Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Mwaka 2016 baada ya kumaliza chuo,Maisha yalikuwa magumu Sana,nilikuwa siwezi hata kupata vocha na Kula kulikuwa ni kwa manati.nikaanza kufanya kazi za saidia fundi kujenga nyumba,,KWA KWELI NILIDHARAULIKA SANA PALE MTAANI!!,niki-apply kazi siitwi hata kwenye interview,nikipeleka CV door to door,wanaishia tu kusema CV ni nzuri lakini kazi sipewi!!home hali ni Mbaya,nikimuangalia mama nasikitika sana, mana Kipindi niko shule ilikuwa inafika kipindi anauza ardhi na vitu muhimu ili nisome, lakini ajira hakuna!!Mwaka 2017 nikaweka vyeti pembeni nikaanza kuokota vyuma chakavu(screper)kwenye Madampo na Mahali popote pale nitakapo pata ilimradi tu isiwe ya kuiba,ilikuwa ni fedheha lakini nilikuwa sina namna nyingine,mwezi wa Saba nikawa nimefikisha tani1½ nikauza nikapata laki5,baada ya hapo nikanunua piglets8 wa kienyeji@30000,nikatumia kama Laki2½ hiv,2wakafa maana nilikuwa nawafuga kibabe, wakabaki6 nikawakuza hadi mwezi3,2018,nikaja kuuza kila mmoja lak1.75 nikapata million 1na elf50..nilikaa mwezi mzima nikitafakari ni biashara gani naweza kufanya..baada ya hapo niliamua kufanya biashara za kujumua mpunga mwezi 5,,nikawa naenda Mbalari na Kamsamba-ya ziwa Rukwa.nilikuwa nachukua shambani kwa Bei rahisi nakuja mjini Mbeya nakoboresha nauza. Mwezi wa 9 pesa ikawa imeshakua million 2.8.msimu wa mpunga ukawa umeisha.nikarudi home kutafakari tena nifanye nini..siku moja napitia baadhi ya timu barani ulaya na africa nikaona Kama Kuna fursa flani,.(maana wakati niko kwenye msoto,ilibidi nijifunze kubeti) ,nikasema potelea mbali wacha nirisk elf 30 leo,nikaingia parimatch wakati ule walikuwa hawakati Kodi nikaweka Odd 35.6,KWELI NIKAAMINI MWENYE NACHO HUONGEZEWA,,tiketi ika-WIN nikapata mili1.10 hiv.,wakati nafanya kazi za saidia fundi hakuna tiketi niliyo bet na ika-WIN..na hakuna pesa niliyopata kiurahisi Kama hii..baada ya hapo nikawa nafanya scalping natafuta odd ndogo nastake pesa kubwa nikakuta pesa inakuwa kiutani utani hadi najishangaa..sikumoja nikajiRISK tena nikaweka STAKE ya mill.2 kwa ODDS.3 nikapata milioni 6,sikuamini Kama ni pesa yangu,,NIKAJIULIZA MBONA KIPINDI KILE KWENYE MSOTO MAMBO HAYAKUWA HIVI,?!maana niliitumia takriban karibu miezi7 kupata Tani moja ya vyuma chakavu!!BAADAE ukafika msimu wa kilimo Nikaenda Mbeya vijijini kulima viazi mviringo nikatumia Kama milio1.8,nikavuna nikapata millioni3.4.mpaka Sasa naendelea kujishughulisha na kilimo ufugaji na NA PESA YANGU TAYARI ILISHAVUKA MILION10,naelekea 20mill.
We Noma Ni Mpambanaji
 
