Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Sim banking app nimeifuta kwenye simu yangu, tatizo ni tawi la bank limeangaliana na nyumbani....sasa hapo sijui nafanyaje!

Nimedumbukiza atm choon ila wapi tatizo nikiona mlango wa bank umefunguliwa mate yananitoka[emoji134][emoji134]

Mnanishaurije wakuu? Nifanyeje?
[emoji2][emoji2][emoji1][emoji1] hama bank
 
Mwaka 2016 baada ya kumaliza chuo,Maisha yalikuwa magumu Sana,nilikuwa siwezi hata kupata vocha na Kula kulikuwa ni kwa manati.nikaanza kufanya kazi za saidia fundi kujenga nyumba,,KWA KWELI NILIDHARAULIKA SANA PALE MTAANI!!,niki-apply kazi siitwi hata kwenye interview,nikipeleka CV door to door,wanaishia tu kusema CV ni nzuri lakini kazi sipewi!!home hali ni Mbaya,nikimuangalia mama nasikitika sana, mana Kipindi niko shule ilikuwa inafika kipindi anauza ardhi na vitu muhimu ili nisome, lakini ajira hakuna!!Mwaka 2017 nikaweka vyeti pembeni nikaanza kuokota vyuma chakavu(screper)kwenye Madampo na Mahali popote pale nitakapo pata ilimradi tu isiwe ya kuiba,ilikuwa ni fedheha lakini nilikuwa sina namna nyingine,mwezi wa Saba nikawa nimefikisha tani1½ nikauza nikapata laki5,baada ya hapo nikanunua piglets8 wa kienyeji@30000,nikatumia kama Laki2½ hiv,2wakafa maana nilikuwa nawafuga kibabe, wakabaki6 nikawakuza hadi mwezi3,2018,nikaja kuuza kila mmoja lak1.75 nikapata million 1na elf50..nilikaa mwezi mzima nikitafakari ni biashara gani naweza kufanya..baada ya hapo niliamua kufanya biashara za kujumua mpunga mwezi 5,,nikawa naenda Mbalari na Kamsamba-ya ziwa Rukwa.nilikuwa nachukua shambani kwa Bei rahisi nakuja mjini Mbeya nakoboresha nauza. Mwezi wa 9 pesa ikawa imeshakua million 2.8.msimu wa mpunga ukawa umeisha.nikarudi home kutafakari tena nifanye nini..siku moja napitia baadhi ya timu barani ulaya na africa nikaona Kama Kuna fursa flani,.(maana wakati niko kwenye msoto,ilibidi nijifunze kubeti) ,nikasema potelea mbali wacha nirisk elf 30 leo,nikaingia parimatch wakati ule walikuwa hawakati Kodi nikaweka Odd 35.6,KWELI NIKAAMINI MWENYE NACHO HUONGEZEWA,,tiketi ika-WIN nikapata mili1.10 hiv.,wakati nafanya kazi za saidia fundi hakuna tiketi niliyo bet na ika-WIN..na hakuna pesa niliyopata kiurahisi Kama hii..baada ya hapo nikawa nafanya scalping natafuta odd ndogo nastake pesa kubwa nikakuta pesa inakuwa kiutani utani hadi najishangaa..sikumoja nikajiRISK tena nikaweka STAKE ya mill.2 kwa ODDS.3 nikapata milioni 6,sikuamini Kama ni pesa yangu,,NIKAJIULIZA MBONA KIPINDI KILE KWENYE MSOTO MAMBO HAYAKUWA HIVI,?!maana niliitumia takriban karibu miezi7 kupata Tani moja ya vyuma chakavu!!BAADAE ukafika msimu wa kilimo Nikaenda Mbeya vijijini kulima viazi mviringo nikatumia Kama milio1.8,nikavuna nikapata millioni3.4.mpaka Sasa naendelea kujishughulisha na kilimo ufugaji na NA PESA YANGU TAYARI ILISHAVUKA MILION10,naelekea 20mill.
Real meaning of hustle, Ila hakuna mahali ulipojaribu ukakwama zaidi ya kuomba kazi
 
Ukiona mwanaume hasa kijana kajinga mjini, Narudia KAJENGA NYUMBA YAKE HASWAA na anamiliki assets zingine! Aisee ujue karuka mitego mingi sana, kafumbia macho makalio ya kila aina ya kina dada, tena wazuri na warembo mno, kufumbia macho anasa nyingi n.k!

