Ulifanya kosa gani Shuleni Hadi kengele ya dharura ikagongwa watu wakaja mstarini kwa ajili yako?

Ulifanya kosa gani Shuleni Hadi kengele ya dharura ikagongwa watu wakaja mstarini kwa ajili yako?

tulibambwa mtandao wangu mzima tukaandika barua, ikawa onyo ukirudia tena huna shule, na shule za kikatoliki hazikwepeshi maneno
Shule za seminary ,ni Kama nchi kunakuwa na masnitch wanaojivika kazi za usalama wa taifa huwezi fanya dili haramu usikamatwe yaani itoshe kusema nahisi kule ndiko tunakowapata afisa vipenyo wazuri zaidi
 
Nilisoma shule ya jesh jina kapuni so kulikuwa na askar mmoja ana mwili mkubwa na c. Unajua walimu huwa kwa wanafunz wana majina yao ya utan so tulikuwa tunamuita jambo kubwa ingawa mwenyew hakufaham na kama alifaham alikosa ushahd so cku iyo aliniagza nikawaambie wanafunz wenzng kuwa ikfika saa 8 wasiondoke kuna matangazo ebwana nikaenda nikawatangazia so kuna ticha mmoja nae ni soja akaniuliza mwlim gan kakutuma utoe hilo tangazo c nikaropoka yule JAMBOKUBWA akaniambia jambokubwa kwa mshangao akanipeleka ofcn matcha wengne walvyosikia ule mkasa wakacheka afu jambokubwa mwenyew yupo hapo alimaind then alikuwa captain yaan nyota 3 akawaita wanafunz wote nao walivyotangaziwa ule mkasa c wakacheka wakaambiwa kwanza wagalegale kweny matope wakala stick advance wote afu ikaja zamu yangu nilikula stick mabao mabut had alipotokea mkubwa wake kanal ndo akamuamuru aache apo nishalowa vbaya mno asee acngetokea yule kanal cjui ingekuwaje
 
nilichongesha muhuri washule,nikafanyia mazoezi sahihi ya basa nikapatia ,nikaenda mjini kufanikisha kitabu Cha risiti , masela wakaanza kulipa ada na michango kwangu........ mpaka Leo shule ilikula hasara Milion of money,kumbe kwenye masela palikuwa na kenge ,akashindwa kujitetea lakini hakunitaja mpaka Leo na meja jeshi la goma congo

ebwana ,Ile siku siisahau mana nilitakiwa nitajwe ila hakunitaja
Mpaka Leo ,pamoja Yuko jeshi la kongo Mimi ndo mshauri binafsi
Hujasoma kaskazini kweli wewe, Hahaha. Arusha, arusha ndo kulikuwa na hii michezo.
 
Uhakika wa mlo mzuri wa walimu Kaka .
Asubuhi chai maziwa na mikate ya soseji huku Wana wanakunywa uji na andazi moja .
Wali kwangu shuleni haikuwa anasa ilikuwa ni routine .
Sasa ticha akikuagiza kuwachunguza Wana unajikuta huwazi Mara mbili maana Wana hawana lolote .

Sema miaka hiyo mnasoma mkiwa miwatu mizima kweli ,Basi kamati ikaundwa siku nikaitwa chemba na wawakilishi wa school mob wakisema nakaza Sana embu nijitafakari na kubadilika ,Sasa Kaka mbele ya wali na pilau la staff basi nilikuwa naambilika ?

Ni hapo wakasema siku watanikungu'ta na badaye wakitimiza Jambo lao
Hahaha, Sasa ulidanganywa nini na walimu mpaka ukatumbukia humo?
 
Hapa ni katika level zote 3 za elimu shule ya Msingi, sekondari na Kidato cha 5 na cha 6.

Mimi nakumbuka niliwahi kamatwa na simu kengele ikagongwa nikaipasua kwa mawe hadharani..
Nilimchomolea rafiki yangu hela kwenye shati kiutani ilikuwa mapumziko mlangoni mwa darasa ili nimrudishie baadaye,kumbe jamaa kaenda kwa ticha.Tukaitwa darasa letu turudi darasani hapo mimi sijagundua tulichoitiwa na pesa ipo mfuko wa shati, Mara namuona ticha ana bakora na Semeni(rafiki yangu)yupo pembeni hapo nikajua nishayakanyaga basi ticha huku ana rundo la stick akasema aliyechukua pesa ya semeni arudishe kabla sijawasachi wote na bakora zisipopatikana,nikasema sizotoi maana zile bakora zitaniishia,ulipita msako huku natetemeka nikazitoa kwenye shati nikazishika mkononi ile ananisachi mfukoni(monitor)mi nimezishika mkononi mikono juu akasema lete begi hapo ndipo nikafanikiwa kuzirudisha mfukoni.Kilichofuata ni kupigwa fimbo 5 kila mmoja.Nilijisikia vibaya sana wenzangu wakipigwa huku wakilalamika kuonewa.Niliendq nae (kwa saa nane) nikamnunulia mihogo.Baada ya siku 2 nikamrudishia hela akashangaa sana nikamwambia alikurupuka kwenda kwa mwalimu,siri tukabaki nayo hadi tulipomaliza shule kama yupo mhanga wa hili tukio samahani sana.Semeni Jarton Mwakyembe uko wapi mkuu?
 
