni ya pesa kufaulu Kidato cha nne, kuna wajuba gharama zao Kwa ujumla tangu Kidato cha Kwanza mpaka cha sita hawafikishi hiyo milioni Moja. Hivyo usiringe Sana Utaonekana mshamba tuu!
Wakati wewe ulitumia mamilioni ya Pesa kupata Pisikali Fulani, kuna Wakulungwa hawatoi hata Mia na wanapata wanawake wazuri kama huyo unayemgharamikia vile watakavyo.
Wakati wewe ulitoa mahari milioni Nne mpaka kumi ili kuoa mwanamke huyo anayekupasua kichwa sasa hivi😉😉 kuna wajuba mahari zao hazifiki hata laki moja na wake zao ni wazuri na wanaishi maisha ya Raha mustarehe.
Wakati wewe ulinunua Gari hilo unalotembelea Kwa gharama kubwa, kuna Wazee WA connection wamenunua Gari hiyo hiyo Kwa bei karibu na nusu bei ya uliyonunulia Gari yako.
Wakati wewe unatumia mamilioni ya Pesa kujilinda dhidi ya wezi na Majambazi na bado unalala Kwa wasiwasi, kuna wakala nje wanalala Kwa Raha mustarehe pasipo hofu yoyote.
Wakati wewe unahangaika upate Jambo Fulani labda ni KAZI au elimu au makazi ili uheshimike, kuna wenzako hata uwe na vyote hivyo bado watakuona mbulula tuu!
Kiufupi,
Maisha yanahitaji Kuridhika, na kutokujipa Stress. Usijitese!
Usi-complicate maisha, fanya Jambo lililo ndani ya uwezo wako. Kanuni inasema usivuke mipaka.
Maisha yanatabia ya kukurudisha kwenye Mpaka wako pale unapovuka mipaka,
Ukihangaika kutumia pesa nyingi ili upate kitu Fulani ambacho sio saizi yako fahamu kuwa Maisha yatakurejesha Kwa aibu katika nafasi yako.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Iringa,
Wakati wewe ulitumia mamilioni ya pesa kufaulu Kidato cha nne, kuna wajuba gharama zao Kwa ujumla tangu Kidato cha Kwanza mpaka cha sita hawafikishi hiyo milioni Moja. Hivyo usiringe Sana Utaonekana mshamba tuu!
Wakati wewe ulitumia mamilioni ya Pesa kupata Pisikali Fulani, kuna Wakulungwa hawatoi hata Mia na wanapata wanawake wazuri kama huyo unayemgharamikia vile watakavyo.
Wakati wewe ulitoa mahari milioni Nne mpaka kumi ili kuoa mwanamke huyo anayekupasua kichwa sasa hivi😉😉 kuna wajuba mahari zao hazifiki hata laki moja na wake zao ni wazuri na wanaishi maisha ya Raha mustarehe.
Wakati wewe ulinunua Gari hilo unalotembelea Kwa gharama kubwa, kuna Wazee WA connection wamenunua Gari hiyo hiyo Kwa bei karibu na nusu bei ya uliyonunulia Gari yako.
Wakati wewe unatumia mamilioni ya Pesa kujilinda dhidi ya wezi na Majambazi na bado unalala Kwa wasiwasi, kuna wakala nje wanalala Kwa Raha mustarehe pasipo hofu yoyote.
Wakati wewe unahangaika upate Jambo Fulani labda ni KAZI au elimu au makazi ili uheshimike, kuna wenzako hata uwe na vyote hivyo bado watakuona mbulula tuu!
Kiufupi,
Maisha yanahitaji Kuridhika, na kutokujipa Stress. Usijitese!
Usi-complicate maisha, fanya Jambo lililo ndani ya uwezo wako. Kanuni inasema usivuke mipaka.
Maisha yanatabia ya kukurudisha kwenye Mpaka wako pale unapovuka mipaka,
Ukihangaika kutumia pesa nyingi ili upate kitu Fulani ambacho sio saizi yako fahamu kuwa Maisha yatakurejesha Kwa aibu katika nafasi yako.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Iringa,