Mwaka 2016 baada ya kumaliza chuo,Maisha yalikuwa magumu Sana,nilikuwa siwezi hata kupata vocha na Kula kulikuwa ni kwa manati.nikaanza kufanya kazi za saidia fundi kujenga nyumba,,KWA KWELI NILIDHARAULIKA SANA PALE MTAANI!!,niki-apply kazi siitwi hata kwenye interview,nikipeleka CV door to door,wanaishia tu kusema CV ni nzuri lakini kazi sipewi!!home hali ni Mbaya,nikimuangalia mama nasikitika sana, mana Kipindi niko shule ilikuwa inafika kipindi anauza ardhi na vitu muhimu ili nisome, lakini ajira hakuna!!Mwaka 2017 nikaweka vyeti pembeni nikaanza kuokota vyuma chakavu(screper)kwenye Madampo na Mahali popote pale nitakapo pata ilimradi tu isiwe ya kuiba,ilikuwa ni fedheha lakini nilikuwa sina namna nyingine,mwezi wa Saba nikawa nimefikisha tani1½ nikauza nikapata laki5,baada ya hapo nikanunua piglets8 wa kienyeji@30000,nikatumia kama Laki2½ hiv,2wakafa maana nilikuwa nawafuga kibabe, wakabaki6 nikawakuza hadi mwezi3,2018,nikaja kuuza kila mmoja lak1.75 nikapata million 1na elf50..nilikaa mwezi mzima nikitafakari ni biashara gani naweza kufanya..baada ya hapo niliamua kufanya biashara za kujumua mpunga mwezi 5,,nikawa naenda Mbalari na Kamsamba-ya ziwa Rukwa.nilikuwa nachukua shambani kwa Bei rahisi nakuja mjini Mbeya nakoboresha nauza. Mwezi wa 9 pesa ikawa imeshakua million 2.8.msimu wa mpunga ukawa umeisha.nikarudi home kutafakari tena nifanye nini..siku moja napitia baadhi ya timu barani ulaya na africa nikaona Kama Kuna fursa flani,.(maana wakati niko kwenye msoto,ilibidi nijifunze kubeti) ,nikasema potelea mbali wacha nirisk elf 30 leo,nikaingia parimatch wakati ule walikuwa hawakati Kodi nikaweka Odd 35.6,KWELI NIKAAMINI MWENYE NACHO HUONGEZEWA,,tiketi ika-WIN nikapata mili1.10 hiv.,wakati nafanya kazi za saidia fundi hakuna tiketi niliyo bet na ika-WIN..na hakuna pesa niliyopata kiurahisi Kama hii..baada ya hapo nikawa nafanya scalping natafuta odd ndogo nastake pesa kubwa nikakuta pesa inakuwa kiutani utani hadi najishangaa..sikumoja nikajiRISK tena nikaweka STAKE ya mill.2 kwa ODDS.3 nikapata milioni 6,sikuamini Kama ni pesa yangu,,NIKAJIULIZA MBONA KIPINDI KILE KWENYE MSOTO MAMBO HAYAKUWA HIVI,?!maana niliitumia takriban karibu miezi7 kupata Tani moja ya vyuma chakavu!!BAADAE ukafika msimu wa kilimo Nikaenda Mbeya vijijini kulima viazi mviringo nikatumia Kama milio1.8,nikavuna nikapata millioni3.4.mpaka Sasa naendelea kujishughulisha na kilimo ufugaji na NA PESA YANGU TAYARI ILISHAVUKA MILION10,naelekea 20mill.
Safi sana mkuu kwa ufafanuzi mzuri sana tofauti na wengine hawasemi jinsi walivyopata hizo pesa zaidi zaidi wanasema tu kiasi kwa mtu alofunguza uzi kwa lengo anaoshia ku stressika kwa jinsi watu walivyopata pesa na njia hawasemi ila wewe umelezea vizuri na Kuna vitu nimejifunza shukrani mkuu.
 
Habari jf

Katka kupambana na maisha kuna malengo tunajiwekea Shida ni changamoto ya kuyafikia. Mwanzo mwa mwaka 2016 nilijiwekea target kufikisha milion 3.

Kwangu ilikua hela nyingi coz nilikua nasoma na hela ambazo nilikua nashika ni laki laki mwisho laki 5 balance ya akiba laki moja!!... Lakini baadae nilipataga kazi kwaiyo kushika milion 3 ikawa siyo kazi but siyo akiba!! Unakuta hiyo milion tatu ndio ufanye kila kitu akiba au saving ndo laki 3 au 5.

Najaribu kupambana nifike milioni 10 wapi!!

Kila ikifika milioni 3 au 4 napata shida natumia. Sasa nilitaka tubadilishane experience na wanajf wenzangu ambao mmeshavuka huko au mna idea

Nb: Hapa naongelea saving, hela unayoisave baada ya kufanya mambo mengine.

Je, wewe ulifikishaje milioni 10 yako ya mwanzo?
Ukiona mwanaume hasa kijana kajenga mjini, Narudia KAJENGA NYUMBA YAKE HASWAA na anamiliki assets zingine! Aisee ujue karuka mitego mingi sana, kafumbia macho makalio ya kila aina ya kina dada, tena wazuri na warembo mno, kufumbia macho anasa nyingi n.k!

So mbinu au ideas zile zile zinaweza kutumika ili kufikia malengo uliyojiwekea, Make kadri unavyozidi kupata mapesa ndivyo Lucifer nae anazidisha urafiki na wewe na kukuonyesha miliki zote za dunia hii hata ambazo hukuwahi kuziwazia kabisa..
 
Kila mwaka huwa nacheza vikoba na huwa natoa laki moja kila mwezi ukiongeza na kiingilio huwa tukivunja nakuwa na 1mil na laki 4 nimefanya hivo kwa muda wa miaka mitatu na mwaka jana tulipovunja mwezi wa 12 ikabidi nikae na kutafakari kwa hiyo ntafanya mzecho huu wa kichaa hadi lini?
Kila mwezi ofisini kwetu watu huwa wananifata kuomba niwape mkopo na mara nyingi huwa nafanya fair mtu anaomba nimpe laki moja hadi laki tano
Ila mwishoni naambulia za uso mtu analudisha laki moja siku nyingine elfu50 hadi deni linaisha
Mwisho nikatafakari nikasema ebu nifanye hii kama fursa mtu akitaka pesa nampa kwa mkopo na liba nikaweka 20% .
Kabla nikakutana na watu wanishauri ila kila niliyemuuliza alinambia usisubutu utatapeliwa
Moyoni nikasema najitosa na hii 1mil na laki4 mwezi wa pili mwaka huu nikaanza rasmi biashara mpaka sasa malengo yangu hadi mwezi wa 12 nifunge nikiwa na mil10 mpaka sasa nimefikisha mill6 na nusu
NOTE: hii pesa huwa siigusi kwa chochote kile
Vizuri sanaaaa embu nipe maujanjaa namie dadaaa
 
Nina ki account cha $ kila mwezi naweka minimum $100. Ikifika mwisho wa mwaka nazitoa zote naamua tu vacation wapi. Sasa hapo wengine wakiona mwisho wa mwaka unasafiri huku na kule wanashangaa!
Binafsi saving kwangu haijawahi kuwa tatizo maana pia naogopa mikopo .

Nina salary ndogo tuu take home haizidi 600k but hapo nasevu half of it .

Sasa nikipata na viposho posho huwa sipingui 2.5-4 ndani ya miezi 6 na nikipata hiyo nanunua investment au nafanya mtaji somewhere.

Ndani ya mwaka naweza fikisha saving ya Kati ya 5ml hadi 6 kwa hiyo hizi naweka kweye assets mwisho wa siku nikijumlisha assets zangu zinavuka hiyo 10 mln.

Kitu cha kukwamisha ni labda nipate mgonjwa wa mda mrefu tofauti na hapo nafikisha,nimejenga kwa staili hii hii na kama nakopa ujue ni kwa friend na si vinginevyo.
 
hii njia bora kabisa kwangu pia

NB;HAKIKISHA UNAJUA MATUMIZI YAKO YA MWEZI NA KUTENGA PESA YA EMERGENCY
Kiufupi watu wanacomlicate maisha,ukiushi kwa kiasi wala hakuna shida ila sasa utaitwa mbinde sijui nani kila jina baya but unapuuzia tuu.

Mimi Nina hadi bajeti ya mademu
 
Anza hata biashara ya barafu usave hata 1000 kwa siku
Sio pesa ndogo hiyo,300k kwa mwezi ni ishu kama huna stable income.

Ila observation yangu nimeona watu wenye vipato vikubwa vya salary lakini mara nyingi wanaishiwa pesa kuliko mwenye mapato ya kawaida,hii inatokana na status
 
Vizuri sanaaaa embu nipe maujanjaa namie dadaaa
Maujanja ni kujitoa tu niliamuamua kukilipua

Nikaanza kwa kupost status natoa mkopo watu wakanicheka ila sikuchoka baada ya mda watu wananifata inbox kuomba mkopo mi nawapa vigezo na masharti tu

Na huwez amini mwezi huo pesa ilichukuliwa yote mpaka sasa sivuki mwezi na pesa ya mwezi uliopita kila mwezi pesa inachukuliwa yote
 
Binafsi saving kwangu haijawahi kuwa tatizo maana pia naogopa mikopo .

Nina salary ndogo tuu take home haizidi 600k but hapo nasevu half of it .

Sasa nikipata na viposho posho huwa sipingui 2.5-4 ndani ya miezi 6 na nikipata hiyo nanunua investment au nafanya mtaji somewhere.

Ndani ya mwaka naweza fikisha saving ya Kati ya 5ml hadi 6 kwa hiyo hizi naweka kweye assets mwisho wa siku nikijumlisha assets zangu zinavuka hiyo 10 mln.

Kitu cha kukwamisha ni labda nipate mgonjwa wa mda mrefu tofauti na hapo nafikisha,nimejenga kwa staili hii hii na kama nakopa ujue ni kwa friend na si vinginevyo.
[emoji3516]
YOU GUY DO COPY MY MOTION.

HOW OLD ARE YOU HOMIE??

Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app
 
Sim banking app nimeifuta kwenye simu yangu, tatizo ni tawi la bank limeangaliana na nyumbani....sasa hapo sijui nafanyaje!

Nimedumbukiza atm choon ila wapi tatizo nikiona mlango wa bank umefunguliwa mate yananitoka[emoji134][emoji134]

Mnanishaurije wakuu? Nifanyeje?
 
