Ulifanyaje kipindi huna hela, yaani maisha yamekupiga total knock out?

Ulifanyaje kipindi huna hela, yaani maisha yamekupiga total knock out?

Watu watakwambia beba zege, choma viazi, osha gari.

Hakuna atakayekwambia njoo mtaa C ukifika kuna mshkaji F mwambie umekuja kubeba zege/ choma viazi/ kuosha gari.

Hii ndiyo tofauti ya members wa mitandao ya kibongo na ile ya nje ya bongo. Hata mtu akisema njia aliyopitia anasema nilipambana mno ila hasemi ni kwa namna gani.

Mkuu, una marafiki/ ndugu hawa ndiyo wanatakiwa wakukumbuke wakisikia michongo. Wanakuamini? Wanajua uwezo wako ingawa upo benchi?

Ingawa sikua nimeajiriwa kabla ya wenzangu ila walijua kua jamaa ishu za sales ataweza. Mmoja aliposikia ishu nikatafutwa nikaenda, now here is the issue, kwa kawaida mimi ni mkimya mno halafu nikagewa hiyo ishu so ikabidi niadopt.

Hichi unachofanya wewe nilishafanya tena humuhumu na ninakuhakikishia una 0.091% za kupata mtu wa kukupa suluhu humu. Wengi humu ni stori nyingi.
 
Kitu kingine nimesahau.

Watu wanaziongezea chumvi CV zao vibaya mno. Wewe unaweza sema hapa nilifanya field miezi miwili huu uzoefu nisiuonyeshe halafu kuna mwenzako kafanya mwezi, anauonyesha na anaupamba.

Mwengine anaandika vitu hajawahi kufanya but the catch is you have to look the part na udefend hiko unachosema unakijua. Mfano wewe unajua kutumia computer ila hujui kutumia excel labda lakini kwenye CV unasema uko vizuri kwenye excel.

Fungua profile linkedin, ijaze details za msingi. Anza kuwafuata HR inbox, ni wala hongo so utajua unaanzia wapi.
 
Issue nipo Moshi, huku hakunaga hizo bolt bin uber, huku ni bajaj mostly na hata kisela kisela ni ngumu kugusa chombo cha mtu, unaweza kung'utwa mpaka usahau kuwa una njaaa.
Pole sana kwa mkoa wa kilimanjaro wajwnja ni wengi sana hapo Town.......kama unaweza hama mkoa hrbu jaribu kuhama kajaribu na sehemu nyingine ukute bahati yako haipo hapo
 
Nenda kwa watu wanaofanya biashara ya catering ,uombe kaz ya ku serve ,utapata na msosi bure,kwa wale wanaopikia nyumban ndo wazuri,
 
Sema niliomba kazi za Takukuru ila nahisi kigezo cha umri ndo kimenipiga knock out directly maana nagonga 30 mwaka huu.
Watu wanaingia humo above that age mzee. Nchi ngumu hii kama huna refa. Yani una sifa sote kabisa, ila unaachwa. Mtoto mmoja wa kamishna sifa hana ila baba anambeba na kitengo kizuri anapata kazi....acha kabisa mkuu
 
MANYEMA PALE SOKONI MZEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE AU WAPI ??? VIPI KUNA MISHE GANI HUKOO MANYEMA ????
Kuulizia kuwa manyema kunamishe gani ni umezingua. Ilitakiwa umcheki bhana pm mwasiliane muonane then along the way ukifika manyema mwenyewe utaangalia au kuelekezwa maana jamaa ameonesha kutaka kukuonesha njia.. Ila wewe unaleta ujuaji.
Sokoni, Unajua kuna mishe gani.
 
Nilipo ishiwa mtaji baada ya kupakia nyanya kuto geita kwenda mabibi sokoni dar

Matenga hayo yanya nilikuwa natumia dalali wangu mala kwa mala Kisha ananitumia hela baada ya kuuza

Ilikuwa ni trh 20 mwezi wa 12 nyaya hizo zilikuwa zinawai hili zikauzwe siku ya sikuu

Dereva alitembea kufika kibaigwa gali likaaribika kibaya zaidi dereva akazima cm akaanza kutengeneza gali lake

trh 22 nikampigia dalali akasema gali aija fika nikimpigia dereva apatikani trh 23 nikaamua kwenda kulipoti polisi wakaamua kutafuta namba hiyo kwa njia ya mtandao wakasema

Kwamala ya mwisho simu yake iliwasiliana kwenye mnala wa kintiku mwisho kibaigwa

Nikaamua kuwa pigia madalali wa kibaigwa na kintingu hili walitafuta gali hilo nikawaeleza lilivyo na namba zake

Madalali wa kibaigwa wakalikuta limepakiwa pembeni mwa barabala huku kibini imeibsmishwa mafundi wako kazini nyuma kwenye kuchanja kuna matenga ya nyanya

Wakampa simu nikamuuliza kulikoni?akasema natengeneza kisha niendelee na safari hiyo trh 24 ikabidi madalali wafaulishe mzigo kwenye gali nyingine kwenda sokoni ifahamike wakati huo nynya zilikuwa na siku 5 tangu zitoke shamba siku 3 ziko Juani juu ya gali

Kufika sokoni siku ya sikuu asubuhi nyaya zote masalo zimeoza yaani uchafu tu hata hela ya kulipia nauli haikupatikana

Ifahamike pesa nilio kuwa nibakinayo mfukoni kama akiba ilitumika kutafuta gali hilo na kuwa tumia madalali kibaigwa

Ilibidi niombe rifuti kutoka runzewe hadi dar nikafika nyumbani sina hata mia

Akili ikafa ghafura milioni yangu 5 ikawa imeyeyuka kimtindo nikaanza kuuza tv hela tunatumia mala simu mala masofa

Sasa nikajikuta sina cha kuuza watoto wanatakiwa kula kwenda shule bahati nzuli silipi kodi maisha yakawa magumu sana

Nikaamua kujiunga na mafundi wa kujenga tukaenda goba nikapewa Sululu na koleo kuchimba msingi tangu asubuhi mpaka saa 12 jioni malipo sh 15000 hela hiyo nilipata lakini mkono ikawa umepasuka hata kula nilishindwa kesho yake sikuludi

Hali ikazidi kuwa mbaya nikawafuta tena mafundi nikakuta kuna kazi ya kubeba zege ndoo ya kilo 20 ninzito usiseme malipo kwa siku 30000 nikakomaa kiume

Wiki 2 nikapata sh kama 250000 baada ya kutoa matumizi

Nikaamua kwenda kukodi tololi Tandale kwa mama 1 anayo mengi ya kukodisha nikaanza kuuza machungwa nanunua Mabibo natembeza miguu akawa inauma sana nikashindwa lakini yalikuwa yana lipa sana kila siku sikosi kuweka sh 20 kama faida

Nikaamua kununua baiskeli anita nikawa na funga vikapu vili mfano wa mizega zega au kama unavyo beba punda mizigo

Nikawa sasa nabeba machungwa mengi na chagua mazuli na mwamvuli wangu naenda kutega kwenye maegesho ya magali madogo

Kama pale makumbusho nauza sana yakibakia naenda pale nwenge sehemu ya mpakani jioni kuna wasafiri wengi pamoja na wanafunzi wa chuo nauza sana saa 3 napeleka basikeli yangu kwa walinzi wa maduka napanda basi nyumbani

Kwa kifupi nilipambana na kazi hiyo kwa msimu 1 tu nikapata 1000,000, ikawa sababu ya kujenga banda la matunda Masaki wakaja libomoa migambo kwenye bomoa bomoa ya mama samia kwa sasa nashukuru nimeludi kwenye kazi yangu ya nynya na vitunguu maji na awamu mwaka huu sio siri kazi nimefanya
Great inspiration.
Sio wale wengine stori zao zinaruka kama CD ya james bond.
 
INAFIKIA ILE HATUA UNASIKILIZIA FUTARI MSIKITI WA JIRANI
HATA KAMA SIO MUISLAMU BIN VUUUU
PINDI LIFE LIMEKUKAMATA NA UKA KAMATIKA YAAANI HUNA HATA MIA MBOVU YA KUNUNULIA MHOGO WA KUPOZA NJAA



GHAFLA BIN TAABAN MWEZI WA RAMADHANI UNAKUWA MSAADA WAKO HAHAHA


LIFE HILIIIIIIIIIIIIIIIII
 
HEYEEEE HEYEEEEE MAISHA NI KUCHANGAMKAAA ASEEEEE
 
Back
Top Bottom