Daah wakuu acha niwape story.
2014 niliamishwa shule na mama na kunipeleka shule ingne wilayani kumbuka mwanzo nlikuwa naskuli city center kbsaa sasa hii ni baada ya mama kuona uhuni umenijaa sana apa mjini.
Sasa bhana iyo shule nlioenda walikuwa wanasoma somo la Agriculture na mimi sikuwahi lisoma kbsaa na apo school nliamia j"4 so wanafunz wenzangu wakawa wananiambia wewe kesho ni test ya agriculture na mwalimu huwaga hajui cha mgeni wala nini we soma, me nkakaza shingo bhana si j5 ikafka na ticha wa agric akaja asee alikuwa anaogopeka shule nzima yaani yule mwamba alikuwa anagonga viboko hatari.
Yaan alipoingia tuu class akasema wote lazeni vichwa kwenye dawati, then akaandika maswali ubaoni, after akasema chaneni karatasi mna dakika 10 tuu za kujibu haya maswali, maswali nayakumbuka mpaka leo yalikuwa hivi
1. a) What is weed?
b) What is weeding?
2. Merits and Demerist of weed
3. Methods of controlling weed
4. Mention 5 common weed
Sasa bhana wenzangu wakawa bize na kujibu maswali, uku mimi nikipekua pekua daftari langu jipya likiwa halina neono lolote ndani zaid tu ya jina kwenye cover, Si teacher akaniona akajua naigia kwa kupekua daftari akaja mpaka nilipo na kusema-:

Teacher: Simama juu na weka kila kitu chako kwenye dawati ad mda wa test utapoisha hakuna kuandika chochote,

Me: Mwalimu mimi ni mgeni nimeamia jana na nlipotoka hili somo halipo

Teacher:Nimekwambia simama juu sitaki kujua we ni mgeni na umefundishwa agriculture au vipi we subiri si iyo karatasi yako umeandika jina?

Me: ndiyo

Basi bhana nilovyomjibu ye akaendelea zake kuzunguka zunguka darasani akikagua wanafunzi wasiigie na mda ulipoisha akakusanya karatasi zake na kuzisahihisha. na alipomaliza akatugawa kutokana na score apa sasa ndo show inaanza.

Teacher: Kama umepata 0-40 pita mbele, 41-59 kaeni kati kati, 60-79, kushoto na 80-100 kaeni kulia. Kama una 0-40 viboko ni 9, 41-59 viboko ni 6, na 60-79 ni vitatu.
Akaanza kuwanyoosha wa fimbo 3 tatu, wakafata wa 6, then tukaja sisi wa viboko 9, maana mimi sikufanya swali lolote hivyo niliscore 0(zero), me nkabaki zangu wa mwisho ili nimuelekeze mimi ni mgeni na hili somo sijawahi kulisoma, kumbe bhana mtu kashanitamani aloooh apo ndo kazi ikaanza yaani tulibishana sana, kila akisema shika vidole mimi nagoma sishiki wala kuinama, asee aliongea kwa hasira na kwa kelele sanaa
NIMESEMA INAMA SHIKA VIDOLE.. Asee alianza kunipiga fimbo kila mahali ndipo nikaamua na mimi kujitetea alooo mtu alikula ngumu mixer mateke yaani tulipigana haswa na kiukweli nlimzidi ad shart lake likachanika na suruali yake ilichafuka mno kwa kiwi ya kiatu changu.

Teacher kuona ishakuwa ivyo akatoa simu akampigia second master na walimu wengne wakaja bhana class wakamuona alivyo na mimi pia wakaniona hali nilyonayo yaani nlikuwa nishaamua liwalo na liwe ila apa sikubali anichape yaani bora nichwapwe na walimu wote ila so yeye, bhas bhana second akamwambia nenda kabadilishe shart na suruali wakati tunaangalia namna ya kumuonya ama kumfukuza huyu mwanafunzi, basi bhana walimu wakatoka na mimi na KENGELE YA EMERGENCE ikapigwa.
Siwezi sema nini kiliendelea ila huyo mwalimu alikuja kuwa karibu na mimi mno na somo lake la AGRICULTURE Nilipenda sana na nililitendea haki ad akawa aninitolea mifano chanya.