Kwanza hongera sana kwa kazi uliyopata ni jambo la kumshukuru Mungu walau una sehemu ya kupata ujira wako!

Kuhusu suala lako, pia naomba nikupongeze kwa kuwa na malengo chanya. Tukirudi kwenye suala lako la msingi ningependa kukwambia yafuatayo:

1) Jitengenezee utaratibu wa kuweka akiba na uwe na nidhamu.
Hapa nataka kusema nini? Kwamba chagua bank ya aina yoyote enenda kafungue saving account [zipo aina mbali mbali za saving account - utachagua itakayo kufaa].

Then after, chagua kiasi chochote ambacho kila mwezi utakuwa unakipeleka kwenye account akiba yako. Mfano kama unapokea 1.5m, hakika kila mwezi ni lazima 500,000 uipeleke kwenye account. [Hii iwe mandatory]

Mfano unaweza kwenda pale KCB Bank ukafungua ile saving inayotoa 7% interest per annum.

Sambamba na kufungua lazima nidhamu ya pesa ishike mkondo wake, bila nidhamu itakuwa ni ngumu sana kufikisha malengo yako [Hakikisha kila mwezi unapeleka hiyo pesa na isipungue hata sent labda uzidishe!

2) Tafuta biashara ndogo ndogo ufanye ili zikuongezee kipato, ujue kutegemea only one source of income ni tatizo! Hii biashara utakayoanzisha ndo itakupa pesa ya kula na itakusaudia usipate tamaa yq kwenda kuchokinoa kwenye saving account yako!

3) Punguza matumizi yasiyokuwa ya lazima, hili kitakusaidia sana kufanikisha point no. 01

Mungu akubariki katika utekelezaji wako, Amina[emoji1317]
Ngoja nikawaulize KCB Bank

7% [emoji848]
 
Maisha haya! Input yako ya ntaji mbona haiendani na output ya faida?

Mimi niliwekeza milion 1.9 na kila siku nikawa natengeneza net profit ya 300k kwa miezi kadhaa!
Biashara gani?
 
Maujanja ni kujitoa tu niliamuamua kukilipua

Nikaanza kwa kupost status natoa mkopo watu wakanicheka ila sikuchoka baada ya mda watu wananifata inbox kuomba mkopo mi nawapa vigezo na masharti tu

Na huwez amini mwezi huo pesa ilichukuliwa yote mpaka sasa sivuki mwezi na pesa ya mwezi uliopita kila mwezi pesa inachukuliwa yote
Nitaanzaa na Mimi aiseee maaana, kila kukicha gharama za maisha zinapanda. Ujakaa vizuri Kodi unavunja kibubu unalipia Kodi, kugeuka ada ya mtoto nihatarii sanaa
 
Sim banking app nimeifuta kwenye simu yangu, tatizo ni tawi la bank limeangaliana na nyumbani....sasa hapo sijui nafanyaje!

Nimedumbukiza atm choon ila wapi tatizo nikiona mlango wa bank umefunguliwa mate yananitoka[emoji134][emoji134]

Mnanishaurije wakuu? Nifanyeje?

Nmecheka.Hamia uswekeni huko uache kuangaliana na Bank.
 
1. Take home ni 1,300,000 baada ya makato yote kazini pamoja na benki wakati wa kutoa

2. Nilishusha maisha tukawa tunaishi nyumba ya kupanga ya chumba kimoja elfu 35000 kwa mwezi, jirani kabisa na kazini, ninatembea kwa miguu saa moja nimeshafika. Mwanzo nilikuwa ninakaa nyumba ya 900,000 kodi ya miezi sita bado na umeme juu.

3. Nikaacha kula bia kila siku, nikawa ninakunywa mbili mwisho wa wiki

4. SIkupanga nyumba ya umeme, nilikopa sola ya Zola ule mtambo mdogo wa kulipia 10000 kwa mwezi

5. Bima, pampers na vyakula special vya mtoto (maana sometimes wanachagua sana vyakula wakiwa wadogo) nikaweka bajeti ya 150,000

6. Ikitokea shida sikuwa ninakopa kwa benki, ninakopa kwa marafiki.

7. Nikawa nina kazi za udeiwaka na udalali mida ya usiku na nje ya Ofisi

Nilipofanya hayo yote niliweza kusevu milioni 10 uliyotaja ndani ya miezi sita ya mwanzo na kuendelea, hapa ninavyoandika hivi nina gari ya kifahari SUV na nina nyumba ya zaidi ya milioni 30 ninayoishi na familia yangu na mama yangu nimemjengea nyumba ya milioni saba huko Kijijini kwetu.

Nimejifunza: FANYA IBADA, punguza bajeti za kifamilia, kama umepanga kaa jirani na Ofisi, ongeza njia za kupata kipato, sevu, wekeza.
 
Back
Top Bottom