So mbinu au ideas zile zile zinaweza kutumika ili kufikia malengo uliyojiwekea, Make kadri unavyozidi kupata mapesa ndivyo Lucifer nae anazidisha urafiki na wewe na kukuonyesha miliki zote za dunia hii hata ambazo hukuwahi kuziwazia kabisa..
Hapo kwenye makalio ya wadada, ni kweli kabisa maana kufumbia macho misambwanda wakati una hela inabidi uwe roho ngumu haswa
 
Nilifungua account maalum ya savings ambayo sitoi.

Nikaweka standing order ya kukata kiasi fulani kila mwezi kwny akaunti ya kawaida.

Nikawa naishi kwa bajeti na napeleka any extra cash huko.

Haikuchukua muda lengo lilifikiwa.

Na bonus ishakua tabia...kuweka akiba.
Big up sana kiongozi...
 
1. Take home ni 1,300,000 baada ya makato yote kazini pamoja na benki wakati wa kutoa

2. Nilishusha maisha tukawa tunaishi nyumba ya kupanga ya chumba kimoja elfu 35000 kwa mwezi, jirani kabisa na kazini, ninatembea kwa miguu saa moja nimeshafika. Mwanzo nilikuwa ninakaa nyumba ya 900,000 kodi ya miezi sita bado na umeme juu.

3. Nikaacha kula bia kila siku, nikawa ninakunywa mbili mwisho wa wiki

4. SIkupanga nyumba ya umeme, nilikopa sola ya Zola ule mtambo mdogo wa kulipia 10000 kwa mwezi

5. Bima, pampers na vyakula special vya mtoto (maana sometimes wanachagua sana vyakula wakiwa wadogo) nikaweka bajeti ya 150,000

6. Ikitokea shida sikuwa ninakopa kwa benki, ninakopa kwa marafiki.

7. Nikawa nina kazi za udeiwaka na udalali mida ya usiku na nje ya Ofisi

Nilipofanya hayo yote niliweza kusevu milioni 10 uliyotaja ndani ya miezi sita ya mwanzo na kuendelea, hapa ninavyoandika hivi nina gari ya kifahari SUV na nina nyumba ya zaidi ya milioni 30 ninayoishi na familia yangu na mama yangu nimemjengea nyumba ya milioni saba huko Kijijini kwetu.

Nimejifunza: FANYA IBADA, punguza bajeti za kifamilia, kama umepanga kaa jirani na Ofisi, ongeza njia za kupata kipato, sevu, wekeza.
Huu ujinga sitakuja kuufanya maisha yangu yote hapa duniani

Nasave kiasi, naishi sehemu nzuri, nakula vizuri, nasiidia wazazi na ndugu muhimu,, nashiriki matukio ya kijamii pia

Maendeleo yapo, sio lazima kujitesa na kujinyima kiasi iko mpaka maana ya kufanya kazi na kufurahia maisha hapa duniani inakosekama
 
Ndiyo hivyo. Shida kubwa watu wengi wakienda shule kidogo anaona biashara za mtaani ni kama kushika uchafu. Kuna kijana mmoja mwalimu s/msingi wa kichaga alipanga chumba kwetu akaona fursa akafungua genge la mbogamboga hapo nje kalitengeneza kwa mabanzi tu ya kawaida. Saizi anauza laki 8 kwa siku. Tunataka kuanza kumtoza kodi lakini tunajishtukia kwa aibu, coz ni kasehemu ambacho wala hatukujua kuwa ni potential. Sasa mwambie graduate wa Mzumbe au Udsm afungue genge.
KING
Sim banking app nimeifuta kwenye simu yangu, tatizo ni tawi la bank limeangaliana na nyumbani....sasa hapo sijui nafanyaje!

Nimedumbukiza atm choon ila wapi tatizo nikiona mlango wa bank umefunguliwa mate yananitoka[emoji134][emoji134]

Mnanishaurije wakuu? Nifanyeje?
Tatizo mnaleta mizaha kwenye vitu serious.

kama weww tu uko hivyo, Je wafanyakazi wa benki wataweza kusev kweli?

kama vipi wewe endelea kutumia tu
 
Ila kusave Kunahitaji moyo, kuna kipindi natembea uchi maana mchezo wa Kila siku hata chupi unashindwa kununua ila chupi kitu gani bwana?
Mbususu inapata natural air flow au sio🤣🤣🤣🤣 huu ubahili ni wa kimataifa
 
Nimewahi kujiwekea eti lazima niwe na 5M kwa acc imetulia wee! haijawahi fika hiyo hela hata.

Lakini hata hivyo huwa wazo linakuja, kuliko kutunza hela [figures kwenye computer] si bora ninunue kitu halisi nikimiliki nikifaidi hivi laivu? Bado najifunza uwekezaji hilo lengo la 5M, 10M 300M litafikiwagwa tu Inshallah!
 
Back
Top Bottom