NOTE: Mwalimu huyo leo hii ni afisa Ugavi mkoa flani, na ata nikiwa chuo tulikuwa tukiwasiliana sana na alinikutanisha na marafiki zake hivyo alikuja kuwa msaaada kwangu. Na agriculture ni somo zuri sana kuwahi kusoma kati ya masomo yangu yote naweza sema hivyo.
 
Kwa sisi wa mbeya ubaridini nakumbuka kuna bro anaitwa hamfrey mchaga uyo jamaa

Yeye alikuwa form 4 mimi nilikuwa form 2 lakini ni kama alikuwa ananikubali sana

Bro alikuwa anauza pombe za viroba shule bei ya kawaida ilikuwa ni 1500 lakini yeye alikuwa anauza kwa 2000

So mimi ndiye nilikuwa supplier wake so ndipo na mimi nilianza kunywa pombe muda huo


Bwana wewe kuna wadaku washkaji wa kisabato wakamsanua mwalimu

Aiseh aiseh lile varangati siji kuja kusahau

Niliamishwa yule hiyo mimi na uyo bro
 
Uhakika wa mlo mzuri wa walimu Kaka .
Asubuhi chai maziwa na mikate ya soseji huku Wana wanakunywa uji na andazi moja .
Wali kwangu shuleni haikuwa anasa ilikuwa ni routine .
Sasa ticha akikuagiza kuwachunguza Wana unajikuta huwazi Mara mbili maana Wana hawana lolote .

Sema miaka hiyo mnasoma mkiwa miwatu mizima kweli ,Basi kamati ikaundwa siku nikaitwa chemba na wawakilishi wa school mob wakisema nakaza Sana embu nijitafakari na kubadilika ,Sasa Kaka mbele ya wali na pilau la staff basi nilikuwa naambilika ?

Ni hapo wakasema siku watanikungu'ta na badaye wakitimiza Jambo lao
Hahaha. Ulizingua mno boss.
 
Utengwe [emoji23][emoji23]
nilikua nauza mzizi wa kuongeza nguvu za kiume maarufu kama MKONGORA. nilikutwa na hiyo mizizi mfuko mzima ule wa kubebea madaftari ulioandikwa SPORT wenye kamba unavaa kama X hivi. kengele ikagongwa nikapata bakora km 20 na ushee, sitasahau! shule nilikuwa naitwa TIPPU TIPPU kwasababu ya biashara ya MKONGORA.
 
Balehe mbaya sana, nikiwa 4m1 nilimpenda madam wangu siku moja nikamvizia akiwa peke yake staff nikaingia nikamwambia ukweli, alooo kwanza aliniwasha makofi huku akipiga kelele akisema " wewe mtoto nitakulaani" kesho yake iligongwa kengele ikaitwa bodi ya shule,Afisa elimu, walimu walikusanyika kama 60 pia waliitwa walimu wa primary kama 30 waje wasaidie kunitandika viboko, nilipigwa sana yaani zaidi ya sana
 
Niliiba godoro la patron wa bwenini kwetu nipeleke mtaani kuwauzia mafundi sofa, ile nimeruka fens naingia lami gari la Headmaster hili hapa nilibebeshwa lile godoro kichwani mpka shuleni kengere ikagongwa wanafunzi wote kwakaja assembly point. Headmaster akauliza hili godoro linaweza kuwa la nani? Shule nzima wakaitikia mpka walimu "patron" (walijua kwasabab patron na matron magodoro Yao yalikuwa ni 4×6 tofauti na yetu sisi wanafunzi.

Nilipigwa viboko kumi na tano on the spot hafu nikapewa adhabu ya kufuta madirisha ya majengo yote ya school, so poa.
 
Spirit ya Savimbi au Maalim Seif hii [emoji23]
Niligombea u_headboy nikashindwa Ila wakati wa kutangaza matokeo nikayakataa mbele ya walimu na watumishi wa shule kwa kelele ,wale wanaonikubali nao wakazifuata kelele zangu .
Nikala fimbo nikapoa ,usiku nikashika mic ya chapple wakati kimetulia watu wapo kujisomea nikawatangazia kuwa Mimi ndiye head boy wa shule na aliyepita hatambuliki na yeyote .

Watu wakapiga kelele za shangwe ,asubuhi kengele ikagongwa nikala suspension ya miezi miwili na faini ya milioni mbili kwa kuvunja viti vya chapple maana wafuasi wangu walifanya fujo wakati najitangaza hivyo waliharibu Mali za chapple .

Nimerudi kutoka kutumikia kifungo nikapewa uongozi wa nidhamu ni hapo nikatulia na kuanza kuwasaliti wanafunzi wenzangu wasaliti japo nao walinikunguta walipoona nimebadilika kabisa .

Hivyo naamini hamna kitu kikubwa Kama kucheza na psychology ya mtu ,maticha walijua kucheza na akili yangu Ila wakaniponza school mob ikataka kuniua .[emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom