Uliishi maisha gani baada ya kupoteza Kazi au Biashara?

Uliishi maisha gani baada ya kupoteza Kazi au Biashara?

Ahsante sana mkuu, huu ni mwaka wa 4 tangu nikumbane na hiyo hali nishaachiwa madhara hasa upande wa miguu kuwa stable, baadhi ya vidole vya miguuni haviko sawa kabisa
Mi uwa nikiwaza sana,chini kidogo ya paji la uso uwa kunakua ganzi kama vile kuna kitu kimeganda, mpaka niwekepo kitu cha baridi ndo napata nafuu kidogo
 
Unaingia kwnye debt cycle na hii ndio hali yangu kwasasa sijawahi shika mshahara wangu kamili kwa muda wa mwaka sasa kila nikipata 60% madeni mimi nabaki na 40% nasurvive kisoja

Lakini watoto wazuri wananipenda hivyo hivyo sijui kwa nini sikuhizi wakati kipindi ninasent hata demu mbovu alikua ananizungusha
Unaingia kwnye debt cycle na hii ndio hali yangu kwasasa sijawahi shika mshahara wangu kamili kwa muda wa mwaka sasa kila nikipata 60% madeni mimi nabaki na 40% nasurvive kisoja

Lakini watoto wazuri wananipenda hivyo hivyo sijui kwa nini sikuhizi wakati kipindi ninasent hata demu mbovu alikua ananizungusha
Hiyo 'aya' ya mwisho imenifurahisha Sana.......😂😂😂😂
 
Ni kukaza mkanda. Mwaka wa nne huu mimi ni jobless mambo uliyoandika hapo ndio maisha yangu ya kawaida ya kila siku.

Sio tu kupoteza mpenzi utajikuta umepoteza hadi marafiki na ndugu zako wa karibu.
Kuna kipindi kilifika nilikuwa na wasiliana na maza tu kwenye simu.
Ndio hali niliyonayo sasa
 
Usiombe biashara ife au kazi iote mbawa, naishi maisha ya kuungaunga mwezi wa pili sasa baada ya kibarua kuota nyasi, poleni sana kwa mliowai kuishi maisha haya, maisha ya kula mlo mmoja na kutojua kesho yako, maisha ya kula leo saa saba mchana mpaka kesho saa saba mchana, hatari ogopa.

Jamaa unakonda ubaki kichwa tu, nimejiapiza hata home likitokea tatizo siwezi kwenda kwa muonekano huu.

Kama umewahi kupita nyakati kama hizi share hapa na wadau siku yako ilivyokua inapita kwa kuungaunga.
Mshukuru Mungu kwa kukupitisha katika kipindi hiki. Kumbuka kuwa kila kitu ni temporary na sio permanent. Ila utajifunza mambo kadhaa ambayo yatakusaidia sana mbeleni.
1. Utawajua marafiki wa kweli
2. Utamfahamu mwenza wako vizuri katika kipindi hiki
3. Utajifunza discipline ya matumizi ya Fedha
4. Utagundua unahitaji a very strong supporting system wakati mwingine utakapoanguka tena
5. Imani yako itazidi sana ( Aidha kwa Muumba au kwa Waganga )

Muhimu ni kutokuta tamaa na kila siku kuendelea kuchungulia fursa mpya.
 
Natamani katika maisha kila mtu apitie hicho kipindi. Ni kipindi utawajua rafiki wa kweli, ndugu wa kweli, utamjua vizuri mpenzi wako (mkeo).
Utafahamu kuwa unaweza kuishi kwa kula mlo mmoja au 2 kwa siku.
Utafahamu kuwa unaweza kutembea kwa miguu yako na ukafanikisha mambo mengi.
Utafahamu kuwa unaweza kuishi uswahilini kodi sh 50K kwa mwezi na maisha yakaenda.
Utajifunza kujibana kifedha ili ufanikishe mambo kadhaa.

