Ulilipokea vipi shambulio la JF?

Ulilipokea vipi shambulio la JF?

Ila kanichekesha ukhuty kaja kwa upole ananiuliza taratibuu eti "dada umeingia jf leo" nikacheka sana yaani.
Hahahahahaaaa.

Mimi kaja kashusha malalamiko mengi kwa huzuni sana.

Nikamwambia na mimi hali iko hivyo hivyo toka jana.

Nikamwambia nimesikia kuna tatizo na linafanyiwa kazi, hapo ndio presha ikashuka
 
Hahahaa, pole sana Hajar nimejikuta nimecheka kwa sauti kwa kusoma jinsi ulivyo hangaika, ama kweli ukitaka kujua thamani ya kitu kikutoke kwanza, kwakweli kila mtu alitaharuki kwa style yake kutokana na shambulio la forum hii pendwa, lakini tunashukuru imekaa sawa kwa haraka
Hahahaaaa. Wacha kabisa halafu kuna mtu anajijua [emoji85] nilikuwa nataka kuongea nae kitu saa kumi ndio nkazidi kupagawa Hajar mie.

Ila bora imerudi hewani sababu ilikuwa balaa.
 
Ilipokataa kuanzia saa kumi hadi saa 12 jioni nikaachana nayo, nilikula Dinner mapema nikashiba sana [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] , kuanzia shiba na uchovu wa kutwa nzima kwa Jamhuri nikajikuta niko hoi, nikaamua kulala ili nijiweke kwenye msawazo.

Bahati nzuri nilishtuka majira ya mid night ndio nikakuta imerejea kidogo na mimi nikaingia japo kwa mbinde.
Hahaaa. Davet njoo huku naona bila hiyo kushiba sana [emoji23] [emoji23] usingizi ungekuwa ndoto.

Hongeta kwa kweli mdogo wangu.
 
Back
Top Bottom