Unayotakiwa kuyafanya:
1. Usikate tamaa
2. Wewe una thamani na uwezo mkubwa tu sema Mungu hajaamua bado.
3. Siku utakapotoka katika hali hiyo usiwasahau waliokushika mikono kukuvusha.
4. Usirudie makosa yaliyokuweka kwenye vikwazo.
5. Tafuta chanzo kingine cha mapato hata kiduka kidogo tu. Kitakusaidia sana kujikwamua.

Mimi kuna kipindi nilikaa mwaka mzima. Japo kwa kipindi cha miezi 8 sikuwa natafuta kazi nilikua vizuri tu, miezi 4 ya mwisho nilifilisika ndio nikajua rangi ya upepo.

Baada ya miaka mitano, nikaja kukaa miezi 7 bila kazi tena. Ila week mambo yalivyofunguka nilikua na kampuni 2 mkononi zote zinanihitaji, nikachagua niliyoona bora zaidi.

Na wakati napeleka guarantor's forms nipewe mkataba, kampuni nyingine wakanipigia niende tupange mshahara na makubaliano mengine. Nikawambia ntakuja kesho yake.

Na mchana wake saa 8 na nusu nilikua na interview na kampuni nyingine.

Nothing is permanent.
God above all.
 
Natamani katika maisha kila mtu apitie hicho kipindi. Ni kipindi utawajua rafiki wa kweli, ndugu wa kweli, utamjua vizuri mpenzi wako (mkeo).
Utafahamu kuwa unaweza kuishi kwa kula mlo mmoja au 2 kwa siku.
Utafahamu kuwa unaweza kutembea kwa miguu yako na ukafanikisha mambo mengi.
Utafahamu kuwa unaweza kuishi uswahilini kodi sh 50K kwa mwezi na maisha yakaenda.
Utajifunza kujibana kifedha ili ufanikishe mambo kadhaa.

Unayotakiwa kuyafanya:
1. Usikate tamaa
2. Wewe una thamani na uwezo mkubwa tu sema Mungu hajaamua bado.
3. Siku utakapotoka katika hali hiyo usiwasahau waliokushika mikono kukuvusha.
4. Usirudie makosa yaliyokuweka kwenye vikwazo.
5. Tafuta chanzo kingine cha mapato hata kiduka kidogo tu. Kitakusaidia sana kujikwamua.

Mimi kuna kipindi nilikaa mwaka mzima. Japo kwa kipindi cha miezi 8 sikuwa natafuta kazi nilikua vizuri tu, miezi 4 ya mwisho nilifilisika ndio nikajua rangi ya upepo.

Baada ya miaka mitano, nikaja kukaa miezi 7 bila kazi tena. Ila week mambo yalivyofunguka nilikua na kampuni 2 mkononi zote zinanihitaji, nikachagua niliyoona bora zaidi.

Na wakati napeleka guarantor's forms nipewe mkataba, kampuni nyingine wakanipigia niende tupange mshahara na makubaliano mengine. Nikawambia ntakuja kesho yake.

Na mchana wake saa 8 na nusu nilikua na interview na kampuni nyingine.

Nothing is permanent.
God above all.
[emoji1666]
 
Acha tu ndugu yangu.
Kuna huo mwaka siwezi kuusahau, nipo mjini Dar mambo yamesimama yaani yamekwama hayasogei wala kwenda.
Kipindi hicho ikanibidi nihame nilikokua naishi kwa jamaa niende Buguruni Ghana kwa jamaa yangu mwingine yeye alikua ni mlinzi.
Nilichapika na maisha yaani unatafuta hata kazi ya kufagia na hupati, kazi za nguvu hakuna, huwezi amini hadi zile za kubeba zege nazo zilihitaji connection ndio upate.
Mungu si athumani, nikapata kibarua Ubungo, mshahara laki na nusu. Ukumbuke hapo kule geto tunaishi room bei 40k kwa mwezi na tunachangia pasu. Nikawa kila siku naamka mapema sana nilikua natumia saa limoja na dakika 20 kutoka Buguruni hadi kibaruani Ubungo na hapo hakuna bajeti ya daladala.
Nilipigika vibaya mno kuna wakati ikawa inanibidi niishi kwa bajeti ya buku tu kwa siku yaani hapo nipate asbuhi, mchana na usiku. Na hapa ndipo nikaweka undugu wa karibu sana na mihogo. Kuna mama mmoja alikua napika mihogo pale Tabata TOT darajani, upande wa kushoto ukiwa unaenda Ubungo aisee alinifaa sana wakati ule nilikua nanunua mihogo ya jero ananipa vipande vinne badala ya vitatu nikipiga na maji yangu ya bomba basi saa kumi ninapopita tena wakati wa kurudi napiga ya jero tena na kachumbari nyingii ndio nitolee hadi kesho.Nakumbuka ilifika hatua nikisikia harufu ya mihogo napata kichefuchefu dadadadeqq!
Mambo yaliendelea hivyo hadi kupata kibarua kingine nikawa nalipwa 250k tukahama pale tulipokua tunakaa tukasogea kule wanaita Buguruni karibu na mabwawa tukapata chumba na kijisebule kidogo kwa 50k tukaanza na kujipikia. Na happ ndio angalau nafuu ikionekana.
Siwezi kusahau ule mwaka kwakweli, nilipata SOMO KAMILI LA NAMNA YA KUUMWA NA NJAA na ndio maana hata leo nikikutana na hustler ama dogo analalamika nja hasa hasa mitaa ya kujitafuta kama vile Buguruni, Temeke na Mbagala basi kiroho safi kama kuna mgahawa jirani namlipia chakula maana najua njaa inavyojua kunyanyasa na kutesa mwili.
Ukiwa na njaa unaweza kulia kwa uchungu na chozi lisitoke, kuna siku mwanangu mlinzi hakua na kitu ikabidi aende sokoni Buguruni kuokota mihogo akatafuna mibichi ndio siku ikaenda. Kingine kuna ile hali ya kujua unawaza kimya kimya kumbe unaongea kwa sauti aise, unashtuka mbona kama mtu anakuangalia ndio unashtuka kuwa ulikua ukiongea kwa sauti.Sijawahi kumshangaa mtu anayeongea mwenyewe barabarani, kitu nitakachofanya ni kumsalimia tu ili ashtuke basi.
Ukikuta mtu anakulilia njaa ya tumbo yaani hajala, jama unaweza kumsaidia fanya hivyo na kama una wasiwasi basi mlipoe mgahawani apooze.​
Hustle
 
Mimi Nina swali,sio kwa ubaya.. huwa inatokana na Nini mtu anafanya kazi miaka mitano,but akipigwa chini miezi miwili tu analia njaa,

Hata akiba ya Kuanza biashara ndogo Huwa hakuna??hata Hela ya kula miezi sita wakati unajitafuta hakuna??

Changamoto inakuga Nini??
Nina mwaka wa14 kazini, nikifukuzwa leo hata mwezi hauishi naanza kusota
 
Usiombe biashara ife au kazi iote mbawa, naishi maisha ya kuungaunga mwezi wa pili sasa baada ya kibarua kuota nyasi, poleni sana kwa mliowai kuishi maisha haya, maisha ya kula mlo mmoja na kutojua kesho yako, maisha ya kula leo saa saba mchana mpaka kesho saa saba mchana, hatari ogopa.

Jamaa unakonda ubaki kichwa tu, nimejiapiza hata home likitokea tatizo siwezi kwenda kwa muonekano huu.

Kama umewahi kupita nyakati kama hizi share hapa na wadau siku yako ilivyokua inapita kwa kuungaunga.
We acha tu,
kipindi inafika maji unayanywa na kusifia matamu kishenzi. wenzio ni ma senior sakta hiyo
 
Hayo mambo yasikie kwa jirani.
Nilijifunza kumtumainia Mungu pekee...the rest yamebaki story tu kwa sasa.
 
Back
Top Bottom